Uchaguzi 2020 Sababu kuu ya Lissu kushindwa, asilimia 80 ya Watanzania wanaishi Vijijini hawamjui Lissu ni nani, Magufuli anajulikana kila kona Vijijini

Huyo "anayejulikana" anajulikana kwa mema au mabaya? Hahahaha basi kazi unayo
Anajulikana kwa kazi zake..siku hizi watu hawakai vijiweni kama zamani..fursa za kutafuta pesa zimefunguka..watu wamejazana mabarabarani..hakuna tishio la mgambo wala jkt wala traffic.
 
Kanda ya Ziwa ndiko walikovhomewa nyavu na kupasuliwa mitumbwi na Luhaga Mpina kwa baraka za Magufuli, Kanda ya ziwa ndiko walikotaifishwa mifugo na TANAPA, Kanda ya ziwa ndio waliovurugiwa vyanzo vyao vya uchumi kila mahali. Unaongea bila utafiti.
 
Watanzania wa Leo sio wa wakati wa Nyerere . juzi nilikua naangalia taarifa ya habari kwenye kibanda umiza huku kijijini. Iliposomwa habari ya Lissu kupitishwa kugombea huwezi amini ukumbi mzima ulilipuka kwa shangwe wote wakaanza kumshangilia . CCM msijidanganye hamkubaliki hata na ngedere.
 
Huku kanda ya ziwa hata kwa ubunge tuu ccm hawatoboi bila wizi.. itakuwa urais?! Huku Lisu ndo habari ya kanda
 
Hivi ww ndo ulisema akitua nchini tu unakula kichwa?
 
Mkuu binafsi sijaona sababu ya kumpa/ kumpigia kura. Kwa anayoyafanya Magufuli sioni kama ataweza hata nusu.
 
Acha uongo. Mbona mimi nipo kanda ya ziwa hata kumsikia tu jina lake huyo jiwe hatutaki.
 
Naona xaxa umechanganyikiwa et lowassa ndo kanda ya kaskazini ,,,kabla ya ujio wa lowassa chadema kaskazini ilikuwa tayari ngome ya chadema ndo maana Mara zote maccm wanadhiriki kukiita chama cha kaskazini
 
Unaposema kanda ya ziwa wanamkubali magufuli umelithibitishaje ,,, c ndo kule aliwadhihaki kuwa yeye hajaleta tetemeko wakati watu wakiomba msaada kagera,,pia yule aliyeulizwa akasimama na kusema serikali haina shamba huku watu wakiteseka alikuwa anawaambia watu wa kanda IPI? Hizo bangi zako peleka huko Magufuli ana kazi kubwa hata Chato kura hapati
 
unajidanganya! By the way mamvi mlimuibia kura kama kawaida yenu ya kuiba nyie! Huyu haibiwi poleni! Muda wa kusaga jiwe na kulitupa baharini umefika count days1,2,3.4,5-----
 
Kanda ya kusini tumedhulumiwa korosho zetu,kaskazini hana chake miaka na miaka kule ata kabla ya lowassa arusha manyara na Kilimanjaro ndo chadema ilipokuwa inajizoleaga ushindi,kanda ya ziwa hela za msaada wakat wa tetemeko alipeleka kwenye miradi ya serikali huku akisema hajaleta tetemeko na kila moja apambane mwenyewe ,kigoma kule naamini pia upinzani upo,Dar-es salaam( sehemu yenye population nyingi) upinzani ,Mbeya ndo usiseme xaxa huyo mwamba wenu anabaki na kanda ya kati ambayo kuna Lissu kule na Nyalandu ndo ataelewa show
 
Utambulisho wa TL kwa asiyemjua ni YULE ALOPIGWA RISASI
 

We jana ulisema Nyalandu atashinda? Imekuwaje tena?
 
Hahaaaa bangi ikipanda kichwani ndo ipo hivo kumbe kule mwamba Mbowe ndo ngome yake ndo maana ata hapigagi kampeni xana maana wanamjua na bado yupo _,,Kama ilikuwa ngome ya slaa alipoondoka 2015 basi chadema ingekufa kule
Ilikuwa ngome ya Slaa mikoa ya Arusha na Manyara ndie alijenga upinzani Manyara na Arusha.Kilimanjaro mzee mtei ndie alijenga hiyo ngome akamwachia mkwe mbowe

Hiyo Kanda nguvu imesambaratika Baada ya Slaa ,Lowasa na Sumaye kuondoka
 
Ajieleze hali ya maisha atutoaje kutoka hapa.
 
Leta ushindi wa jiwe jimbo kwa jimbo! vile vile tupe zile computer zetu mlizopora mlimani city! Sasa BASI!
 
Mkuu Chadema wanachotaka ni ruzuku full stop. Hapa zinatafutwa kura za wabunge na za Rais kwa ajili ya kupata ruzuku. Hii ya kushika dola wanawazuga tu wao, wanajua fika mgombea walienae hana uwezo wa kushinda.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…