Sadock Kabuko
JF-Expert Member
- Mar 26, 2013
- 1,166
- 1,075
Wakuu Heshima Kwenu.
Kwa hali ya siasa na kampeni zinavyoendelea ni wazi kabisa CCM itashinda kwa kishindo, kwa CCM mpya chini ya Dkt Magufuli CCM imesukwa vya kutosha iko imara na kwa uchaguzi huu CCM itashinda kwa kishindo zipo sababu kadhaa zitakazopelekea CCM kushinda kwa kishindo
1. Udhaifu wa upinzani Tanzania
Ni dhahiri kabisa upinzani wetu sio haujajikita kuchukua dola badala yake wamejikita katika kufanya majaribio ya kushika dola, sera na hata imani kwa wananchi ni dhaifu sana, wananchi wengi hawawamini wapinzani, ikiwa tu wameshindwa ndani ya vyama vyao kuaminiana na kuwa kitu kimoja, na wameshindwa kuungana na kusimamisha mgombea mmoja ni dhahiri kabisa upinzani hauko imara. Ikiwa wameshindwa hata kupeleka fedha za kuendeshea ofisi za wilaya na mikoa chama licha ya kuwa na ruzuku ni ukweli usiopingika wananchi hawawezi kuamini vyama vya namna hiyo.Kwani kuongoza nchi sio majaribio na kupitia sababu hii CCM itashinda kwa kishindo na wapinzani wataishia kulalamika kwamba wameibiwa kura kama ilivyo kawaida yao.
2. Uelewa wa wananchi kuhusu siasa
Wananchi wengi siku hizi ni waelewa na wanajua kuchambua mambo wanajua mbichi ni ipi na mbivu ni ipi hakika Rais Magufuli ameeleweka sana kwa wananchi, wananchi wamelewa sana siasa zake, ambazo ni za kuleta maendeleo watanzania, kwa nchi ilipokuwa imefikia tulihitaji siasa za CCM mpya chini ya Dkt Magufuli ili tuweze kupata maendeleo. Kitendo cha wanasiasa wengi kuhamia CCM imedhirika wazi kabisa na kila mwananchi anaelewa kabisa ni chama kipi kinachoweza kumletea maendeleo ya kweli, Aidha Raisi Magufuli ametuonesha sura halisi za wapinzani wengi wao ni wa roho wa madaraka na upinzani tanzania umeshikiliwa na watu wachache wenye masilahi yao binafsi.
3. Sera dhaifu za wapinzani
Kwa kampeni hizi zinazoendelea ni wazi kabisa wapinzani hawana sera za kumfanya mwananchi wa kawaida kuwaamini na kuwachagua mfano mzuri ni Mgombea kupitia CHADEMA ndg. Tundu Lissu, hakuna mwananchi ambaye hajui kwamba Tundu Lissu alipigwa risasi na hakuna aliyefurahia kitendo kile ndio maana hata viongozi wa CCM wakiongozwa na makamu wa Raisi Mh. Samia Suluhu walifika hospitali kumuona, kila mtu alifurahi kuona amelejea akiwa na afya njema.
Kwanini nimemtolea mfano ni miongoni mwa wagombea ambao hawana sera za kumshawishi mwananchi wa kawaida kumchagua kwa sababu sera zake nyingi zimejikita kukosoa maendeleo ambayo yameletwa na Raisi Magufuli, karibia nusu ya kampeni zake haelezi nini atawafanyia watanzania badala yake amejikita kueleza namna alivyopigwa risasi, kitu ambacho hakimshawishi mwananchi wa kawaida kumchagua. Kushindwa kwa wapinzani kuweka bayana mambo ambayo watawafanyia wananchi badala yake sera zao zimelenga kukosoa mema yaliyofanywa na CCM kwa kuyageuza kuwa mabaya.
4. CCM kukubalika miongoni mwa vijana
Baada ya Mh. Magufuli kuchagulia na kuisuka CCM, chama hiki kimeleta mvuto sana miongoni mwa vijana hii ni baada ya Magufuli kutekeleza yale ambayo vijana wengi walikuwa wakitamani kuyaona yakitendeka ndani ya chama, hivyo kupelekea vijana wengi kujiunga na CCM na kukiunga mkono chama. Aidha miaka ya nyuma ilikuwa ni dhambi kwa kijana kuvaa sare za chama, lakini kwa sasa vijana wengi hujivunia sana na kuona fahari kuwa wana-CCM. Sababu hii pia itakipa ushindi mkubwa
5. Upinzani kudanganywa na wanamitandao
Hakuna asiyejua kwamba wapinzani wengi hutegemea taarifa na propaganda za mitandaoni kama sehemu yao ya kupima uungwaji mkono jambo ambalo huwatanganya kwani asilimia kubwa ya wapiga kura hawana asses na mitandao ya kijamii, aidha wanapropaganda wengi hutumia lugha ya matusi,kejeli n.k kama njia mojawapo ya kuwafurahisha wamiliki wa vyama vyao. Kwanini CCM itashinda kupitia udhaifu huu hakuna asiyejua CCM imejikita sana kumsaidia mwananchi wa kawaida ambaye yeye maji,barabara,afya na umeme ndio kipaumbele kikubwa sana kwake. CCM kupitia Raisi Magufuli wamethubutu kuyatekeleza hayo. Vyama vya upinzani kwa kutengemea wafuasi wao ambao wamejawa na matusi na kejeli kupitia mitandao ya kijamii na wengi wao sio wapiga kura ni wapiga ramli watashindwa sana katika uchaguzi huu.
NB; Siku zote dawa hata kama ni chungu kubali kuinywa ili upone
Kwa hali ya siasa na kampeni zinavyoendelea ni wazi kabisa CCM itashinda kwa kishindo, kwa CCM mpya chini ya Dkt Magufuli CCM imesukwa vya kutosha iko imara na kwa uchaguzi huu CCM itashinda kwa kishindo zipo sababu kadhaa zitakazopelekea CCM kushinda kwa kishindo
1. Udhaifu wa upinzani Tanzania
Ni dhahiri kabisa upinzani wetu sio haujajikita kuchukua dola badala yake wamejikita katika kufanya majaribio ya kushika dola, sera na hata imani kwa wananchi ni dhaifu sana, wananchi wengi hawawamini wapinzani, ikiwa tu wameshindwa ndani ya vyama vyao kuaminiana na kuwa kitu kimoja, na wameshindwa kuungana na kusimamisha mgombea mmoja ni dhahiri kabisa upinzani hauko imara. Ikiwa wameshindwa hata kupeleka fedha za kuendeshea ofisi za wilaya na mikoa chama licha ya kuwa na ruzuku ni ukweli usiopingika wananchi hawawezi kuamini vyama vya namna hiyo.Kwani kuongoza nchi sio majaribio na kupitia sababu hii CCM itashinda kwa kishindo na wapinzani wataishia kulalamika kwamba wameibiwa kura kama ilivyo kawaida yao.
2. Uelewa wa wananchi kuhusu siasa
Wananchi wengi siku hizi ni waelewa na wanajua kuchambua mambo wanajua mbichi ni ipi na mbivu ni ipi hakika Rais Magufuli ameeleweka sana kwa wananchi, wananchi wamelewa sana siasa zake, ambazo ni za kuleta maendeleo watanzania, kwa nchi ilipokuwa imefikia tulihitaji siasa za CCM mpya chini ya Dkt Magufuli ili tuweze kupata maendeleo. Kitendo cha wanasiasa wengi kuhamia CCM imedhirika wazi kabisa na kila mwananchi anaelewa kabisa ni chama kipi kinachoweza kumletea maendeleo ya kweli, Aidha Raisi Magufuli ametuonesha sura halisi za wapinzani wengi wao ni wa roho wa madaraka na upinzani tanzania umeshikiliwa na watu wachache wenye masilahi yao binafsi.
3. Sera dhaifu za wapinzani
Kwa kampeni hizi zinazoendelea ni wazi kabisa wapinzani hawana sera za kumfanya mwananchi wa kawaida kuwaamini na kuwachagua mfano mzuri ni Mgombea kupitia CHADEMA ndg. Tundu Lissu, hakuna mwananchi ambaye hajui kwamba Tundu Lissu alipigwa risasi na hakuna aliyefurahia kitendo kile ndio maana hata viongozi wa CCM wakiongozwa na makamu wa Raisi Mh. Samia Suluhu walifika hospitali kumuona, kila mtu alifurahi kuona amelejea akiwa na afya njema.
Kwanini nimemtolea mfano ni miongoni mwa wagombea ambao hawana sera za kumshawishi mwananchi wa kawaida kumchagua kwa sababu sera zake nyingi zimejikita kukosoa maendeleo ambayo yameletwa na Raisi Magufuli, karibia nusu ya kampeni zake haelezi nini atawafanyia watanzania badala yake amejikita kueleza namna alivyopigwa risasi, kitu ambacho hakimshawishi mwananchi wa kawaida kumchagua. Kushindwa kwa wapinzani kuweka bayana mambo ambayo watawafanyia wananchi badala yake sera zao zimelenga kukosoa mema yaliyofanywa na CCM kwa kuyageuza kuwa mabaya.
4. CCM kukubalika miongoni mwa vijana
Baada ya Mh. Magufuli kuchagulia na kuisuka CCM, chama hiki kimeleta mvuto sana miongoni mwa vijana hii ni baada ya Magufuli kutekeleza yale ambayo vijana wengi walikuwa wakitamani kuyaona yakitendeka ndani ya chama, hivyo kupelekea vijana wengi kujiunga na CCM na kukiunga mkono chama. Aidha miaka ya nyuma ilikuwa ni dhambi kwa kijana kuvaa sare za chama, lakini kwa sasa vijana wengi hujivunia sana na kuona fahari kuwa wana-CCM. Sababu hii pia itakipa ushindi mkubwa
5. Upinzani kudanganywa na wanamitandao
Hakuna asiyejua kwamba wapinzani wengi hutegemea taarifa na propaganda za mitandaoni kama sehemu yao ya kupima uungwaji mkono jambo ambalo huwatanganya kwani asilimia kubwa ya wapiga kura hawana asses na mitandao ya kijamii, aidha wanapropaganda wengi hutumia lugha ya matusi,kejeli n.k kama njia mojawapo ya kuwafurahisha wamiliki wa vyama vyao. Kwanini CCM itashinda kupitia udhaifu huu hakuna asiyejua CCM imejikita sana kumsaidia mwananchi wa kawaida ambaye yeye maji,barabara,afya na umeme ndio kipaumbele kikubwa sana kwake. CCM kupitia Raisi Magufuli wamethubutu kuyatekeleza hayo. Vyama vya upinzani kwa kutengemea wafuasi wao ambao wamejawa na matusi na kejeli kupitia mitandao ya kijamii na wengi wao sio wapiga kura ni wapiga ramli watashindwa sana katika uchaguzi huu.
NB; Siku zote dawa hata kama ni chungu kubali kuinywa ili upone