Sababu ya kocha Simba SC kutomuingiza Kagere

Boko hakukosa goli alipiga shuti likagonga mwamba. Muogopeni Mungu
 
Nadhani kocha hampendi Kagere sio kwamba Kagere bora sana lakini ni bora kuliko Mugalu kuhusu Simba kuwa bora sana ni wazuri lakini sio bora sana Kaizer ni team dhaifu katika team zote zilizoingia hatua hii na wametutoa haijalishi tumewafunga 3 na pia tulikuwa na washabiki wao walitufunga 4 bila mashabiki kwa hiyo advantage fulani tulipata.
 
Mmeanza,na kishingo mlimsakama hivyohivyo
 
Kwa maoni yangu, sababu zako zote mbili sio sahihi. Usiklaumu kocha wala Mugalu. Simba ina kocha bora sana na Mugalu kafanya kazi yake zaidi ya matarajio (+100%)

Nakuhakikishia, bila Mugalu, Bocco asingefunga yale magoli mawili na huenda hata Chama asingefunga na Simba ingeweza kufungwa au hata kutoka draw.

Mugalu ni mzuri wa kukaa na mipira na pia alikua anawafanya mabeki wa Kaiser wapoteane kati ya kumkaba Bocco au Mugalu, japo Mugalu hafungi lakini anawatanua sana mabeki na kuwapa nafasi wengine wapite na kufunga. Tatizo la Kagere huwa ni wakuletewa tu na hawezi kukaa na mpira na ni mtu wa kunyemelea na sio kupambania nafasi...sasa Kaiser walikua wanajaa nyuma asingepata chance yeyote na pia Kagere sio mzuri wa kutoa pasi...yeye ni kufunga tu yeye kama yeye kwahiyo inabidi wengine ndio wacheze kumtafuta, wakishindwa hana msaada.

Kwa upande wa kocha, SA alitumia 4-2-3-1 wakati Kaiser walitumia 3-4-3...sasa Kaiser walikua wajanja, wakati wanashambuliwa walikua hao wa4 wa katikati wanakua nyuma jumla 7 na wakati wanashambulia wanakua mbele jumla 7. Ndio maana SA kulikua na msitu nyuma. Simba SA walikua pia wanajihami sana kwahiyo mbele mara nyingi walikua 4 na labda wakiongozeka ni wawili jumla 6. Wakishambuliwa wanabaki 6 wakati jamaa wanakua 7.

Jana Simba walikua 4-4-2 wakati Kaiser wakabaki na ile ile 3-4-3, sasa pamoja na Simba kuwa 6 wanaposhambulia lkn hata wakiwa hawashambulii lkn uwepo wa Bocco na Mugalu uliwafanya wale wanne wa Kaiser wapungue kwenda mbele ili wabaki kuongeza nguvu nyuma na wakati huohuo wana waacha wale wa4 wa Simba wa katikati wawe free zaidi na muda wote kukaa golini kwa Kaiser, ndio maana Kocha wa Simba alivyoona kafanikiwa kumiliki mpira katikati akamtoa Mzamiru (maana hawahitaji kupokonya tena mipira) akamuingiza Morrison ili kwenda kuongeza nguvu kwenye kuipanguwa beki ya Kaiser

Huo ndio mtazamo wangu.
 
KAGERE Ni striker mzuri kwa ligi za mavumbini sio CAF CHAMPIONSHIP.

japokua haiondoi ukweli kua Mugalu Ni garasa la maana kule mbele.
 
Vyema ampe nafasi na Kagere kuliko kukomaa na Mugalu muda wote no matter what.
KAGERE alipewa nafas ile gemu ya Al ahly away akaanza kabisa From 1st minute.

Alichokicheza mule kila mtu alikiona, Ni garasa mara 100 ya Mugalu.
 
Ila kitu nachokuhakikishia mimi simkubali Mugalu nampendekeza zaidi MK14,ila kuna kitu cha kiufundi pengine anacho ambacho kwa sisi mashabiki hatuwezi kukiona.
Kocha Gomes anakaa na wachezaji kwa muda na anawaona wakiwa mazoezini.
Simba nguvu moja.
Inawezekana weee umezoea kumuona MK14 Kwenye ligi ya ndani.

Ila ukimuona kwny hii michuano ya CAF mechi zote alizoingia,

Utakubaliana na Mimi kua KAGERE sio international player kabisa.
 
Mbona kagere ndo garasa kabisa.

Mechi na alhaly ameanza, ila kila zikipigwa cross hayupo position, mipira ya rebounds inapigwa yeye hayupo.

Anazurura TU uku na kule uwanjan.

Mara Mia ya Mugalu anajua kujiposition at Kama uwezo wake wa kufunga bado Ni butu.
 
KAGERE alipewa nafas ile gemu ya Al ahly away akaanza kabisa From 1st minute.

Alichokicheza mule kila mtu alikiona, Ni garasa mara 100 ya Mugalu.
Kikosi kilichoanza unakikumbuka alicheza na kina nani? Unamuhukumu vipi mchezaji kwa gemu moja? Game ngapi mugalu ni mashuzi tu?

Yote 9, 10 ndio mfungaji wetu bora misimu miwili ama mi3 mfululizo.. Nyongeza kwa dk chache alizopewa nahisi ana wastani wa magoli mengi kuliko mugalu.
 
Kwa mugalu kagere ni bora zaidi, hata huko caf alifanya vema msimu wa 2018/19
KAGERE keshapewa nafas Sana na kocha, ila kila anachokicheza hakieleweki.

Mechi na Al ahly kagere alijisahau kabisa Kama Ni striker nae akawa anarudi nyuma kukaba.

Mabeki kuona ivyo, nao wakaanza kupanda.

Kumbuka vizur ata Lile goli la Al ahly,pass ya goli ilitoka kwa beki aliepanda baada ya kuona nyuma hamna hatar yoyote.

KAGERE anaigarimu timu, vinginevyo ajirekebishe
 
Game iyo moja ilitosha yeye kuitetea Nafas, kumbuka michuano ya CAF Ina mechi chache Sana.

Hakuna kugamble, ukipigwa unatupwa nje
 
Goli lilikuwa boko la mkude, kifupi kamuharibu na saikolojia, kumpiga benchi, akimchezesha ni gemu isiyo na uzito, mara ampange na watu wa kikosi cha pili, unadhani akicheza na ndemla atapata huduma kama anayopata kqa chama!?

Tuwe serious, kwa mugalu kagere ni bora mnoo..

Lete takwimu
 
Game iyo moja ilitosha yeye kuitetea Nafas, kumbuka michuano ya CAF Ina mechi chache Sana.

Hakuna kugamble, ukipigwa unatupwa nje
Ni game ambayo kwa simba ilikuwa ni kukamilisha ratiba tu.
 
Kazi ya striker ni kufunga magoli mjomba sio uzuri wa kukaa na mpira, huo mpira aliokaa nao uneisaidia nini timu mbona tumetoka kama angefunga kwa zile nafasi alizopoteza habari ingekuwa tofauti, habari ya kukaa na mpira waachie viungo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…