Sababu ya wastaafu wengi kuishi maisha magumu baada ya kustaafu

Sababu ya wastaafu wengi kuishi maisha magumu baada ya kustaafu

Kichwa Cha mleta thread ndio wanakubali ujinga wa kipewa wastafuu hela kiduchu hela zao tena wanapangiwa jinsi ya kitumia wakati kifo nje nje ..mfano mzuri General Mbunge kastafu 2023 na kafa jana ..angepewa hela yake zote familia si wangefaidika..TUACHANE NA GEN MBUGE YEYE ALIKUWA KWENYE HIGH TABLE CAKE AMEACHA VITEGA UCHUMI VINGI ,FIKIRIA MWALIMU WA MAKONDE NDANI NDANI HUKO ALIYESTAFU KAMA MBUGE 2023 ALAFU KAFA JANA PENSHENI IMEMSAIDIA NINI FAMILIA YAKE
Utaratibu wa kulipa pensheni yote kwa mkupuo sio mzuri sana.
Na pensheni kiasi chote kinatakiwa kuhesabika kwa mstaafu akiwa hai, akiwa ametangulia basi next of kin waweze kukomboa kiasi chote kilichobaki.
Tofauti na hapo ni utapeli wa serikali kwa watumishi wake.
 
Wafanyakazi wengi hawana elimu ya fedha.

Wakiajiriwa wanakopa hela halafu wana nunua gari wana ipaki kuanzia asubuh mpaka jioni huku inadai mafuta na service costs na hela inakatwa.

Lakini pia wafanyakazi wengi hawajishughulishi na bussness yoyote wakistaafu wanapoteza hela kwenye biashara ambazo hawajawahi kufanya.

Elimu ya fedha ni tatizo kwa watumishi wengi sana.
 
Kichwa Cha mleta thread ndio wanakubali ujinga wa kipewa wastafuu hela kiduchu hela zao tena wanapangiwa jinsi ya kitumia wakati kifo nje nje ..mfano mzuri General Mbunge kastafu 2023 na kafa jana ..angepewa hela yake zote familia si wangefaidika..TUACHANE NA GEN MBUGE YEYE ALIKUWA KWENYE HIGH TABLE CAKE AMEACHA VITEGA UCHUMI VINGI ,FIKIRIA MWALIMU WA MAKONDE NDANI NDANI HUKO ALIYESTAFU KAMA MBUGE 2023 ALAFU KAFA JANA PENSHENI IMEMSAIDIA NINI FAMILIA YAKE
Tatzo sana mkuu. Watu wapewe hela zao tena ikiwezekana muda wowote wanaoitaka si zao bwana.
 
Tumeshuhudia kundi kubwa la wastaafu kuishi maisha magumu baada ya kustaafu hii husababishwa na mambo kadhaa miongoni mwa mambo yafuatayo

Kutojiandaa kustaafu
Wafanyajazi wengi huwa hawajiandai kustaafu na wamekuwa wakiishi maisha kama watakuwa waajiriwa maisha yao yote hali inayopelekea kutojijengea misingi ya namna ya kuishi baada ya kustaafu..

Kuegemea mshahara pekee
Hii ni sababu nyingine wafanyakazi wengi hutegemea mshahara wake pekee katika kuendesha maisha anakuwa hana kitegauchumi kingine kitakachompatia pesa baada ya kustaafu

Mshahara milioni, matumizi milioni
Hii hutokea wafanyakazi wengi hutumia mshahara wake wote anaoupata kiasi chakutokuwa na akiba hali inayopelekea kuwa na control ndogo ya pesa mfano anafanyakazi kwa mwez anatumia milioni akistaafu na kszini haendi inamaana matumizi yatazidi milioni moja baada ya muda kupoteza pesa zote za kiinua mgongo

Kufungua biashara baada ya kustaafu
Mtu hajawahi kuwa na biashara hajui changamoto za biashara akistaafu ndiyo anafungua biashara tena baada ya kushauliwa biashara ya kufanya na unavyojua kila biashara inalipa ukisimuliwa kwakuwa hana uzoefu anajikuta anashindwa kuendesha biashara mwisho anapoteza pesa

Hivyo basi mwajiliwa ukianza biashara ukiwa kazini kuna uwezekano mkubwa wa kufanikiwa baada ya kustaafu maana kuruka sarakasi hawajifunzi ukubwani.

View attachment 3124451
Unajenga nyumba ama unafungua biashara ambayo huna uzoefu nayo, upweke bagoshaa ni Jambo la muda TU.

Nukuu ya baba wa taifa.
""UTII UKIZIDI SANAA HUZAA UOGA, UOGA UKIZIDI SANA HUZAA UNAFIKI NA KUJIPENDEKEZA NA MWISHO WAKE NI MAUTI""
 
Utaratibu wa kulipa pensheni yote kwa mkupuo sio mzuri sana.
Na pensheni kiasi chote kinatakiwa kuhesabika kwa mstaafu akiwa hai, akiwa ametangulia basi next of kin waweze kukomboa kiasi chote kilichobaki.
Tofauti na hapo ni utapeli wa serikali kwa watumishi wake.
Kama sio utaratibu nzuri kwa nini Kanda zingine hakuna kikokotoo ? ,je wao wanajua kupanga matumizi kuliko wengine ?huoni Kuna upendeleo wa kikokotoo kwa baadhi ya kanda?
 
Back
Top Bottom