Sababu za kiroho kwanini Mike Tyson alipigwa na Evander mwaka 1996

Sababu za kiroho kwanini Mike Tyson alipigwa na Evander mwaka 1996

Mkanyaga mafuta anapotafuta wafuasi. Vp Mohammed Ali?
Muhammad Ali was not putting his God in his fights. It was between him and his opponents and not his God Vs his opponent's God.

Mods wekeni option ya fimbo hapa slow learners kama huyu Jamaa tuwe tunawatandika fimbo.
 
Ndugu yangu nachelea kusema kuwa unaweza ukawa hauko sahihi kwa hoja yako hii kutokana na ukweli kwamba, kwa uelewa wangu mimi, Allah Akhbar ni neno la kiarabu linalomaanisha Mungu Mkubwa. Kwa hiyo alichokuwa ana-chant Tyson na wafuasi wake, angeweza kuki-chant hata kwa kutumia maneno hayo ya Kiswahili, au angeweza pia kutumia kiingereza "God is Greatest". Hii lugha haina uhusiano na Uislam, kwa sababu tuseme kama Tyson angekuwa ni mwarabu halafu kwa dini akawa ni mkristo, bado angetumia maneno hayo kwa lugha ya kiarabu, yakiwa na maana ile ile ya Mungu ni mkubwa. Naomba nitoe tahadhari kwa baadhi yetu wakristo huwa tuna ufahamu mdogo ambao wakati mwingine huwa unatupelekea kuhusisha baadhi ya maneno ya kiarabu na Uislamu. Neno kwa mfano Salaam Aleikhum, si salamu ya waislamu, ni salamu ya kila mtu inayomaanisha Amani iwe nawe.

Still, mimi napendelea zaidi kushauri kuwa kama wewe ni muislamu, u-concentrate zaidi na mambo ya Kiislamu, na kama wewe ni Mkrsito vivyo hivyo. Hata hivyo tushirikishane zaidi mambo mema yaliyopo kwenye dini zetu hizi mbili, badala ya kuangalia tofauti zetu zaidi. Kwenye mgogoro wa uchinjaji nyama kwa mfano, aliwahi kuibuka Mzee wa Upako kwenye media akakemea sana hali hii, na kikubwa zaidi alichosema ni kwamba DINI HIZI MBILI DUNIANI, UISLAMU NA UKRISTO ZINASHAHIBIANA KWA KARIBU SANA KWENYE MAUDHUI YAKE NDANI YA MAANDIKO MATAKATIFU YA KILA MOJAWAPO YA DINI HIZI.
Zaidi kwa upande wangu mimi huwa ninaona UISLAMU ni Dini ambayo, inazidi ku-cement zaidi juu ya uwepo wa Yesu, kwa sababu Qurani pia inakiri uwepo wake. Tungekuwa peke yetu wakristo tu na pakawa hapana dini nyingine yenye kutambua uwepo wa Yesu, possibly wangekuwa wanajitokeza watu na kuhoji kuwa pengine Yesu hakuwepo na ingekuwa ni ngumu kidogo, kuliko ilivyo sasa, kuwapa majibu ya kuwaridhisha juu ya uwepo wake. Lakini kwa sasa hivi mtu akibisha kuhusu uwepo wa Yesu, unachotakiwa kufanya ni kumtuma tu aende msikitini akawaulize waumini wa Kiislamu au Mashehe halafu watampatia majibu. Unaona sasa Uislamu ulivyo msaada kwa Ukristo? Tena msaada mkubwa mno kwa sababu kitu kikubwa kabisa ambacho mwanadamu anatakiwa akifahamu ili aweze kuwa Mkristo, ni uwepo wa Kristo, yaani Yesu!
Wewe ndio hujui ndugu, Allah na Mungu wa Israel ni vitu viwili tofauti kabisa. Inasemekana wakati muhammad amekuwa mtume alikuta watu wa eneo lile wanaabudu Miungu watatu, sasa Mohammad akawaambia mnatakiwa kumwabudu Mungu mmoja tu! Hivyo akawaambia wachague Mungu mmoja miongoni mwa hao watatu ambaye ndiye atakuwa Mungu wao rasmi. Kwa hiyo wale watu wakamchagua Allah awe Mungu wao, na wale miungu wengine wakabebwa wakaenda kuwekwa millimani huko. Sasa huyu Allah alikuwa man made na mpaka leo watu wanasali kuelekea uelekeo alipo Allah., ulishawah kujiuliza why wakisali lazima waelekee upande mmoja tu? Sasa Mungu wa Israel (Jehova) yeye yuko mahali pote, ukitaka kusali unaangalia uelekeo wowote tu!. Tatizo mkiishaingia dini fulani huwa mnapofuka macho, huwa hamtafakali kabisa!. Hii dunia ina miungu weeeengi! Wapo akina Baali, Dagon, Allah, Jehova (pia anaitwa Yahwe) n.k. Sasa kama unadhani hao niliowataja ni Mungu mmoja wewe utakuwa haupo serious kabisa. Hata ukisoma vitabu vya dini kuu mbili vipo tofauti kama mbingu na ardhi.. Dini moja inasema tukienda peponi tutakuwa tutapewa wanawake vigoli wenye macho makubwa kama vikombe na pia tutakaa kwenye bustani ambayo katikati yake unapita mto ambao maji yake ni pombe.. Sasa imajini upo kwenye bustani na vigoli zaidi ya mmoja wamekuzunguka halafu kuna mto wa pombe unapita hap pembeni, hivi kutakuwa na usalama hapo? Upande mwingine wanasema watatembea kwenye bustani ya kioo! Tatizo hizi dini huwa zinawakataza kusoma vitabu vya dini nyingine kwa hiyo ulichofundishwa au kusoma utakariri hicho hicho.. Ingia youtube tafuta bandiko linasema Allah na Jehova ni kitu kimoja?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Muhammad Ali was not putting his God in his fights. It was between him and his opponents and not his God Vs his opponent's God.

Mods wekeni option ya fimbo hapa slow learners kama huyu Jamaa tuwe tunawatandika fimbo.
Tatizo hawajakuelewa mkuu!. Mimi nimeshawishika kuamini na nadhani tatizo kubwa watu wengi hapa walikuwa hawamjui tyson. Yule jamaa was a beast, alikuwa anawadunda wapinzani wake vibaya mno! Kwa kweli kwenye lile pambano hakuna mtu aliyetarajia tyson kupigwa vile. Mimi nilisononeka mno siku hiyo kwa vile mpaka leo sijawah kuona fighter kama tyson. Nadhan kosa lake kuu ni kuingiza udini akidhan Allah ni Yahwe!.. Hata wacheza mpira ambao akifunga goal anakimbia na kusujudi hadi ardhin huwa wanapotea kwenye anga za soka kiajabu ajabu. Mohammad Ally hakuwah kuingiza udini kwenye fighting zake, thats why akafika mbali sana!.. Shida hapa kuna miungu wawili mmoja anajipigania mwenyewe na kuwapigania wafuasi wake na mwingine anapiganiwa na wafuasi wake hadi wanajitoa mhanga

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom