Ndugu yangu nachelea kusema kuwa unaweza ukawa hauko sahihi kwa hoja yako hii kutokana na ukweli kwamba, kwa uelewa wangu mimi, Allah Akhbar ni neno la kiarabu linalomaanisha Mungu Mkubwa. Kwa hiyo alichokuwa ana-chant Tyson na wafuasi wake, angeweza kuki-chant hata kwa kutumia maneno hayo ya Kiswahili, au angeweza pia kutumia kiingereza "God is Greatest". Hii lugha haina uhusiano na Uislam, kwa sababu tuseme kama Tyson angekuwa ni mwarabu halafu kwa dini akawa ni mkristo, bado angetumia maneno hayo kwa lugha ya kiarabu, yakiwa na maana ile ile ya Mungu ni mkubwa. Naomba nitoe tahadhari kwa baadhi yetu wakristo huwa tuna ufahamu mdogo ambao wakati mwingine huwa unatupelekea kuhusisha baadhi ya maneno ya kiarabu na Uislamu. Neno kwa mfano Salaam Aleikhum, si salamu ya waislamu, ni salamu ya kila mtu inayomaanisha Amani iwe nawe.
Still, mimi napendelea zaidi kushauri kuwa kama wewe ni muislamu, u-concentrate zaidi na mambo ya Kiislamu, na kama wewe ni Mkrsito vivyo hivyo. Hata hivyo tushirikishane zaidi mambo mema yaliyopo kwenye dini zetu hizi mbili, badala ya kuangalia tofauti zetu zaidi. Kwenye mgogoro wa uchinjaji nyama kwa mfano, aliwahi kuibuka Mzee wa Upako kwenye media akakemea sana hali hii, na kikubwa zaidi alichosema ni kwamba DINI HIZI MBILI DUNIANI, UISLAMU NA UKRISTO ZINASHAHIBIANA KWA KARIBU SANA KWENYE MAUDHUI YAKE NDANI YA MAANDIKO MATAKATIFU YA KILA MOJAWAPO YA DINI HIZI.
Zaidi kwa upande wangu mimi huwa ninaona UISLAMU ni Dini ambayo, inazidi ku-cement zaidi juu ya uwepo wa Yesu, kwa sababu Qurani pia inakiri uwepo wake. Tungekuwa peke yetu wakristo tu na pakawa hapana dini nyingine yenye kutambua uwepo wa Yesu, possibly wangekuwa wanajitokeza watu na kuhoji kuwa pengine Yesu hakuwepo na ingekuwa ni ngumu kidogo, kuliko ilivyo sasa, kuwapa majibu ya kuwaridhisha juu ya uwepo wake. Lakini kwa sasa hivi mtu akibisha kuhusu uwepo wa Yesu, unachotakiwa kufanya ni kumtuma tu aende msikitini akawaulize waumini wa Kiislamu au Mashehe halafu watampatia majibu. Unaona sasa Uislamu ulivyo msaada kwa Ukristo? Tena msaada mkubwa mno kwa sababu kitu kikubwa kabisa ambacho mwanadamu anatakiwa akifahamu ili aweze kuwa Mkristo, ni uwepo wa Kristo, yaani Yesu!