Sababu za msingi zinazopelekea 'afande' wa ulawiti asikamatwe ni hizi?

Sababu za msingi zinazopelekea 'afande' wa ulawiti asikamatwe ni hizi?

Naingia kwenye mada moja kwa moja na kwa ufupi bila kuwachosha. Wiki hii tumeshuhudia vijana 4 kati ya 6 waliofanya uhalifu wa kumlawiti binti wa Yombo Dovya wakifikishwa mbele za Pontio Pilato na kusomewa mashtaka, ijapokuwa walikana kuhusika na kitendo hicho kibaya.

Jambo la kushangaza na ambalo watanzania wengi wanashindwa kupata majibu ni kwanini 'afande' aliyewatuma wale wahuni (na ambaye alisikika akiombwa msamaha na binti aliyekuwa akibakwa na kulawitiwa mubashara) hakamatwi? Swali la pili ni je, wale watuhumiwa 2 wa ulawiti waliobaki ni akina nani na kwanini hawakamatwi? Je, wana uhusiano wowote na huyo afande asiyekamatika? Hiki ndicho kitendawili ambacho watanzania wangependa kupata majibu yake.

Kabla ya kutoa majibu na kueleza kwanini afande hakamatiki, naomba nirejee kesi 2 zinazofanana na hii ya afande zilizowahi kufikishwa mahakamani na kugonga mwamba.

Kesi ya kwanza ni ile ya aliyekuwa kamanda wa upelelezi wa Dar es Salaam, ndugu Abdallah Zombe ambaye aliwatuma askari polisi kuwaua wafanyabiashara wa madini na kuwapora mamilioni ya fedha. Kwa ufupi, kesi ilipotinga mahakamani, wale askari waliotumwa kuua walijitetea kuwa walifanya mauaji yale kwa kutii amri ya mkubwa wao wa kazi, ndugu Zombe. Baada ya kesi kuunguruma kwa muda mrefu, huku wananchi wakidhani Zombe hachomoki kwenye kesi ile, hatimaye aliachiwa huru. Wale askari waliohusika na mchakato wa mauaji wakahuhumiwa vifungo vya maisha na kunyongwa. Lakini baadaye askari wale walikata rufaa na baadhi yao kufanikiwa kujichomoa. Aliyekutwa na hatia ni mmoja wao anayeitwa Bageni, ambaye alihukumiwa kunyongwa hadi kufa.

Katika kesi hii kuna facts mbili za kisheria zilizotumika. Fact ya kwanza ni ile ya mtu mzima mwenye akili timamu kutumwa na mtu mwingine kutekeleza uhalifu. Sheria haimhukumu aliyetuma bali humhukumu mtumwaji, hata kama mtumaji anajulikana na yeye mwenyewe kukiri kuwa kweli aliwatuma. Ndio maana Zombe aliachiwa huru bila shuruti.

Fact ya pili katika kesi hii ni uhusika wa mtu binafsi katika kutenda uhalifu. Baadhi ya askari waliachiwa huru kwa kuwa hawakuhusika kuwapiga risasi wafanyabiashara. Aliyehusika kufyatua risasi na kuua ni mmoja tu, naye ni Bageni. Ndio maana askari wengine waliachiwa huru, akahukumiwa Bageni tu.

Turejee kwenye kesi ya pili iliyomhusu mke wa Bilionea Msuya kuwatuma watu kumuua wifi yake (mdogo wake bilionea Msuya). Mahakamani ilithibitika kweli mke wa bilionea Msuya aliwatuma watu kufanya uhalifu. Na pia kisu kilichotumika kufanya mauaji kilipatikana na alama za vidole za wahalifu. Lakini mahakama ilitumia busara za kisheria kuwaachia huru watuhimiwa wote, akiwemo mke wa Msuya. Kwanini? Kwa sababu mtumaji hana kosa kisheria. Pia hata kama fingerprints za wahalifu zilionekana kwenye kisu, hakuna mtu mwenye uhakika kama kweli wao ndio waliua. Umeona eeh?

Sasa turejee kwenye hoja yetu ya msingi. Kuna baadhi ya mitandao ya kijamii (sio JF) imemtaja na kumuonesha hadharani afande aliyewatuma wale wafiraji kumdhulumu binti wa watu haki yake ya msingi. Pia haiwezekani binti aliyedhulumiwa amuombe afande msamaha hadharani halafu polisi wasimuombe awapeleke nyumbani kwa afande ili wamkamate. Haiwezekani.

Ni wazi kwamba afande anajulikana isipokuwa hata kama atakamatwa hatakuwa na kesi ya kujibu, kwa kuzingatia mfano wa kesi mbili nilizozitaja hapo juu ambazo watumaji waliachiwa huru bila shuruti. Kwa hiyo, polisi wanaona hata kama wakiamua kumpeleka afande mahakamani wataambulia patupu. Illmradi wahalifu wamekamatwa, hakuna haja tena ya kusumbuka na afande kwa kuwa hata akipelekwa mahakamani, hana kesi ya kujibu.

Sheria inatambua kwamba mtu mzima unapotumwa kutenda uhalifu nawe ukakubali kufanya hivyo, sheria itakuangukia wewe uliyetenda uhalifu na wala sio mtu aliyekutuma. Kwa hiyo, watanzania, hasa wale msiojua sheria, tulizeni mumkari na muendelee kuwa watulivu wakati wabakaji na wafiraji waliohusika kumdhalilisha binti wa Yombo Dovya wakishughulikiwa kwa mujibu wa sheria.

Nawasilisha.
Umetuingiza chaka mkuu.

Sheria inamhukumu hata mtu aliyeshiriki tu kupanga njama za uhalifu tena anaweza kuwa Principal offender ama accessory before/after the facts.

Kwasababu mfumo wa kisheria wa Tanzania unafuata legislation/statutes na common law basi under common law mtu aliyeshiriki kupanga njama za uhalifu anaweza kuwa Principal offender in the first degree, or Principal offender in the second degree ama accessory before or after the fact kutegemeana na role played in the commission of the offence.

Kwa ufupi afande aliyewatuma naye ni mhalifu kwa mujibu wa sheria mkuu.
 
Naingia kwenye mada moja kwa moja na kwa ufupi bila kuwachosha. Wiki hii tumeshuhudia vijana 4 kati ya 6 waliofanya uhalifu wa kumlawiti binti wa Yombo Dovya wakifikishwa mbele za Pontio Pilato na kusomewa mashtaka, ijapokuwa walikana kuhusika na kitendo hicho kibaya.

Jambo la kushangaza na ambalo watanzania wengi wanashindwa kupata majibu ni kwanini 'afande' aliyewatuma wale wahuni (na ambaye alisikika akiombwa msamaha na binti aliyekuwa akibakwa na kulawitiwa mubashara) hakamatwi? Swali la pili ni je, wale watuhumiwa 2 wa ulawiti waliobaki ni akina nani na kwanini hawakamatwi? Je, wana uhusiano wowote na huyo afande asiyekamatika? Hiki ndicho kitendawili ambacho watanzania wangependa kupata majibu yake.

Kabla ya kutoa majibu na kueleza kwanini afande hakamatiki, naomba nirejee kesi 2 zinazofanana na hii ya afande zilizowahi kufikishwa mahakamani na kugonga mwamba.

Kesi ya kwanza ni ile ya aliyekuwa kamanda wa upelelezi wa Dar es Salaam, ndugu Abdallah Zombe ambaye aliwatuma askari polisi kuwaua wafanyabiashara wa madini na kuwapora mamilioni ya fedha. Kwa ufupi, kesi ilipotinga mahakamani, wale askari waliotumwa kuua walijitetea kuwa walifanya mauaji yale kwa kutii amri ya mkubwa wao wa kazi, ndugu Zombe. Baada ya kesi kuunguruma kwa muda mrefu, huku wananchi wakidhani Zombe hachomoki kwenye kesi ile, hatimaye aliachiwa huru. Wale askari waliohusika na mchakato wa mauaji wakahuhumiwa vifungo vya maisha na kunyongwa. Lakini baadaye askari wale walikata rufaa na baadhi yao kufanikiwa kujichomoa. Aliyekutwa na hatia ni mmoja wao anayeitwa Bageni, ambaye alihukumiwa kunyongwa hadi kufa.

Katika kesi hii kuna facts mbili za kisheria zilizotumika. Fact ya kwanza ni ile ya mtu mzima mwenye akili timamu kutumwa na mtu mwingine kutekeleza uhalifu. Sheria haimhukumu aliyetuma bali humhukumu mtumwaji, hata kama mtumaji anajulikana na yeye mwenyewe kukiri kuwa kweli aliwatuma. Ndio maana Zombe aliachiwa huru bila shuruti.

Fact ya pili katika kesi hii ni uhusika wa mtu binafsi katika kutenda uhalifu. Baadhi ya askari waliachiwa huru kwa kuwa hawakuhusika kuwapiga risasi wafanyabiashara. Aliyehusika kufyatua risasi na kuua ni mmoja tu, naye ni Bageni. Ndio maana askari wengine waliachiwa huru, akahukumiwa Bageni tu.

Turejee kwenye kesi ya pili iliyomhusu mke wa Bilionea Msuya kuwatuma watu kumuua wifi yake (mdogo wake bilionea Msuya). Mahakamani ilithibitika kweli mke wa bilionea Msuya aliwatuma watu kufanya uhalifu. Na pia kisu kilichotumika kufanya mauaji kilipatikana na alama za vidole za wahalifu. Lakini mahakama ilitumia busara za kisheria kuwaachia huru watuhimiwa wote, akiwemo mke wa Msuya. Kwanini? Kwa sababu mtumaji hana kosa kisheria. Pia hata kama fingerprints za wahalifu zilionekana kwenye kisu, hakuna mtu mwenye uhakika kama kweli wao ndio waliua. Umeona eeh?

Sasa turejee kwenye hoja yetu ya msingi. Kuna baadhi ya mitandao ya kijamii (sio JF) imemtaja na kumuonesha hadharani afande aliyewatuma wale wafiraji kumdhulumu binti wa watu haki yake ya msingi. Pia haiwezekani binti aliyedhulumiwa amuombe afande msamaha hadharani halafu polisi wasimuombe awapeleke nyumbani kwa afande ili wamkamate. Haiwezekani.

Ni wazi kwamba afande anajulikana isipokuwa hata kama atakamatwa hatakuwa na kesi ya kujibu, kwa kuzingatia mfano wa kesi mbili nilizozitaja hapo juu ambazo watumaji waliachiwa huru bila shuruti. Kwa hiyo, polisi wanaona hata kama wakiamua kumpeleka afande mahakamani wataambulia patupu. Illmradi wahalifu wamekamatwa, hakuna haja tena ya kusumbuka na afande kwa kuwa hata akipelekwa mahakamani, hana kesi ya kujibu.

Sheria inatambua kwamba mtu mzima unapotumwa kutenda uhalifu nawe ukakubali kufanya hivyo, sheria itakuangukia wewe uliyetenda uhalifu na wala sio mtu aliyekutuma. Kwa hiyo, watanzania, hasa wale msiojua sheria, tulizeni mumkari na muendelee kuwa watulivu wakati wabakaji na wafiraji waliohusika kumdhalilisha binti wa Yombo Dovya wakishughulikiwa kwa mujibu wa sheria.

Nawasilisha.
Kwa hiyo nikiwalipa watu na kuwatuma waje kukufanyia uhalifu mimi sina kosa pindi wakubainika? 🤔
 
Siyo tu kukosekana kwa ushahidi lakini pia haki lazima izingatiwe unapotamani yule binti aliyefanyiwa ukatili atendewe haki pia usisahau kwamba pia hata hao wengine wanastahili haki tukiendekeza kupeleka watu mahakamani ili wakachomokee huko huku ikijulikana kwamba wanakwenda kuchomoka ni uonevu ni kwanini tunalazimisha kwamba anaye tajwa na Meya mtaafu ndiye muhusika? Je,ni kweli ana mume? Upelelezi wa kesi kama hii hauitaji mihemuko wala chuki binafsi kwa taasisi usiyoipenda kwasababu bado mtazunguka kwenye shamba ileile ya ukiukwaji wa haki za binadamu mfano mzuri RPC aliyenukuliwa kwa kuwekewa maneno ambayo hakuyakusudia imempa usumbufu mkubwa na kama binadamu haki yake haitajadiliwa ila mwandishi wa habari aliyemuhoji ataonekana wa maana huku akiwa ameharibu maisha ya mtu kwaajili ya maslahi binafsi kwa mwamvuli wa kuhabarisha umma.
Kila mwananchi anajichukulia sheria mikononi mwake na kujitwishwa mamlaka ya upelelezi bila kusomea fani hiyo ni sawa na watu kujifanya wanajua kila kitu mpaka kumkosoa DAKTARI aliyesomea na kubobea kwenye fani.
Matarajio ni kukuza mtafaruku katika jamii pia waandishi wa habari watakuwa katika wakati mgumu wa kupata taarifa maana wanautaalamu wa kubadilisha kinachosemwa na kuleta taharuki ili habari iuzwe bila kujali kama italeta athari gani katika jamii.
 
Naingia kwenye mada moja kwa moja na kwa ufupi bila kuwachosha. Wiki hii tumeshuhudia vijana 4 kati ya 6 waliofanya uhalifu wa kumlawiti binti wa Yombo Dovya wakifikishwa mbele za Pontio Pilato na kusomewa mashtaka, ijapokuwa walikana kuhusika na kitendo hicho kibaya.

Jambo la kushangaza na ambalo watanzania wengi wanashindwa kupata majibu ni kwanini 'afande' aliyewatuma wale wahuni (na ambaye alisikika akiombwa msamaha na binti aliyekuwa akibakwa na kulawitiwa mubashara) hakamatwi? Swali la pili ni je, wale watuhumiwa 2 wa ulawiti waliobaki ni akina nani na kwanini hawakamatwi? Je, wana uhusiano wowote na huyo afande asiyekamatika? Hiki ndicho kitendawili ambacho watanzania wangependa kupata majibu yake.

Kabla ya kutoa majibu na kueleza kwanini afande hakamatiki, naomba nirejee kesi 2 zinazofanana na hii ya afande zilizowahi kufikishwa mahakamani na kugonga mwamba.

Kesi ya kwanza ni ile ya aliyekuwa kamanda wa upelelezi wa Dar es Salaam, ndugu Abdallah Zombe ambaye aliwatuma askari polisi kuwaua wafanyabiashara wa madini na kuwapora mamilioni ya fedha. Kwa ufupi, kesi ilipotinga mahakamani, wale askari waliotumwa kuua walijitetea kuwa walifanya mauaji yale kwa kutii amri ya mkubwa wao wa kazi, ndugu Zombe. Baada ya kesi kuunguruma kwa muda mrefu, huku wananchi wakidhani Zombe hachomoki kwenye kesi ile, hatimaye aliachiwa huru. Wale askari waliohusika na mchakato wa mauaji wakahuhumiwa vifungo vya maisha na kunyongwa. Lakini baadaye askari wale walikata rufaa na baadhi yao kufanikiwa kujichomoa. Aliyekutwa na hatia ni mmoja wao anayeitwa Bageni, ambaye alihukumiwa kunyongwa hadi kufa.

Katika kesi hii kuna facts mbili za kisheria zilizotumika. Fact ya kwanza ni ile ya mtu mzima mwenye akili timamu kutumwa na mtu mwingine kutekeleza uhalifu. Sheria haimhukumu aliyetuma bali humhukumu mtumwaji, hata kama mtumaji anajulikana na yeye mwenyewe kukiri kuwa kweli aliwatuma. Ndio maana Zombe aliachiwa huru bila shuruti.

Fact ya pili katika kesi hii ni uhusika wa mtu binafsi katika kutenda uhalifu. Baadhi ya askari waliachiwa huru kwa kuwa hawakuhusika kuwapiga risasi wafanyabiashara. Aliyehusika kufyatua risasi na kuua ni mmoja tu, naye ni Bageni. Ndio maana askari wengine waliachiwa huru, akahukumiwa Bageni tu.

Turejee kwenye kesi ya pili iliyomhusu mke wa Bilionea Msuya kuwatuma watu kumuua wifi yake (mdogo wake bilionea Msuya). Mahakamani ilithibitika kweli mke wa bilionea Msuya aliwatuma watu kufanya uhalifu. Na pia kisu kilichotumika kufanya mauaji kilipatikana na alama za vidole za wahalifu. Lakini mahakama ilitumia busara za kisheria kuwaachia huru watuhimiwa wote, akiwemo mke wa Msuya. Kwanini? Kwa sababu mtumaji hana kosa kisheria. Pia hata kama fingerprints za wahalifu zilionekana kwenye kisu, hakuna mtu mwenye uhakika kama kweli wao ndio waliua. Umeona eeh?

Sasa turejee kwenye hoja yetu ya msingi. Kuna baadhi ya mitandao ya kijamii (sio JF) imemtaja na kumuonesha hadharani afande aliyewatuma wale wafiraji kumdhulumu binti wa watu haki yake ya msingi. Pia haiwezekani binti aliyedhulumiwa amuombe afande msamaha hadharani halafu polisi wasimuombe awapeleke nyumbani kwa afande ili wamkamate. Haiwezekani.

Ni wazi kwamba afande anajulikana isipokuwa hata kama atakamatwa hatakuwa na kesi ya kujibu, kwa kuzingatia mfano wa kesi mbili nilizozitaja hapo juu ambazo watumaji waliachiwa huru bila shuruti. Kwa hiyo, polisi wanaona hata kama wakiamua kumpeleka afande mahakamani wataambulia patupu. Illmradi wahalifu wamekamatwa, hakuna haja tena ya kusumbuka na afande kwa kuwa hata akipelekwa mahakamani, hana kesi ya kujibu.

Sheria inatambua kwamba mtu mzima unapotumwa kutenda uhalifu nawe ukakubali kufanya hivyo, sheria itakuangukia wewe uliyetenda uhalifu na wala sio mtu aliyekutuma. Kwa hiyo, watanzania, hasa wale msiojua sheria, tulizeni mumkari na muendelee kuwa watulivu wakati wabakaji na wafiraji waliohusika kumdhalilisha binti wa Yombo Dovya wakishughulikiwa kwa mujibu wa sheria.

Nawasilisha.
Unaeleza kama tuko kijiwe cha kahawa! Kwa mujibu wa sheria mpangaji na mtekelezaji wote ni wahusika na ikithibitika mahakamani wote watahukumiwa kwa mujibu wa sheria. Mengine ni ukiukwaji wa sheria na hayapaswi kutolewa mfano.
 
Hili ndo nilikuwa nasema watu wanataka watu wapandishwe kizimbani kwa mihemko tu hawajui mahakamani ni ushahidi usio shaka ndo unasimama, kwa hiii kesi kumkuta na hatia huyu mama ni kazi sana maana inabidi ueleze kinaga ubaga chain yake na hao watu na uthibitishe kuwa yeye aliwatuma jambo ambalo si rahisi. Hii dunia ya mitando ni ngumu sana kwenda nayo maana kila mtu ni mtaalam na hisia ni bora zaidi kuliko ukweli
Upuuzi tu, mbona kwenye kuwakamata wapinzani hawatendi kisheria?

Kwenye suala la kukamata polisi wenzao utasikia sheria, kukamata wapinzani hakuna sheria.

Huyo mama angekamatwa tu aonekane.
 
Siyo tu kukosekana kwa ushahidi lakini pia haki lazima izingatiwe unapotamani yule binti aliyefanyiwa ukatili atendewe haki pia usisahau kwamba pia hata hao wengine wanastahili haki tukiendekeza kupeleka watu mahakamani ili wakachomokee huko huku ikijulikana kwamba wanakwenda kuchomoka ni uonevu ni kwanini tunalazimisha kwamba anaye tajwa na Meya mtaafu ndiye muhusika? Je,ni kweli ana mume? Upelelezi wa kesi kama hii hauitaji mihemuko wala chuki binafsi kwa taasisi usiyoipenda kwasababu bado mtazunguka kwenye shamba ileile ya ukiukwaji wa haki za binadamu mfano mzuri RPC aliyenukuliwa kwa kuwekewa maneno ambayo hakuyakusudia imempa usumbufu mkubwa na kama binadamu haki yake haitajadiliwa ila mwandishi wa habari aliyemuhoji ataonekana wa maana huku akiwa ameharibu maisha ya mtu kwaajili ya maslahi binafsi kwa mwamvuli wa kuhabarisha umma.
Kila mwananchi anajichukulia sheria mikononi mwake na kujitwishwa mamlaka ya upelelezi bila kusomea fani hiyo ni sawa na watu kujifanya wanajua kila kitu mpaka kumkosoa DAKTARI aliyesomea na kubobea kwenye fani.
Matarajio ni kukuza mtafaruku katika jamii pia waandishi wa habari watakuwa katika wakati mgumu wa kupata taarifa maana wanautaalamu wa kubadilisha kinachosemwa na kuleta taharuki ili habari iuzwe bila kujali kama italeta athari gani katika jamii.
Upuuzi tu umeandika.
 
Huyo mtu ni mbumbumbu wa sheria, analeta story za kahawani. Kwa mujibu wa sheri kula njama na kutekeleza uhalifu yote ni makosa.
Yah! Iyo topiki nimeikumbuka maana ilikua assignment ya group nikaachiwa nifanye mwenyewe...
Labda mleta mada ndio afande mwenyewe anajitetea😆..

Conspiracy occurs when two or more persons agree to commit a crime-an essential feature for committing organized crime. One purpose of the conspiracy offence is to extend liability "backwards" by criminalizing the planning (or agreement) stage of a criminal offence.
 
Pia usisahau upepelelezi dhidi ya kupigwa risasi Lissu ulisumbua sababu dereva hayupo hivyo kama afande hakutajwa kwa jina ni ngumu mnooo maana ni kama hayupo ila yupo ila kama haonekani. Najaribu kuwaza kiafande afande kulingana na akili ulizoonyesha hapa.
 
Umetuingiza chaka mkuu.

Sheria inamhukumu hata mtu aliyeshiriki tu kupanga njama za uhalifu tena anaweza kuwa Principal offender ama accessory before/after the facts.

Kwasababu mfumo wa kisheria wa Tanzania unafuata legislation/statutes na common law basi under common law mtu aliyeshiriki kupanga njama za uhalifu anaweza kuwa Principal offender in the first degree, or Principal offender in the second degree ama accessory before or after the fact kutegemeana na role played in the commission of the offence.

Kwa ufupi afande aliyewatuma naye ni mhalifu kwa mujibu wa sheria mkuu.
Mkuu usiwe buh lawyer. Unafikiri kwanini Zombe na mke wa Msuya au wahalifu waliotumwa na mke wa Msuya (na fingerprints zao zikapatikana kwenye visu vilivyotekeleza mauaji) hawakutiwa hatiani?
 
Mtoa mada pengine umesahau kipindi kesi ya zombe kuna mashahidi muhimu waliuawa ili kuficha ushahidi, bila baadhi ya mashahidi kufa ni vigumu sana kuchomoka ndiyo maana watu tunataka huyo afande apande kizimbani haijalishi atachomoka au anafungwa.
Hata huyo zombe hakuishi Kwa Amani Hadi anakufa Kwa kifupi ni kama alikuwa jela tu
 
Back
Top Bottom