Sababu za msingi zinazopelekea 'afande' wa ulawiti asikamatwe ni hizi?

Sababu za msingi zinazopelekea 'afande' wa ulawiti asikamatwe ni hizi?

Mtoa mada ni kilaza sana hapo hajui kuna makosa ya kula njama na kufadhili uhalifu na haikuwa najukumu yake ya kazi
Kama ni hivyo unavyodhani, kwanini Zombie na mke wa Msuya hawakutiwa hatiani? Kama hujui jambo ni bora kukaa kimya kuliko kuonyesha ukilaza wako hadharani.
 
Hata mbinguni utahukumiwa kwa matendo sio maneno
Na ndio maana serikali yetu tukufu iliona hilo na kutunga sheria zisizohukumu watumaji bali zinazowahumu waliotenda. Sheria zetu ni za kibiblia zaidi
 
Naingia kwenye mada moja kwa moja na kwa ufupi bila kuwachosha. Wiki hii tumeshuhudia vijana 4 kati ya 6 waliofanya uhalifu wa kumlawiti binti wa Yombo Dovya wakifikishwa mbele za Pontio Pilato na kusomewa mashtaka, ijapokuwa walikana kuhusika na kitendo hicho kibaya.
View attachment 3074754
Watuhumiwa 4 waliombaka na kumlawiti binti wa Yombo Dovya wakiwa mahakamani

Jambo la kushangaza na ambalo watanzania wengi wanashindwa kupata majibu ni kwanini 'afande' aliyewatuma wale wahuni (na ambaye alisikika akiombwa msamaha na binti aliyekuwa akibakwa na kulawitiwa mubashara) hakamatwi? Swali la pili ni je, wale watuhumiwa 2 wa ulawiti waliobaki ni akina nani na kwanini hawakamatwi? Je, wana uhusiano wowote na huyo afande asiyekamatika? Hiki ndicho kitendawili ambacho watanzania wangependa kupata majibu yake.

Kabla ya kutoa majibu na kueleza kwanini afande hakamatiki, naomba nirejee kesi 2 zinazofanana na hii ya afande zilizowahi kufikishwa mahakamani na kugonga mwamba.

Kesi ya kwanza ni ile ya aliyekuwa kamanda wa upelelezi wa Dar es Salaam, ndugu Abdallah Zombe ambaye aliwatuma askari polisi kuwaua wafanyabiashara wa madini na kuwapora mamilioni ya fedha. Kwa ufupi, kesi ilipotinga mahakamani, wale askari waliotumwa kuua walijitetea kuwa walifanya mauaji yale kwa kutii amri ya mkubwa wao wa kazi, ndugu Zombe. Baada ya kesi kuunguruma kwa muda mrefu, huku wananchi wakidhani Zombe hachomoki kwenye kesi ile, hatimaye aliachiwa huru. Wale askari waliohusika na mchakato wa mauaji wakahuhumiwa vifungo vya maisha na kunyongwa. Lakini baadaye askari wale walikata rufaa na baadhi yao kufanikiwa kujichomoa. Aliyekutwa na hatia ni mmoja wao anayeitwa Bageni, ambaye alihukumiwa kunyongwa hadi kufa.

Katika kesi hii kuna facts mbili za kisheria zilizotumika. Fact ya kwanza ni ile ya mtu mzima mwenye akili timamu kutumwa na mtu mwingine kutekeleza uhalifu. Sheria haimhukumu aliyetuma bali humhukumu mtumwaji, hata kama mtumaji anajulikana na yeye mwenyewe kukiri kuwa kweli aliwatuma. Ndio maana Zombe aliachiwa huru bila shuruti.

Fact ya pili katika kesi hii ni uhusika wa mtu binafsi katika kutenda uhalifu. Baadhi ya askari waliachiwa huru kwa kuwa hawakuhusika kuwapiga risasi wafanyabiashara. Aliyehusika kufyatua risasi na kuua ni mmoja tu, naye ni Bageni. Ndio maana askari wengine waliachiwa huru, akahukumiwa Bageni tu.

Turejee kwenye kesi ya pili iliyomhusu mke wa Bilionea Msuya kuwatuma watu kumuua wifi yake (mdogo wake bilionea Msuya). Mahakamani ilithibitika kweli mke wa bilionea Msuya aliwatuma watu kufanya uhalifu. Na pia kisu kilichotumika kufanya mauaji kilipatikana na alama za vidole za wahalifu. Lakini mahakama ilitumia busara za kisheria kuwaachia huru watuhimiwa wote, akiwemo mke wa Msuya. Kwanini? Kwa sababu mtumaji hana kosa kisheria. Pia hata kama fingerprints za wahalifu zilionekana kwenye kisu, hakuna mtu mwenye uhakika kama kweli wao ndio waliua. Umeona eeh?

Sasa turejee kwenye hoja yetu ya msingi. Kuna baadhi ya mitandao ya kijamii (sio JF) imemtaja na kumuonesha hadharani afande aliyewatuma wale wafiraji kumdhulumu binti wa watu haki yake ya msingi. Pia haiwezekani binti aliyedhulumiwa amuombe afande msamaha hadharani halafu polisi wasimuombe awapeleke nyumbani kwa afande ili wamkamate. Haiwezekani.

Ni wazi kwamba afande anajulikana isipokuwa hata kama atakamatwa hatakuwa na kesi ya kujibu, kwa kuzingatia mfano wa kesi mbili nilizozitaja hapo juu ambazo watumaji waliachiwa huru bila shuruti. Kwa hiyo, polisi wanaona hata kama wakiamua kumpeleka afande mahakamani wataambulia patupu. Illmradi wahalifu wamekamatwa, hakuna haja tena ya kusumbuka na afande kwa kuwa hata akipelekwa mahakamani, hana kesi ya kujibu.

Sheria inatambua kwamba mtu mzima unapotumwa kutenda uhalifu nawe ukakubali kufanya hivyo, sheria itakuangukia wewe uliyetenda uhalifu na wala sio mtu aliyekutuma. Kwa hiyo, watanzania, hasa wale msiojua sheria, tulizeni mumkari na muendelee kuwa watulivu wakati wabakaji na wafiraji waliohusika kumdhalilisha binti wa Yombo Dovya wakishughulikiwa kwa mujibu wa sheria.

Nawasilisha.
Kwenye kamusi ya KISWAHILI ya TUKI...neno AFANDE maana yake ni MFIRAJI
 
Majamaa walikuwa wana tamka afande kuna ushahidi gani kama ni afande wa jeshi
Maana mtaani watu wanaitana makamanda viongozi wakuu etc
Binti aliyelawitiwi atatoa ushahidi. Lakini hata afande akipelekwa mahakamani hafungwi.
 
Kama ni hivyo unavyodhani, kwanini Zombie na mke wa Msuya hawakutiwa hatiani? Kama hujui jambo ni bora kukaa kimya kuliko kuonyesha ukilaza wako hadharani.
RUSHWA ADUI WA HAKI.
Sio kila anayeitwa hakimu au jaji anatenda haki.
hao ndo wanaongoza kwa kula rushwa.sioni ajabu hao uliowataja kuachiwa HURU.maana wana mikono mirefu.
 
Mimi ningependa huyo afande naye aunganishwe kwenye kesi hii kama kuchomoka akachomokee Mahakamani, sababu yangu kubwa ni kutaka umma umfahamamu kuwa ni yeye aliyefadhili uharamia uliofanyika ili iwe pia ni fundisho kwake.
Exactly hv hakuna sheria sheria inayosema ukipanga uhalifu au kula njama ya uhakifu kuna hukumu manake naonaga hataa kiwanja uiwa facilatator unapatwa na hukumu au afrka ni Afrika
 
Hata mbinguni utahukumiwa kwa matendo sio maneno
Mbinguni kila mtu atasimama mbele za haki. Sheria zote za hapa duniani zitatupwa; zitatumika sheria za Mungu. Hapa ndipo kila mtu atakapolia na kusaga meno.
 
Kesi hii ya ulawiti imechukua sura mpya baada ya ndugu wa Afande kumtetea kuwa Afande ni mjane wa muda mrefu, hana mume na ushahidi wa kifo cha mumewe wanao. Katika hali kama hii, naona tayari binti wa Yombo Dovya ameishakosa haki yake kama nilivyobainisha kwenye uzi huu. Inauma sana.

Sasa sababu za huyo Afande kutoa adhabu Kwa Binti wa Dovya Yombo ni nini , ni mpaka ujue Hilo ndio utakuwa katika nafasi nzuri ya kuiongelea hilo, kuna weza kuwepo na dhana ya Binti wa Dovya Yombo kuwa ni kisababishi au kichocheo cha kifo cha mume au ana urafiki na rafiki wa Afande
 
Sasa sababu za huyo Afande kutoa adhabu Kwa Binti wa Dovya Yombo ni nini , ni mpaka ujue Hilo ndio utakuwa katika nafasi nzuri ya kuiongelea hilo, kuna weza kuwepo na dhana ya Binti wa Dovya Yombo kuwa ni kisababishi au kichocheo cha kifo cha mume au ana urafiki na rafiki wa Afande
Hapa ndipo patakuwa pagumu kuthibitisha mahakamani lakini kwa kuwa binti wa Yombo bado yupo, nadhani akina Madeleka watapangua hizo hoja misa ya kwanza tu.
 
Back
Top Bottom