Sababu za Yanga kumuajili Abdihamid Moalin kama meneja wa ufundi huenda zikawa hizi. Kuna vipaji vitaibuliwa msimu huu

Sababu za Yanga kumuajili Abdihamid Moalin kama meneja wa ufundi huenda zikawa hizi. Kuna vipaji vitaibuliwa msimu huu

OMOYOGWANE

JF-Expert Member
Joined
Dec 30, 2016
Posts
4,701
Reaction score
11,920
Wakuu mpo!

OMOYOGWANE sipoi, wengi wameshangaa sana kuona kocha wa KMC anaacha kazi na kujiunga Yanga katika nafasi ambayo siyo ya ukocha mkuu wala kocha msaidizi ila kapewa kazi ya kuwa mkurugenzi wa Ufundi.

MAJUKUMU YA MKURUGENZI WA UFUNDI NI YAPI?

Mkurugenzi wa ufundi kazi yake ni kuandaa programu maalum kwaajili ya kuimarisha kiwango cha mchezaji mmoja mmoja ktk timu mfano Mzize anapoteza nafasi nyingi za wazi unakuta kauvuka msitu wa mabeki kisha kabaki yeye na kipa ktk kupiga mpira kapiga vibaya kapaisha usawa wa kimo cha mnazi, sasa kazi ya mkurugenzi wa ufundi ni kuandaa programu maalum kwa mzize ya kumfua na kumpa mbinu za kiufundi ili aweze kufunga kwa kila nafasi atakayo pata

Kazi ya mkurugenzi wa ufundi ni kuandaa program maalum ktk tumu ya vijana ili kuibua vipaji

Kulishauri benchi la ufundi (kocha mkuu na kocha msaidizi)

Kusimamia nidhamu ya mchezaji mmoja mmoja kwa kumpa elimu ya kisaikolojia ili kuyamudu mazingira ya ndani na nje ya uwanja mfano kejeli mitandaoni

Kufanya vetting ktk usajili wa wachezaji wapya wanao endana na falsafa ya tumu

KWANINI YANGA WAMMEMUAJILI MOALIN?
Moalin amekuwa kiwanda cha kuibua vipaji vingi kila anapopita kuanzia AZAM mpaka KMC, kila msimu KMC inaibua vipaji vipya nadhani sihitaji kutoa maelezo mengi si mnamuona Awesu, Lanso, Salim na wengine wengi

Falsafa ya mpira anaofundisha ndio falsafa ya Yanga, soka safi pasi nyingi hamna butua butua. Si mnaiona KMC mpira inaocheza.

Anajicho la kuibua vipaji

Tutegemee vipaji vingi msimu hu kutoka YANGA SC

Viva Moalin viva Yanga

Nawasilisha.
 
Umesema Awesu Awesu? kumbe kabla hajawa Azam na KMC alikua Madini fc?
Ibrahim Lanso ni zao za ZPL zanzibar premier league
Chogo wee
 
Umesema Awesu Awesu? kumbe kabla hajawa Azam na KMC alikua Madini fc?
Ibrahim Lanso ni zao za ZPL zanzibar premier league
Chogo wee
Nimesema kazi ya moalin ni kumfua mchezaji mmoja mmoja na kuubua vipaji nikatoa na mfano wa mzize hivi unajua kusoma na kuelewa kweli?

Kutoka Madini wala ZPL sio ishu ishu ni kiwango mpaka mchezaji aobekane
 
Ngoja tuone
Lakini lanso alishacheza muda tu sana zanzibar kule hata tukamuona mapinduzi mara kama 4 hivi

Awesu labda useme kuwa moalim alimfua zaidi ila jamaa kitambo sana anacheza
 
Huyo alikuja kama kocha msaidizi, baada ya mzungu kumgomea kwamba hamuhitaji ndio wakabadili gia angani. Kwa hiyo wanahitaji muda kumpa majukumu halisi badala ya sarakasi
 
Huyo alikuja kama kocha msaidizi, baada ya mzungu kumgomea kwamba hamuhitaji ndio wakabadili gia angani. Kwa hiyo wanahitaji muda kumpa majukumu halisi badala ya sarakasi
Aaahh Mwasibu CPA feki OKW BOBAN SUNZU ovyo kabisa umerudi tena huku salama lakini?
 
Walimleta kocha masaidizi huyo dili likabuma.
By the way kwa mazingira ya mpira wa Tanzania na Africa kwa ujumla hicho cheo ni sawa na cheo cha makamu wa Rais tu hana meno tofauti na ulaya
 
Ngoja tuone
Lakini lanso alishacheza muda tu sana zanzibar kule hata tukamuona mapinduzi mara kama 4 hivi

Awesu labda useme kuwa moalim alimfua zaidi ila jamaa kitambo sana anacheza
Mkuu sasa hivi unamuonaje mzize?

Unamuonaje KIBWANA yule akiyekuwa anacheza benchi na huyu anayekipiga sasa?


Unamuonaje Boka? Kaanza kubadirika

Kuna vipaji vingine vyaja
 
Mkuu sasa hivi unamuonaje mzize?

Unamuonaje KIBWANA yule akiyekuwa anacheza benchi na huyu anayekipiga sasa?


Unamuonaje Boka? Kaanza kubadirika

Kuna vipaji vingine vyaja
I see that you are making sense.
 
Mkuu sasa hivi unamuonaje mzize?

Unamuonaje KIBWANA yule akiyekuwa anacheza benchi na huyu anayekipiga sasa?


Unamuonaje Boka? Kaanza kubadirika

Kuna vipaji vingine vyaja
mkuu
kuna muda unajiuliza kwanini gamondi hakupenda kumtumia kabisa kibwana hata katika zile mechi ndogo?
leo saed anamuamini tena katika mechi ngumu kama jana, na kijana hajatuangusha kabisa amefanya kabwiti akaomba maji

boka ana shida ya kupiga tackling sana kwenye boksi hilo tu ila uwezo wa kupanda anaoa mkubwa sana sana
 
Back
Top Bottom