Mkuu
MOSSAD II nadhani unachojaribu kuwanyooshea kidole wasabato hakina mantiki yoyote. Makosa au madhambi ya mtu mmoja ama watu wachache hayawezi kuhalalisha kuichafua jumuiya nzima ama taasisi nzima.
Kwa mfano zimekuwepo kesi nyingi za mapadri kuwalawiti waumini wao, tena wengine wanawaingilia watoto wa kiume, Je hapo tuseme kwamba hayoi ndiyo mafundisho ya kanisa katoliki? Kumekuwa na matukio ya mapadri wa kikatoliki kuzaa na wanawake wengine hata wengine wanazini na wake za watu, je hayo ndiyo mafundisho ya kanisa katoliki?La hasha.
Pia kumekuwa na matukio ya wachungaji na maaskofu wa makanisa ya kiprotestant na kilokole (wenyewe wanajiita makanisa ya kiroho) ambapo wanazini na waumini wao, wengine wanawalawiti na kuwafanyia vitendo vingi ambavyo ni kinyume na mafundisho yao na mafundisho ya biblia, je hapo tuyalaumu makanisa au madhehebu yao kwamba hayo ndio mafundisho wanayowapatia waumini wao au wachungaji na maaskofu wao? hasha.
Sitaki kuzungumzia matendo maovu yanayofanywa na viongozi wa dini nyengine zisizo za kikristo kwakuwa hawana mafungamano katika hoja hii kwakuwa naona wakristo wa madhehebu mengine ndio mmesimama kidete kuwashambulia wasabato kwa sababu ambazo mnazifahamu ninyi wenyewe, ingawa kwa mtazamo wa haraka haraka inaonyesha ni chuki ya aina gani mliyonayo dhidi ya wasabato.
Kwa mifano hiyo michache nataka kujenga hoja yangu kwamba waumini wa kanisa la SDA ni wanadamu kama walivyo waumini wa madhehebu mengine ya kikristo kama Wakatoliki, KKKT, Moravian, Menonite, TAG, EAGT, FGBF, Jeshi la Wokovu, AIC pamoja na madhehebu mengine yote ya kikristo.
Waumini wa madhehebu haya yote wamekuwa wakifanya mambo ambayo ni kinyume na mafundisho yao ya madhehebu yao lakini pia wamekuwa wakifanya matendo ambayo ni kinyume na mafundisho ya biblia. Sasa utakuwa ni upofu wa akili kama unajielekeza kuwakashifu wasabato wote kwakutumia watu wachache ambao umewaona wakifanya makosa basi unawajumuisha wasabato wote.
Kila mmoja ana historia ya kuishi na watu wa dini nyengine tofuti na yake ama kuishi na watu wa madhehebu mengine ya kikristo tofauti na dhehebu lake na huko kote tunashuhudia madudu mengi yanayofanyika kinyume na maandiko matakatifu. Wengine kama ulivyo wewe tunao mchanganyiko wa ndugu zetu wanaoabudu katika madhehebu tofauti pamoja na kuwa familia moja.
Mimi katika familia yangu yupo wasabato, wapo wakatoliki, wapo walokole(TAG & EAGT), wapo AIC, wapo KKKT, wapo jeshi la wokovu, wapo Ufufuo na Uzima na pia wapo waislamu. Kwa mchanganyiko huu tuna uzoefu na ushuhuda wa kutosha juu ya mienendo na matendo ya kila mmoja kwahiyo hatuoni sababu ya kunyosheana vidole kwa sababu tu ya imani ya mmoja ambayo wewe huiamini ama hudhani kuwa ni sahihi.
Kwahiyo tuache kukashifiana na kutukanana kwakuwa hayo si mafundisho ya biblia takatifu, na kama kweli ungekuwa unaisoma kwa unyenyekevu na kwa uwezo wa Roho Mtakatifu Biblia bila shaka ungekuwa na staha ya Kristo unapojibishana na wenzako.