Father of Chemistry
JF-Expert Member
- May 21, 2021
- 401
- 1,282
Mawakili wa upande wa utetezi kwenye kesi namba mbili ya mwaka 2022, inayomkabili aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya na wenzake wanne wameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi kuwa hali ya Sabaya ni mbaya baada ya kufanyiwa upasuaji mkubwa wa kichwa Julai 27,2022.
Sabaya alifikishwa Mahakamani hapo leo huku kichwa chake kikiwa na bandeji huku mkononi akiwa na kifaa cha kuchomekea dripu.
Wakili upande wa mashtaka Sabitina Mcharo aliieleza Mahakama hiyo kuwa upelelezi bado haujakamilika na kwamba wanasubiri kibali kutoka kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali cha kuipa uwezo Mahakama hiyo kuendelea kuisikiliza kesi hiyo.
Wakili upande wa mashtaka Sabitina Mcharo aliieleza mahakama hiyo kuwa upelelezi bado haujakamilika na kwamba wanasubiri kibali kutoka kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali cha kuipa uwezo mahakama hiyo kuendelea kuisikiliza kesi hiyo.
Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo Elibariki Philly ameahirisha kesi hiyo hadi Agosti 12,2022.
source
#MillardAyoMAHAKAMANI
Sabaya alifikishwa Mahakamani hapo leo huku kichwa chake kikiwa na bandeji huku mkononi akiwa na kifaa cha kuchomekea dripu.
Wakili upande wa mashtaka Sabitina Mcharo aliieleza Mahakama hiyo kuwa upelelezi bado haujakamilika na kwamba wanasubiri kibali kutoka kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali cha kuipa uwezo Mahakama hiyo kuendelea kuisikiliza kesi hiyo.
Wakili upande wa mashtaka Sabitina Mcharo aliieleza mahakama hiyo kuwa upelelezi bado haujakamilika na kwamba wanasubiri kibali kutoka kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali cha kuipa uwezo mahakama hiyo kuendelea kuisikiliza kesi hiyo.
Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo Elibariki Philly ameahirisha kesi hiyo hadi Agosti 12,2022.
source
#MillardAyoMAHAKAMANI