Sabaya amekiri makosa yote yaliyokuwa yanamkabili na Uhujumu Uchumi. Walionyanyaswa na Sabaya waende wapi Kushitaki?

Kukiri makosa na kuhukumiwa kwa Sabaya kwaweza kufungua milango ya madai dhidi ya Sabaya na mwajiri wake (serikali) kwa walioathirika.
Lazima wananchi wanapopata tatizo watazame mbali kutafuta recovery.
Serikali lazima ihusishwe ili kupata fidia toshelezi kwa kuwa Sabaya binafsi atakosa uwezo wa kulipa na pia serikali inahusika kwenye makosa kwani ilimuajiri.
Wanasheria wakae mkao mzuri wa kuwasaidia waathirika, kujenga utamaduni wa kuheshimu sheria katika uongozi na pia kutoa fundisho kwa watu wanapopata madaraka wayatumie kwa kutoa haki kwa busara.
 
Wite waliofanyiwa ushetani na Sabaya, wafungue kesi za madai dhidi yake na dhidi ya Serikali ambayo ilikuwa mwajiri wake.Waombe kulipwa fidia angalao ya bilioni 2 kila mmoja kwa kusababishiwa ulemavu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…