Sad news: Taifa kuongozwa na katiba ya ccm kuanzia 2015

Sad news: Taifa kuongozwa na katiba ya ccm kuanzia 2015

Hemed Mzee Hemed

Senior Member
Joined
Jun 26, 2013
Posts
186
Reaction score
41
Chama Cha Mapinduzi kimedhihirisha mikakati yake haramu ya kuhakikisha katiba mpya itabeba MATAKWA yote ya NEC.. Jioni ya leo kuanzia saa 9-11 jioni kulikuwa na kikao kikuu cha wilaya/halmashauri ya kinondoni kujadili mapendekezo ya rasimu ya katiba mpya.. Kikao hicho kimefanyika Mwananyamala ukumbi wa CCM. Mgeni rasmi alikuwa NAPE Nnauye - Katibu wa itikadi na uenezi.

Wahusika katika kikao hicho cha halmashauri ya wilaya ya kinondoni walikuwa ni viongozi wote wa CCM ktk wilaya ya kinondoni. Hawa ni viongozi wa kata zote (yaani Mwenyekiti, katibu na katibu mwenezi) viongozi wa majimbo yote matatu (kinondoni, Kawe na Ubungo), Viongozi wa wilaya (Mwenyekiti, katibu, na katibu mwenezi), na madiwani wa kata zote za wilaya ya kinondoni. Wengine walikuwa ni wageni waalikwa kama vile viongozi wa mkoa, Wajumbe wa mabaraza ya katiba (wengi mno), mgeni - Nape Nnauye, na mimi (sitamtaja aliyenialika kuepuka kumtia hatiani).

Nape Nnauye ndiye aliyekuwa msemaji mkuu na ujumbe aliouleta ni waraka wa NEC kuhusu mabadiliko ya katiba ya nchi!... rasimu - -
1. Wanapinga vikali serikali tatu!... Msimamo wao ni kufuata mfumo uliomo kwenye KATIBA YA CCM (yaani mfumo wa serikali mbili).
2. Wanapinga Vikali mawaziri kutokuwa wabunge!... Msimamo wao Waziri ni lazima awe MBUNGE.
3. Wanapinga vikali mgombea binafsi kwenye nafasi ya uraisi.
4. Wanatarajia kuibadili karibu rasimu nzima na kupitisha matakwa ya NEC ya CCM!...

Wanajiamini kuwa watafanikiwa kwakuwa wananguvu 73% Bungeni na 99% katika MABARAZA ya katiba... Nimeshuhudia kejeli dhidi ya vyama vya upinzani hasa CUF na CHADEMA. Hata wajumbe kutoka majimbo ya Kawe na UBUNGO wanaitwa watu wa Mdee na watu wa Mnyika. Nilipouliza nikaambiwa walizembea na kuwaacha wapinzani kujitwalia majimbo kirahisi.

Mytake: Kama hali iko hivi nchi nzima, AMINI MSIAMINI HAKUNA KATIBA MPYA, ni heri vyama vya siasa vianze kupigania TUME HURU ya UCHAGUZI si KATIBA. Narudia tena Kwa MIKAKATI hii ya CCM katiba itakayopatikana haitakuwa na jipya...
 
very sadi indeed...chadema nao saivi hoi, hawana maamuzi magumu.....watz tujaribu kuiga yalio jiri MISRII, tusiache nch yetu iwe mali ya familia flan flan
 
hawawezikujifunza kutoka misri kwa kuweka maslahi ya taifa mbele.

kwao makada ni bora bila kujali ni wezi tena wanapitia ccm kujijengea himaya na kulindana.

kupitia ccm wanalenga kutengeneza katiba ya kuleana na kulindana baada ya kukwapua na kuuza maliasili zetu
 
Chama Cha Mapinduzi kimedhihirisha mikakati yake haramu ya kuhakikisha katiba mpya itabeba MATAKWA yote ya NEC.. Jioni ya leo kuanzia saa 9-11 jioni kulikuwa na kikao kikuu cha wilaya/halmashauri ya kinondoni kujadili mapendekezo ya rasimu ya katiba mpya.. Kikao hicho kimefanyika Mwananyamala ukumbi wa CCM. Mgeni rasmi alikuwa NAPE Nnauye - Katibu wa itikadi na uenezi.

hata ninyi mtaani mnaweza mkajikusanya na kujadili, kulikuwa na uzi humu maaskofu walikaa na kujadili, sioni mbaya mtanzia akaa na kuijadili..?

mbona waoga hivo ... CCM itaendelea kuongoza hii nchi bado hakuna chama mbadala ndani ya hii tzn
 
quote_icon.png
By Chris Lukosi
Hivi wapi nitaweza kupata maembe dodo?



Hivi huyu ni mtu mwenye akili timamu?!..

upungufu wa kinga mwilini umepunguza na forebrain yake

Nimekupata mkuu!
 
leo karibu nchi nzima kamati za siasa za magamba na wajumbe wa mabaraza wamefanya vikao na kuweka hiyo misimamo.yaani ni majanga jamani.
 
Hivi kwani vyama vingine vya siasa vinazuiwa kujadili hii rasimu? Acheni umburula mkakae huko na nyie mjadili mnayoyataka kwny katiba. Kwa uoga huu hamuwezi kuiongoza Tz.
 
nyie mnaogopa nini? mmekaa kama sio wanaume? mwanaume halalamiki sana anafanya vitendo acheni wajipange watakavyo ikifika siku ya kupiga wakaanza kuchakachua ni mapanga sha sha tu kwa kwenda mbele,,,,wanaowatumia ni binadamu kama sisi wala hawana ROHO MBILI NI MOJA TU IKITOKA NDO IMETOKA.
 
Back
Top Bottom