Sad Truth: Sijivunii na mama wa mtoto wangu

Sad Truth: Sijivunii na mama wa mtoto wangu

Analyse

JF-Expert Member
Joined
Jan 19, 2014
Posts
17,637
Reaction score
47,413
1st Portion:

Na hii sio utani, sijivunii mama wa mtoto wangu. Sio kwamba nililazimishwa kuwa nae, hapana. Na katika kipindi chote nipo nae kwenye mahusiano nilikua muda mwingi anatawala mawazo yangu, na hata kuachana kwetu, ni yeye ndio aliniambia muda umefika nikatafute mtoto mwenzangu wa kudate nae. Katika kipindi chote nipo nae, sikuwahi kujua umri wake halisi ni miaka mingapi, Ila makadirio alinizidi miaka kati ya 25 hadi 30. Sijakosea, ilo ndo gape la umri kati ya mimi na mama wa mtoto wangu.

Kati ya vitu ninavyojutia sana, kimoja wapo ni ili tukio la huyu mama. Kitendo cha kukataa shule na kukimbilia mjini, sijawahi kukijutia kama ambavyo najutia kuzaa na huyu Maza. Katika huu Uzi, sito-base sana kipindi cha mahusiano yetu, Ila nitaongelea sana baada ya yeye kufahamika home, maana hapo ndio hasa niliona ukubwa wa ujinga niliofanya. Maana sterehe zangu zilileta mtikisiko kwenye familia, kibaya zaidi sikuwepo home.

Nilikutana nae kwa namna ya ajabu kwanza. Our first meeting alikuwa very harsh kwangu. Baada ya kutimuliwa kwenye nyumba niliyokuwa nafanyia kazi kwa kosa la kumtelezesha mke wa bosi kwenye malumalu, kama mtakumbuka, niliondoka bila kuwa na uelekeo maalum. Ila mwisho wa siku niliangukia buguruni sokoni. Nilifanya sana vibarua pale.

Mazingira yale kulikuwa na bi mkubwa mmoja ana kigrosary chake cha kizushi. Kama ulisoma story yangu, kuna grosary nilikua nakunywa soda, then nikamwambia muhusika abadilishe channel, maana kipindi kilichopo kilikuwa kinanipa machungu, then yule muhusika akanijibu shit. Sasa huyu muhusika/ Maza mwenye kigrosary, ndo huyu nilikuja kuzaa nae.

Wakati nafanya vibarua pale sokoni, sikuwa na sehem maalum ya kulala. Hivyo ningeweza kulala popote katika mazingira yale. Mara chache chache nilikuwa nalala pembeni ya kile kigrosary na jamaa wengine niliowakuta. Kuna siku nilichelewa kuamka, maana tulikuwa na kawaida ya kuamka mapema sana.

Hiyo siku yule Maza alikuta bado mazingira yale, japo sikuwa nimesinzia. Wala hakunikaripia, aliniacha nikaondoka kistaarabu tu. Mida ya jioni, nilikuwa nakatisha eneo lake, akaniita. Akaniuliza wewe ni mgeni maeneo haya, umetokea wapi na imekuwaje unalala nje? Siku ya kwanza nakuona ulikuwa smart, imekuwaje? Ikabidi nimfungukie tu, japo sikumwambia kama nilikimbia home. Nilimsimulia tu kisa cha kutimuliwa kwa yule Mzee niliyekuwa nafanya kazi kwake. Mwisho wa siku akaamua kunipa kazi pale kwenye grosary yake. Tulikubaliana niwe nasaidia manunuzi, usafi, ubebaji na uletaji bidhaa n.k, ujira wangu ikawa ni msosi.

Siku zilivyoenda akaanza kuniamini, nikawa hadi nasimamia biashara yake. Ikafika kipindi akanipeleka mpaka kwake, alikuwa anakaa maeneo ya gongo la mboto, japo alikuwa na makazi mengine kisarawe. Sababu ya misele yake na kazi, ndo maana alikuwa anakaa nyumba ya gomz, sababu ya ukaribu. Baada ya kufanya kazi kwake kwa miezi kama miwili, ndo akanipeleka pale gomz.

Mimi ndio nilikua naamka mapema nawahi kwenye grosary yake kufungua na kuweka mazingira vizuri, then yeye anakuja baadae. Na hata baadhi ya siku angewahi kuondoka kabla yangu, na mara nyingi tuliondoka wote.

Kuna siku alirudi amelewa maana siku hiyo alihudhuria kitchen party. Akilewa ni anaongea sana alaf usumbufu ni mwingi, mara fanya hiki, mara kile n.k. kiufupi anakuwa kama Muhindi kwa jinsi anavyotuma. Hii siku ndio ka mara ya kwanza nilitembea nae. Palivyokucha nilikuwa naona aibu as if wapangaji walijua nilichofanya (alikuwa amepangisha vyumba vilivyobaki).

Hata yeye nilikua naona aibu kumwangalia usoni. Nikawa nakwepa kukaa naye muda mwingi. Yeye akawa ananicheka tu, siku kama ya pili akaniambia najua kinachofanya uwe na aibu. Sikuelewa alimaanisha nini. Ila siku hiyo tulivyorudi home akanipa tena show, kesho yake tena, na tena. Mpaka ikawa rasmi sasa, na ile aibu ikatoka.

Tuliendelea na huu mchezo kwa muda mrefu mpaka ikawa sio Siri tena. Huyu Maza alishawahi kuolewa mara mbili hapo kabla, Ila aliachika kwenye ndoa zote sababu ya mambo yake ya kuendekeza starehe, lakini pia alikua akishika mimba zinaharibika/ zinatoka, so hakuwahi kuzaa. Taarifa zilipokuwa wazi kuwa anatembea na katoto, ndugu zake walikuwa wananichukia , kila siku wanampigia simu, maneno kibao, lakini sielewi alikua na akili gani yule Maza, Wala hakuonekana kujali.

After kama miezi 7 au 8 ya kuwa pamoja, alikuja kushika mimba. Alivyogundua ana mimba, kutokana na historia yake akajua hii haitodumu, so siku moja tunafunga hesabu, akanijulisha kuwa ana mimba, then akaniambia kabla haijatoka, nifanye mchakato wa kutafuta sehemu ya kwenda. Nikashangaa, namuuliza sasa Mimi nitaenda wapi? Akanijibu "We mtoto, Mimi sio mama yako, katafute mtoto mwenzio mfanye maisha"

Kiukweli sikutegemea angebadilika haraka vile. Akili yangu yote alikua kaiteka yeye. Na mpaka leo nikiona mtu anadate na mshangazi/jimama, simshangai. Mashangazi yaoneni tu vile vile. Sikuwa na jinsi, ikabidi siku hiyo nisirudi kwake, nikaamua kutafuta usawa mwingine. Nikamuacha yeye na grosary yake huku akisubiria ile mimba itoke. HAIKUTOKA

[emoji26][emoji26][emoji26]

Endelea hapa Sad Truth: Sijivunii na mama wa mtoto wangu
 
Pole mzee, majuto ni sehemu ya Maisha. Ukiona hujutii baadhi ya mambo uliyotenda basi kama mwanadamu ambaye ukamilifu wake unategemea udhaifu alionao unakua haupo sawa.
Kama kuzaa ushazaa nae siku moja ongea nae mjadili msatakabari wa mtoto wenu umsikie inakuaje. Usiache damu yako ilelewe na mzazi mmoja wakati wewe U hai.

Akileta ukaidi mshirikishe mzee wako atajua jinsi ya kufanya, kuna familia haziibiwi watoti. Mzee ataongea maneno ya kikurungwa huyo mama atakutafuta mweyewe😊

Halafu seems like chuki uliyoitengeneza zaidi kwa huyo mama haina mashiko ni kwa sababu uli-Experience Post traumatic stress Disorder (PSTD) iliyosababishwa na wewe kuachwa Mazingira magumu na huyo mama. Jaribu kuangalia the beauty side of her ili uCope with that PSTD.

Sema 25yrs parefu sana mzee🚶🚶
___UPDATES_

Samahanini nilitoa ushauri bila kujua Kwamba hii ni simulizi inayoendelea. Nilijua ni Current Matter that need to be addressed promptly.
Very Sorry ndugu wasomaji

FB_IMG_16516802956061878.jpg
 
2nd Portion:

.......Baada ya kutoka kwa yule Maza, sikuendelea muda mrefu kupiga ushanta pale sokoni, ndio likaja lile wazo la kwenda mgodini Msumbiji ( yaliyoendelea after hapo yapo kwenye ile story). Huku nyuma yule Maza, mimba ilikua hadi akajifungua, Mimi sina habari, maana nilihisi ingetoka, sikuwa na simu na hatuna mawasiliano. Inaonekana baada ya kuanza malezi, alikuja akawa anaona kero na usumbufu.

Ile mtoto kuumwa umwa, clinic etc. Hapo nadhani ndio lilimjia wazo la kumpeleka mtoto home kwetu. Wazazi wangu walikuwa wanaishi mkoani, tena kijijini sio town. Kipindi nafanya kazi kwa yule Maza, alikuwa ananijua taarifa zangu nyingi, mfano kwetu tupo wangapi, majina ya wazee wangu, Kijiji walichopo n.k. Unajua ubaya au uzuri wa vijijini, ukifahamu taarifa za mtu, unaweza ukafika hadi anapoishi kwa kuulizia tu. Basi ndicho alichofanya yule Maza, alifanya jitihada hadi akafika home kabisa. Matukio mengi yaliyotokea wakati sipo, nilipata taarifa zake toka kwa sister, mama, baba na wadogo zangu wengine, kwa nyakati tofauti tofauti.

Yule Maza alipofika home, alikaribishwa vizuri tu. Unajua kijijini kwetu mgeni ukifika ambaye hawakujui kabisa, wala hawakuulizi umefata nini, wao wanakukirimu, then wanakupa nafasi. Sasa yule Maza baada ya ukaribisho, ndio akajitambulisha, akaniulizia Mimi, akaambiwa sijaonekana pale nina kama miaka miwili. Akawaambia kuwa ananifahamu vizuri, na huko nilipokuwa nimeacha mtoto ambae ndio yule. Unajua pamoja na utukutu wangu, Mimi ni kipenzi cha wote kwenye familia yetu. Ile habari ya kuwa yule mtoto ni wangu, wakaipokea vizuri, tena ukiangalia Wana muda mrefu hawajaniona. Dada angu alifurahi sana, hapo ndo akaomba mtoto ambebe, maana muda wote alikuwa bado kashikwa na yule Maza. Sasa wakati yule Maza anaendelea kuongea nao pale, Mama yangu akauliza mama wa mtoto yuko wapi, mbona hajaja? Yule Maza ndo kuwafungukia kuwa yeye ndio mama wa mtoto. Mshua kusikia vile alinyanyuka kwenye kiti kama vile amepigwa shoti, akawa anamwangalia yule Maza akihisi ameskia vibaya, dada na mama wao wakabaki wametoa macho. Yule Maza akarudia tena kauli yake, kuwa yule mtoto ni wangu, na yeye ndio nimezaa nae. Unaambiwa mama yangu alipiga ukunga mmoja mkubwa sana.

Baba alitoka sebleni speed mpaka chumbani kwake, then akatoka kabeba kibegi kama anasafiri. Mama akamuuliza, "Baba nanii unaenda wapi?" Mshua akawajibu huku anaondoka, kuwa anaenda serikali za mtaa kwa ajili ya ule mgogoro wa ardhi. (Huu mgogoro ulikuwa ni wa muda mrefu sana, na mshua alikuwa kila akiitwa anakataa kwenda, siku hiyo ndo akaona aitikie wito). Akawa anasisitiza, akirudi asimkute yule Maza.

Mama na dada wakabaki na yule Maza pale, hawaelewi wafanye nini. Yule Maza yeye katulia tu anawachora. Mama mara kaingia jikoni, mara chumbani, mara nje ili mradi hakuwa na utulivu. Yule Maza nae kila akitaka kumuita dada angu, alikuwa anamuita "Wifi", hapo ndio mama angu anazidi kuvurugwa. Dada nae akitaka kumuita yule Maza "Wifi" akili inakataa, ulimi unakuwa mzito. Siku hiyo mshua hakurudi home, na bi mkubwa Wala hakukumbuka kumuulizia. Dada ilibidi ampe kampani mama, akalala chumbani kwake ili kumpunguzia mawazo. Yule Maza akalala chumba cha dada. Niliivuruga sana familia yangu.

Usiku wakati wapo chumbani mama na dada huku, dada akawa anamwambia mama, labda yule Maza anawatania tu au amepotea nyumba, wasubirie pakuche waongee nae vizuri. Mama akawa anabisha, kuwa yule Maza hajakosea nyumba. Akawa anamwambia dada "Hivi katika kuzunguka kwako kote pua za namna ile ulishawahi kuziona wapi kama sio kwenye ukoo wa baba ako?, Yule mtoto ni wa hapa, cheki pua yake, tena nahisi ni wa baba ako, wanamsingizia tu mwanangu kwavile hayupo, we huoni baba ako alivyokimbia hapa?"

Katika kukua kwangu, hakuna siku ambayo niliona baba na mama wakigombana sababu ya swala la uaminifu. Hii ni kwa mara ya kwanza niliwaingiza katika mgogoro wa aina hiyo. Nakumbuka kipindi niko mdogo sana, tulikua tunatoka sokoni na mshua, wakati tupo njiani alitokea mwanamke from nowhere akamchapa Kofi la maana mshua, then akasepa bila kuongea chochote. Mshua alibaki ametoa macho tu, hata mimi nilibaki surprised maana sikuelewa imekuwaje kuwaje, nilishindwa kumuuliza mshua, nikatarajia ataongea kitu, nae hakuwahi niambia chochote mpaka leo. Lile tukio lilionwa na wengi, maana ilikuwa asubuhi, story zikamfikia mama. Aliniuliza sana, nikawa nakataa kuwa hapajatokea kitu kama hicho, so kitendo cha huyu Maza kuja na mtoto alaf anasema wangu, basi mama akaona ni yale yale tu, tunafichiana na mshua, yule mtoto ni wa baba, na yule Maza ni mchepuko [emoji26][emoji26][emoji26].

Kesho yake mshua alipiga simu kuuliza kama yule Maza ameondoka, alivyoambiwa bado yupo, faza akasema anaenda kumtembelea mdogo wake anaumwa, akirudi asimkute yule Maza. Jioni kabisa alirudi, tena baada ya kufatwa na mdogo wangu kuwa Kuna ugomvi home, mama anasema yule ni mke mdogo wake( baba), so mshua alikuwa anaitwa akamchukue mchepuko wake na mtoto wa uzeeni. Baba kufika home, anaingia sebleni kwa hasira, anapokewa na kelele. Yule Maza nae anamwambia "Afadhali mkwe umekuja". Ile kauli ya kuitwa mkwe ndo inazidi kumchanganya Baba, Mama nae anaona kama wanamuigizia. Kiufupi pakawa vululu vululu. Kipindi wao wanajiandaa kukaa kikao wajadili vizuri ili swala, yule Maza akawaaga kuwa anaondoka, kikao cha familia hakimuhusu. Akamuacha mtoto, akaondoka wala hana wasi wasi. Mshua wetu jinsi alivyo, akiwa katika hali ya kawaida, akitaka kumuongelea Mama yetu, huwa anatumia maneno kama "Mama fulani", "Kamuite Mama", "Mama yupo?" n.k Ila akishavurugwa, yule anakuwa sio mama yetu tena, bali ni mke wake. Utasikia anasema, nitawafukuza wote nibaki na mke wangu, au oeni mpeleke stress kwa wake zenu, niachieni mke wangu. Kiufupi mshua anamuelewa sana mke wake, na mkewe (Mama yetu) analijua ilo, lakini kizaa zaa nilicholeta kilisahaulisha vyote, mama akawa haelewi kitu.

Ile kauli ya mchuma janga ula na wakwao, hapa ndio niliona. Msala wangu, tabu imeenda kwa familia. So yeyote anayesoma hapa, namshauri awe makini sana na mambo anayofanya, asirudishe mzigo kwa familia.

Wazazi at last walikuja wakaelewana, Ila wakashindwa kuamua kuhusu mtoto. Baba alikua hataki kabisa kukubali kuwa yule mtoto nimezaa na yule Maza. Mama nae akawa anasema kuhusu mtoto, anauhakika kabisa ni wetu, Ila kuhusu mama wa mtoto ndo hawezi sema chochote mpaka Mimi niulizwe. Katika ile story niliyokuwa naelezea hustle zangu, Kuna kipindi nilikutana na mshua ghafla bila kutarajia, alaf mshua akanikazia. Kipindi Mimi namwangalia mshua kwa hudhuni nikitegemea atanionea huruma, kumbe yeye alikua anajaribu kutafakari hii ng'ombe (Mimi) ndo kweli imezaa na yule Maza? Akaniacha nikaendelee kusota kwanza. Alaf alivyorudigi home Wala hakuwaambia kama tulikutana

Hatimae nikarudi nyumbani. Siku niliyorudi home kwa mara ya kwanza toka niondokage, ndo nilijua kuwa kumbe mshua ni kichaa zaidi yangu........

Endelea hapa Sad Truth: Sijivunii na mama wa mtoto wangu
 
.......Baada ya kutoka kwa yule Maza, sikuendelea muda mrefu kupiga ushanta pale sokoni, ndio likaja lile wazo la kwenda mgodini Msumbiji ( yaliyoendelea after hapo yapo kwenye ile story). Huku nyuma yule Maza, mimba ilikua hadi akajifungua, Mimi sina habari, maana nilihisi ingetoka, sikuwa na simu na hatuna mawasiliano. Inaonekana baada ya kuanza malezi,
Ha ha ha.....story nzur Sana[emoji4][emoji106]
 
Na hii sio utani, sijivunii mama wa mtoto wangu. Sio kwamba nililazimishwa kuwa nae, hapana. Na katika kipindi chote nipo nae kwenye mahusiano nilikua muda mwingi anatawala mawazo yangu, na hata kuachana kwetu, ni yeye ndio aliniambia muda umefika nikatafute mtoto mwenzangu wa kudate nae. Katika kipindi chote nipo nae, sikuwahi kujua umri wake halisi ni miaka mingapi, Ila makadirio alinizidi miaka kati ya 25 hadi 30. Sijakosea, ilo ndo gape la umri kati ya mimi na mama wa mtoto wangu.

Kati ya vitu ninavyojutia sana, kimoja wapo ni ili tukio la huyu mama. Kitendo cha kukataa shule na kukimbilia mjini, sijawahi kukijutia kama ambavyo najutia kuzaa na huyu Maza. Katika huu Uzi, sito-base sana kipindi cha mahusiano yetu, Ila nitaongelea sana baada ya yeye kufahamika home, maana hapo ndio hasa niliona ukubwa wa ujinga niliofanya. Maana sterehe zangu zilileta mtikisiko kwenye familia, kibaya zaidi sikuwepo home.

Nilikutana nae kwa namna ya ajabu kwanza. Our first meeting alikuwa very harsh kwangu. Baada ya kutimuliwa kwenye nyumba niliyokuwa nafanyia kazi kwa kosa la kumtelezesha mke wa bosi kwenye malumalu, kama mtakumbuka, niliondoka bila kuwa na uelekeo maalum. Ila mwisho wa siku niliangukia buguruni sokoni. Nilifanya sana vibarua pale.

Mazingira yale kulikuwa na bi mkubwa mmoja ana kigrosary chake cha kizushi. Kama ulisoma story yangu, kuna grosary nilikua nakunywa soda, then nikamwambia muhusika abadilishe channel, maana kipindi kilichopo kilikuwa kinanipa machungu, then yule muhusika akanijibu shit. Sasa huyu muhusika/ Maza mwenye kigrosary, ndo huyu nilikuja kuzaa nae.

Wakati nafanya vibarua pale sokoni, sikuwa na sehem maalum ya kulala. Hivyo ningeweza kulala popote katika mazingira yale. Mara chache chache nilikuwa nalala pembeni ya kile kigrosary na jamaa wengine niliowakuta. Kuna siku nilichelewa kuamka, maana tulikuwa na kawaida ya kuamka mapema sana.

Hiyo siku yule Maza alikuta bado mazingira yale, japo sikuwa nimesinzia. Wala hakunikaripia, aliniacha nikaondoka kistaarabu tu. Mida ya jioni, nilikuwa nakatisha eneo lake, akaniita. Akaniuliza wewe ni mgeni maeneo haya, umetokea wapi na imekuwaje unalala nje? Siku ya kwanza nakuona ulikuwa smart, imekuwaje? Ikabidi nimfungukie tu, japo sikumwambia kama nilikimbia home. Nilimsimulia tu kisa cha kutimuliwa kwa yule Mzee niliyekuwa nafanya kazi kwake. Mwisho wa siku akaamua kunipa kazi pale kwenye grosary yake. Tulikubaliana niwe nasaidia manunuzi, usafi, ubebaji na uletaji bidhaa n.k, ujira wangu ikawa ni msosi.

Siku zilivyoenda akaanza kuniamini, nikawa hadi nasimamia biashara yake. Ikafika kipindi akanipeleka mpaka kwake, alikuwa anakaa maeneo ya gongo la mboto, japo alikuwa na makazi mengine kisarawe. Sababu ya misele yake na kazi, ndo maana alikuwa anakaa nyumba ya gomz, sababu ya ukaribu. Baada ya kufanya kazi kwake kwa miezi kama miwili, ndo akanipeleka pale gomz.

Mimi ndio nilikua naamka mapema nawahi kwenye grosary yake kufungua na kuweka mazingira vizuri, then yeye anakuja baadae. Na hata baadhi ya siku angewahi kuondoka kabla yangu, na mara nyingi tuliondoka wote.

Kuna siku alirudi amelewa maana siku hiyo alihudhuria kitchen party. Akilewa ni anaongea sana alaf usumbufu ni mwingi, mara fanya hiki, mara kile n.k. kiufupi anakuwa kama Muhindi kwa jinsi anavyotuma. Hii siku ndio ka mara ya kwanza nilitembea nae. Palivyokucha nilikuwa naona aibu as if wapangaji walijua nilichofanya (alikuwa amepangisha vyumba vilivyobaki).

Hata yeye nilikua naona aibu kumwangalia usoni. Nikawa nakwepa kukaa naye muda mwingi. Yeye akawa ananicheka tu, siku kama ya pili akaniambia najua kinachofanya uwe na aibu. Sikuelewa alimaanisha nini. Ila siku hiyo tulivyorudi home akanipa tena show, kesho yake tena, na tena. Mpaka ikawa rasmi sasa, na ile aibu ikatoka.


Tuliendelea na huu mchezo kwa muda mrefu mpaka ikawa sio Siri tena. Huyu Maza alishawahi kuolewa mara mbili hapo kabla, Ila aliachika kwenye ndoa zote sababu ya mambo yake ya kuendekeza starehe, lakini pia alikua akishika mimba zinaharibika/ zinatoka, so hakuwahi kuzaa. Taarifa zilipokuwa wazi kuwa anatembea na katoto, ndugu zake walikuwa wananichukia , kila siku wanampigia simu, maneno kibao, lakini sielewi alikua na akili gani yule Maza, Wala hakuonekana kujali.

After kama miezi 7 au 8 ya kuwa pamoja, alikuja kushika mimba. Alivyogundua ana mimba, kutokana na historia yake akajua hii haitodumu, so siku moja tunafunga hesabu, akanijulisha kuwa ana mimba, then akaniambia kabla haijatoka, nifanye mchakato wa kutafuta sehemu ya kwenda. Nikashangaa, namuuliza sasa Mimi nitaenda wapi? Akanijibu "We mtoto, Mimi sio mama yako, katafute mtoto mwenzio mfanye maisha"

Kiukweli sikutegemea angebadilika haraka vile. Akili yangu yote alikua kaiteka yeye. Na mpaka leo nikiona mtu anadate na mshangazi/jimama, simshangai. Mashangazi yaoneni tu vile vile. Sikuwa na jinsi, ikabidi siku hiyo nisirudi kwake, nikaamua kutafuta usawa mwingine. Nikamuacha yeye na grosary yake huku akisubiria ile mimba itoke. HAIKUTOKA

[emoji26][emoji26][emoji26]
Cha kaka kakuzidi miaka 25? Am sorry yuko right. Kafute age mates wako
 
Back
Top Bottom