...... Mzee wetu alikuwa na kawaida moja, ukitokea msala alafu Mama akaupoza. Hapendagi kumbishia, Ila next time ukiingia kwenye 18 zake atakupa kipigo na cha msala uliopita. So, hiki kipigo kilichokuwa kinaendelea muda huu, ilikuwa ni majumuisho na ule msala wa kuondoka home. Mzee alikua anakaza mikono kadiri anavyokumbuka matukio niliyofanya, ikafika hatua sauti ya Mama nikawa siiskii kabisa, nikaona hapa sasa nakufa. Katika kujitetea ikabidi nimng'ate, nilikaza meno mpaka akaniachia. Kawaida ya mshua akishakuachia, wakati ww unahangaika kuvuta pumzi, yeye anawahi kusimama ili akurushie ngumi za mfululizo. Alivyoniachia tu, sikutaka hata kusubiria, nikatoka nduki, mshua akaunga tela. Tukaanza kufukuzana kuizunguka nyumba. Mama nae kule ndani anafanya kazi ya kuhama madirisha tu, mara yuko dirisha ili, mara lile kutegemeana na sisi tuko upande upi. Round moja tu, Mzee akakaa chini, na Mimi nikatulia upande niliokuwepo kwanza navuta pumzi.
Mzee akaamua kuingia ndani, me nikaenda zangu kuoga then tukarudi kuendelea na kikao Mimi na Yeye. Safari hii Mama hakutaka tuongelee nje tena, tukakaa sebleni. Mama akatuletea chai, tukawa tunakunywa huku tunapiga story sasa.
Mzee ananiuliza "Unakunywa pombe?" Nikajibu hapana."Unavuta bangi?" Nikajibu hapana. "Sasa ilikuwaje ukachukua lile tank? Akili yako ilikua wapi?". Nikakosa jibu la kumpa, nikawa mbali kimawazo. Akaendelea tena"Hivi huu ujasiri uliutoa wapi haswa, mbona hufanani na ndugu zako?" Mama akadakia "Hafananii na ndugu zake, anafanana na wewe, inamaana ushajisahau?" Mzee nae akawaka "Walau Mimi (Mshua) nilichukua mtu wa umri wangu" ( Unajua Bi mkubwa wangu nae amejaa jaa, japo ni mdogo kiumri kwa Baba). Mama nae akamjibu " Swala sio kuchukua wa umri wako, kwani wakati unanifata ulijuaga umri wangu, we siuliangalia kilichokuvutia?. Mwanao ashakuletea mkwe, inabidi umkubali tu"
Lile neno mkwe likaonekana kumkera Mzee. Unajua Mama yetu wala sio mtu wa kukaa na kitu moyoni. Muda huu anajibizana na Mzee, Yeye Mama alikua anatabasamu kabisa, Ila Mzee kakunja ndita. Battle ikatoka kwangu, ikahamishiwa kwa Mama, Mzee akaanza kumwambia Mama yeye ndio chanzo cha yote haya. Mshua akamwambia Mama "Nilikwambia tuzae mapema ukawa unasema tusubirie subirie, matokeo yake mtoto alikuwa anakulia kiunoni, huyu kazaliwa akiwa mtu mzima" Unajua katika familia yetu, watoto waliotangulia wote wamepishana miaka miwili miwili kasoro kaka yangu ninayemfuata amenizidi miaka 7. So alichokuwa anamaanisha Mzee ni kwamba hiyo miaka 7 yote ambayo walikuwa wanasubiria, Mimi nilikua naendelea kukua tu, dah [emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]
Anyway, msala ulikuja ukapoa tukaongea kistaarabu, Ila Mzee alikuwa so disappointed. Akawa ananiambia kuwa anastaili kujifunza toka kwangu maana Mimi ni legend, Nina namna zangu za kurun things ambazo hajawahi imagine.
Alinipa ushauri wake kuhusiana na mambo mbali mbali. Ila katika maongezi nae ndio nikagundua kuwa watu wetu wa karibu huwa wanaumizwa sana na mambo ya ajabu tunayofanya. Ile kauli ya mchuma janga ula na wa kwao, ilidhihirika mbele yangu. Sema kwavile ilishatokea hapakuwa na namna. Kutokana na hiki kisanga Mzee wangu ni mara chache sana kuniita jina langu,mara nyingi ananiita legend. Sipendagi akiniita hivyo, Ila Sina namna ya kumzuia, niliyataka. Mara chache chache huwa ananitania kuhusu yule Maza, now days anachukulia as a joke tu. Ananiambiaga nikiamua kuoa, nisisite kuwajulisha. Ila wao hawatonipush maana wanahofia nisije kuwafanyia surprise nyingine
** ********* ****** ***
Tukafunga huo ukurasa kuhusu mtoto na yule Maza. Ndio tukaanza kuongea kuhusu harakati zangu zingine. Alitaka kujua ilikuwaje tukakutana pale Magingo kwenye soko la tangawizi. Nilimuelezea kwa ufupi mizunguko yangu mpaka kufikia ile siku tunaonana, Yeye akiwa kama Boss, Mimi nikiwa kama kibarua..
Nadhani hayo Sina haja ya kuyaongelea hapa, maana nilishayaelezea kwa urefu sana kwenye ule Uzi safari yangu.
Nilizaliwa miaka kadhaa iliyopita. Katika familia ya watoto 7, mimi nilikuwa wa 6. Kama watoto walivyo, nilikuwa mtundu kiasi ila sio mtukutu. Nakumbuka nikiwa darasa la 5,niliitwa mbele na ticha nikafanye swali la hesabu. Nikafanya swali kwa mbwembwe, nilikuwa nasumbuliwa na mafua, kabla...
www.jamiiforums.com
** ** ***
Kwa sasa dogo alishatoka kwa Dada anaishi kwa Babu na Bibi yake. Yule Maza sina mawasiliano nae, japo kwasasa anaishi nyumbani kwake Kisarawe. Mpaka now inanipaga ukakasi nikiingia kwenye mahusiano kujielezea kuwa nina mtoto, hasa kuepuka swali la mama yake yuko wapi? Kwanini mliachana? Akirudi je? n.k
So, kwa kifupi sipo nae (maana najua ili swali litaulizwa tu). Dogo hajawahi kumuulizia Mama yake, labda kwavile walitengana akiwa mdogo sana so hakupataga ile bond ya Mama. Yule Maza nilishawahi kutana nae mara moja maeneo ya mawasiliano ubungo, tuliongea mawili matatu kuhusu mwanangu, then kila mmoja akaendelea na safari yake. Namba yake ninayo, pia anayo yangu japo hatuna mawasiliano.Huyu Maza hakuwahi kupata mtoto kabla ya huyu, nashangaa kwanini aliamua kumpeleka home kwetu, nilitarajia angemng'ang'ania kama dhahabu, but haikuwa hivyo.
Anyway, hiyo ndio ilikua story yangu. Until next time,
Na hii sio utani, sijivunii mama wa mtoto wangu. Sio kwamba nililazimishwa kuwa nae, hapana. Na katika kipindi chote nipo nae kwenye mahusiano nilikua muda mwingi anatawala mawazo yangu, na hata kuachana kwetu, ni yeye ndio aliniambia muda umefika nikatafute mtoto mwenzangu wa kudate nae. Katika kipindi chote nipo nae, sikuwahi kujua umri wake halisi ni miaka mingapi, Ila makadirio alinizidi miaka kati ya 25 hadi 30. Sijakosea, ilo ndo gape la umri kati ya mimi na mama wa mtoto wangu.
Kati ya vitu ninavyojutia sana, kimoja wapo ni ili tukio la huyu mama. Kitendo cha kukataa shule na kukimbilia mjini, sijawahi kukijutia kama ambavyo najutia kuzaa na huyu Maza. Katika huu Uzi, sito-base sana kipindi cha mahusiano yetu, Ila nitaongelea sana baada ya yeye kufahamika home, maana hapo ndio hasa niliona ukubwa wa ujinga niliofanya. Maana sterehe zangu zilileta mtikisiko kwenye familia, kibaya zaidi sikuwepo home.
Nilikutana nae kwa namna ya ajabu kwanza. Our first meeting alikuwa very harsh kwangu. Baada ya kutimuliwa kwenye nyumba niliyokuwa nafanyia kazi kwa kosa la kumtelezesha mke wa bosi kwenye malumalu, kama mtakumbuka, niliondoka bila kuwa na uelekeo maalum. Ila mwisho wa siku niliangukia buguruni sokoni. Nilifanya sana vibarua pale.
Mazingira yale kulikuwa na bi mkubwa mmoja ana kigrosary chake cha kizushi. Kama ulisoma story yangu, kuna grosary nilikua nakunywa soda, then nikamwambia muhusika abadilishe channel, maana kipindi kilichopo kilikuwa kinanipa machungu, then yule muhusika akanijibu shit. Sasa huyu muhusika/ Maza mwenye kigrosary, ndo huyu nilikuja kuzaa nae.
Wakati nafanya vibarua pale sokoni, sikuwa na sehem maalum ya kulala. Hivyo ningeweza kulala popote katika mazingira yale. Mara chache chache nilikuwa nalala pembeni ya kile kigrosary na jamaa wengine niliowakuta. Kuna siku nilichelewa kuamka, maana tulikuwa na kawaida ya kuamka mapema sana.
Hiyo siku yule Maza alikuta bado mazingira yale, japo sikuwa nimesinzia. Wala hakunikaripia, aliniacha nikaondoka kistaarabu tu. Mida ya jioni, nilikuwa nakatisha eneo lake, akaniita. Akaniuliza wewe ni mgeni maeneo haya, umetokea wapi na imekuwaje unalala nje? Siku ya kwanza nakuona ulikuwa smart, imekuwaje? Ikabidi nimfungukie tu, japo sikumwambia kama nilikimbia home. Nilimsimulia tu kisa cha kutimuliwa kwa yule Mzee niliyekuwa nafanya kazi kwake. Mwisho wa siku akaamua kunipa kazi pale kwenye grosary yake. Tulikubaliana niwe nasaidia manunuzi, usafi, ubebaji na uletaji bidhaa n.k, ujira wangu ikawa ni msosi.
Siku zilivyoenda akaanza kuniamini, nikawa hadi nasimamia biashara yake. Ikafika kipindi akanipeleka mpaka kwake, alikuwa anakaa maeneo ya gongo la mboto, japo alikuwa na makazi mengine kisarawe. Sababu ya misele yake na kazi, ndo maana alikuwa anakaa nyumba ya gomz, sababu ya ukaribu. Baada ya kufanya kazi kwake kwa miezi kama miwili, ndo akanipeleka pale gomz.
Mimi ndio nilikua naamka mapema nawahi kwenye grosary yake kufungua na kuweka mazingira vizuri, then yeye anakuja baadae. Na hata baadhi ya siku angewahi kuondoka kabla yangu, na mara nyingi tuliondoka wote.
Kuna siku alirudi amelewa maana siku hiyo alihudhuria kitchen party. Akilewa ni anaongea sana alaf usumbufu ni mwingi, mara fanya hiki, mara kile n.k. kiufupi anakuwa kama Muhindi kwa jinsi anavyotuma. Hii siku ndio ka mara ya kwanza nilitembea nae. Palivyokucha nilikuwa naona aibu as if wapangaji walijua nilichofanya (alikuwa amepangisha vyumba vilivyobaki).
Hata yeye nilikua naona aibu kumwangalia usoni. Nikawa nakwepa kukaa naye muda mwingi. Yeye akawa ananicheka tu, siku kama ya pili akaniambia najua kinachofanya uwe na aibu. Sikuelewa alimaanisha nini. Ila siku hiyo tulivyorudi home akanipa tena show, kesho yake tena, na tena. Mpaka ikawa rasmi sasa, na ile aibu ikatoka.
Tuliendelea na huu mchezo kwa muda mrefu mpaka ikawa sio Siri tena. Huyu Maza alishawahi kuolewa mara mbili hapo kabla, Ila aliachika kwenye ndoa zote sababu ya mambo yake ya kuendekeza starehe, lakini pia alikua akishika mimba zinaharibika/ zinatoka, so hakuwahi kuzaa. Taarifa zilipokuwa wazi kuwa anatembea na katoto, ndugu zake walikuwa wananichukia , kila siku wanampigia simu, maneno kibao, lakini sielewi alikua na akili gani yule Maza, Wala hakuonekana kujali.
After kama miezi 7 au 8 ya kuwa pamoja, alikuja kushika mimba. Alivyogundua ana mimba, kutokana na historia yake akajua hii haitodumu, so siku moja tunafunga hesabu, akanijulisha kuwa ana mimba, then akaniambia kabla haijatoka, nifanye mchakato wa kutafuta sehemu ya kwenda. Nikashangaa, namuuliza sasa Mimi nitaenda wapi? Akanijibu "We mtoto, Mimi sio mama yako, katafute mtoto mwenzio mfanye maisha"
Kiukweli sikutegemea angebadilika haraka vile. Akili yangu yote alikua kaiteka yeye. Na mpaka leo nikiona mtu anadate na mshangazi/jimama, simshangai. Mashangazi yaoneni tu vile vile. Sikuwa na jinsi, ikabidi siku hiyo nisirudi kwake, nikaamua kutafuta usawa mwingine. Nikamuacha yeye na grosary yake huku akisubiria ile mimba itoke. HAIKUTOKA
...... Mzee wetu alikuwa na kawaida moja, ukitokea msala alafu Mama akaupoza. Hapendagi kumbishia, Ila next time ukiingia kwenye 18 zake atakupa kipigo na cha msala uliopita. So, hiki kipigo kilichokuwa kinaendelea muda huu, ilikuwa ni majumuisho na ule msala wa kuondoka home. Mzee alikua anakaza mikono kadiri anavyokumbuka matukio niliyofanya, ikafika hatua sauti ya Mama nikawa siiskii kabisa, nikaona hapa sasa nakufa. Katika kujitetea ikabidi nimng'ate, nilikaza meno mpaka akaniachia. Kawaida ya mshua akishakuachia, wakati ww unahangaika kuvuta pumzi, yeye anawahi kusimama ili akurushie ngumi za mfululizo. Alivyoniachia tu, sikutaka hata kusubiria, nikatoka nduki, mshua akaunga tela. Tukaanza kufukuzana kuizunguka nyumba. Mama nae kule ndani anafanya kazi ya kuhama madirisha tu, mara yuko dirisha ili, mara lile kutegemeana na sisi tuko upande upi. Round moja tu, Mzee akakaa chini, na Mimi nikatulia upande niliokuwepo kwanza navuta pumzi.
Mzee akaamua kuingia ndani, me nikaenda zangu kuoga then tukarudi kuendelea na kikao Mimi na Yeye. Safari hii Mama hakutaka tuongelee nje tena, tukakaa sebleni. Mama akatuletea chai, tukawa tunakunywa huku tunapiga story sasa.
Mzee ananiuliza "Unakunywa pombe?" Nikajibu hapana."Unavuta bangi?" Nikajibu hapana. "Sasa ilikuwaje ukachukua lile tank? Akili yako ilikua wapi?". Nikakosa jibu la kumpa, nikawa mbali kimawazo. Akaendelea tena"Hivi huu ujasiri uliutoa wapi haswa, mbona hufanani na ndugu zako?" Mama akadakia "Hafananii na ndugu zake, anafanana na wewe, inamaana ushajisahau?" Mzee nae akawaka "Walau Mimi (Mshua) nilichukua mtu wa umri wangu" ( Unajua Bi mkubwa wangu nae amejaa jaa, japo ni mdogo kiumri kwa Baba). Mama nae akamjibu " Swala sio kuchukua wa umri wako, kwani wakati unanifata ulijuaga umri wangu, we siuliangalia kilichokuvutia?. Mwanao ashakuletea mkwe, inabidi umkubali tu"
Lile neno mkwe likaonekana kumkera Mzee. Unajua Mama yetu wala sio mtu wa kukaa na kitu moyoni. Muda huu anajibizana na Mzee, Yeye Mama alikua anatabasamu kabisa, Ila Mzee kakunja ndita. Battle ikatoka kwangu, ikahamishiwa kwa Mama, Mzee akaanza kumwambia Mama yeye ndio chanzo cha yote haya. Mshua akamwambia Mama "Nilikwambia tuzae mapema ukawa unasema tusubirie subirie, matokeo yake mtoto alikuwa anakulia kiunoni, huyu kazaliwa akiwa mtu mzima" Unajua katika familia yetu, watoto waliotangulia wote wamepishana miaka miwili miwili kasoro kaka yangu ninayemfuata amenizidi miaka 7. So alichokuwa anamaanisha Mzee ni kwamba hiyo miaka 7 yote ambayo walikuwa wanasubiria, Mimi nilikua naendelea kukua tu, dah [emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]
Anyway, msala ulikuja ukapoa tukaongea kistaarabu, Ila Mzee alikuwa so disappointed. Akawa ananiambia kuwa anastaili kujifunza toka kwangu maana Mimi ni legend, Nina namna zangu za kurun things ambazo hajawahi imagine.
Alinipa ushauri wake kuhusiana na mambo mbali mbali. Ila katika maongezi nae ndio nikagundua kuwa watu wetu wa karibu huwa wanaumizwa sana na mambo ya ajabu tunayofanya. Ile kauli ya mchuma janga ula na wa kwao, ilidhihirika mbele yangu. Sema kwavile ilishatokea hapakuwa na namna. Kutokana na hiki kisanga Mzee wangu ni mara chache sana kuniita jina langu,mara nyingi ananiita legend. Sipendagi akiniita hivyo, Ila Sina namna ya kumzuia, niliyataka. Mara chache chache huwa ananitania kuhusu yule Maza, now days anachukulia as a joke tu. Ananiambiaga nikiamua kuoa, nisisite kuwajulisha. Ila wao hawatonipush maana wanahofia nisije kuwafanyia surprise nyingine
** ********* ****** ***
Tukafunga huo ukurasa kuhusu mtoto na yule Maza. Ndio tukaanza kuongea kuhusu harakati zangu zingine. Alitaka kujua ilikuwaje tukakutana pale Magingo kwenye soko la tangawizi. Nilimuelezea kwa ufupi mizunguko yangu mpaka kufikia ile siku tunaonana, Yeye akiwa kama Boss, Mimi nikiwa kama kibarua..
Nadhani hayo Sina haja ya kuyaongelea hapa, maana nilishayaelezea kwa urefu sana kwenye ule Uzi safari yangu.
Nilizaliwa miaka kadhaa iliyopita. Katika familia ya watoto 7, mimi nilikuwa wa 6. Kama watoto walivyo, nilikuwa mtundu kiasi ila sio mtukutu. Nakumbuka nikiwa darasa la 5,niliitwa mbele na ticha nikafanye swali la hesabu. Nikafanya swali kwa mbwembwe, nilikuwa nasumbuliwa na mafua, kabla...
www.jamiiforums.com
** ** ***
Kwa sasa dogo alishatoka kwa Dada anaishi kwa Babu na Bibi yake. Yule Maza sina mawasiliano nae, japo kwasasa anaishi nyumbani kwake Kisarawe. Mpaka now inanipaga ukakasi nikiingia kwenye mahusiano kujielezea kuwa nina mtoto, hasa kuepuka swali la mama yake yuko wapi? Kwanini mliachana? Akirudi je? n.k
So, kwa kifupi sipo nae (maana najua ili swali litaulizwa tu). Dogo hajawahi kumuulizia Mama yake, labda kwavile walitengana akiwa mdogo sana so hakupataga ile bond ya Mama. Yule Maza nilishawahi kutana nae mara moja maeneo ya mawasiliano ubungo, tuliongea mawili matatu kuhusu mwanangu, then kila mmoja akaendelea na safari yake. Namba yake ninayo, pia anayo yangu japo hatuna mawasiliano.Huyu Maza hakuwahi kupata mtoto kabla ya huyu, nashangaa kwanini aliamua kumpeleka home kwetu, nilitarajia angemng'ang'ania kama dhahabu, but haikuwa hivyo.
Anyway, hiyo ndio ilikua story yangu. Until next time,
Legend kweli nimeukubali uandishi wako, japokuwa ukikataa shule ila hii story ukisoma unapata mpaka taswira ya tukio. Kweli nimecheka sana kwa umwamba wa mzee wako. Ikiwezekana tunga kitabu juu ya haya uliyotusimulia.
Dah!! Mwanangu we ni msimulizi mzuri kinyama [emoji23][emoji1787]
Umenikunbusha kisa kimoja hivi, enzi hizo nasoma Kurasini shule ya msingi, nilikuwa nina mwanangu kwao keko, dingi yake anapiga kazi bandari, dingi ni mtu fulani yupo simple, dingi kijana, shingoni ana nyororo ya silva, yule mzee kwa masimulizi ya rafiki yangu alikuwa hashiki fimbo kuchapa mtoto ni mabanzi tu, na hata kaka zake huwa anawagonga tu hachagui umri.
Sasa siku hiyo tumetoka kiskuli mie ubao unagonga akaniambia tupitie maskani tukabonyee kisha ndio nipande gari niende home(kigamboni)
Kufika kwao tunamkuta mzee yupo sebuleni kavimba kimtindo, maana hakunichangamkia kiviiile, kama kawaida yake maana alikuwa ananikubali kinyama jinsi ninavyogonga namba(hisabati) nikahisi kuna jambo, tukampa hi, tukaingia sehemu ya kubonyea.
Ghafla tunasikia kamzozo kuchungulia dingi anawaka kinyama, kumbe braza wake mkubwa alizingua siku hiyo. Sikuwahi kumuona yule mzee kavimba kama vile, japo habari zake nilikuwa nazisikia tu. Nikaona hili chezo halinipiti bure, mwanangu nae akawa kasimama tunachungulia kupitia kale kadirisha ka kupitishia msosi. Upande wa pili naona bimkubwa wake yupo anashuhudia mchezo.
Chezo likaanza mzee kaongea maneno mawili matatu, akaweka banzi la kwanza, akaweka banzi jingine, mabannzi mfululizo, braza akaona nitakufa akawa anaona nitakufa bure, akawa anapangua pangua, mzee akawa anapiga anauliza unataka kupigana, akakunja ngumi sasa yule braza sijui bangi nae akakunja, zikapigwa mbili 3, braza akabahatisha mbili, 3 zikawa zimeingia kwa dingi,nikaona leo mzee anaumbuka dingi hakulalamika akajipanga vizuri, ebana eeh, yule mzee vilimtoka vitu, alipiga ngumi mithili ya rashidi matumla kwenye ubora wake, braza mtu akatoa sauti hafifu mama nakufa, sijui alikula gumi la mbavu[emoji23][emoji1787]
Bimkubwa akaona eeh, asiniulie mwanangu, tumbo la uzazi nahisi lilimcheza kidogo[emoji23][emoji38]
Braza kupata upenyo nduki nene, maza analalamila baba nanii utakuja kuniulia mtoto, mzee likamtoka kubwa kum[emoji2959]ko, ina maana unampenda mwanao kuliko mimi, mbona aliponipiga ulikaa kimya[emoji23], mzee akatoka,
Mwanangu anasema jamaa hakurudi ndani ya siku 3, kuja karudi na baba yake mkubwa kusolve lile swala[emoji23]
Umeandika ili ufurahishe. Acha kushadadia story za wanaume, kwa hasle alizopitia huyu mwamba wewe hata robo hujafikia. " ni mwasilika" ndo takataka gani.
Mzee pamoja na kuwa anakupiga masumbwi ya nguvu. Ikitokea umerudisha, ombea asiumie, akiumia huo ni msala mwingine. Broh wetu wa kwanza aliambiwa ashakuwa mwanaume sasa, akaanzishe mji wake
Nikimkumbuka huyu mzee huwa nacheka tu, ila alikuwa mtu fulani smart saana, hata mkiongea pia unaona kabisa huyu mzee mtu poa, kumbe ana unyama mwingi mwaisa. [emoji23]
Nikikumbuka pale yule braza alipoita mama nakufa[emoji23][emoji1787]
Na pale alipompa [emoji2959]kubwa mkewe, na kumwambia anampenda mwanae, mbona ye alipogigwa hakusema kitu, huwa mbavu sina kabisa. [emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Legend kweli nimeukubali uandishi wako, japokuwa ukikataa shule ila hii story ukisoma unapata mpaka taswira ya tukio. Kweli nimecheka sana kwa umwamba wa mzee wako. Ikiwezekana tunga kitabu juu ya haya uliyotusimulia.
Legend kweli nimeukubali uandishi wako, japokuwa ukikataa shule ila hii story ukisoma unapata mpaka taswira ya tukio. Kweli nimecheka sana kwa umwamba wa mzee wako. Ikiwezekana tunga kitabu juu ya haya uliyotusimulia.
Umeandika ili ufurahishe. Acha kushadadia story za wanaume, kwa hasle alizopitia huyu mwamba wewe hata robo hujafikia. " ni mwasilika" ndo takataka gani.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.