Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 53,857
- 121,995
Dingswayo, nadhani kwa hapa tulipo, huna haja wala sababu ya kiutafuta CV yake, yeye tayari ameishajusfy uwezo wake kwenye hii tasnia ya habari kwa lever ya watu kumpongeza na kulipongeza Mwanahalisi, nadhani kwa hapa panatosha, CV ya nini tena ili hali kazi yake inafahamika?.Kuna ambaye ana CV ya huyu mwandishi wa habari? Nataka kujua, licha ya hulka yake, ni wapi ambapo amepata mafunzo ya kumpa ustadi huo.
Maadam kijana anafanya kazi nzuri, hakuna haja ya kumfuatilia mpaka ndani chumbani, ila kwa uzoefu wangu kwenye tasnia ya habari, haswa uendeshaji wa gazeti kama afanyavyo Kubenea, lazima nikiri, kama hakuna mtu ambaye Kubenea yuko nyuma yake, na hana upande fulani anaoufanyia kazi, then, nami najiunga kumpongeza kwa juhudi zote hizi na kulifikisha Mwanahalisi hapo lilipofika.