partey
Member
- Nov 16, 2020
- 50
- 56
Tusaidizane kutunza Roho zetu, Maisha yetu, tuombeane heri na mema katika Matumizi ya Vyombo vya moto, leo tuzungumzie "Gari".
Pata Elimu ya Mambo 10 ya Kuzingatia
Kabla na Wakati wa
Kuendesha Gari.
Kuendesha gari ni suala linalohitaji umakini na utulivu mkubwa, hasa pale unapoendesha gari umbali mrefu. Mara kwa mara kumeshuhudiwa ajali mbalimbali ambazo kimsingi zinatokana na madereva kutokuzingatia kanuni muhimu katika utumiaji wa vyombo vya usafiri.
Ili kuhakikisha usalama wako pamoja na watumiaji wengine wa barabara, yapo mambo kadhaa unayopaswa kuyazingatia kabla na
wakati wa kuendesha gari umbali mrefu.
1. #Kagua na andaa gari Kabla ya safari yoyote gari linahitaji kukaguliwa na kuandaliwa, hasa kabla ya safari ndefu. Kuna mambo kadhaa unayohitaji kuyakagua kwenye gari lako:
Kagua hali na ubora wa magurudumu.
Hakikisha magurudumu yamejaa vizuri na
hayajazeeka.
Kagua mafuta lainishi (oil).
Hakikisha gari
yako ina mafuta lainishi ya kutosha tena ya ubora unaotakiwa.
Kagua kiasi cha maji.
Maji? Ndiyo maji ni muhimu sana kwenye gari kwa ajili ya kupooza injini ya gari pamoja na kusafishia vioo.
Kagua utendajikazi wa injini. Hakikisha injini yako inafanya kazi vizuri.
Kagua sehemu nyingine za gari kama vile breki, kiongeza mwendo (accelerator),
usukani, taa, honi, viashiria (indicators),
n.k.
Hakikisha unalikagua gari lako vyema na
kuliandaa kwa ajili ya safari.
Unaweza pia
kumtumia mtaalamu wa magari ili akusaidie
kulikagua na kuliandaa kwa safari yako.
2. #Pumzika
Ili uweze kuendesha gari vyema wakati wa safari ndefu ni muhimu kupumzika kwa kiasi cha kutosha kabla na wakati wa safari.
Hakikisha kabla ya safari unapata muda wa kutosha wa kulala ili kuepusha kusinzia barabarani kunakoweza kusababisha ajali.
Unapokuwa barabarani unaweza pia kupumzika baada ya umbali fulani ili usichoke sana.
Kumbuka! Kupumzika uwapo safarini kutakuwezesha kupata nguvu zaidi na kutoa nafasi ya gari lako kupoa ili kuepusha ajali ya gari kuwaka moto.
3. #Fahamu_sheria na kanuni. Kuna kanuni zinazotawala matumizi ya barabara pamoja na vyombo vya usafiri. Ili kuepuka kuingia kwenye matatizo, hakikisha unafahamu vyema sheria za barabarani za eneo unalokwenda
Cont...
Pata Elimu ya Mambo 10 ya Kuzingatia
Kabla na Wakati wa
Kuendesha Gari.
Kuendesha gari ni suala linalohitaji umakini na utulivu mkubwa, hasa pale unapoendesha gari umbali mrefu. Mara kwa mara kumeshuhudiwa ajali mbalimbali ambazo kimsingi zinatokana na madereva kutokuzingatia kanuni muhimu katika utumiaji wa vyombo vya usafiri.
Ili kuhakikisha usalama wako pamoja na watumiaji wengine wa barabara, yapo mambo kadhaa unayopaswa kuyazingatia kabla na
wakati wa kuendesha gari umbali mrefu.
1. #Kagua na andaa gari Kabla ya safari yoyote gari linahitaji kukaguliwa na kuandaliwa, hasa kabla ya safari ndefu. Kuna mambo kadhaa unayohitaji kuyakagua kwenye gari lako:
Kagua hali na ubora wa magurudumu.
Hakikisha magurudumu yamejaa vizuri na
hayajazeeka.
Kagua mafuta lainishi (oil).
Hakikisha gari
yako ina mafuta lainishi ya kutosha tena ya ubora unaotakiwa.
Kagua kiasi cha maji.
Maji? Ndiyo maji ni muhimu sana kwenye gari kwa ajili ya kupooza injini ya gari pamoja na kusafishia vioo.
Kagua utendajikazi wa injini. Hakikisha injini yako inafanya kazi vizuri.
Kagua sehemu nyingine za gari kama vile breki, kiongeza mwendo (accelerator),
usukani, taa, honi, viashiria (indicators),
n.k.
Hakikisha unalikagua gari lako vyema na
kuliandaa kwa ajili ya safari.
Unaweza pia
kumtumia mtaalamu wa magari ili akusaidie
kulikagua na kuliandaa kwa safari yako.
2. #Pumzika
Ili uweze kuendesha gari vyema wakati wa safari ndefu ni muhimu kupumzika kwa kiasi cha kutosha kabla na wakati wa safari.
Hakikisha kabla ya safari unapata muda wa kutosha wa kulala ili kuepusha kusinzia barabarani kunakoweza kusababisha ajali.
Unapokuwa barabarani unaweza pia kupumzika baada ya umbali fulani ili usichoke sana.
Kumbuka! Kupumzika uwapo safarini kutakuwezesha kupata nguvu zaidi na kutoa nafasi ya gari lako kupoa ili kuepusha ajali ya gari kuwaka moto.
3. #Fahamu_sheria na kanuni. Kuna kanuni zinazotawala matumizi ya barabara pamoja na vyombo vya usafiri. Ili kuepuka kuingia kwenye matatizo, hakikisha unafahamu vyema sheria za barabarani za eneo unalokwenda
Cont...