Safari Sevens 2018, RFUEA Grounds Nairobi

pingli-nywee

JF-Expert Member
Joined
Sep 16, 2015
Posts
11,923
Reaction score
13,350
Safari7s imerudi RFUEA! Hafla hiyo ya raga, ya kila mwaka, itakuwa 9-11 Novemba. Wakenya jinyakulieni tiketi zenu mapema, hii kitu inakuwaga raha sio mchezo. Hivi ndivyo shughuli ya sherehe za kufunga mwaka huwa inaanza. https://www.kru.co.ke/safari7s/ Timu kumi na mbili, kikombe kimoja. Washindi wa Safari7s iliyopita, Shujaa watakuwepo. Timu ya kimataifa, Samurai pia watakuwepo bila kusahau Homeboyz wa Kenya pia. Hivi ndio kunaedaga.
 
Hao wachezaji wa raga huwa wanapatikana wapi? I mean huwa wanapewa malezi na chakula maalumu na Serikali? Kwa maana nikiwa Kenya sikuwahi kuona watu wakubwa namna hiyo, labda wanafanya kama Japani na Sumo, ambapo wana sumo hupewa chakula maalumu ili wawe wakubwa!

Sijawahi ona Mkenya mkubwa namna hiyo Wakenya wengi vidogo dooogo!
 
Mkikuyu njoo nikufunze mchezo wa raga. Pengine utabadilika uwe mkenya. Naona unapenda Kenya sana hadi ukajiita kiuk.Ama wewe ni umadhubuti. Jf haina captcha
 
Responsible adults drink responsibly!!! hahaha , I will not remember that
 
Acha pumba zako wewe, hamna cha chakula maalum wala nini, hawa ni wakenya wa kawaida tu. Alafu wakenya na watz nani ndio wadogo wadogo? Maanake Kenya kuna Nilotes wengi sana na kawaida yao huwa ni 6ft+.
 
Watz na dharau lol.
 
Responsible adults drink responsibly!!! hahaha , I will not remember that
Hahaha! [emoji1] Ndio maana huwa wanasema raga ni 'a hooligans' game played by gentlemen'. Tusker huwa zinauzwa kupindukia kwenye hafla kama hizi za raga lakini hutasikia hata siku moja habari za vurugu zozote zile kutoka kwa mashabik.
 
Tanzania ndio imejaa kamungunas. Watu wafupi wafupi tu.
 
Nigerians ask the same question how we make an international rugby 7's team..rugby is 2nd most played sport in KE high sch's which act like academies
 
Leo, siku ya kwanza ya Safari7s ilikuwa ni siku ya kina dada kumenyana katika mchuano wa Women Under-19. Timu ya hidden talent mwisho wa siku ilibuka mshindi kwenye fainali, kati ya timu kumi na mbili, baada ya kuigaragaza Huruma 28-0. Kesho mchuano unaanza rasmi na Samurai, timu ya kimataifa ambayo humo ndani kuna wachezaji wakenya, waganda, wasauz na wahong'kong', watamenyana na Red Wailer. Kisha baadaye Spain Vs. Uganda na Uganda Vs. Morans wa Kenya. Mchuano wa kina dada pia, kati ya timu nne(mbili za Kenya na mbili za Uganda), utakuwa unaendelea, mechi ya Kwanza ikiwa ya Kenya Lionesses Vs. Uganda Lady Cranes. Timu nane bora zitakazoibuka kwa wanaume, kati ya kumi na mbili, zitaendelea na mchuano huo jumapili.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…