Safari ya Watanzania Kushiriki "World Skateboarding Championships 2015" Afrika Kusini

Safari ya Watanzania Kushiriki "World Skateboarding Championships 2015" Afrika Kusini

silent_soldier

Senior Member
Joined
Aug 10, 2015
Posts
193
Reaction score
62
Natamani kukutana na Watanzania pamoja na marafiki mbalimbali nikiwa njiani.

Tarehe 30 Septemba natarajia kwenda Afrika Ya Kusini kwa Basi. Nitasafiri mpaka Msumbiji. Kutoka Msumbiji nitapanda basi la Intercape Moja kwa Moja mpaka Johannesburg, South Africa.

Kutoka JoBurg nitatumia gari mpaka Kimberley South Africa umbali wa Kilomita 427.

Naenda Afrika ya Kusini Kuhudhuria Mashindano ya Kimataifa ya Mchezo wa Skateboarding, World Skateboarding Championships 2015, The Kimberley Diamond Cup at Kumba Skate Plaza.

Mashindano haya yatafanyika kuanzia Tarehe 7 Oktoba Mpaka 10 Oktoba. Ni matarajio yangu kuwa nitakutana na watu wengi na kujenga urafiki.

Mwisho wa yote tunawaomba Watanzania mje kushuhudia Mashindano haya na kumuunga Mkono Mshiriki pekee atakayeiwakilisha Bendera ya 255 Tanzania.

Asanteni.
 
Mkuu, skateboarding ni kama ile inayochezwa pale Moroko? Tuwekee picha na wasifu kamili wa mwakilishi wetu tumfahamu...
 
Back
Top Bottom