Safari yangu ndefu ya Uigizaji

Safari yangu ndefu ya Uigizaji

Ngengemkenilomolomo

JF-Expert Member
Joined
Mar 21, 2015
Posts
270
Reaction score
450
Habar wakuu,

Katika maisha, kila mtu huishi kwa njia tofauti, na wengine huishi kwa kuamini kuwa ipo siku watatoka na kufanikiwa kimaisha kupitia kitu flani (live 4 ur dream).. Binafsi mimi napenda Sanaa na naamini kuwa ninacho kipaji kikubwa cha ku-act.

Nakumbuka nilijaribu sana kuwatext wasanii weng wa maigzo kupitia akaunti zao na fan blogs zao, nikiwaomba wanisaidie ili niweze kuonesha kipaji changu bila mafanikio.Siku moja nilimtext mdogo wake Odama na akaniahidi kuwa ataongea na dada ake lakini mpaka leo sijaona jibu lolote kutoka kwake!

Kila siku najipa moyo na napenda siku moja niwe kama au zaid ya Role Model wangu ambae kwa sasa ni marehemu (R.I.P Kanumba), na siku moja napenda kusimama katka muvi moja na Jaden Smith.

Naomba Mungu aniongoze katka kutimiza ndoto yangu, na kitu kinachonipa imani na nguvu ya kutokata tamaa ni wimbo wa R. Kelly - I believe I can fly..

Kwa yeyote anaeweza kunifikisha sehemu ambayo naamini naweza nikatmiza ndoto zangu, anakarbishwa kwa maoni, ushauri au msaada.

Asante..
 
Seeker Dee

Ni vizuri sana kuamini katika ndoto ya maisha yako, nakushauri tu usiache kupambana, endelea kuweka juhudi katika kila unalolifanya, hata hao mastaa unaowaona wanaishi maisha mazuri uku kila mtu akiwasifia na kuwaona mungu watu, na wenyewe walipitia kama wewe au pengine zaidi, Cha muhimu ni uvumilivu na kufanya kazi kwa bidii kuhakikisha unatimiza ndoto zako, ni kosa kubwa sana kuacha ndoto ya maisha yako ipoteee, pia mtangulize mungu utafanikiwa tu ndugu.
 
Last edited by a moderator:
Hongera kwa kipaji
Ushauri ungeenda kujiunga na kikundi cha sanaa ya uigizaji kilichopo karibu nawewe naona itakuwa mwanzo mzuri wa kipaji chako kukua zaidiii
 
Umeisha fanya jitihada gani mpaka sasa,zaidi ya kutext wasanii wengine?
 
Una ndoto za kufika mbali na ku act hadi na jaden smith..halafu role model wako kanumba! Hujafanya juhudi ya kusoma sanaa zaid ya kumtafuta mdogo wake odama!!!..ama kweli kua uyaone!
 
Back
Top Bottom