Safari yangu ya kwenda Bulombola ilivyonikutanisha na Mrembo wa Kaskazini

Tajiri Mapesa

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2020
Posts
707
Reaction score
728
Habari za leo wanaJamiiForums, leo nimeamua kufunguka na kutoa kisa changu cha kweli kilicho nitokea mwaka 2013, basi mambo yalikua hivi;

Ilikuwa ni mwezi wa sita mwaka 2013, nikiwa nipo nyumbani nikasikia tetesi kwamba majina ya wa wanafunzi walio hitimu kidato cha sita yametoka. Lkn sikujua ni kwaajili ya nini, ilinibidi niulize vzuri, kumbe yalikua ni majina ya wanafunzi walio chaguliwa kwenda jeshini,

Mapigo ya moyo yalianza kwenda kasi huku nikiomba Jina langu lisiwemo maana niliskia jeshini kuna mateso sana.

Nilichukua simu yangu ya tekno ya batani yenye kamshale nkaingia kwenye mtandao wa gugo nkapakua majina, ghafura moyo wangu ulishatuka paa, mara baada ya kuliona Jina langu. Nilikua nimechaguliwa Kambi ya Burombola kigoma 821 KJ, KJ yaan kikosi cha jeshi. Tangazo lilisema tunatakiwa kuripoti kambini kabla ya tarehe 24 mwezi sita

Kipindi hicho nilikua nafanya kazi ya uwalimu katika shule moja ya sekondari iliyopo mkoani Mbeya. Mimi ndiye nilikuwa mwalimu wa fizikia wa kutegemewa katika shule ile.

Nliogopa sana lkn sikua na jinsi maana mkuu wa jesh alitangaza kuwa ambaye hata huzuria atachukuliwa hatua za kisheria. Ntafanyeje mimi nilibaki na mawazo kichwani, nikasema hamna shida acha tu niende. Ilinibidi niache kazi na kuanza kujipanga ili kwenda jeshini

Nilianza kufanya mazoezi ya kukimbia nyumbani ili kujiweka tayari kwaajili ya jeshi. Nilifanya mazoezi ya pushapu na kukimbia, mapenzi ya nyoka pamoja na zoezi la kubeba dunia.

Saa moja asubuhi nilipanda basi la kosta mpaka Mbeya mjini. Nkafika stend kuu nikachukua ticket ya kwenda sumbawanga, asubuhi sana basi liliondoka mbeya kuelekea sumbawanga tukafka sumbawanga mida ya saa sita mchana. Nlikua nakuogopa sana sumbawanga, watu walikua wakisimulia kuwa kuna wachawi wengi alafu ni kubaya. kumbe ni kuzur kabisa alafu ni mjini.



Mida ya jioni, nilichukua chumba cha kulala sumbawanga bahati nzuri nkakutana na wenzangu wengine gesti house nao pia walikuwa wanaenda jeshini, niliwagundua kwa kuwa walikuwa wamenyoa vipara, nkasema hapa bora tuwe wengi. Usiku nikiwa kitandani nilikuwa makini kuangalia juu ya dari na kwenye kona za chumba, maana niliogopa kukabwa. Baadaye usingizi ulinichukua, nilikuja kushituka asubuhi, kwa kweli usiku nililala usingizi mzuri sana.

Asubuhi sana mida ya saa 11 tuliondoka sumbawanga kwa basi kuelekea mpanda, tukafka mpanda saa nane mchana maana ni mbali, lkn nlikua naskia waziri mkuu anatokea mpanda ananyumba, kweli nilitmani kupaona kwake, ilinibidi niende mpaka kwake, alikuwa na wake zake wengine pale japo yeye alikua anaish Dar, nyumban kwake palikua ni pa kawaida sana. Skutegemea kama ile nyumba ni ya waziri kumbe mawaziri nao huwa wanaishi maisha ya kawaida kabisa

Mida ya saa 11 jioni nilienda stendi kukata tiketi, ya kwenda kigoma. Kipind kile gari ya kwenda kigoma ilikuwa ni moja tu, inaenda kigoma j3 na j5 bac ukichelewa ndio bas.

Kwel siku ile nilikuta basi limekwisha jaa, ila waliniahidi inabidi nisubiri mpaka kesho yake asubuhi sana, walinieleza tukiwapita polisi ndipo nitapanda maana walikuwa wanakataza kujaza watu

Asubuhi niliamka kwa kuchelewa sana kwani basi lilikuwa limekwisha niacha na basi la kwenda kigoma lilikua ndio hilo tu na hiyo ndio ilikua ni tarehe ya kuripoti kambini

Basi basi lilikua limesha niacha, nilibaki stendi skua na cha kufanya nkaanza kulia nitafanya nini, ndipo nilipo mwomba bodaboda anisaidie kulifukuzia basi, nilitoa noti mbili za elfu 10 nkamlipa akaniambia tutalifukuzia

Safari ya kulifukuzia basi ilianza, hiyo ilikua ni saa moja asubuhi, barabara ya mpanda mpaka kigoma ni vumbi jingi, mimi nilipanda nyuma bodaboda ilikua inakimbia kwa mwendo wa kasi sana, tuliendesha umbali wa kama km 12 tukafanikiwa kulikuta basi likasimama ndipo nikapata

Ndani ya basi hamkua na siti hivyo nilisimama watu wote walikua wamechafuka sababu ya vumbi, nilipata rafki kwenye basi tukawa tunapiga naye stori za jeshi. Basi lilifika uvinza nikiwa njiani niliuona mto magadi wenye maji ya Chumvi,

Tulishuka uvinza tukala chakula, tukaendelea na safari, tulifka kigoma mjini saa 12 jioni sana. Sikuwai fika kigoma mjini ndio ilikua mara yangu ya kwanza ni pa kawaida sana utafkiri sio mkoa. Mida ya saa 12 na 1/2 jion nilitafuta daladala ya kwenda Bulombola nkaipata nkapanda Daladala ilikua inaendeshwa kwa kasi sana, utadhani inaendeshwa na mwanajeshi, nikiwa njiani nkaliona ziwa Tanganyika karibu na barabara,

Mara tu tukashushiwa kwenye geti la Kambi. Kweli tulishuka wengi hadi wazungu wachina na wahindi pia walishuka wakiwa na majiko yao ya stove kwaajili ya kupikia.

Itaendelea……



 
Dah bro umenikumbusha mbali sana hapo burombola nakumbuka kuna mtoto nilitokea kumpenda sana sema katika michakato ya kumtemea madini ilikuwa ngumu sababu ya maovyoovyo siku moja tuko kwenye six week nikammendea ile tumelala nikamla mate nilishangaa sana alirespond positively mpk nikaanza kupima oil bahati mbaya makamanda wakapiga filimbi tuamke dah ile moment sitasahau kumbe mtoto naye alikuwa na nyegez zake tu dah
 
Hivi huu ujinga wa itaendelea unawsaidia nn? Why usiandike mkasa wako umalize ndo upost? Au sio real story mnaubuni so mwendeleze unatunga bado
Eti ndiyo season...tehtehteh
 
Hii post inanikumbusha mbali wakati huo Nina full kombati npo kwenye mashamba ya mpunga na silaha yangu nipo guard zamu yangu hapo napigwa na baridi kwelikweli mpaka natoa kamasi puani kwenye mfuko wa koti kuna picha ya mtoto nilipiga nae naichomoa namuuangalia nakumbuka good memory napata morali nasema yes one day nitarudi uraiani nikuone ..


I miss her a lot


82_? KJ




Sent using Jamii Forums mobile app
 
Funguka bibie

Ma service man

Na ma privite

Walikuwa wanakusumbua kuruta wa mungu ?

Au ulikuwa unadosolewa kwa kua ulizidi kuwa nanga

Sent using Jamii Forums mobile app
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] Nimeishia kucheka tyuuuh lol, yaan weeee khaaaaah

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…