moodykabwe
JF-Expert Member
- Aug 16, 2015
- 625
- 602
Akiwa kama Mtendaji Mkuu wa Klabu ya Simba Bidada, Mrembo Barbara ameweka nadhiri ya kufanya matembezi ya hiari ili kuimaliza Afrika nzima.
Naam, mara ya kwanza alianza kwa kuwaminisha waajiri wake na mashabiki wa Simba kuwa safari zake ni za kujenga uhusiano na klabu nyingine.
Kujenga uhusiano si jambo mbaya ila unajenga uhusiano na ushirikiano katika nyanja zipi?
Kinachoonekana na kuendelea katika ziara hizi ni kuzionesha klabu nyiingine Tanzania na kuzitambia, walakini huu ni unafiki na Simba hawajui wanachokitafuta bali kugombanisha watu.
Siku si nyingi Bidada huyo alionekana yupo bize na viongozi wa Al-Ahly ya Misri kwa madai ya kufungua ukurasa wa kushirikiana.
Kitu cha ajabu kabisa, kabla ya mwezi kupita akaonekana tena yupo na viongozi wa Zamalek pia ya nchini Misri nako ikaelezwa kuwa anajenga uhusiano. Inachekesha sana.
Nani asiyejua upinzani wa Al-Ahly na Zamalek nchini Misri? Hizi timu mbili ni zaidi ya mahasimu katika soka na ushindani wa kiuchumi.
Sasa leo kwenda kukaa katikati yao wote wiwili na kupiga picha ni kuonesha kuwa ni kwa namna gani amekosa ajenda na kutokujua nini anakitafuta.
Ni sawa leo uwe na uhusiano na taifa la Palestina huku pia ni swahiba wa Israel, dunia itakushangaa na wataalamu wa diplomasia wataanza kukuombea.
Kilichopo kwa Bidada huyu ni kukosa ajenda, kushindwa kujua Simba inahitaji nini kwa wakati gani na kutoka kwa nani.
Pia ikumbukwe gharama zote za safari yake zinagharamiwa na Mo (Mohammed Dewji), ambaye anaweka kwenye kitabu chake ili siku Tume ya Ushindani FCC ikicharuka na kutengua 'ndoa' ya Simba na Mo nazo ziwe miongoni mwa gharama ambazo uongozi wa Msimbazi watatakiwa kuzilipa.
Unaweza kujiuliza tangu ameanza kuzunguka kama pia Afrika nzima kipi kimeongezeka kwa Simba?
Unaweza kujibu pengine matokeo mazuri ya klabu bingwa Afrika hatua ya makundi na hapo utajiuliza mbona wameendelea kutumia michezo ileile waliyotumia wakati bidada hajajiriwa?
Wanasimba endeleeni kufurahia 'selfie' za Bidada wenu na sasa ameingia hadi kwenye viongozi wa CAF pasipo kuchagua upande... anapuyanga tu.
Akirudi Bongo mwambieni wataalamu wa Diplomasia wanasema unapotamani kujenga uhusiano kuna hatua zake ikiwemo kujua vipaumbele vyako na kuchagua upande sio kupuyanga kama unacheza muziki wa Reggee.
Za ndanindani, inasemekana hata Shambuliaji la msimu, jitu la miraba minene, mtambo wa mabao, Senior Straiker Junior Lokosa huyu bibie Barbara ndo alikuja na jina lake kutokea kwenye matembezi yake huko.
Kiko wapi?
Naam, mara ya kwanza alianza kwa kuwaminisha waajiri wake na mashabiki wa Simba kuwa safari zake ni za kujenga uhusiano na klabu nyingine.
Kujenga uhusiano si jambo mbaya ila unajenga uhusiano na ushirikiano katika nyanja zipi?
Kinachoonekana na kuendelea katika ziara hizi ni kuzionesha klabu nyiingine Tanzania na kuzitambia, walakini huu ni unafiki na Simba hawajui wanachokitafuta bali kugombanisha watu.
Siku si nyingi Bidada huyo alionekana yupo bize na viongozi wa Al-Ahly ya Misri kwa madai ya kufungua ukurasa wa kushirikiana.
Kitu cha ajabu kabisa, kabla ya mwezi kupita akaonekana tena yupo na viongozi wa Zamalek pia ya nchini Misri nako ikaelezwa kuwa anajenga uhusiano. Inachekesha sana.
Nani asiyejua upinzani wa Al-Ahly na Zamalek nchini Misri? Hizi timu mbili ni zaidi ya mahasimu katika soka na ushindani wa kiuchumi.
Sasa leo kwenda kukaa katikati yao wote wiwili na kupiga picha ni kuonesha kuwa ni kwa namna gani amekosa ajenda na kutokujua nini anakitafuta.
Ni sawa leo uwe na uhusiano na taifa la Palestina huku pia ni swahiba wa Israel, dunia itakushangaa na wataalamu wa diplomasia wataanza kukuombea.
Kilichopo kwa Bidada huyu ni kukosa ajenda, kushindwa kujua Simba inahitaji nini kwa wakati gani na kutoka kwa nani.
Pia ikumbukwe gharama zote za safari yake zinagharamiwa na Mo (Mohammed Dewji), ambaye anaweka kwenye kitabu chake ili siku Tume ya Ushindani FCC ikicharuka na kutengua 'ndoa' ya Simba na Mo nazo ziwe miongoni mwa gharama ambazo uongozi wa Msimbazi watatakiwa kuzilipa.
Unaweza kujiuliza tangu ameanza kuzunguka kama pia Afrika nzima kipi kimeongezeka kwa Simba?
Unaweza kujibu pengine matokeo mazuri ya klabu bingwa Afrika hatua ya makundi na hapo utajiuliza mbona wameendelea kutumia michezo ileile waliyotumia wakati bidada hajajiriwa?
Wanasimba endeleeni kufurahia 'selfie' za Bidada wenu na sasa ameingia hadi kwenye viongozi wa CAF pasipo kuchagua upande... anapuyanga tu.
Akirudi Bongo mwambieni wataalamu wa Diplomasia wanasema unapotamani kujenga uhusiano kuna hatua zake ikiwemo kujua vipaumbele vyako na kuchagua upande sio kupuyanga kama unacheza muziki wa Reggee.
Za ndanindani, inasemekana hata Shambuliaji la msimu, jitu la miraba minene, mtambo wa mabao, Senior Straiker Junior Lokosa huyu bibie Barbara ndo alikuja na jina lake kutokea kwenye matembezi yake huko.
Kiko wapi?