Saida Karoli: Meneja wangu amemtapeli Diamond mamilioni, mi nilimpa wimbo bure

Kwan wimbo ni mali ya saida au mali ya meneja
 

Wewe ndio hata uelewi wapi niliposema kuwa lazima mkutane studio ndio mfanye wimbo pamoja?!

Na sio lazima Diamond akutane na Saida...Diamond ana viongozi wanne Ricardo Momo,Sallam,Tale na Fella unataka kusema Saida alivyokwenda Studio kutia sauti yake viongozi wote hawa wa Diamond hawakuwepo siku hiyo?

Maana unachotengeneza wewe ionekane kuwa Saida hakuwa anajua lolote ili mumpe kesi meneja wake kumbe na nyie mnausika kumpiga changa dada wa watu.

Jibuni hoja hizo hela alizosema Diamond alimpa Saida alimpa saida yupi na hizo 25% ambazo zinakwenda kwa mama ni mama yupi au mama ake Diamond?

Saida anazidi kuweka mambo hadharani...na umwambie baba ako Diamond tabia za kuongeza ongeza sifuri sio fresh maana sasa anaelekea kuumbuka na kuonekana tapeli.
 
Kwan wimbo ni mali ya saida au mali ya meneja
Sijui mkataba wao ukoje maana inawezekana na wimbo ukawa mali ya producer pia.

ninachosema ni kuwa Diamond alisema kampa hela Saida alafu wakamalizana na Meneja wake sasa Saida kaja kuweka wazi kuwa Yeye alitoa wimbo bure na diamond alimpa hela meneja wake na sio yeye

Sasa swala lipo hivi kwanini Diamond na uongozi wake walidanganya?
 
Acha kukurupuka, kumbe hata mwenye hakimiliki ya wimbo humjui alafu unaleta porojo?
Diamond amefuata taratibu zote zilizotakiwa na jamaa yuko makini sana
Story zako za kuongeza sifuri kawasimylie watoto wenzio wa instagram
 
Nipeni namba ya maneger nina dada yangu anatafuta mchumba mwenye angalau 20milion kwenye account yake ya bank. . maana kipindi hiki ni kigumu kiuchumi ila naona maneger kavuka kiwango.
 
Beat ni mali ya producer na wala sio saida wala meneja.....
 
Mm nakumbuka alipokuw anaulizwa icho alisema alienda kuonana na aliyekuwa meneja wa saida karoli ndo wakapatana kuwa inabidi watoe asilimia 25 za publidhing na wakatoa kiasi kazaa cha hela kwa huyo meneja maana ndo mliki halali wa uwo wimbo.....lakini hakusema kuwa wameonana na saida mbona unajaribu kubadilisha ukweli kuwa uwongo punguza chuki ndo utapanuka kimawazo
 
Na nakumbuka kuna interview moja domo aliulizwa kuhusu hilo swala la kufaidika saida na iyo project ya Salome...domo akasema wenyewe wameonana na uongozi wa saida ule wa zamani coz ndo wamiliki halali kisheria ndo aliyewaruhusu kutoa iyo ngoma na kuna kiasi kazaa cha hela ilibidi walipe kwa huyo meneja muta ajili ya publishing na hakusema kuwa izo hela kamlipa saida karoli....cc mzaramo acha kupotosha watu ingia YouTube usikilize upya ukiona sehem kasema iyo percent walimpa saida nitag
 

Elimu ndogo ya Saida ndio chanzo cha yote haya. WCB wangetumia akili ya busara tu, wakamlipa chochote huyu mama. Kama alivyoongea mwenyewe, anaamini akitoa wimbo wake kwa msanii mwingine itasaidia ainuke, ni mtazamo wake kwa elimu aliyonayo. Ukijua hili, unampa tu kitu kidogo kama ruzuku maana mwisho wa siku wimbo ni wake na wewe umeuchakachua kwa style yako. Wasanii na meneja wake wa zamani wasitumie advantage ya ku benefit kwa mgongo wake only kwa sababu elimu yake ni ndogo. This is not fair kabisa
 
Huyo meneja aitwa Felician Muta, namchukia sana huyo mzee tangu alivyomwingiza kingi na kumsainisha saida mikataba ya Mangungo huku akitumia fursa ya kutokujua kusoma wala kuandika kwa Saida hapo mwanzoni.
Huyo Muta (FM) alikua anamiliki Silent Inn na FM Music band (kuna waliostukaga na kujitoa wakaanzisha FM Academia. Nadhani ndio ngwasuma ya sasa).

Pia alikua anamiliki FM Music Studio akirekodi kanda za bolingo sana. Baadae niliskia kaokoka baada ya sailentini kuvunjwa.

Hakuna alichoanzisha ambacho haikua magumashi. Labda hiyo studio ila sina hakika km alikua na rights kurekodi zile kanda.
 
Hilo ungemwambia FM maana kamnyoosha Saida tangu zamani sana. Saida aliambulia Mark 2 na kupangushiwa nyumba Sinza. Wahaya wengi kwa kupenda dhuluma hawajambo (in the name of mikataba).

Yuko mwingine nae kaingiza wabongo wote mkenge kalamba bn70 kagawa hapo km 30 saa hz kila mtu mamlakani kalowa hawezi kumwambia kitu. Hadi msaidizi wa kadinali kapewa rushwa na kabeba.
 
Wapi niliposema kuwa walionana na Saida?
 
Acha kukurupuka, kumbe hata mwenye hakimiliki ya wimbo humjui alafu unaleta porojo?
Diamond amefuata taratibu zote zilizotakiwa na jamaa yuko makini sana
Story zako za kuongeza sifuri kawasimylie watoto wenzio wa instagram
Tumeshamaliza hapa nashukuru Umeelewa.Ngoja niendelee kufafanulia wengine ambao bado wapo gizani kama ulivyokuwa wewe.
 
Mbona Ali kiba alitudanganya kasoma mpaka chuo alafu kingereza hajui, uwongo ni sehemu moja wapo ya kunogesha story
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…