Made in Tanzania:
condom za tanzania zinapasuka kama maputo kwanini nisitumie condom za nje
cement ya tanzania zinaangusha majengo we jengo kifusi kimekuwa mchanga mchanga kwanini nisinunue za nje
juice za bakhresa zina ma uchafu chafu kesi zake zimeletwa hapa mara nyingi nadhan tumeshuhudia kwanini nisinywe TANG
makochi na fanicha ziko pale keko barabarani zimepangwa vumbi lote la barabarani liaishia pale unanunua kochi jeupe lakini ukiliangalia ni jeusi kwanini nisiende kwa Mchina
suti unashonesha ila unapata suti baada ya kumweka fundi polisi ndio anamalizia nguo yako kwanini nisinunue Gucci
viatu vile vya mbeya design mbovu kiatu kimekaa kama mkate bwana na sio ngozi kwanini nisinunue viatu vya Italy
Sabuni zinazotengenezwa na wajasiliamali wetu hazikawii kuchubua mikono kwanini nisinunue Dettol
ARV mnawatengenezea feki
Bia Bingwa ulikuwa ukinywa lazima uharishe kwanini watu wasinywe heinekeen
Hicho kigari cha VETA ni SUZUKI, not made in Tanzania, ni Modified......oh,no!....Asembled....aah hapana...Sjui nini in Tanzania, la Chini ni IVECO, Bandikwad Nembo ya Nyumbu in Tanzania!
Ata hizi bidhaa za nje zinazoingia zinachangia sana pato la taifa zikisimamiwa vizuri ndio maana tra wanasema wanakusanya 600ml kwa siku chache tu...huu ni ushuru wa bidhaa za nje,ukiingiza cement kwa mfano Tbs wanatakiwa kupima ubora na gharama ya kupima ni 350,000/tsh hachilia mbali ushuru wa tra na gharama za port...kama tax ikisimamiwa vizuri ni sawa tu bidhaa za nje zije watu wapate ajira na tra wakusanye mapato..nchi nyingi zinakua kwa kukusanya ushuru na kuutumia vizuri,tukitengeneza bidhaa nzuri zenye ushindani si lazima tutegemee soko la ndani twaweza ku export nje..india,pakistan,bangladesh,nepal ni nchi zinazoongoza kwa kunywa chai yaani hawa jamaa wanakuywa sana chai na Kenya wame monopolise soko lao la chai wanapenda sana chai ya kenya,tutengeneze bidhaa nzuri zitapata soko la ndani na nje...ukienda Geita mananasi yanaoza wakati tunakuywa juice za nchi zisizona mananasi..njombe nyanya zinaoza ndoo moja tsh 500 tungekuwa na kiwanda kizuri cha tomato ketchap zenye ubora mzuri tungeuza nje na ndani ya nchi...tulikuwa na kiwanda cha dabaga nakikumbuka sana pale iringa lakini hakuna mazingira mazuri kwa viwanda maana umeme ni wa kubahatisha sana...tutengeneze bidhaa bora soko la ndani na nje ni kubwa sana
Nitaanza kununua bidhaa za Tz pale ambapo jamaa zangu wa TBS na TFDA wakianza kuwa serious.
Ila niko na mkakati binafsi jana tuu nilitoka kataa maziwa packed yale toka Zambia nikanunua ya ASAS.
Kwa bidhaa ambazo nina uhakika na ubora wake huwa nanunua sana
Unaweza oma vyema comment yangu ukaielewa?Bahati nzuri iko kwa kiswahili nilizani ni rahisi kuielewaUsiniambie hata MANANASI, Maembe, Nyanya (made in Tanzania) nk unataka hadi TBS na TFDA waje wakague ndipo ule na vinginevyo utanunua nyanya na Juice za Makopo. Kama hao ndiyo wanakagua bidhaa, basi hata za nje ni mbovu na huko ndiyo hatari zaidi maana watu wanaokota bidhaa zinazotakiwa kutupwa na wanakuja kubadilisha tarehe na kuuza.
Hata huyu Mwenyekiti sijui wa CCM aliyekamatwa na bidhaa feki za kutengenezea madawa ya kurefusha maisha kwa waathirika wa ukimwi, hizo bidhaa zilikuwa zimetoka South Africa. Mlimani City mwanzo walisifika sana hadi watu walipogundua kuwa wanauza bidhaa zilishokwisha muda wake kutoka South Africa.
TBS na TFDA ndiyo wakaguzi wa bidhaa zinazotoka nje pia. Ni hawa TBS walikuwa wakikagua na kutoa Kibali cha matari ya magari kutoka nje na matairi kibao yamepasuka na kuuwa Watanzania wengi tu kwenye ajali za Mabasi. Au umesahau? Haya bana, waaamini tu hao TBS na TFDA kwa ukakuzi wao wa bidhaa za nje kuwa huko wanafanya kazi kwa ufanisi ila za ndani ndiyo wanazembea.
Nitaanza kununua bidhaa za Tz pale ambapo jamaa zangu wa TBS na TFDA wakianza kuwa serious.
Unaweza oma vyema comment yangu ukaielewa?Bahati nzuri iko kwa kiswahili nilizani ni rahisi kuielewa
condom za tanzania zinapasuka kama maputo kwanini nisitumie condom za nje
cement ya tanzania zinaangusha majengo we jengo kifusi kimekuwa mchanga mchanga kwanini nisinunue za nje
juice za bakhresa zina ma uchafu chafu kesi zake zimeletwa hapa mara nyingi nadhan tumeshuhudia kwanini nisinywe TANG
makochi na fanicha ziko pale keko barabarani zimepangwa vumbi lote la barabarani liaishia pale unanunua kochi jeupe lakini ukiliangalia ni jeusi kwanini nisiende kwa Mchina
suti unashonesha ila unapata suti baada ya kumweka fundi polisi ndio anamalizia nguo yako kwanini nisinunue Gucci
viatu vile vya mbeya design mbovu kiatu kimekaa kama mkate bwana na sio ngozi kwanini nisinunue viatu vya Italy
Sabuni zinazotengenezwa na wajasiliamali wetu hazikawii kuchubua mikono kwanini nisinunue Dettol
ARV mnawatengenezea feki
Bia Bingwa ulikuwa ukinywa lazima uharishe kwanini watu wasinywe heinekeen
Ndugu Watanzania,
MADE IN TANZANIA KWANZA.
[/CENTER]
Mimi huwa na nunua Africafe Amazon mara kwa mara na wakati mwingine bahatisha chaibora kwa supplier, kwakweli nafahari sana na vitu vya kwetu.
Uzuri nilisha wai kuwa mwalimu so nimeelewa wapi tunapishana kwa kiswahili chepesi
TBS na TFDA wakiwa serious na ukaguzi pia na utoaji wa bidhaa such that tukawa na bidhaa genuine sokoni apo ndipo nitakuwa nanunua bidhaa bse right now 30% ya bidhaa sokoni ni feki this is general za nje na ndani.
Mfano kuna jamaa wanatengeneza the so called nondo unaweza kunja ata kwa mkono yes made in Tz but poor quality, wachina wanafyatua bati kule vingunguti na wanafoji mihuri na are cheaply sold in the market yes made in Tanzania but poor quality.Otherwise kwa vitu ambavyo nina ufahamu navyo ambavyo sihitaji TBS au TFDA huwa nanunua hasa vyakula na matunda ya asili au products ambazo nilishawai tumia au shauliwa na wataalamu.
Uzuri wangu kabla sijanunua kitu ni lazima niwaconsult wahusika au wadau wa iyo item au waliowai tumia bse niko na friends from almost all the fields based on the my 20 years of study plus 10 years of work.
jamani kuhusu kuhusu nyanya za packet-mie ni mnunuzi mkubwa! sababu-kila wakati umeme unakatka manyanya yanaozaoza frijini na muda wa kwenda sokoni kila wakati sinao so kwanini nisinunue nyanya za pakistan...??? Ili kampeni hii ifanikiwe ni kila mtu aplay part yake
Mkuu mada yako ina maana sana , ila nadhani kuna mambo serikali inatakiwa iyafanye kwanza (hasa kwenye kodi na kusimamia ubora ),ndipo watu wataanza kufikiria hizo home made.La sivyo tutalaumiana bure. Huwezi ,kwa akili ya kawaida ukanunua cement ya dar kwa 15000 wakati kuna cement bora tu kutoka pakistan kwa 12500.
Ni kweli nyanya zinaharibika ila siyo kiasi hicho. Zinaweza kuishi hata siku nne bila kuharibika.
Kama unanunua Nyanya za Makopo na kuzitumia sana na tena kutoka Pakistan na wakaguzi wenyewe ndiyo hayo TFDA, basi jiandae siku moja uje uambiwe una KANSA. Vyakula vya Makopo vikimbieni kama Ukoma na utumie tu pale kuna ULAZIMA na huna jinsi nyingine ya kufanya. Mngelijua mnalishwa nini kwenye hayo Makopo, haki ya nani ungelielewa ninasema nini na ungelihakikisha hata saa 12 asubuhi unawahi kwanza sokoni kununua vyakula Fresh na matunda na ndiyo unaenda kazini.
Vyakula vya Makopo? Kila la kheri ila nakuombea Mungu akuepushe na madhara yake kwa uchafu unaowekwa humo ndani.
Sijakataa sikonge ila hali ndo inafanya kuwa hivyo, ila unajua nyanya na mbogamboga zinavyolimwa mwanawane, mie nimeshashuhudia hizi mbogamboga za DAR wanaweka ile sijui mnaita chumvi chumvi tena niliwauliza wakaniambia inakuza haraka sasa wataalamu wa killimo nisaidieni katika hili, sijui kama kuna atakaepona na hiyo saratani
Chumvi chumvi ni mbolea Mwanawane. Hata Mtwara ndiyo wanataka kujenga kiwanda cha kutengenezea mbolea.
Zimekuwa zikitumika kwa miaka mingi sana. Nafikiri huwa zipo pale ili kuongezea madini yanayopungua kwenye ardhi. Haina madhara kwa binadamu na kwa ardhi kwa sababu ni vitu ambavyo siku zote zipo ardhini ila ni kidogo. Kwa uzalishaji wa mahidi na tumbaku, inatumika sana kwa mikoa kama huku kwetu Tabora. Kuna ya CHANGARAWE na CHUMVI CHUMVI. Ngoja wataalamu wa kilimo waje watakuelezea zaidi.
Naona Mwanawane wewe mtoto wa mjini maana hata mbolea ya Chumvi chumvi huifahamu? Hata Ulaya wanazitumia sana hizi mbolea na nyingine nyingi kama za kuuwa magugu (Siyo nzuri kwa ardhi na binadamu), kuuwa wadudu nk.