Saido Ntibanzokiza afunguka ya Moyoni! Inasikitisha

Saido Ntibanzokiza afunguka ya Moyoni! Inasikitisha

Kipindi hicho nikiwa nacheza mpira ligi za mchangani tu ilikuwa ligi ya mwambambe aise tuliletewa maji ya maiti tuoge walahi na jamaa yangu tulikimbia kama hatuna akili vizuriii maana tulikimbia peku.
Km kuoga maji ya maiti ulikimbia,je kula yai viza mbona ungezimia?Kuna stori zingne za vijiwen lakin mtu anaziamin
 
"Nimezunguka Nchi Nyingi Kisoka Ila Yanga Ndio Timu Iliyonishangaza Kimfumo, Sizani Kama Ni Sahihi Afisa Uhamasishaji Kupanga Kikosi Yani Amekuwa Na Nguvu Kuliko Kocha, Binafsi Sijavutiwa Kubaki Hapa.

Mimi ni kijana wa kiislam ni nguvu kuniambia nile yai viza ili timu ishinde na hii ndio chanzo cha mgogoro na viongozi. Hapa tanzania giant ni mmoja tu simba sc kutokana na mfumo wake bora wa uendeshaji.

Tuwaeleze mashabiki ukweli kuliko kuwaficha na kujikuta wanajenga chuki na wachezaji. Kaze aliambia alale kwenye sakafu wiki moja kuelekea derby ya mzunguko wa kwanza pia aligoma ndio chanzo cha kuchukiwa na baadhi ya viongozi.

Natamani kucheza Azam maana ndio timu ninayoona itanipendeza. Kocha mpya nimejitahidi kuongea nae japo nilishindwa kumueleza yaliyo nyuma ya pazia maana nilikuwa nimesimamiwa na viongozi ambao ni chanzo cha mgogoro"

Saido Ntibazonkiza (akihojiwa na mwandishi wa burundi Nuhu Kwizela.


Wacha weeeee
 
Kuna vitu vya kujiuliza mtu km una akili timam.Hv dunia hii ni binadam gan atakubal kula yai viza?Huu ni uzushi.
Lakin suala la kukatazwa kulala kitandan,halaf uambiwe ulale chini hili ni la kawaida.Mashart ambayo waganga weng wanatoa.Na weng wanayaweza.
Za kuambiwa changanya na zako.
Kibwana shomari
 
Huyu Saido ni mchezaji mzuri ila ana kibri sana. Yaani amejengwa ktk hali ya kudhani yeye ni bora kuliko wengine wote. Hata anapokaa na wenzie huwa anajiona ni wa tofauti sana.wenzake wanakasirishwa anakuwa na special treatment. Kibri anacho na hayo maneno anayaongea sana kwa watu kuonesha yeye hana shida sana ila Yanga ndo yenye shida naye.
 
Kuna vitu vya kujiuliza mtu km una akili timam.Hv dunia hii ni binadam gan atakubal kula yai viza?Huu ni uzushi.
Lakin suala la kukatazwa kulala kitandan,halaf uambiwe ulale chini hili ni la kawaida.Mashart ambayo waganga weng wanatoa.Na weng wanayaweza.
Za kuambiwa changanya na zako.
Watu wanakunywa maji ya maiti sembuse yai viza, yanaliwa mzee
 
Huyu Saido ni mchezaji mzuri ila ana kibri sana. Yaani amejengwa ktk hali ya kudhani yeye ni bora kuliko wengine wote. Hata anapokaa na wenzie huwa anajiona ni wa tofauti sana.wenzake wanakasirishwa anakuwa na special treatment. Kibri anacho na hayo maneno anayaongea sana kwa watu kuonesha yeye hana shida sana ila Yanga ndo yenye shida naye.
Vilabu alivyopitia hakuna hata mchezaji mmoja wa yanga anaeweza kupita acha awe na kibri....
 
Haya mambo nouma Sana , hasa Africa kuna ushirikina mkubwa Sana kwenye soka, kpind tukiwa wadogo kwenye ligi za ng'ombe za kijiji , Kaka zangu wakiwa wanachezea timu ya kijijini tulikuwa tunaenda Kwa waganga Kama wote yaani , sometyme mganga anakuja usiku , mnaenda uwanjani usku wa manane kuweka madawa na moja ya shrti maarufu ni kuwa , mpira ukianza Tu , mchezaji wa Kwanza wa timu yenu atakayeunasa mpira shart aupige nje....
Mbali na ulozi huo bado tulikuwa tunachapika Tu , sometyme tunashinda , ilikuwa amsha amsha sana na mipira ilikuwa inapasuka hatari
Umenikumbusha Ajibu akiwa uto ule game yao na Simba, mpira kuanza tu akaupiga nje!
 
Kwenye soka la bongo sio Yanga wala Simba wasioroga...
 
Yanga ni timu yangu lakini tuna miaka 20 kwa sasa kuifikia simba
Usidanganywe na yanayotokea, Simba ni imepata mtu mwenye fedha tu na ikawa na mabadiliko ya muda mfupi. Simba kama Simba haina fedha wala kujengeka kitaasisi.Moo akisema anajitoa hapo Simba, Simba haina tofauti na Gwambina au KMC.

Sent from my TECNO K7 using JamiiForums mobile app
 
Kama anacho kiongea huyo mchezaji kina ukweli, basi viongozi wa Yanga wanazingua. Mambo gani sasa ya kulishana mayai viza na kulazana chini!

Mimi ni Mwananchi, ila kamwe siwezi kuunga mkono vitendo vya kipuuzi. Kwanza Msolla atuambie mchakato wa kuibadilisha Yanga umeishia wapi! Badala ya kutuletea tu kila siku stori feki za Morrison, na kufukuza makocha kila wanapo jisikia.

Ni vyema wakamuajiri Kocha bora ili adumu muda mrefu kwenye klabu, badala ya kuokoteza tu mtaani.
Mkuu habari za uongo, yai viza linaliwa vipi?? Nyau FC wanaokoteza uzushi wa kubance mambo yao.

Sent from my TECNO K7 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom