Saikolojia ya fedha na kanuni za mafanikio

Saikolojia ya fedha na kanuni za mafanikio

Peter Agostino

Senior Member
Joined
Sep 23, 2016
Posts
105
Reaction score
229
Kwanza hebu tufahamu maana ya neno lenyewe Saikolojia ni kitu gani, Saikolojia ni elimu ya akili au nafsi. Kwahiyo saikolojia ya fedha ni elimu ya jinsi tunavyoichukulia fedha ndani ya akili zetu.

Saikolojia ya pesa ni kitu muhimu sana tunapozungumzia suala zima la mali na utajiri kwa sababu fedha maana yake ni NGUVU na vilevile ni muhimu sana nguvu hii mtu ukajifunza kuitendea matendo yaliyokuwa chanya ikiwa utataka iongezeke na kuwa nyingi.

Ili kutambua hasa ni jinsi gani mtu unavyoweza ukatengeneza pesa nyingi ni lazima kwanza ufahamu ni kwanini watu hawapati pesa, kuna sababu kadhaa ni kwanini watu hukosa pesa na kumi kati yake ni hizi zifuatazo;

1. Fedha ni lazima ipendwe.

Mara nyingi watu huwa hawana mapenzi na fedha, je unafahamu maana ya kuipenda fedha na saikolojia chanya ya fedha? Hebu jaribu kufikiria kidogo kisha utoe jibu, wengine watajibu kwamba, “mimi ninachokipenda ni kutumia pesa” na bila shaka hayo ndiyo mawazo ya waliokuwa wengi. Kwamba mapenzi yao kwenye pesa yameegemea zaidi katika MATUMIZI. Watu hawapendi pesa bali wanachokipenda wao ni kile kitu pesa inachoweza kununua na hili ni kosa kubwa sana!

Hebu jiulize tena swali jingine hili, “Kwanini wikiendi unawatoa out watoto wako na kuwanunulia midoli na magari ya kuchezea? Jibu rahisi unaweza ukajibu ni kwa sababu unawapenda. Kuwapeleka matembezini na kuwanunulia watoto wako zawadi hakumaanishi kuwa unawapenda sana bali upendo wa kweli kwao unadhihirishwa na jinsi UNAVYOWAJALI. Hivi ndio kusema kwamba yoote yale unayowafanyia wanao lengo lake kubwa ni kuwajali na kuwatunza na hali ni hivyohivyo ilivyo kwa pesa, pesa inahitaji matunzo na kupendwa.

Nitatoa mfano wa watu wawili wanaokwenda sokoni kununua pochi(wallet) ya kutunzia fedha. Wazo la mtu wa kwanza ni kwamba yeye anahitaji tu pochi mpya kama urembo ingawa pia ataitumia kuwekea fedha zake. Mtu wa pili yeye lengo lake mahsusi anahitaji pochi kwa ajili ya kuzifanya fedha zake zikae salama kwa raha mustarehe. Sasa hebu tuseme kama wewe ndio ungelikuwa PESA, niambie ungelichagua kuingia katika pochi ipi kati ya ya hizo pochi mbili?

Bila shaka yeyote ile wengi mngelichagua pochi ya mtu wa pili kwa kuwa hakuna asiyependa kupendwa, usalama, starehe, amani na kujaliwa!!! Na hii ndio saikolojia yenyewe ya pesa, ukitaka pesa iwe rafiki kwako na kuongezeka ni lazima uipende na kuijali.

2. Kauli hasi(-) kuhusiana na pesa.

Kuwa makini sana kuhusiana na maneno uayotamka kama vile, Sina pesa, Vyuma vimekaza, hali yangu kifedha ni tete sana nk. Maneno kama haya yanaweza yakasababisha kweli ukakosa kabisa pesa. Badala ya maneno hasi kama hayo unaweza ukatamka hivi, Pesa ipo njiani kuja kwangu, ipo siku tu, one day yes!, pesa tayari inagonga mlangoni pangu, pesa naziona zinanichungulia dirishani nk.

Kuwa kama Dokta Shika yule jamaa aliyekwenda kununua maghorofa akiwa senti tano mfukoni hana, unajua saikolojia aliyotumia yule jamaa ilivyomsaidia? Hata madai ya fedha zake urusi pengine hayakuwa na mashiko kivile lakini saikolojia ile ya kuamini pesa ilikuwa ikimchungulia dirishani, iliweza kumfanya apate shavu la nguvu kutoka kwa makampuni kibao nchini yakiwemo ya bahati na sibu hatimaye akapata mpunga(pesa) iliyomsaidia kuvuka mahali pagumu alipokuwa.

Katika Saikolojia ya pesa, pesa pia unaweza ukaifananisha na mtoto mchanga, mtoto mdogo anapoanza kujifunza vitu mbalimbali kama vile kutambaa au kutembea wazazi wake na walezi humsifia na kumpa moyo kwa kusema, “Umekua mwanangu ee” “Kazana nitakununulia pipi” nk. hapo mtoto kweli hukazana mpaka ameweza kabisa kile anachojifunza tena kwa muda mfupi ajabu!

Pia ASILI hututendea sisi binadamu kwa namna kama hiyohiyo ya mtoto mdogo anavyotendewa na wazazi wake, pindi tu tunapoanza kuchukua hatua chanya za awali katika jambo lolote lile maishani ikiwemo kutafuta pesa, asili hutupa mara moja matokeo ya upendeleo kusudi tuweze kuwa na uhakika na nguvu ya kuendelea mbele tukifahamu kwamba tupo katika uelekeo sahihi na tunahitaji kufika mbali zaidi ya pale tulipokuwa. Jitahidi kubadilisha kabisa mtazamo wako wa fedha kuwa chanya kwa maneno kama haya;

  • Napenda pesa na nazipata kwa urahisi
  • Natengeneza pesa na kuzitumia kwa urahisi
  • Mara zote naweza kuingiza pesa kiasi ninachotaka nk.
3. Wekeza ndani yako mwenyewe

Usiache kununua kile ulichopanga kununua kwa ajili yako mwenyewe, vinginevyo ASILI itaichukua fedha hiyo kwa namna nyingine tofauti kabisa. Kwa mfano anaweza kuja rafiki au ndugu akajifanya kukukopa na asijekukulipa tena kamwe au anaweza kutokea kibaka/mwizi kusikojulikana na kuikwapua fedha hiyo hivihivi ikapotea nk.

4. Kuwa Mkarimu na mtoaji kwa watu wengine.

Ukarimu hapa haumaanishi utapanye ovyo pesa zako kuwaridhisha watu hapana, inamaanisha usiwe bahili kupita kiasi, kwa mfano pale unapotakiwa kufanya malipo au kumlipa mtu chake fanya hivyo bila manunguniko wala kisirani rohoni, unaponunua vitu vipya nk. unahitaji kuwa na saikolojia nzuri ya fedha.

5. Uoga wa kufikwa na majanga au kufilisika.

Fedha ni aina ya NGUVU na inatakiwa kutunzwa(unapoiweka kama akiba) ukitumia maneno chanya+ mfano;

  • Akiba hii ni kwa ajili ya safari na wala siyo “kwa ajili ya kipindi cha uzeeni”
  • Kwa ajili ya dharura na wala siyo kwa ajili ya majanga
  • Kwa ajili ya kuboresha afya na wala siyo kwa ajili ya kutibu magonjwa
Makala hii imetolewa katika blog ya jifunzeujasiriamali, na imeandaliwa na mwandishi wa vitabu vya ujasiriamali Peter Augustino Tarimo
 
Mada nzuri sana hii, na bandiko murua kabisa, lakini ajabu ndo kama hivi yaani
 
Back
Top Bottom