Sakata la Fei Toto, Yanga inachekesha na kusikitisha

Iyo taasisi wakati inawabeba kwa morison mlishangilia na kuipigia makofi sasa mambo ayapo upande wenu mnabwata kama walevi wa kimpumu ovyo kabisa nyie
 
Hoja siyo Fei kuitaka Yanga.Kama ni maswala ya kupendana hata Yanga haimpendi Fei.Hoja ni matakwa ya mkataba.Kama alikuwa na uwezo huo ,asingesaini Yanga.Kwanza hiyo nguvu ya kuongea hivyo kaipata Yanga,mwanzoni alisaini Singid United,Yanga alipelekwa n Mwigulu.Je,huko alikuwa amesaini shilingi ngapi? Ujinga ni kutukana waliokuokota jalalani.
 
Mkataba una terms and conditions( vigezo na masharti) hivyo ndo huwabana parties to that contract.Fei as a party to the contract vs Young Africans has to fulfill his contractual obligations.Hata uende CAS huo ndo msingi.
 
Unaumiza akili yako bure, hii vita siyo ya Feisal na yanga, ni vita ya waliompa pesa Fei apambane na muajiri wake.
Hii hanatofauti na vita ya Ukraine vs Russia.
Wamemrubuni dogo kwa pesa, yanga wametegua mtego, kumdai dogo pesa hawawezi.


Sent from my Redmi Note 8 Pro using JamiiForums mobile app
 
Mama yake juzi kathibitisha anapewa mln 4 na azimtoshi sasa labda wewe mke wake utuambie alikua akipatiwa shilingi ngapi
 
Yanga sio kwamba wanamng'ang'ania Fei, ila hawataki aondoke kwa njia aliyoamua kuitumia. Kwavile imeshindikana mbele ya TFF, basi aende mamlaka za juu. Ila huko kote ataendelea kupoteza muda.

Njia nzuri ya kulimaliza ili jambo, ni timu inayomtaka kupeleka maombi rasmi kwa Yanga, maana inaonekana tayari wameshaelewana wao kwa wao (hiyo timu na Fei), wakishamalizana na Yanga, mambo yatakuwa mepesi.
 
Halafu hao wapuuzi wana hela ila cha ajabu wanashindwa kutumia njia stahiki ambazo zitawafanya wampate mchezaji wanayemtaka kuliko kutumia njia zisizo sahihi kama wanavyofanya sasa
 
Mama yake juzi kathibitisha anapewa mln 4 na azimtoshi sasa labda wewe mke wake utuambie alikua akipatiwa shilingi ngapi
Milioni 4 kutomtosha, ilo ni swala binafsi, halihusiani na club. Walichotakiwa hao wawakilishi wake, ni kuomba kuboreshewa maslahi ya kijana wao, na sio kukurupuka na kutaka kuondoka, as if alikuwa msalani.
 
Mkuu trust me, hapa wewe ndio mvivu kufikiri.

Unapofushwa na mahaba
 
Wewe dunduka Hebu toka usingizini usije ukajinyea , Fei Toto anashauriwa vibaya na madunduka wenzake haiwezekani uvunje mkataba kienyeji halafu utegemee public sympathy kwenye ishu ya mkataba ni kushindana vifungu vya mkataba full stop yeye kwa sababu anaonyesha kiburi wacha tuone mwisho wake kama ana uwezo wa kushindana taasisi kubwa kama Yanga na tuone nani atakuwa mhanga ktk ishu hii, nyinyi madunduka suala hili haliwahusu ni wakati wenu sasa WA kujadili jinsi ya kupunguza magoli mtakapokwenda Casablanca Morocco nipo pale mtanishukuru
 
Simba wengi ni wambea wa kuifuatilia Yanga na kusahau kuwa wana mechi kubwa na Raja
 
Kwanini swala hili TFF imeamua kulifanya siri haitaki kutoa mchanganuo wa kanuni zilizotumika kuhukumu pamoja na sheria aliyovunja Feisal kila mtu aone

Hiyo ndio hoja yangu mimi
Wala haijafanya Siri, isipokuwa wanafata Sheria na kanuni zao. Huwa wanatoa taarifa kwa imma, juu ya wito walioutoa kwa pande mbili zenye mgogoro, na baada ya kumaliza kikao, huwa wanatoa taarifa tena kwa umma juu ya hatma ya hicho kikao.

Taarifa in details na sababu ya wao kufikia hayo maamuzi, huwa pande zote mbili wanapatiwa kwa printed documents. Moja kati ya hizo pande mbili, ikiamua kuleak hizo taarifa, ni juu yao, swala linakuwa halipo TFF tena.

Kwahiyo mkuu, subiria document tareh 6
 
Uswahili wa namna hii ndio unatukwamisha. Lengo la mkataba ni pande zote zitekeleze kile walichoafikiana. Yanga wanasisitiza Feisal atekeleze sehemu yake ya mkataba, hawamng'ang'anii ila wanamkumbusha wajibu wake.

Sent from my SM-A6050 using JamiiForums mobile app
 
Tatizo watu wanajadili mihemko tu,mtu kasaini mkataba mwenyewe wa milioni 4.Katika hiyo milion 4 kaamua kula ugali na sukari,lawama zinaenda kwa Yanga. Kama aliona haitoshi kuna njia alipaswa kufuata kupata maslah zaidi. imetokea pale liverpool,Klopp anachukua wachezaji hawana majina wanasaini mikataba ya pesa kidogo baadae kabla mkataba haujaisha sababu ya mchango anaoonesha wanasaini mkataba mpya kuongeza miaka ya kukaa klabuni na mshahara unaongezeka.
 
Ninachokiona ni huyo kijana Fei anatiwa adabu. Awe na nidhamu ndani na nje ya kiwanja.

Ukweli ni kuwa kijana aliwatusi sana Yanga kuwatumbukizia vijisenti vyake kwenye akaunti yao kuwa eti anawalipa na kuvunja mkataba.

Tunamshauri awache kibri, aombe msamaha na kama snataka kuhama afate sheria na kanuni.

Fei alikosa washauri wa maana na ana kibri cha ujingaanaojazwa nao na mama'ke.

Nashangaa wstu hawaelewi kuwa biashara ya utumwa ipo na inaendekea kisheria duniani.
 
Mnashindwa kuelewa hoja

Ulifatilia kesi ya Morrison?

Kama ulifatilia utaelewa nachomaanisha
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…