Sakata la Kashfa ya Richmond: The Facts

Sakata la Kashfa ya Richmond: The Facts

Wazee, hivi hawa bureaucrats wameona waTz wote hamnazo, what should we do?
 
Kwa kweli hivi ni vituko vya mchana.

Messr Richmond Development Company (RDC) haikuwa kampuni bali kikundi cha watu. Baada ya kuona wamecheza faul kwa kufuata ushauri mbaya wa wanasiasa (vigogo) waliamua kuwakimbia wanasiasa hao, matokeo yake ni kwamba wameunda an Imaginary Company Messrs Dowans Holdings na kusema ni ya UAE. Lakini katika uchunguzi wangu wa awali hii Kampuni haipo huko na wala haijasajiliwa huko. Nina rafiki yangu ambaye babake anafanya ministry of economy, katika list ya kwanza ya Kampuni zilizosajiliwa UAE haipo, mpaka sasa hivi tumepitia Kampuni 317 ambazo zimesajiliwa kihalali.

Habari nyingine ni kwamba Messrs Dowan ni kwamba haijasajiliwa Tanzania kama ilivyo Kisheria kwa kampuni yo yote inayofanya kazi Tanzania. Baada ya kupitia Business Registration na Licence haipo.
 
Aljazeera,
Thanx a million bob, maanake hata mimi nimejaribu kufuatilia hilo lakini hadi sasa hivi mtupu!...
Hawa wahindi na viongozi wanatuona sisi vipi lakini?....I mean wamefanikiwa kutudanganya mara ya kwanza, leo hii wanafanya kuwa ibada! hata baada ya wananchi kuamuka!...

Mwanagenzi,
Nadhani jibu la maswali yako yote hapo juu yamekamilika vizuri!... kwanza kumbuka tu kuwa Dowans wanapoingia wameomba muda zaidi.. kwa hiyo tarehe ya kuanza kazi imekuwa extended kuwapa muda zaidi. Pili, TIME brother time matters!
Hakuna shirika ambalo linaweza kununua contract bila kuangalia faida na hasara zake...Which means RDC wameisha nunua mitambo ya hizo 20 ambazo RDC wameuza kwa Dowans bila sisi kupata umeme bado. hakuna kati yetu anayefahamu RDC imeuzwa kwa kiasi gani, meaning wameweka kijifaida baada ya Dowans kuridhika na mkataba kuwa wataweza kuendesha kwa faida mbali na ununuzi wa hii kampuni.
Hivyo basi, wakati biashara hii inatembea sisi tupo kizani..na uzalishaji umesimama, wawekeshaji wengine wameisha funga virago kuhamia Kenya!.. Je, unafahamu ni kiasi gani cha fedha tanzania hupoteza kila siku Umeme unapotatika?...Now, ukishapata hesabu zidisha kwa muda wote ambao tumekuwa tukipigwa chenga na hawa RDC. Hata kama Umeme utarudi kuwa kawaida, Tanzania imelala kiuchumi vibaya sana kwa muda wa hiyo miezi. Hii peke yake ni scandal kubwa sana ambayo inatakiwa kuzungumziwa bungeni na hata watafutwe wale waliohusika...Kifupi wote wahusika wanatakiwa kulipa hasara zote za Umeme.
Nimefurahi sana kuona Tanecso wanaanza kudindisha, na itakuwa balaa kwa RDC na hao Dowans wa Kuchonga!
 
Wanabodi,
Hii ndiyo sababu nchi za wenzetu (western world) hawa privatize source za UMEME... Sisi machinga tuliposikia neno privatize basi ndio kila kitu!...
Tumekwsiha kwa sababu ya makosa yaliyoyokea toka mwanzo wa privatization. Jukumu la Umeme limekuwa sio la serikali bali mikononi mwa watu na serikali eti ndiye mgawaji!...Haya pekee ni maajabu ya Mussa...
 
Tanesco wanadindisha nini wakati kwenye contract watu walisema, hata rais kuwa wanavyochelewa watalipa fidia Je ni kiasi gani wao Tanesco wamelipwa na RDC kama fidia kwa uchelewaji?

Tanesco hadi kukubali kuhamisha Mkataba kwa kampuni ambayo hata Bongo haijawa registered? Hawa serikali na Huyu JK wote Vichwa Vya mwendawazimu kweli kweli.

Na bado uozo walioleta ndio unaanza kuonekana
 
Rais wetu Mzee JK ana mkono wake kwenye hili hata akiongea juu ya RDC mwangalie usoni anavypo pata shida kujenga hoja.JK hakuwa na sifa za kuwa Rais maana hajawahi ku deliver ila kwa ubishi wenu mkampa kisa mnasema hana kitanmbi .Lakini wako akina Dr.nani yule wa wa Uchini hana kitambi na hana mwili lakini ni mwizi wa kutupa anatumaliza hata sasa .
 
....Lakini kama ndio 'kasi' hii, basi kuna mambo makubwa. Hii Richmond mbona inakuwa balaa hivi! Hivi inawezekana kweli hawa viongozi wetu wakawa wajinga kiasi hiki mara hii tu?
Tuseme kuna mambo mawili:
1. Wana haraka sana ya uroho, kiasi kwamba hawaoni kuwa upuuzi huu wa Richmond watu wataanza kujiuliza kulikoni huko.
2. Ni ma-mbumbumbu- hawajui maana ya mikataba wanayoiingiza nchi.
Either way, we will be doomed.
 
rich-monduli ni kampuni ya rafiki zake Lowassa. wameiba sasa wamewaachia Dowans, kampeni ya wawekezaji, marafiki zake Kikwete.
 
Mkandara,
You have nail the point, TIME IS MONEY, TIME IS EVERYTHING!!!!!

Hawa RDC walijua kuwa muda ukifika wangeanza kudaiwa kama hawajatimiza ahadi ya mkataba waliopewa kwa hiyo wanajua mapesa yangewatoka.

Kwa hiyo mimi sishangai kama wameuza mkataba kwa hawa Do-What? au wamechange jina tu kuongezewa muda.

Sijui ukweli upo wapi au mkataba walio-sign RDC unasemaje lakini maswali ya haraka haraka yanayonijia ni kwamba-----

1: Hawa RDC kwa kukatisha mkataba kabla hata hawajafikisha mwaka mmoja hawakutakiwa kulipa fidia yeyote?

2: Kama wameshindwa kazi, JE TANESCO/SERIKALI ilitangaza hiyo zabuni upya au walipeana kishemeji tena?

3: Je tuna taarifa yeyote ni lini RDC waliifahamisha TANESCO/SERIKALI kuwa wasingeweza kuendelea na hiyo zabuni kwasababu ni juzi tu JK aliwatetea hawa wababaishaji!

Maswali ni mengi lakini naona tutakuwa tuna-deal na vichwa vya wendawazimu ambao hata hayo makaratasi ya mikataba hawakuisoma. Wao alimradi mifuko imetuna na watoto wanatanua ulaya!!
 
Msipige kelele watanzania wenzangu, si mlisema JK kateuliwa na mungu.Na mmemchagua ili kunusulu mgawanyiko ndani ya chama.Ni mapema nnooooo kulalamika, bado anamiaka 9 madarakani.Na LOWASA miaka 10.
 
Huyu jamaa JK mlisema si mla rushwa na anaichukia sana . Mlisema ni mpenda haki na mkamalizia kwa kusema ana sura nzuri na mpenda watu ana jichanganya.Sasa haya yameisha lini ?
 
Lisilowezekana duniani kote linawezekana Tanzania.Watanzania tutaendelea kuvumilia ufirauni huu mpaka lini? Ni kweli tumefikia kuwa wapole kiasi hiki?sisi ni wapole au wajinga?Tumefikia hatua ya kuwaachia kikundi kidogo cha wanasiasa uchwala waendeshe nchi kadri watakavyo? Watanzania inatakiwa tubadilike sasa.
 
Issue hapa ni kwamba serikali haitaki kukiri kwamba imevurunda katika swala zima la Richmond. Then, kama TANESCO wanasema umeme sasa mambo safi (which is great) kwa sababu mabwawa yamejaa, vipi tena mtera haijaanza kuzalisha umeme? Je, si kweli kwamba tatizo la mtera ni zaidi ya maji? Je, muda umefika sasa kwa TANESCO kukiri kwamba matope ni tatizo kwa mtera kama alivyosema Lipumba?
 
Mwana Kijiji: basi bwana nimekubali, wewe kiboko. Kama huna muda wa kuipeleka hiyo article kwenye magazeti ya nyumbani nipe idhini nimtumie rafiki yangu najua ataipublish. Wanasaikolojia wanasema njia moja ya kupima uwezo wa mtu wa kufikiri ni jinsi anavyoweza kucheza na maneno. That was a great demonstration of a great mind! Alas, it will end up in deaf ears as CCM have no culture of listening to voices other than their own.
 
Mwanakijiji,
Ama kweli mazingaombwe!...
Niliwahi kuona mchezo wakuigiza wa Mzee Majuto akiandaa pambano la ngumi kati ya msera toka Marekani aliyechacha nyang'anyang'a - Bobby Johnson (Richmond) na Mpambe wa Kibongo (Tanesco). Majuto na washikaji wake (Uongozi wa CCM) walisha uza tiketi mapema na kila Pambano lilivyozidi kunoga, Majuto alikuwa akitafuta upenyo wa kukimbia na makusanyo yote.
But guys, one thing though, tusiwe wasahaulifu kiasi hicho!
Mkataba wa RDC uliwekwa wakati wa Mkapa!.. Tumemsikia Mzee ES akiwataja wote waliohusika na mkataba huo....toka Balozi, Sumaye na wengineo. hawa watu wanatakiwa kusimama mahakamani kujibu mashtaka ya raia. Ni haki yetu kumshika JK shati na kumuuliza kwa nini anawatetea watu ambao anafahamu kabisa walifanya makosa makubwa...
Hili liwe swali ambalo atakuwa akiulizwa kila anapokwenda na RUSHWA ile agenda kubwa ya wananchi..

Tusipoteze ushahidi wetu kumweka kizimbani JK ambaye ndiye tunayemtegemea kufungua mashtaka haya..
Toka sasa, RUSHWA ndio iwe adui wetu mkubwa kuliko hata Umaskini.. We can deal na Umaskini baada ya kuondoa RUSHWA, laasivyo tutazidi kutokomea ktk shimo la chewa!...
 
Hapana Mkandara, fuatilia vizuri hili saga, huu mkataba wa RDC umepikwa na kupakuliwa wakati wa akina JK na EL.
 
Back
Top Bottom