Sakata la Kashfa ya Richmond: The Facts

Sakata la Kashfa ya Richmond: The Facts

...inabidi Alinde P Yake Labda Akitoka Huyu Msekwwa Wanaweza Kumfikiria Maskini...
Pdidy thnx for exposing this. Wameshaona aliyebaki kuwanyonga akina Zitto ni mzee wa Spidi pekee (ili kila kukicha hoja ziitwe za kitoto); hiyo ni indiketa, atawafirigisa mpaka basi.
=================
 
Jamani tume ya Richmonduli iliishia wapi? Au nimepitwa? naona Balali katumeza sana tumemsahau DITO, IPTL DEGE etc
 
FD, wakati Baraza la Mawaziri litakapojiuzulu/kupanguliwa wiki ijayo itakuwa ni masaa machache kabla ya ripoti hiyo kuletwa Bungeni.
 
Jamani,

Nimejaribu kugugo (google) Dowans Holdings S.A na kila kitu ni kutoka magazeti ya Tanzania na JF. Jee hi ni kampuni gani ambayo tunaipa fedha nyingi kiasi hiki ambayo wala haifahamiki?

Who authorised the mkataba transfer from Richmond to Dowans? Maana nasikia hapakuwa na kipengele kuruhusu assignment and assumption of contract by other party!!

Sasa ni vipi Serikali ya Tanzania na Tanesco wameingia mkataba mpya kurithi mkataba mbovu?

...hii kampuni ya kwenye briefcase inawezekana imeanzishwa miezi michache tuu iliyopita na hao hao wasanii wetu AKA mafisadi ili wale zaidi,hakuna huruma kabisa na hawa mafisadi wanataka kuhakikisha wanamaliza kila kitu,angalia the whole price ya hiyo project nzima unaweza kulia na mtambo ni kanyabwoya tuu ushatumika huko wamepaka rangi sasa ndio wametuletea kwa bei mara kumi ya machine mpya,tumejaza vilaza na mafisadi tuu
 
Mzee Mkjj, nipo hapa polini kwangu. Napewa taarifa kuwa Mawaziri Wote Wameitwa leo tena Ikulu na Msanii Mtalii wetu JK. Kulikoni Mzee? Plz miibue polini kwa kunijulisha what is happening around magogoni!
 
labda wanapewa mkakati wa kutembea nchi nzima kumakazia balali au kuisifia ripoti ya bot.
 
CCM MPs to discuss position on Richmond

-PM Lowassa to chair crucial caucus meeting ahead of next week�s debate

THISDAY REPORTER
Dodoma

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) legislators are set to hold a crucial caucus meeting here tomorrow, ahead of the upcoming parliamentary debate on the final report of a Bunge committee assigned to investigate the controversial Richmond power generation deal.

Insiders have told THISDAY that the meeting will also discuss the Bank of Tanzania (BoT) special audit findings, whose report is also expected to come up for debate in the House next week.

The meeting, to be chaired by Prime Minister Edward Lowassa by virtue of his position as the official leader of government business in the National Assembly, is expected to seek a common ground on both sensitive issues.

The regular caucus meetings of ruling party MPs usually determine matters of policy, parliamentary strategy and tactics, and even disciplinary measures to be taken against ’disobedient’ or rebel MPs who do not tow the party line.

’’We have already been notified that there will be a meeting on Tuesday (tomorrow) to discuss what our position as CCM lawmakers should be on the Richmond and BoT audit debates next week,’’ one ruling party MP, who asked not to be named, told THISDAY.

The secretary of the CCM parliamentary caucus, Ali Ameir Mohamed (Donge-CCM), also confirmed that the meeting would be held tomorrow, but insisted that it was just a normal meeting held regularly, and was not being specifically convened to discuss the Richmond and BoT issues.

It has been suggested that even though the caucus may try to bring maverick lawmakers in line beforehand, several senior government officials should expect a ’’serious telling off’’ from ruling party MPs when the Richmond and BoT debates come up in parliament.

’’President Kikwete has given us the go-ahead to reprimand even ministers who have become a burden to the government - and we intend to do just that,’’ said another CCM lawmaker.

Although findings of the parliamentary committee on the dubious Richmond deal have not yet been made public, well-placed sources are already describing the report as a ’’bombshell.’’

To demonstrate the seriousness of the matter, the Speaker of the National Assembly, Samwel Sitta, who flies to the US this week, has put a temporary hold on the much-anticipated House debates on Richmond and BoT until he returns next week.

Sitta has instructed the Deputy Speaker, Ms Anna Makinda, not to allow MPs to debate either of the two topics during his absence because he wants to personally preside over the matter.

He assured THISDAY that both debates will now take place during the third and final week of the current Bunge session (February 11 to 15).

The parliamentary committee that investigated the controversial, 172.9bn/- Richmond power generation deal was chaired by Dr Harrison Mwakyembe (Kyela-CCM). Other members were Ms Stella Manyanya (Special Seats-CCM) as vice-chairperson, Lucas Selelii (Nzega-CCM), Herbert Mntangi (Muheza-CCM) and Mohamed Mnyaa (Mkanyageni-CUF).

There were reports of high-level meddling during the parliamentary probe on Richmond, with the committee warning at one point that some testifying witnesses faced the risk of perjury for deliberately misleading the investigation.

A government procurement watchdog has also issued an official report saying the process that eventually led to the awarding of the contract to the US-based Richmond Development Company was interfered with by high-level government officials.

According to the report by the state-run Public Procurement Regulatory Authority (PPRA), Richmond was awarded the contract despite having already been disqualified as incompetent by the Tanzania Electric Supply Company Limited (TANESCO).

The parliamentary inquiry into the Richmond affair followed dissatisfaction voiced by many MPs over the Prevention and Combating of Corruption Bureau (PCCB)�s declaration last May - after conducting its own investigation - that the deal was ’’clean.’’
 
Sasa nime elewa why Spika kavunja safari . Maana anataka kujua namna ya kuwabana watu wanao toa hoja nje ya watakavyo kubaliana kwa CCM na wapinzani kukandamizwa na kuzimwa hoja zao kabisa .
 
Sasa nime elewa why Spika kavunja safari . Maana anataka kujua namna ya kuwabana watu wanao toa hoja nje ya watakavyo kubaliana kwa CCM na wapinzani kukandamizwa na kuzimwa hoja zao kabisa .

Kwenye caucus Sitta is just mbunge kama walivyo wabunge wengine. Vidume vya caucus ni Lowassa, Ameir na Makamba
 
CCM MPs to discuss position on Richmond

-PM Lowassa to chair crucial caucus meeting ahead of next week�s debate

THISDAY REPORTER
Dodoma

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) legislators are set to hold a crucial caucus meeting here tomorrow, ahead of the upcoming parliamentary debate on the final report of a Bunge committee assigned to investigate the controversial Richmond power generation deal.

Insiders have told THISDAY that the meeting will also discuss the Bank of Tanzania (BoT) special audit findings, whose report is also expected to come up for debate in the House next week.

The meeting, to be chaired by Prime Minister Edward Lowassa by virtue of his position as the official leader of government business in the National Assembly, is expected to seek a common ground on both sensitive issues.

The regular caucus meetings of ruling party MPs usually determine matters of policy, parliamentary strategy and tactics, and even disciplinary measures to be taken against ’disobedient’ or rebel MPs who do not tow the party line.

’’We have already been notified that there will be a meeting on Tuesday (tomorrow) to discuss what our position as CCM lawmakers should be on the Richmond and BoT audit debates next week,’’ one ruling party MP, who asked not to be named, told THISDAY.

The secretary of the CCM parliamentary caucus, Ali Ameir Mohamed (Donge-CCM), also confirmed that the meeting would be held tomorrow, but insisted that it was just a normal meeting held regularly, and was not being specifically convened to discuss the Richmond and BoT issues.

It has been suggested that even though the caucus may try to bring maverick lawmakers in line beforehand, several senior government officials should expect a ’’serious telling off’’ from ruling party MPs when the Richmond and BoT debates come up in parliament.

’’President Kikwete has given us the go-ahead to reprimand even ministers who have become a burden to the government - and we intend to do just that,’’ said another CCM lawmaker.

Although findings of the parliamentary committee on the dubious Richmond deal have not yet been made public, well-placed sources are already describing the report as a ’’bombshell.’’

To demonstrate the seriousness of the matter, the Speaker of the National Assembly, Samwel Sitta, who flies to the US this week, has put a temporary hold on the much-anticipated House debates on Richmond and BoT until he returns next week.

Sitta has instructed the Deputy Speaker, Ms Anna Makinda, not to allow MPs to debate either of the two topics during his absence because he wants to personally preside over the matter.

He assured THISDAY that both debates will now take place during the third and final week of the current Bunge session (February 11 to 15).

The parliamentary committee that investigated the controversial, 172.9bn/- Richmond power generation deal was chaired by Dr Harrison Mwakyembe (Kyela-CCM). Other members were Ms Stella Manyanya (Special Seats-CCM) as vice-chairperson, Lucas Selelii (Nzega-CCM), Herbert Mntangi (Muheza-CCM) and Mohamed Mnyaa (Mkanyageni-CUF).

There were reports of high-level meddling during the parliamentary probe on Richmond, with the committee warning at one point that some testifying witnesses faced the risk of perjury for deliberately misleading the investigation.

A government procurement watchdog has also issued an official report saying the process that eventually led to the awarding of the contract to the US-based Richmond Development Company was interfered with by high-level government officials.

According to the report by the state-run Public Procurement Regulatory Authority (PPRA), Richmond was awarded the contract despite having already been disqualified as incompetent by the Tanzania Electric Supply Company Limited (TANESCO).

The parliamentary inquiry into the Richmond affair followed dissatisfaction voiced by many MPs over the Prevention and Combating of Corruption Bureau (PCCB)�s declaration last May - after conducting its own investigation - that the deal was ’’clean.’’

Wameinama...
Wameinuka...

Wanaona haya hao sisiemu haooooo......
 
CCM MPs to discuss position on Richmond

-PM Lowassa to chair crucial caucus meeting ahead of next week�s debate

THISDAY REPORTER
Dodoma

Insiders have told THISDAY that the meeting will also discuss the Bank of Tanzania (BoT) special audit findings, whose report is also expected to come up for debate in the House next week.

The regular caucus meetings of ruling party MPs usually determine matters of policy, parliamentary strategy and tactics, and even disciplinary measures to be taken against 'disobedient' or rebel MPs who do not tow the party line.

''We have already been notified that there will be a meeting on Tuesday (tomorrow) to discuss what our position as CCM lawmakers should be on the Richmond and BoT audit debates next week,'' one ruling party MP, who asked not to be named, told THISDAY.



Kwa kweli hii ni Kali. Kwa mtaji huu WADANGANYIKA WASITARAJIE MAISHA BORA. Kwanini waweke msimamo wa pamoja kama CCM? Demokrasia imeshabakwa na MAFISADI, hivyo tusitarajie fair and honest contributions kutoka kwa Wabunge wa Chama Twawala.
 
Hata wakikaa vikao na kuweka msimamo ni kujidanganya tu.

I think we have reached the point of no return.

Time will tell.
 
Posted Date::2/6/2008
Kamati yawahusisha Waziri Mkuu, mawaziri Kashfa ya Richmond
* Richmond ni ujasiri wa kifisadi
* Zabuni ilitolewa kwa shinizo

* Uongozi wa Takukuru kitanzini

Na Waandishi Wetu, Dar na Dodoma
Mwananchi

KAMATI Teule ya Bunge ya Kuchunguza Mchakato wa Zabuni ya Uzalishaji Umeme wa Dharura imependekeza kuwa viongozi wote waliosimamia na kuhakikisha kuwa Kampuni ya Richmond Development LLC inashinda zabuni hiyo wawajibishwe.

Akiwasilisha taarifa ya kamati hiyo bungeni jana, Mwenyekiti wake, Dk Harrison Mwakyembe, alisema wamebaini na kuridhika ukiukaji mkubwa wa taratibu na sheria za nchi.

Dk Mwakyembe alisema, kamati imeona mawasiliano ya karibu kati ya Waziri Mkuu, Edward Lowassa na Waziri wa Nishati na Madini wa zamani, Dk Ibrahim Msabaha na wa sasa, Nazir Karamag, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Arthur Mwakapungi katika hatua mbalimbali za zabuni hiyo, lakini hawakukiri kutumwa au kuagizwa kubeba kampuni hiyo ya Marekani na kwamba, kwa mfumo wa uongozi na utawala bora wanawajibika wenyewe.

Baada ya uchunguzi wake na kubaini mianya inayoashiria rushwa, kamati imependekeza wahusika kuwajibishwa na mamlaka husika, huku Waziri Mkuu akitakiwa kupima uzito wa suala hilo kwa kuamua kuwajibika mwenyewe au bunge kumwajibisha.

Alisema uhuru mkubwa ambao viongozi wa Wizara ya Nishati na Madini waliutumia bila wasiwasi kuhakikisha kampuni waliyotaka inapewa zabuni ya umeme unoanyesha kuwa ulitokana na maelekezo ya mara kwa mara waliyopata kutoka kwa Waziri Mkuu katika kila hatua ya mchakato huo.

Aliendelea kuwa, upendeleo wa dhahiri ambao Richmond ilipata kutoka taasisi mbalimbali za serikali ni kama Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) ambacho kilifikia hatua ya kufumbia macho baadhi ya taratibu zake za msingi ili kuipa kampuni tanzu ya Richmond Development Company LLC cheti cha uwekezaji haraka iwezekanavyo bila kutimiza masharti ya Bodi za Makandarasi na Wahandisi na Wizara ya Nishati na Madini kuikingia kifua kampuni hiyo isichukuliwe hatua za kisheria.

Lowassa amehusishwa na upendeleo wa kampuni hiyo kutokana na barua yake Juni 21, 2006 akiagiza kuwa Richmond ipewe zabuni hiyo na kwamba.

Mwenyekiti wa kamati hiyo alisema, Ibara ya 52 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977 inatamka wazi kuwa Waziri Mkuu ndiye mwenye madaraka ya juu ya udhibiti, usimamiaji, utekelezaji wa siku hadi siku wa kazi na shughuli za serikali na ndiye kiongozi wa shughuli za serikali Bungeni.

Alisema kamati haikufurahishwa na taarifa zinazomgusa moja kwa moja Lowassa katika kupendelea Kampuni ya Richmond Development na kwamba, kamati imetimiza wajibu wake kwa uwazi na ukweli kama ilivyoagizwa na Bunge.

"Kwa kuzingatia umuhimu wa nafasi aliyonayo Waziri Mkuu katika uendeshaji wa shughuli za serikali na uongozi wa nchi kwa ujumla, ni wajibu wake yeye mwenyewe kupima uzito wa matokeo ya uchunguzi huu na wajibu wake kikatiba ndani na nje ya Bunge," alisema na kuongeza:

"Vile vile ni wajibu wa Bunge ambalo linathibitisha uteuzi wake kwa mujibu wa Ibara ya 51 inayothibitisha uteuzi wake kuangalia ikiwa matokeo ya uchunguzi huu hayajaathiri hadhi na uzito wake ndani ya Bunge."

Wengine waliopendekezwa kuwajibishwa ni Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi, aliyeshabikia na kuingilia uhuishaji wa mkataba huo ambao ulikuwa tayari umekoma, Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk Msabaha ambaye alikuwa waziri katika wizara hiyo kabla ya kuhamishwa.

Hata hivyo, Dk Mwakyembe alisema, Dk Msabaha akiwa nje ya kiapo alieleza kamati kwamba, yeye ni mbuzi wa kafara kwa sababu biashara hiyo ilikuwa ya Lowassa na mshirika wake, Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz.

Viongozi wengine ambao wamehusihwa na tuhuma hizo za kuingiza taifa kwenye mkataba na kampuni ya mfukoni na kusababisha hasara kwa nchi.

Maafisa wa wizara hiyo waliopendekezwa kuwajibishwa ni Katibu Mkuu wa Nishati na Madini, Arthur Mwakapugi na Kamishna wa Nishati, Bashir Mrindoko.

Mrindoko anadaiwa kushindwa kumshauri Katibu Mkuu mpya wa Wizara kuhusu udhaifu wa Richmond Development ambao ulijulikana na wizara hiyo tangu mwaka 2004 kwenye Mkataba wa bomba la mafuta.

Rungu la uwajibika ambalo linashikiliwa na Rais Jakaya Kikwete pia, limeelekezwa kuangukia Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (Takukuru) kutokana na taarifa yake kuwa taifa halikupata hasara kutokana na mkataba huo.

"Taarifa hiyo imemong’oa kwa kiasi kikubwa hadhi na heshima ya chombo hiki muhimu cha kitaifa kilichopewa dhamana na rushwa na sio kuipamba, ili kurejesha heshima ya umma katika taasisi hiyo, Kamati teule inapendekeza yafanyike mabadiliko ya haraka ya uongozi wa taasisi hiyo," alisema.

Wengine wanatatakiwa kuwajibishwa ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Johnson Mwanyika ambaye katika majadiliano yake na Kamati Teule alionyesha kutoelewa kabisa kilichokuwa kinatendeka na wasaidizi wake na mwakilishi wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali Wakili wa Serikali, Donald Chidowu ambaye ushiriki wake katika GNT haukuwa na tija yeyote, hivyo kuchangia kuingiza nchi katika mkataba wa aibu.

Kamati Teule imeanisha katika taarifa hiyo vitendo vya ubabe, ujeuri na kiburi vilivyofanywa na viongozi wa Wizara ya Nishati na Madini alimradi kampuni waliyotaka iteuliwe kiasi cha kupindisha hata maamuzi ya Baraza la Mawaziri bila wasiwasi wowote.

Dk Mwakyembe alisema, wengine wanaotakiwa kuwajibishwa ni wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Tanesco ambao walishindwa kuzuia shinikizo kutoka uongozi wa juu.

Naye Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Profesa Benno Ndullu, ametakiwa kuendesha uchunguzi na kubaini wakurugenzi waliohusika kwenye malipo ya kampuni hiyo na kuwachukulia hatua za nidhamu.
 
Posted Date::2/6/2008
Richmond chanzo cha kupanda bei ya umeme Tanzania
Na Waandishi Wetu
Mwananchi

KUPANDA kwa bei ya umeme kumebainika kuwa, pamoja na sababu nyingine, kumechangiwa na mkataba wa Kampuni Richmond Development Company LLC, iliyopewa kuzalisha umeme wa dharura.

Akiwasilisha taarifa ya Kamati Teule ya Bunge jana, Mwenyekiti wa Kamati Teule ya Bunge, Dk Harrison Mwakyembe alisema mkataba wa Richmond ni mzigo kwa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco).

Dk Mwakyembe alisema mzigo huo unabebeshwa na watumiaji hatimaye walipa kodi na kuingiza hasara taifa kwa sababu ina vipengele vinavyoumiza Tanesco.

"Mkataba kati ya Tanesco na Richmond na sasa Dowans Holdings S.A, kama ilivyo mikataba kati ya Tanesco na IPTL, SONGAS, AGGREKO na Alstom Power Rentals, inatoa unafuu usiostahili kwa makampuni hayo ya umeme na kuiumiza Tanesco na hatimaye watumiaji na walipa kodi kimapato," alisema.

Alisema mikataba hiyo ina vipengele vya kuibana Tanesco kulipia kampuni hizo kodi zinazohusika na uendeshaji, matengenezo na marekebisho ya mara kwa mara ya mitambo, gharama za bima, ada za mawakili na washauri elekezi, gharama za mafuta na gesi ya kuendeshea mitambo na gharama za ukodishaji mitambo.

Dk Mwakyembe alisema, Tanesco kila mwezi hulipa sio chini ya wastani wa Sh2 bilioni kwa kila kampuni, izalishe au isizalishe umeme.

Januari 23, mwaka huu Tanesco ilitangaza kupanda kwa gharama za matumizi ya umeme kwa asilimia sita na kati ya 66 na 215 kwa ajili kuunganishi wateja wapya.

Ongezeko hilo lililoanza kutumika Februari Mosi, mwaka huu lililalamikiwa na watumiaji, lakini Tanesco ikidai kuwa gharama za uendeshaji zimepanda bila kuziainisha.

Kulingana na bei ya sasa uniti moja inauzwa kwa Sh40 badala ya Sh38, huku watumiaji wakubwa ikipanda kutoka Sh121 kwa 'unit' hadi Sh128.

Tanesco ilisema imelazimika kuongeza bei ya umeme kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kupanda kwa gharama za uzalishaji, kupanda kwa gharama ya mafuta, mfumko wa bei na ulinganisho wa bei zake na majirani.

Kamati Teule ya Bunge, ilitoa rai kwa serikali mikataba hiyo kupitiwa upya mapema iwezekanavyo kama ilivyofanya kwa ile ya mikataba ya madini.

"Bila kufanya hivyo, mzigo mkubwa wa gharama za umeme utawaelemea wananchi na kushindwa kufikia azma ya serikali ya maisha bora kwa kila Mtanzania," alisema Dk Mwakyembe.

Alisema kutokana na uchunguzi wa kina waliouainisha katika taarifa hiyo, kamati imejiridhisha na inatamka bayana kuwa mchakato wa zabuni ya kuzalisha umeme wa dharura wa MW 100, uliiwezesha Richmond kuteuliwa na baadaye kurithiwa na Dowans Holdings S.A, haukufuata taratibu.

"Uligubikwa na vitendo vya ukiukwaji taratibu, kanuni na sheria za nchi na hivyo kujenga kiwingu cha mashaka ya upendeleo, ubadhirifu na rushwa ambavyo vimechangia kumuongezea mwananchi mzigo wa gharama za umeme," alisema na kuongeza:

"Kamati Teule imethibitisha bila ya shaka lolote kuwa uteuzi wa Kampuni dhaifu kifedha, kiufundi na kiuzoefu na ambayo haina usajili Marekani wala Tanzania kama kampuni yenye ukomo wa hisa, yaani Richmond, ulitokana na kubebwa bila woga wala aibu na viongozi waandamizi wa Serikali".

Alisema kati ya Januari na Oktoba, 2007 Dowans Holdings S.A imewasilisha Tanesco hati za madai kwa malipo ya uwekezaji wa mitambo dola za Marekani 4,373,738.40 na uzalishaji umeme dola 16,487,495.46.

Dk Mwakyembe alisema hadi kufikia Desemba 2007, Dowans Holdings S.A inatamka kwamba Tanesco haijalipa madai yake kuanzia Januari 2007 hadi Novemba 2007, huku Benki ya CRDB Bank ikithibitisha kutofungua Barua ya Dhamana ya Benki nyingine baada ya ile ya awali ya dola za Marekani 30,696,598.

Alisema Novemba 28, 2007 Tanesco ilimwandikia Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini kuhusu mchakato wa kufidia madeni ya gharama za ucheleweshaji wa umeme dola za Marekani 10,000 kwa siku 243 za ucheleweshaji, sawa na dola 2,430,000 na marejesho ya malipo ya awali dola 1,279,026.

Mwakyembe alibainisha kuwa kampuni inatakiwa kulipwa zaidi ya Sh150 milioni kwa siku, hata kama haikuzalisha umeme gharama hizo zinabaki pale pale. Malipo yanaanza rasmi kuanzia Oktoba 4, 2007, siku ambayo uzinduzi wa mitambo ulifanyika.

 
Posted Date::2/6/2008
Serikali yashauriwa kuwaadhibu washiriki kashfa ya Richmond
Na Mwandishi Wetu
Mwananchi

KAMATI Teule ya Bunge ya Kuchunguza Mchakato wa Zabuni ya Uzalishaji Umeme wa Dharura ulioipa ushindi Kampuni ya Richmond, imependekeza viongozi wa taasisi mbalimbali waliohusika kuwajibishwa.

Hatua hiyo imefikiwa baada ya kamati kuridhika kuwa ukiukwaji mkubwa wa mchakato wa kanuni, sheria na taratibu ili kukidhi maslahi binafsi.

Taarifa ya kamati hiyo iliyowasilishwa bungeni jana na mwenyekiti wake, Dk Harrison Mwakyembe, inaonyesha jinsi Wizara ya Nishati na Madini ilivyopindisha maamuzi ya Baraza la Mawaziri kwa kusitisha mpango uliokuwa umekaribia utekelezaji wa kuzalisha umeme kupitia mitambo ya kukodi ya kampuni ya CDC Globeleq bila kuufikisha ujumbe wa serikali kwa kampuni hiyo.

Badala yake, wizara ilirekebisha masharti yao ili mradi huo utekelezwe na kwamba, uamuzi huo ulifanyika siku ile ile Baraza la Mawaziri lilipotoa maagizo, siku nne baada ya kuanza mgao wa umeme kwa mikoa yote ya Tanzania Bara inayounganishwa na Gridi na Taifa.

"Tumeonesha vilevile maamuzi yenye jeuri na kiburi ya kukiuka kwa makusudi Sheria ya Ununuzi wa Umma ya mwaka 2004 na Kanuni zake za mwaka 2005, licha ya Baraza la Mawaziri kusisitiza kwamba Sheria ya Ununuzi wa Umma na kanuni zake izingatiwe. Kama vile Wizara hiyo haihusiki kabisa na utawala wa sheria na utawala bora," alisema Dk Mwakyembe na kuongeza:

"Ikailazimisha Tanesco isiheshimu ushauri wa kitaalamu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) na kuingilia mchakato wa zabuni wa procurement entity nyingine kwa kuiweka pembeni Bodi ya Zabuni ya Tanesco, kuiagiza shirika livunje sheria kwa kuwabadilisha wajumbe wa Bodi yake ya Zabuni na Wizara kufanya maamuzi ya ununuzi kwa niaba ya Tanesco na kuulazimisha uongozi wake kusaini mkataba na kampuni ambayo Tanesco waliikataa mara tatu kwa vigezo vya kitaalamu kuwa haifai kwa kazi hiyo. Huo ulikuwa udhalilishaji mkubwa wa viongozi na watendaji ndani ya Tanesco."

Dk Mwakyembe alisema, mwezi mmoja tu kabla ya zabuni ya kuzalisha umeme wa dharura, Wizara ya Nishati na Madini ilikuwa imeiandikia Richmond Development Company LLC, kuitaarifu kuwa imeshindwa kutekeleza mkataba baina yake na wizara kuhusu mradi wa bomba la mafuta.

Alisema ukimya wa wizara kuhusu udhaifu wa Richmond Development Company LLC, kuliipa Kamati Teule mashaka kuhusu uadilifu wa viongozi wa Wizara hiyo.

"Tumeonyesha vile vile kuwa Richmond Development Company LLC ilikingiwa kifua na kufunguliwa kila mlango na Wizara: majaribio ya Richmond Development Company LLC kubadilisha masharti ya Barua ya Dhamana ya Benki (LC) yaliungwa mkono na Wizara ya Nishati na Madini kwa hamasa kubwa kiasi cha kupuuza maelekezo ya Wizara ya Fedha kwa kulazimisha kufanya mabadiliko katika LC hiyo nje ya mkataba wa makubaliano wa fedha kwenye akaunti ya escrow," alisema Dk Mwakyembe.

Miongoni mwa vielelezo vya upendeleo wa Richmond Development Company LLC, ni kuanza kazi bila kujiandikisha Bodi ya Usajili ya Makandarasi na wahandisi wake kuacha kujiandikisha Bodi ya Usajili ya Wahandisi na jinsi Wizara ya Nishati na Madini ilivyokuwa wima kuitetea kampuni hiyo ya Kimarekani.

Alisema Kamati Teule imejionea jinsi Richmond Development Company (T) Ltd, kampuni tanzu ya Richmond Development Company LLC, ilivyopata Cetificate of Incentives kutoka Tanzania Investment Centre bila kukidhi masharti ya msingi kama vile ushahidi wa mtaji wa kutosha kutekeleza mradi.

Hata hivyo, Dk Mwakyembe alisema, Tanesco waliwahi kuvunja mkataba kati yao na Richmond baada ya kampuni hiyo ya Marekani kushindwa kutekeleza sehemu yake ya mkataba na kwa kutoa taarifa za uongo kuhusu hadhi ya kampuni hiyo.

"Lakini Wizara ya Nishati na Madini iliyoingilia kati na, bila aibu, kuwezesha mkataba huo urithiwe na kampuni nyingine katika kipindi ambacho nchi ilikuwa haihitaji kabisa umeme wa ziada licha ya kuwepo fursa za wazi kisheria kwa Tanesco kuvunja mkataba huo bila ya athari za hasara zozote," alisema.

Dk Mwakyembe, ambaye kitaaluma ni Mwanasheria na aliwahi kuwa Mhadhiri wa Sheria katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, alisema ubebwaji wa Richmond na Wizara ya Nishati na Madini ulichangiwa na kurahisishwa zaidi na ukosefu wa umakini wa maafisa ndani ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Alisema badala ya kuwa washauri wa sheria wa serikali, wanageuka kuwa wasindikazaji, huku wakati mwingi wawakilishi wake hawafiki kwenye vikao, hivyo kukosa uelewa mpana wa michakato mbalimbali.

"Hata wakifika, mchango wao wa kuilinda nchi dhidi ya vifungu vya sheria vya kutumaliza, hauonekani. Katika suala hili la Richmond Development Company LLC, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ilichangia sana kulea ubabaishaji kwa kutohudhuria vikao vya majadiliano na kufumbia macho dosari bayana au pengine kutojali," alisema.

Alisema mahojiano ya Kamati Teule na Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Mwakilishi wake kwenye majadiliano ya mikataba, yanajieleza yenyewe na kwamba, ulikuwa wajibu wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kugundua kuwa Richmond sio kampuni yenye ukomo wa hisa.

Dk Mwakyembe alisema, utetezi mkuu uliotolewa na viongozi wa Wizara ya Nishati na Madini ni kwamba, nchi ilikuwa katika dharura, lakini umekataliwa na kamati kwa sababu unapotosha maana halisi ya dharura ya ununuzi ya chini ya Kanuni ya 42.

 
Posted Date::2/6/2008
Kamati ya Bunge yatoa sura tofauti za kampuni ya Richmond
Na Waandishi Wetu
Mwananchi

KAMPUNI ya Richmond Development LLC iliyopewa zabuni ya kuzalisha umeme wa dharura, sasa imebainika wazi kuwa haikuwa na sifa na uwezo bali usanii mtupu.

Taarifa ya Kamati Teule ya Bunge iliyowasilishwa jana mjini Dodoma na Mwenyekiti wake, Dk Harrison Mwakyembe, inabainisha sura mbalimbali za kampuni hiyo ambayo haikidhi vigezo vya kupewa kazi hiyo.

Dk Mwakyembe alisema, Richmond inatambulishwa kwa kina na ufasaha katika mkataba kati yake na Tanesco uliosainiwa Juni 23, 2006 kwamba ilisajiliwa chini ya sheria za Jimbo la Texas, Marekani na yenye anuani ifuatayo: 5825 Schumacher, Houston Texas 77057, Marekani.

Hata hivyo, kifungu cha 5.1 (a) cha mkataba huo kinatoa maelezo ya ziada kuhusu kampuni hiyo kuwa, ina ukomo wa hisa (limited by shares) ambayo uwepo wake Tanzania haukinzani na sheria za nchi, kifungu hicho kidogo kinamalizia kwa kutamka bayana kuwa ina nguvu na mamlaka yote stahili ya kampuni kumiliki au kukodisha, kutumia mali zake na kuendesha biashara zake kama ilivyokusudiwa Tanzania.

Dk Mwakyembe alisema uchunguzi wa kina uliofanywa na Kamati Teule ndani na nje ya nchi kwa msaada wa ofisi ya Ubalozi wa Tanzania Washington D.C, Marekani na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, ulionyesha picha tofauti na iliyomo kwenye mkataba huo.

Alisema wamejiridhisha kuwa hakuna kampuni yenye jina la Richmond Development Company LLC iliyokuwa imesajiliwa Jimbo la Texas wakati wa kusaini mkataba huo au iliyosajiliwa baada ya mkataba huo hadi Desemba 31, 2007, ripoti hiyo ilipowasilishwa kwa Spika wa Bunge.

Aliendelea kuwa, Kampuni mashuhuri ya mawakili ya Virginia, Marekani inayoitwa Hunton & Williams LLP, Oktoba 2006 ilitoa ushauri wa kitaalam kwa Bodi ya Wakurugenzi ya Tanesco, ikiituhumu Richmond Development Company LLC kwa upotoshaji wa hadhi yake kikampuni na kutoa tamko lisilo sahihi kuhusu hadhi yake chini ya sheria za Texas.

Mwenyekiti huyo alisema ukaguzi wa kumbukumbu za Katibu wa Jimbo la Texas uliofanywa na kampuni hiyo ya mawakili Oktoba 2006, ulionyesha kuwa hakuna kampuni yenye jina la �Richmond Development Company LLC� iliyokuwa imeanzishwa na kuendesha shughuli zake jimboni humo.

Alisema wajumbe wa kamati waliotembelea Marekani kati ya Desemba 10 na 16, 2007 waliambiwa na Mohamed Gire, mmiliki wa kampuni hiyo iliyoshinda zabuni ya umeme Tanzania, kuwa Richmond Development Company LLC ni jina mbadala la biashara la kampuni yake iitwayo RDEVCO LLC.

Dk Mwakyembe alisema sheria zinaweka taratibu za kuzingatia ili kuepusha vitendo vya kitapeli katika matumizi ya majina mbadala ya kibiashara.

Aalismea Tanzania na nchi zingine za Jumuiya ya Madola, zipo sheria maalum za usajili wa majina ya biashara na kwamba Marekani mtu hawezi kukurupuka na kuanza kutumia jina mbadala bila kupitia usajili maalumu.

"Katika Jimbo la Texas ambako Gire anaishi, ni kosa la jinai kutumia jina mbadala bila kulisajili. Usajili wa jina mbadala unadumu kwa miaka mitano ambapo mtumiaji lazima asajili jina hilo upya kati ya tarehe 1 Januari na 31 Disemba ya mwaka wa tano," alifahamisha.

Alisema kamati imekagua hati hiyo kwa kina na kuona kuwa, badala ya kumsaidia Gire, inazidi kuthibitisha kuwa si mfanyabiashara mwadilifu ila tapeli kwasababu ina saini ya afisa mmoja tu badala ya wawili na badala ya kutamka kuwa RDEVCO LLC imesajili jina la Richmond Development Company LLC.

Alisema anuani iliyotumiwa iliwafikisha wajumbe wa kamati yake kwenye jengo lenye jina la Richmond Printing LLC, jina walilothibitisha kuwa la kampuni iliyosajiliwa chini ya Sheria ya Kampuni yenye Ukomo wa Hisa ya Texas, kwa madhumuni ya kuendesha biashara ya uchapishaji na biashara zingine zinazoruhusiwa na sheria kwa kampuni ya aina hiyo.

Tanzania, Richmond ilianza kusikika kwa mara ya kwanza mwaka 2003 na kwa kishindo likihusishwa na mradi mkubwa wa takriban Sh400 bilioni wa ujenzi wa bomba la mafuta la urefu wa kilomita 1,150 kutoka Dar es Salaam-Mwanza.

Kutokana na upungufu huo mkubwa, Wizara ya Nishati na Madini ilisita kuipa RDC mradi huo muhimu na kuitaka kwanza irekebishe yaliyojitokeza.

"Richmond Development Company LLC, kwa maneno mengine, si kampuni ya mchana bali ya usiku, kampuni ya mfukoni au ya sanduku la barua (mail box company)! Hiyo ndiyo kampuni ambayo shirika la umma, Tanesco, iliingia nayo mkataba wa mabilioni ya fedha za walipa kodi wa Tanzania," alisema.

Alisema Kampuni ya Wanasheria ya Marekani ya Hunton & Wiliams LLP, iliyopewa kazi na Bodi ya Wakurugenzi ya Tanesco kuichunguza Richmond Development Company LLC, inathibitisha kuwa Juni 23, 2006 siku ambayo mkataba huo ulisainiwa, Richmond Development Company LLC haikuwa na nguvu za kisheria wala mamlaka yoyote ya kikampuni kuiwezesha kuendesha shughuli zake Tanzania.

Kamati Teule ilibaini kutokana na ushauri mbalimbali iliopata wa kisheria, kuwa tatizo la uhalali wa Richmond ya Tanzania lilikuwa pale pale kwani kifungu cha 3(1) cha Sheria ya Makampuni kinataka watu wawili au zaidi kuwa na uwezo wa kufungua kampuni.

"Ni wazi kuwa picha iliyojengwa kwenye mkataba tunaouongelea hapa kuhusu hadhi na uhalali wa Richmond Development Company LLC nchini Tanzania, ilikuwa ya kisanii, ya uongo na isiyo na msingi wowote kisheria," alisema na kuongeza:

"Kinachosikitisha hapa ni kuwa Februari 2006, yaani mwezi moja tu baada ya Wizara ya Nishati na Madini kuiandikia barua Richmond Development Company LLC kuwa haina imani nayo, kampuni hiyo ya Gire, ikajitosa kwenye zabuni nyingine ya Wizara hiyo hiyo ya Nishati na Madini, zabuni ya kuingiza nchini jenereta za kuzalishia umeme wa dharura wa Megawati 100."

Alisema serikali ingejaribu kuchunguza sifa za rejareja za Richmond Development Company LLC hata kwa kuandikia Ubalozi wa Marekani Dar es Salaam au kukagua tovuti yake (www.rdevco.com), ukweli ungelidhihirika kuwa sio chochote wala lolote.

Dk Mwakyembe alisema, tovuti yake imesheheni makosa madogo madogo ya Kiingereza na kupambwa na taarifa za juu juu za miradi ambayo �kampuni� hiyo inadai kuitekeleza, hivyo kuzua maswali mengi hali inayoashiria upeo mdogo wa elimu wa wamiliki wa kampuni hiyo.

 
Hii kampuni ya Richmond printing inayomilikiwa na Mohamed Gire (the same one of rdevco) ilifutiwaga kibali kwasababu ya kutolipa kodi, ikarudishiwa kibali 1996 cha biashara baada ya kulipa hizo kodi. I have attached a copy of the reinstatement letter kutoka kwa Mohamed Gire akiomba kampuni yake irudishiwe ruksa ya kufanya biashara.

Lazima wachunguzwe hawa huko marekani, waambie wabunge wawaambie ubalozi wa marekani huko wasaidie.
 

Attachments

Its shameful, i don't know why we are not patriotic,whyyyyyyyyyyyyyyyyy, by the way i here the rumors that this guy, Mo' Gire is a Tanzanian
 
Do you know that!

Every Second that ticks TANESCO pays the white elephant - Richmond 'Printing company' Limited, One point five US dollars (US$ 1.5 per second)!

This is a country where current world bank statistics shows that per capita income is US$ 350 per year(360 days) that means on average, virtually all Tanzanians are living under one dollar a Day, while Richmond 'pekee' is paid US$1.5 everysecond.

Well, may be dollar may be confusing lets put this way:-

TANESCO pays Richmond Tshs 105,000/= every minute! Every minute! Day and Night, regardless whether there is production or not…that means by the time you finish reading this three minutes mail, Richmond has banked Tshs 315,000!

This means that every 10 minutes! Poor Tanzanians pays the white elephant - Richmond Company One million Tanzanian Shillings (Tshs 1,000,000/=) every ten minutes.

By the end of business today you will still have to pay Tshs 152,000,000 to Richmond which will go to Richminds!.

NB:Newly Swahili jargons 'Bangusilo'Scapegoat' and Kilongola' Accountable leader'.
 
Back
Top Bottom