Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 28,297
- 68,017
SAKATA LA KIFO CHA KATIBU NA KILE ALICHOTUACHIA.
Na Robert Heriel
Ishu hii inasikitisha na kuhuzunisha mno. Ni tukio baya pia linalofedhehesha.
Tukio la unyama na udhalilishaji uliovuka mipaka kuvua Utu WA Mtu.
Unapozungumzia kutoka na Mke WA Mtu sio Jambo la mchezo. Kila mtu anajua Kwa namna yake maumivu yake.
Hata hivyo nimeshangaa baadhi ya watu wakifurahia na kuleta mizaha kwenye sakata hili. Haipendezi, kwani sio tukio zuri kimaadili na Kwa kizazi kinachochipuka.
Tukio hili linamakosa makubwa matatu.
1. Usaliti
2. Uongo
3. Uuaji
1. Usaliti.
Iwe isivyo Usaliti ndio chanzo kikuu cha Jambo hili. Kutokuwa na uaminifu Kati ya wahusika.
Katika usaliti kuna Aina mbili ya Wasaliti,
i. Msaliti WA wazi
ii. Msaliti wa kificho.
Hata hivyo Kwa kesi za namna hii ambazo mmoja amekufa ni rahisi marehemu kubebeshwa zigo la Usaliti wa wazi.
Hata hivyo Msaliti WA kificho lazima awepo tuu kivyovyote ingawaje watu huweza kumficha lakini mazingira au ushahidi humfichua.
Unajua ni Kwa nini? Ni Kwa sababu Msaliti wa wazi(mtuhumiwa) mara nyingi hushirikiana na Msaliti WA kificho.
Kama sivyo, Msaliti WA kificho angetakiwa atoe ripoti mapema ili kujenga Trust Kwa kutoshirikiana na Msaliti lakini kitendo cha kuficha mchakato mzima alafu kuja kusema wakati tukio linatokea, kiukweli sio rahisi kueleweka.
2. Uongo
Palipo na usaliti lazima uongo utumike kivyovyote. Uongo ndio unaoratibu usaliti.
Kumbuka usaliti mara zote hufanyika Kwa Siri. Ili ukweli usijulikane. Kwa tukio la namna hii mhusika mmoja akiwa amekufa/hayupo ni rahisi Ukweli mwingi kufichwa.
Na mhusika huyo kubebeshwa hata mizigo isiyo ya kweli.
Kisheria au kimahakama, huwezi sikiliza upande mmoja, lazima usikilize pande zote mbili. Sasa Kama upande mmoja haupo basi ni muhimu kivyovyote uchunguzi kufanyika.
Matukio ya namna hii ya usaliti yaliyojengwa Kwa kamba ya uongo ni kawaida majibu ya uongo kupatikana.
Kumbuka mchakato mzima ulikuwa ni Wa Siri tena Siri za usaliti, hivyo hatutegemei wahusika wa tukio walilofanya sirini waseme kweli hadharani. Hiyo kwenye Logic haliwezekaniki.
Kama walikuwa wanaficha wakiwa sirini utategemea waseme kweli hadharani? Tena mmoja akiwa hayupo? Never!
3. Uuaji/ Mauaji.
Malipo ya usaliti mara nyingi ni KIFO. Hiyo ni kawaida ya nature.
Kuna Aina ya vifo katika suala la usaliti.
1. Kujiua
2. Kuuawa
3. Kufa Kwa Ajali.
1. Kujiua
Hii ilitokea hata Kwa Yuda aliyemsaliti Yesu.
Hii ni matokeo ya hatia ya nafsini mwa mtu. Mtu anaamua kujiua ili kuepukana na mzigo wa hatia nafsini mwake.
Hata hivyo hii ni nadra Sana kutokea Kwa mazingira ya Usaliti wa Sirini.
Mfano, mtu uwe unamsaliti Mumeo/Mkeo, hajui. Anakufanyia mazuri siku zote. Hutoweza kujiua ingawaje utakuwa unahisi Hatia.
Mara nyingi watu hujiua pale watu wengi wanapojua Usaliti wao.
Kwa kisa kama cha Yuda, Yuda kama isingegundulika na watu wengi kwamba yeye ndiye Msaliti WA Yesu uwezekano WA kujiua ungekuwa ni mdogo.
Mara nyingi ukubwa wa hatia na aibu ndio huamua mtu kujiua Kwa habari za Usaliti.
Tukio linaloendelea linanjia mbili, kama Mhusika anayesalitiwa hakuwa anajua na hapa namzungumzia Baba mchungaji, basi uwezekano wa marehemu kujiua ni mdogo.
Kwani hakuna sababu ya kujiua ikiwa mtu tayari anamke, na Kama ni katongoza kanyimwa ni ishu ya kawaida.
Lakini kama Aliyesalitiwa alijua basi kuna uwezekano marehemu alijiua Kwa Hatia na aibu kutokana na mahusiano ya karibu baina yao.
ii. Kuuawa.
Katika usaliti wa mapenzi mtu huweza kuuawa Kwa namna mbili;
Moja, anayeibiwa mke/mumeo kujua hivyo anaweza ratibu mauaji.
Pili, Wasaliti(wanaochepuka pamoja) kugeukana, Kwamba mchepukaji mmoja anaweza kutaka kusitisha mahusiano hayo ya Siri wakati mwingine akawa ndio amekolea.
Sasa huyu anayetaka yaendelee anageuka tishio Kwa asiyetaka yaendelee. Huyu asiyetaka yaendelee mara nyingi lazima awe na hadhi ya juu kuliko mwenzake kikawaida, hivyo Kwa kuogopa aibu itampasa alazimishe kuyakatisha hayo mahusiano.
Hii inaweza sababisha Mchepuko kuandaa Mchakato wa mauaji kuficha usaliti wao.
Mauaji ya hivi ni ngumu Sana kuyashtukia ukilinganisha na Yale ya aliyeibiwa mke au mume, kwani aliyeibiwa mke au mume hufanya mauaji Kwa hisia za hasira Kali ya wivu WA mapenzi.
Wakati Msaliti mchepuko kumgeuka na kumuua mwenzake hutumia akili zaidi kuliko Hisia. Kwani Hana chuki na mtu anayemuua isipokuwa ni ishu ya maslahi tuu yasiyogusa wivu wa mapenzi.
3. Kufa Kwa Ajali.
Hii inatokea pale unatokea pale unakimbia kufumaniwa au kufumania na kujikuta katika Ajali inayosababisha mauti ya mtu.
Hii mara nyingi haiwezi kuwa tukio la mauaji Ila litahesabika kama Ajali iliyosababisha Kifo.
Usaliti unaleta uchungu unaosababisha wivu uifanye akili isiwe makini.
Katika kuendea mambo haya kuna mambo ya kuzingatia;
1. Ukaribu na mazoea
Ukaribu wa mwenza na watu wengine.
Kikawaida atakayechepuka na Mume au mke wako ni walewale watu waliokaribu naye. Aidha wanaofanya kazi pamoja, au mashemeji wanaotaniana naye.
Kisheria mke au mume WA mtu hapaswi kuwa na mazoea ya namna yoyote na Mtu wa jinsia nyingine.
Ni vile tuu Dunia ya sasa watu wamekuwa wabishi tuu. Lakini hakunaga urafiki baina ya mwanamke na Mwanaume.
2. Muda wa mahusiano
Ni uongo wa wazi kabisa, ati mtu akutongoze leo alafu umkatalie leoleo alafu kesho aende akajiue. Huo ni uongo.
Lazima kuna ukomavu wa mahusiano baina ya wahusika.
Ujambazi na wizi ndio hauna muda katika mauaji. Yaani unaweza kuuawa na Majambazi au wezi bila hata ya muda wa ukomavu.
Lakini kwenye mapenzi, ili mtu ajiue kisa wewe basi lazima Factor ya Muda wa katika mahusiano lazima uwe ni factor kuu.
3. Usiri
Ogopa mtu ambaye anakuambia msichunguzane. Huyo ni mhuni. Hakuna mapenzi bila kuchunguzana. Hayo sio mahusiano. Mahusiano mazuri lazima watu wachunguzane.
Ukiona mambo ya usiri yapo kwenye relationship yako ujue hapo hakuna mahusiano.
Usaliti umejengwa katika msingi wa Haiti weka akilini hiyo.
Wakati upendo umejengwa katika msingi wa Uwazi.
Taikon huwaga nasema, siwezi ishi na mtu nisiyemchunguza nikajua kinachoendelea, Sisi wengine tunaumia zaidi pale tusipojua kinachoendelea, kiasili ni wapelelezi, tunapeleleza kila kitu kinachotuhusu, sio kazi na Miradi tuifanyayo, sio watoto wetu, sio Mali zetu n.k. Sisi tunajua umuhimu wa kupata taarifa mapema. Tunajua informations is power.
Nawambia usikubali kuishi na mtu alafu usimchunguze mtakuja kupata ambush hiyo itakayowaacha mdomo wazi.
Ukisikia Kanuni isemayo, Trust no one maana yake ndio hiyo. Usiwe comfortable kama Mpumbavu.
4. Usimuamini Mwanamke hata ungeshikiwa bunduki.
Kanuni hii itakufanya usiumie kiboya boya. Itakufanya muda wote uwe macho, uwe Makini na kila nyendo ya Mkeo.
Zingatia Wanawake wanakawaida ya kufanya juu chini ili umuamini. Hilo asije aka-achieve kwako. Hakikisha mwanamke Ajue kuwa haumuamini. Ili kazi yake iwe kukuaminisha kuwa yeye ni muaminifu.
Zingatia ili mwanamke achepuke ni lazima ahakikishe mumewe anamuamini Sana.
Au kama haumuamini basi atatoka na mtu unayemuamini😂😂 Yaani Yule ambaye unaamini hawezi kukugeuka ndiye huyohuyo Mkeo anaweza kutoka naye miaka nenda Rudi.
Usipomuamini mwanamke itakufanya uwe makini na nyendo zake,..
Weka akili hii; Mwanamke hata uwe muaminifu kwake kiasi gani kamwe hawezi kukuamini Kwa sababu kiasili yeye sio mwaminifu(rahisi kudanganywa) na Dalili pekee ya kuthibitisha maneno yangu ni kuhusu tabia Yao ya kukupeleleza.
Mwanamke kila utakalo lifanya atakuwa analizingatia, kila utakalolisema litamuingia kichwani na atalikumbuka,
Ingawaje atakuwa msahalifu wa mambo mengine Kama ya majukumu yake ya nyumbani lakini kamwe mambo yanayokuhusu au utakayoyasema mdomoni mwako hawezi kuyasahau.
Mwanamke anakupeleleza kila iitwapo leo Kwa sababu hakuamini. Iweje wewe umuamini.
Wanaume wajanja na wahuni hutengeneza Trust Kwa wake zao ili kuweza kuchepuka Kwa urahisi bila kushtukiwa.
Huwapa wake zao Simu zao watumie muda wote, ikiwezekana mpaka Kadi ya benk na namba za Siri.
Nipumzike Sasa
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Na Robert Heriel
Ishu hii inasikitisha na kuhuzunisha mno. Ni tukio baya pia linalofedhehesha.
Tukio la unyama na udhalilishaji uliovuka mipaka kuvua Utu WA Mtu.
Unapozungumzia kutoka na Mke WA Mtu sio Jambo la mchezo. Kila mtu anajua Kwa namna yake maumivu yake.
Hata hivyo nimeshangaa baadhi ya watu wakifurahia na kuleta mizaha kwenye sakata hili. Haipendezi, kwani sio tukio zuri kimaadili na Kwa kizazi kinachochipuka.
Tukio hili linamakosa makubwa matatu.
1. Usaliti
2. Uongo
3. Uuaji
1. Usaliti.
Iwe isivyo Usaliti ndio chanzo kikuu cha Jambo hili. Kutokuwa na uaminifu Kati ya wahusika.
Katika usaliti kuna Aina mbili ya Wasaliti,
i. Msaliti WA wazi
ii. Msaliti wa kificho.
Hata hivyo Kwa kesi za namna hii ambazo mmoja amekufa ni rahisi marehemu kubebeshwa zigo la Usaliti wa wazi.
Hata hivyo Msaliti WA kificho lazima awepo tuu kivyovyote ingawaje watu huweza kumficha lakini mazingira au ushahidi humfichua.
Unajua ni Kwa nini? Ni Kwa sababu Msaliti wa wazi(mtuhumiwa) mara nyingi hushirikiana na Msaliti WA kificho.
Kama sivyo, Msaliti WA kificho angetakiwa atoe ripoti mapema ili kujenga Trust Kwa kutoshirikiana na Msaliti lakini kitendo cha kuficha mchakato mzima alafu kuja kusema wakati tukio linatokea, kiukweli sio rahisi kueleweka.
2. Uongo
Palipo na usaliti lazima uongo utumike kivyovyote. Uongo ndio unaoratibu usaliti.
Kumbuka usaliti mara zote hufanyika Kwa Siri. Ili ukweli usijulikane. Kwa tukio la namna hii mhusika mmoja akiwa amekufa/hayupo ni rahisi Ukweli mwingi kufichwa.
Na mhusika huyo kubebeshwa hata mizigo isiyo ya kweli.
Kisheria au kimahakama, huwezi sikiliza upande mmoja, lazima usikilize pande zote mbili. Sasa Kama upande mmoja haupo basi ni muhimu kivyovyote uchunguzi kufanyika.
Matukio ya namna hii ya usaliti yaliyojengwa Kwa kamba ya uongo ni kawaida majibu ya uongo kupatikana.
Kumbuka mchakato mzima ulikuwa ni Wa Siri tena Siri za usaliti, hivyo hatutegemei wahusika wa tukio walilofanya sirini waseme kweli hadharani. Hiyo kwenye Logic haliwezekaniki.
Kama walikuwa wanaficha wakiwa sirini utategemea waseme kweli hadharani? Tena mmoja akiwa hayupo? Never!
3. Uuaji/ Mauaji.
Malipo ya usaliti mara nyingi ni KIFO. Hiyo ni kawaida ya nature.
Kuna Aina ya vifo katika suala la usaliti.
1. Kujiua
2. Kuuawa
3. Kufa Kwa Ajali.
1. Kujiua
Hii ilitokea hata Kwa Yuda aliyemsaliti Yesu.
Hii ni matokeo ya hatia ya nafsini mwa mtu. Mtu anaamua kujiua ili kuepukana na mzigo wa hatia nafsini mwake.
Hata hivyo hii ni nadra Sana kutokea Kwa mazingira ya Usaliti wa Sirini.
Mfano, mtu uwe unamsaliti Mumeo/Mkeo, hajui. Anakufanyia mazuri siku zote. Hutoweza kujiua ingawaje utakuwa unahisi Hatia.
Mara nyingi watu hujiua pale watu wengi wanapojua Usaliti wao.
Kwa kisa kama cha Yuda, Yuda kama isingegundulika na watu wengi kwamba yeye ndiye Msaliti WA Yesu uwezekano WA kujiua ungekuwa ni mdogo.
Mara nyingi ukubwa wa hatia na aibu ndio huamua mtu kujiua Kwa habari za Usaliti.
Tukio linaloendelea linanjia mbili, kama Mhusika anayesalitiwa hakuwa anajua na hapa namzungumzia Baba mchungaji, basi uwezekano wa marehemu kujiua ni mdogo.
Kwani hakuna sababu ya kujiua ikiwa mtu tayari anamke, na Kama ni katongoza kanyimwa ni ishu ya kawaida.
Lakini kama Aliyesalitiwa alijua basi kuna uwezekano marehemu alijiua Kwa Hatia na aibu kutokana na mahusiano ya karibu baina yao.
ii. Kuuawa.
Katika usaliti wa mapenzi mtu huweza kuuawa Kwa namna mbili;
Moja, anayeibiwa mke/mumeo kujua hivyo anaweza ratibu mauaji.
Pili, Wasaliti(wanaochepuka pamoja) kugeukana, Kwamba mchepukaji mmoja anaweza kutaka kusitisha mahusiano hayo ya Siri wakati mwingine akawa ndio amekolea.
Sasa huyu anayetaka yaendelee anageuka tishio Kwa asiyetaka yaendelee. Huyu asiyetaka yaendelee mara nyingi lazima awe na hadhi ya juu kuliko mwenzake kikawaida, hivyo Kwa kuogopa aibu itampasa alazimishe kuyakatisha hayo mahusiano.
Hii inaweza sababisha Mchepuko kuandaa Mchakato wa mauaji kuficha usaliti wao.
Mauaji ya hivi ni ngumu Sana kuyashtukia ukilinganisha na Yale ya aliyeibiwa mke au mume, kwani aliyeibiwa mke au mume hufanya mauaji Kwa hisia za hasira Kali ya wivu WA mapenzi.
Wakati Msaliti mchepuko kumgeuka na kumuua mwenzake hutumia akili zaidi kuliko Hisia. Kwani Hana chuki na mtu anayemuua isipokuwa ni ishu ya maslahi tuu yasiyogusa wivu wa mapenzi.
3. Kufa Kwa Ajali.
Hii inatokea pale unatokea pale unakimbia kufumaniwa au kufumania na kujikuta katika Ajali inayosababisha mauti ya mtu.
Hii mara nyingi haiwezi kuwa tukio la mauaji Ila litahesabika kama Ajali iliyosababisha Kifo.
Usaliti unaleta uchungu unaosababisha wivu uifanye akili isiwe makini.
Katika kuendea mambo haya kuna mambo ya kuzingatia;
1. Ukaribu na mazoea
Ukaribu wa mwenza na watu wengine.
Kikawaida atakayechepuka na Mume au mke wako ni walewale watu waliokaribu naye. Aidha wanaofanya kazi pamoja, au mashemeji wanaotaniana naye.
Kisheria mke au mume WA mtu hapaswi kuwa na mazoea ya namna yoyote na Mtu wa jinsia nyingine.
Ni vile tuu Dunia ya sasa watu wamekuwa wabishi tuu. Lakini hakunaga urafiki baina ya mwanamke na Mwanaume.
2. Muda wa mahusiano
Ni uongo wa wazi kabisa, ati mtu akutongoze leo alafu umkatalie leoleo alafu kesho aende akajiue. Huo ni uongo.
Lazima kuna ukomavu wa mahusiano baina ya wahusika.
Ujambazi na wizi ndio hauna muda katika mauaji. Yaani unaweza kuuawa na Majambazi au wezi bila hata ya muda wa ukomavu.
Lakini kwenye mapenzi, ili mtu ajiue kisa wewe basi lazima Factor ya Muda wa katika mahusiano lazima uwe ni factor kuu.
3. Usiri
Ogopa mtu ambaye anakuambia msichunguzane. Huyo ni mhuni. Hakuna mapenzi bila kuchunguzana. Hayo sio mahusiano. Mahusiano mazuri lazima watu wachunguzane.
Ukiona mambo ya usiri yapo kwenye relationship yako ujue hapo hakuna mahusiano.
Usaliti umejengwa katika msingi wa Haiti weka akilini hiyo.
Wakati upendo umejengwa katika msingi wa Uwazi.
Taikon huwaga nasema, siwezi ishi na mtu nisiyemchunguza nikajua kinachoendelea, Sisi wengine tunaumia zaidi pale tusipojua kinachoendelea, kiasili ni wapelelezi, tunapeleleza kila kitu kinachotuhusu, sio kazi na Miradi tuifanyayo, sio watoto wetu, sio Mali zetu n.k. Sisi tunajua umuhimu wa kupata taarifa mapema. Tunajua informations is power.
Nawambia usikubali kuishi na mtu alafu usimchunguze mtakuja kupata ambush hiyo itakayowaacha mdomo wazi.
Ukisikia Kanuni isemayo, Trust no one maana yake ndio hiyo. Usiwe comfortable kama Mpumbavu.
4. Usimuamini Mwanamke hata ungeshikiwa bunduki.
Kanuni hii itakufanya usiumie kiboya boya. Itakufanya muda wote uwe macho, uwe Makini na kila nyendo ya Mkeo.
Zingatia Wanawake wanakawaida ya kufanya juu chini ili umuamini. Hilo asije aka-achieve kwako. Hakikisha mwanamke Ajue kuwa haumuamini. Ili kazi yake iwe kukuaminisha kuwa yeye ni muaminifu.
Zingatia ili mwanamke achepuke ni lazima ahakikishe mumewe anamuamini Sana.
Au kama haumuamini basi atatoka na mtu unayemuamini😂😂 Yaani Yule ambaye unaamini hawezi kukugeuka ndiye huyohuyo Mkeo anaweza kutoka naye miaka nenda Rudi.
Usipomuamini mwanamke itakufanya uwe makini na nyendo zake,..
Weka akili hii; Mwanamke hata uwe muaminifu kwake kiasi gani kamwe hawezi kukuamini Kwa sababu kiasili yeye sio mwaminifu(rahisi kudanganywa) na Dalili pekee ya kuthibitisha maneno yangu ni kuhusu tabia Yao ya kukupeleleza.
Mwanamke kila utakalo lifanya atakuwa analizingatia, kila utakalolisema litamuingia kichwani na atalikumbuka,
Ingawaje atakuwa msahalifu wa mambo mengine Kama ya majukumu yake ya nyumbani lakini kamwe mambo yanayokuhusu au utakayoyasema mdomoni mwako hawezi kuyasahau.
Mwanamke anakupeleleza kila iitwapo leo Kwa sababu hakuamini. Iweje wewe umuamini.
Wanaume wajanja na wahuni hutengeneza Trust Kwa wake zao ili kuweza kuchepuka Kwa urahisi bila kushtukiwa.
Huwapa wake zao Simu zao watumie muda wote, ikiwezekana mpaka Kadi ya benk na namba za Siri.
Nipumzike Sasa
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam