Sakata la kutoridhika na utendaji wa serikali

Sakata la kutoridhika na utendaji wa serikali

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Kumekucha!

Vilio vya kutoridhika na utendaji wa serikali ambavyo vimekuwapo kwa miaka mingi, hatimaye sasa vinasikika kila kona:

IMG_20210715_213635_704.jpg


1. Zinazoitwa tozo za uzalendo,
2. Kodi zaidi zikiwamo kwenye mafuta ya vyombo vya moto,
3. Ongezea la nauli za mabasi na usafiri kwa ujumla kutokana #2,
4. Kuongezeka kwa mfumuko wa bei zaidi kwenye bidhaa na huduma zote kutokana na #2 na #3,
5. Nk

Kwa hakika havikubaliki. Serikali inabidi ijitathmini haraka na kufanya marekebisho mapema.

Kwamba posho za wabunge, Mawaziri, na vigogo wengine hazitambui tozo, kodi wala uzalendo hii nayo haikubaliki. Kwamba kuna wabunge bungeni kinyume cha sheria wakilipwa mabilioni ya pesa hili nalo haikubaliki. Kwamba kuna ufujaji wa pesa kwa mujibu CAG kuhusisha BOT, TPA, nk, haya hayakubaliki.

Kwamba kuna mashirika yanayozalisha hasara kwa taifa, nayo haikubaliki.

Nasi wahanga wa songombingo hizi za serikali, mambo ya kuweka maslahi ya vyama kichawa chawa yafike mwisho. Tuweke maslahi ya taifa mbele. Kwa pamoja tuwakemee wanaotaka kutufanya watwana katika nchi yetu wenyewe kwa kutanguliza ubinafsi wao mbele.

Hawa ni watumishi wetu wala si watawala wetu. Hawa ndiyo wanaotakiwa kutupigia sisi magoti yakiwamo pia makofi ya kutushangilia. Tunapaswa kuwafahamisha uvumilivu wetu umefika kikomo.

Kwa pamoja tunaweza.

Down na uchawa chawa uchwara wa vyama, wote !!!!!
 
Serikali imeshamshinda mama hii. huko BOT na TPA watu wamejichotea mahela lakini hawaguswi tumebakia kupigwa sound tu. anayeshushiwa rungu ni mwananchi wa kipato cha chini . wtf

Si sahihi kutozana tozo kwa majina ya uzalendo hali pesa lukuki zikipotea ndivyo sivyo.

1. Wabunge 19 bungeni kinyume cha utaratibu
2. Wizi wa pesa kwa mujibu wa CAG
3. Hasara za kuzalishwa na mashirika
4. Nk

Hayakubaliki.

Ukiongezea na hizi tozo na kodi juu, kwa hakika hii ni big NO!

Maendeleo hayana chama!
 
Wee nguchiru endelea na kampeni yako ya kuvuaa barakoa na kuongeza hofu juu ya Corona.
This is the only thing that you're capable of it. Wacha mle na mshibe Uhuru wa kutukana na democrasia ya kishoga.

Nguchiro ni wewe. Profile yako inaongea zaidi:

IMG_20210715_182340_353.jpg


Ni wale wa Msimu. Karibu hii ni wave #3.

Ila tufahamiane, hamtutishi.
 
Bado sasa tutakatwa tozo kwenye ndoa,kisha tozo kwenye imani na mwisho kabisa tozo ya ongezeko wa thamani kwenye uhai, kila mwananchi alipe 10% ya ongezeko wa umri na akishindwa kulipa sheria kali za wanasiasa zichukue mkondo wake.
 
Bado sasa tutakatwa tozo kwenye ndoa,kisha tozo kwenye imani na mwisho kabisa tozo ya ongezeko wa thamani kwenye uhai, kila mwananchi alipe 10% ya ongezeko wa umri na akishindwa kulipa sheria kali za wanasiasa zichukue mkondo wake.

Tusipowakemea tutarajie kodi ya kuwa hai.
 
Kumbe ukiachana na upuuzi wa corona unakuaga na akili.
Acha uduanzi tushikamane Tanzania ni yetu sio ya wajinga wajinga wachache
 
Tusipowakemea tutarajie kodi ya kuwa i.
Kama niwazavyo ni sahihi basi tuwe na roho ya kiungwana kabisa kukubali hata kuichangia serikali nusu ya kila tulicho nacho kwa kuwa tulikubali bila shuruti kubatizwa kuwa wanyonge. Tuauige mfano wa enzi za utawala wa ki chief ambapo wananchi walikuwa wanaporwa kila kitu in the name of royal family.
 
Kama niwazavyo ni sahihi basi tuwe na roho ya kiungwana kabisa kukubali hata kuichangia serikali nusu ya kila tulicho nacho kwa kuwa tulikubali bila shuruti kubatizwa kuwa wanyonge. Tuauige mfano wa enzi za utawala wa ki chief ambapo wananchi walikuwa wanaporwa kila kitu in the name of royal family.

Hata nusu haitawatosha. Uzoefu ni kuwa wakipewa 5 watataka 10.

Njia pekee ni kuwapa lugha wanayoielewa zaidi - ile kauli ya Mungu.
 
Huyu jamaa waga mpuuzi Sana,naona Sasa promotion ya Corona imekuwa overwhelmed na tozo ya uzalendo.
Nyumbu ni nyumbu tu hata Kama waga anakunywa bia

Mpuuzi mbona ni wewe? "Waga" ndiyo lugha za huko kwenu?

Corona tunasubiri chanjo hakuna jipya huko - mwendo mdundo!

Usiache kujifunza kiswahili jombi. Bila shaka huko shamba jogoo eti ndiyo wewe 😂😂😂😂😂.

Hiiiiii bagosha!
 
Kuna watu wanamshauri huyu bibi vibaya ilimradi tu marehemu aonekane alikuwa anayaweza na asiposhtuka mapema, stori itajirudia.
Mama anajiangusha mwenyewe. Hivi kweli mtu kama Mwingulu anafaa kuwa hata naibu waziri tu? Hivi huyu mama ''kichaa'' wa wizara ya Afya amefikaje hapo? Kosa kubwa la mama ni kuendelea na uozo aliacha Magufuli. Akitaka kuongoza vizuri ni lazima afanye maamuzi magumu sana. Akubali kubadili mfumo wetu wa utawala na jinsi tunavyopata viongozi wetu. Kwa hali ilivyo sasa hata ukimpa urais Lissu au Obama hakitabadilika kitu. Mimi naamini baada ya mwaka rais Samia atakuwa amechuja kweli kweli.
 
Tatizo kupitishwa kwa bajeti huwa kunafanywa kama formality, hakuna mwenye nguvu ya kuizuia bajeti...wamezoea tutalamika halafu baada ya siku 2 ama 3, kelele zitapungua na maisha yataendelea tu !
 
Mama anajiangusha mwenyewe. Hivi kweli mtu kama Mwingulu anafaa kuwa hata naibu waziri tu? Hivi huyu mama ''kichaa'' wa wizara ya Afya amefikaje hapo? Kosa kubwa la mama ni kuendelea na uozo aliacha Magufuli. Akitaka kuongoza vizuri ni lazima afanye maamuzi magumu sana. Akubali kubadili mfumo wetu wa utawala na jinsi tunavyopata viongozi wetu. Kwa hali ilivyo sasa hata ukimpa urais Lissu au Obama hakitabadilika kitu. Mimi naamini baada ya mwaka rais Samia atakuwa amechuja kweli kweli.

Kutokuona matatizo yaliyopo kwenye katiba iliyopo na kutaka kuikumbatia kama ilivyo ndiyo mwanzo wa udhaifu wenyewe.

Hayupo mwenye nia ya kuitoa nchi hii kutoka hapa ilipo atakayeikumbatia katiba hii, labda awe ni mwenye maslahi binafsi ya kutosha tu.
 
Tatizo kupitishwa kwa bajeti huwa kunafanywa kama formality, hakuna mwenye nguvu ya kuizuia bajeti...wamezoea tutalamika halafu baada ya siku 2 ama 3, kelele zitapungua na maisha yataendelea tu !

Hadi pale watakapoisikia kauli yetu kama wananchi ndipo watapotambua nchi ni yetu na waliyo nayo ni dhamana tu kwa niaba yetu.
 
Kumekucha!

Vilio vya kutoridhika na utendaji wa serikali ambavyo vimekuwapo kwa miaka mingi, hatimaye sasa vinasikika kila kona:

1. Zinazoitwa tozo za uzalendo,
2. Kodi zaidi zikiwamo kwenye mafuta ya vyombo vya moto,
3. Ongezea la nauli za mabasi na usafiri kwa ujumla kutokana #2,
4. Kuongezeka kwa mfumuko wa bei zaidi kwenye bidhaa na huduma zote kutokana na #2 na #3,
5. Nk

Kwa hakika havikubaliki. Serikali inabidi ijitathmini haraka na kufanya marekebisho mapema.

Kwamba posho za wabunge, Mawaziri, na vigogo wengine hazitambui tozo, kodi wala uzalendo hii nayo haikubaliki. Kwamba kuna wabunge bungeni kinyume cha sheria wakilipwa mabilioni ya pesa hili nalo haikubaliki. Kwamba kuna ufujaji wa pesa kwa mujibu CAG kuhusisha BOT, TPA, nk, haya hayakubaliki.

Kwamba kuna mashirika yanayozalisha hasara kwa taifa, nayo haikubaliki.

Nasi wahanga wa songombingo hizi za serikali, mambo ya kuweka maslahi ya vyama kichawa chawa yafike mwisho. Tuweke maslahi ya taifa mbele. Kwa pamoja tuwakemee wanaotaka kutufanya watwana katika nchi yetu wenyewe kwa kutanguliza ubinafsi wao mbele.

Hawa ni watumishi wetu wala si watawala wetu. Hawa ndiyo wanaotakiwa kutupigia sisi magoti yakiwamo pia makofi ya kutushangilia. Tunapaswa kuwafahamisha uvumilivu wetu umefika kikomo.

Kwa pamoja tunaweza.

Down na uchawa chawa uchwara wa vyama, wote !!!!!

E0NhMwdXIAAW0HL (1).jpeg
 
Hadi pale watakapoisikia kauli yetu kama wananchi ndipo watapotambua nchi ni yetu na waliyo nayo ni dhamana tu kwa niaba yetu.
Sauti yetu wanaisikia lakini hawaisikilizi, ni kama kelele za chura...hazimzuii tembo kunywa maji. Wananchi ndio tunatakiwa kutambua kuwa sisi ndio wenyenchi, hapo ndio unaweza kutegemea mabadiliko !
 
Back
Top Bottom