Elections 2010 Sakata la mauaji ya Dereva wa CCM Maswa na hatima ya Shibuda

CCM waache siasa hizi za ajabu ajabu kama hivi, then wao ndio wataleta balaa
 
Nimetoa mfano wa Hassan Nzege ambaye alikuwa mwandishi wa habari na mwendeshaji wa vipindi vya televisheni kwa kutumia jukwaa lake hilo aliandika na kutoa taarifa za upande mmoja kushawishi kundi lingine na kilichotokea mpaka leo tunajua huko rwanda sasa kwa kuwa pasco ni mzoefu katika uandishi na vipindi vya televisheni alitakiwa awe na taarifa za kutosha kuhusu vitu hivi sio anakurupuka tu kama alivyofanya hivyo na aishie kusema anafuatilia upande wa pili - wakati ujumbe umeshatumwa umeshaingia vichwani mwa watu watu wameshaanza kupata woga na aina nyingine ya chuki kwenye jamii -- kwa sababu tu ana uwezo wa kuandika na kutoa mawazo yake
 
Radhi siombi msimamo wangu ni huo aandike habari zake kwa umakini sio kwa ushabiki yeye ni mzoefu wa haswa televisheni anajua anachofanya


Shy pls read the post between its line, part of it reads:

Kwa vile Shibuda ni interested party, upande wake wa story lazima upatiwe balance ya upande wa pili wa CCM na hatimaye kuthibitishwa na authorities za Jeshi la polisi.

Naendelea kufuatilia upande wa pili na uthibitisho wa polisi, pia nafanya juhudi za kumtafuta mpiganaji Fredirick Katulanda ambaye siku zote husimama wima bila kuegemea upande wowote.


Unataka huyu ndugu abalance vip uandishi wake?
 
Mnabishana na huyo mnapoteza muda wenu bure. Huyu ni wa kuweka kwenye list ya ku-ignore!
 

Trash!
 
Radhi siombi msimamo wangu ni huo aandike habari zake kwa umakini sio kwa ushabiki yeye ni mzoefu wa haswa televisheni anajua anachofanya

Mkuu, sijaona ameshabikia nn, inawezekana wewe ndy umesoma habari hiyo kishabiki! Ameeleza wazi habari amezitoa upande gani, na kakwambia anafanya juhudi kupata habari za upande mwingine!...Dah! kazi ipo.:A S-fire1:
 
Wadanganyika bana..mnagombana kumpigania mfalume na familia yake..mmeliwa
 
Kinachonisikitisha ni michango na conclusion za baadhi ya watu humu zisizo na uthibitisho, unapoandika kwamba wafuasi wa Chadema wamemuua dereva una uhakika gani?
 
Breaking news huwa zimekamilika?I hope mods wanafuatilia sasa na muda si mrefu watacomfirm.

Habari ulete wewe, halafu mods ndy wafuatilie kutuhabarisha vzr?!!!!...dah, hawa memba wa jf sku hizi tabu sana! HOMA YA UCHAGUZI.
 
Breaking news huwa zimekamilika?I hope mods wanafuatilia sasa na muda si mrefu watacomfirm.

Sio kazi ya Modes ku confirm habari zinazoletwa na members.
Aliyeleta taarifa anapaswa afanye hivyo au member yeyote mwenye taarifa hizo .... be guided accordingly.
 

Yona Maro, mpaka mtu ataje jina ndiyo ieleweke kuwa ni name calling, acha kutupotezea muda hapa.
 
Wahusika lazima wachukuliwe hatua kali. Huwezi kupoteza maisha ya mtu shauri ya siasa tu.

Tusianze kwenda ambako majirani zetu walishafikia.

Dalili zilionyesha mapema; hata kama mtu amefanya kosa kwanini waanze kumpiga, kwani wao kuchukua hatua wamegeuka polisi?

Wanasiasa wote lazima wakemee vurugu za aina yoyote maana hazina maana na zitaleta majanga yasiyo na maana.
 
Update One.
Nimefanikiwa kumpata mpiganaji Fredirick Katulanda, kwanza amenithibitishia ni kweli damu imemwagika kwa kifo kimetokea kweli.
Pia ni kweli John Shibuda, jana amelala mahabusu, leo ameachiliwa kwa dhamana ndogo na kurejea mikonani mwa polisi mpaka sasa.
Amenithibitishia kuwa polisi wamethibitisha tukio hilo.
Vesion ya CCM kwa mujibu wa Katulanda, gari la mgombea wa CCM na la Mgombea wa Chadema yalipishana, Gari Chadema wameshuka 'kuchimba dawa' gari la CCM wakajipitia zao (naasume walizomeana), baada ya kupita mtu mmoja kwenye gari ya CCM akadondosha kofia, hivyo gari la CCM likasimama mbele, aliyedondosha kofia akarudi nyuma kuifuata, ndipo wafuasi wa Chadema wakamdaka na kumtembezea kichapo, wenzao kuona hivyo wakarudi kumsaidia ndipo wakavamiwa na wafuasi wa Chadema na ndipo ikafuatiav piga nikupige iliyosababisho kifo cha dereva.

Katika hatua nyingine, Katulanda ameendelea kupasha kuwa Mgombea wa CCM kwa jimbo hilo, anatafutwa na polisi kwa kosa la kumshambulia OCD wa Maswa. RPC amesema tukio la kifo ni tukio jingine, na hilo la shumbulio kwa OCD ni tukio jingine na hayana uhusiano.

Bado nafuatilia taarifa rasmi toka kwa RPC Mwanza.

Tunaendelea.
 
Mkuu Pasco,

Ina maana Shibuda nae yupo selo? sijaelewa. RIP aliepoteza maisha.
 
Mkuu Pasco,

Ina maana Shibuda nae yupo selo? sijaelewa. RIP aliepoteza maisha.
Selous, yes Shibuda yuko chini ya ulinzi, ila pia anashikiliwa kiuheshimiwa heshimiwa, jana amelala selo, leo asubuhi akaruhusiwa kwenda home kupata breakfast ya nguvu na kujipiga soap soap na kurejea mikononi mwa polisi. Mpaka nilipoongea nae, alikuwa bado ameshikiliwa ila pia anaruhusiwa kupiga simu etc.

Usishangae hizi ndizo hizo doble standards kwenye mahabusu zetu. Wale mafisadi wa EPA kabla hawajakamatwa, mahabusu maalum zilikarabatiwa pale gereza la Ukonga, wakafunga viyoyozi na plasma TV kubwa ukutani, halafu wanaletewa misosi na cataring ya New Africa hoteli, mahabusu wale wanachagua wangependa kula nini. Wanaangaliwa afya zao Regency Hospital kwa kubebwa na yale magari ya Knikt Support, ndio hivyo hatulingani kama vidole. Bado nafuatilia taarifa ya RPC.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…