Elections 2010 Sakata la mauaji ya Dereva wa CCM Maswa na hatima ya Shibuda

ni kweli Shibuda hakuwepo na hii ni njama sasa ngoja tusubirie jibu la nec sijui watasemaje hawa nec
 
Watu waliokuwa wananafuatilia mauaji yaliyOtokea kwenye jimbo la maswa wamepeleka maombi kwenye tume ay uchaguzi kuomba chadema wasimamishwe wasiendelee na kampeni kwenye hilo jimbo
source: TBC -TAARIFA YA HABARI SAA MBILI
my take:
:frusty:
Jamani hamu ya kuingia msituni inanijia mwenzenu kwa uonevu huu unaofanya na CCM, najisikia kujitoa muhanga
 
CCM wanapenda kutumia maiti kama ngazi. Hatujasahau walivyotumia kifo cha wangwe kama mtaji na sasa wanasherekehea kifo cha kafara mwingine. Kweli CCM mmefulia
 
Ni kweli huyu jamaa anahujumiwa na nathani mbinu za CCM ni kumlazimisha ajitoe kugombea! Jamani kwanini watu wasiandamane kulazimisha aachiwe?
 
Jamani wana jamii hivi ni halali Kwa Mh Chibuda kuwekwa ndani kwa maelekezo ya Kikwete? Hivi hii nchi hulka binafsi zinazidi utashi wa Sheria! Inakuwaje ahusishwe na mauaji ya dereva wakati hakuwepo katika tukio? Habari nilizopata Bw. Chibuda amepewa condition ya kuachiwa nayo ni kujitoa kugombea Ubunge kwa Chadema, sasa hii ni haki? kwanini wana jimbo wasiandamane kulazimisha aachiwe Mbunge wao? Uvumilivu unanishinda mie!
 
Kifo cha dereva wa CCM kilisababishwa na CCM-Dk.Slaa




Na Muhibu Said



24th October 2010












Mgombea urais kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willibrod Slaa, ameelezea vurugu zilizosababisha kifo cha dereva wa gari la Chama Cha Mapinduzi (CCM), wilayani Maswa, mkoani Shinyanga na kusema zimetokana na CCM kujitakia maafa.
Aidha, Dk. Slaa anatarajiwa kufanya mikutano mitatu jijini Dar es Salaam leo katika majimbo ya Kawe, Kinondoni, Ilala na Ubungo. Dk. Slaa alitoa kauli hiyo wakati akihutubia mkutano wa hadhara wa kampeni zake katika uwanja wa Benki, mjino Mombo, wilaya ya Korogwe, mkoani Tanga jana.
Alisema kinyume na ilivyodaiwa na baadhi ya watu kwamba Chadema imeleta maafa Maswa, dereva huyo alipigwa hadui kufa baada ya wafuasi wa CCM kuvamia mkutano wa kampeni wa Chadema wilayani humo.
“Kwa hiyo kusema Chadema imeleta maafa Maswa nasema hapana. CCM imejitakia maafa,” alisema Dk. Slaa. Alisema baada ya mkutano wao kuvamiwa na wafuasi wa CCM, Chadema walistahili kujihami na kujitetea.
Hata hivyo, Dk. Slaa alisema kabla ya maafa hayo kutokea, tangu aanze kampeni zake Agosti 29, ameshafanya mikutano 460 ambayo pamoja na mambo mengine aliitumia kuhubiri amani wakati huu wa kuelekea kwenye uchaguzi mkuu.
Alisema amekuwa pia akikemea vijana wa CCM maarufu kama ‘Green Guard’, ambao alisema hupelekwa kwenye makambi kufunzwa ukakamavu lakini baadaye wanaleta vurugu kwenye uchaguzi. Alieleza kushangazwa na kitendo cha polisi kumkamata mgombea ubunge wa jimbo la Maswa Magharibi kupitia Chadema, John Shibuda, kwa sababu ya vurugu hizo.
Alisema kukamatwa kwa Shibuda ni uonevu kwa sababu wakati vurugu zinatokea, alikuwa jukwaani akihutubia mkutano wake wa kampeni.
Akijibu swali la mwananchi katika mkutano wake uliofanyika mjini Muheza, Dk. Slaa alisema akiingia madarakani, atalipokea suala la kurejeshwa kwa Mahakama ya Kadhi Tanzania Bara lilipofikia katika mazungumzo yanayoendelea baina ya kamati ya Waislamu na ile ya serikali na kuliwekea msimamo.
Katika swali lake, mwananchi huyo, Othman Akida, alisema ni muda mrefu sasa Waislamu nchini wamekuwa na tatizo la kutokuwa na mahakama hiyo, hivyo akataka kujua Dk. Slaa akiwa Rais atawasaidiaje waumini wa dini hiyo.
Wakati huo, Kaimu Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika, alisema maandalizi ya kumpokea Dk. Slaa yamekamilika.
“Dk. Slaa atapokelewa kwa msafara wa watu kwa baskeli, pikipiki na magari kuanzia Kiluvya jimboni ubungo, atafanya mkutano Tanganyika Packers Kawe kuanzia saa 6:00 mchana, ataelekea Magomeni shule ya msingi na Mchikichini,” alisema.



CHANZO: NIPASHE JUMAPILI
 
Jamani wana jamii hivi ni halali Kwa Mh Chibuda kuwekwa ndani kwa maelekezo ya Kikwete?Habari nilizopata Bw. Chibuda amepewa condition ya kuachiwa nayo ni kujitoa kugombea Ubunge kwa Chadema

Hizo habari umezipata wapi - kwamba kaambiwa ajitoe ubunge?

Well, kama NI KWELI naona wanachemka tu. Si anaweza kukubali kwamba anajitoa then akifika kitaa anauchuna. Watamrudisha ndani?
 
Hizo ni njama tu za kutaka kupunguza makali ya CHADEMA. Wanaoanzisha fujo ni CCM wenyewe. Wafanye vyovyote Tanzania mwaka huu ni ya Chadema

Mwaka huu hata wapiga kura tutazuiriwa kupiga kura kosa, eti Dr Slaa Ph D ya ukweli na sera za kuwafumbua macho waTZ. Vipi ariyemmwaga mtama afande wa wiraya yntu tena mbere ya afande wa mkoa hiyo tharau tuliyofanyiwa waTZ wote rimewekwaje kwa mujibu wa kanuni,taratibu na sheria za nji hii na siyo kwa mujibu wa kubebana kwa mbereko za ki sisiemu za kuvunja kanuni, taratibu na sheria kwa rengo la kurindana
 
Hapo hakuna uhusiano wowote kati ya kugombea ubunge na mauaji,mauaji ni kosa la jinai,linashughulikiwa kijinai,mambo ya kugombea ni masuala ya sheria za uchaguzi,tume ndo inaweza kumtoa asigombea kama amevunja sheria za uchaguzi.Kimazingira hakuna ushahidi kuwa amevunja sheria ya uchaguzi,kwanza alikuwa jukwaani wakati tukio linatokea.Pili kama taarifa zilivyosema wafuasi wa chadema walikuwa wanaelekea kwenye eneo la mkutano wa kampeni utakaofuata ndipo wakakutana na wafuasi wa ccm ambao haikujulikana walikuwa wanaelekea wapi.Kwa hiyo ukiangalia hapo unaona kuwa chadema hawakuwafuata ccm,bali ccm waliwafuata chadema,chukulia wamekutana kama ilivyosemwa,inakuwaje kofia isidondoke sehemu yoyote ile isipokuwa pale ambapo chadema wapo?Hii inaonesha kuwa ccm wamekuwa na tabia y uchokozi halafu wanakimbilia polisi maana wanajua polisi wameshapewa maelekezo na wakuu wa chama.
Kwa kuangalia mfululizo wa matukio ya ghasia yaliyotokea mpaka hivi sasa utagundua ccm wanatoa vijisababu tu ilimradi kujikosha wakati wanaingilia mikutano na misafara ya chadema waziwazi.Polisi nao wanawaacha tu wakijua fika ni nini kitatokea.Sasa mzaa mzaa hutumbuka usaha,walizoea mambo yataishia watu kujeruhiwa,lakini sasa ni maafa.
CCM wanafanya vibaya mno kuwatumia vijana kama chambo,sasa ona mtu anapoteza maisha halafu wao wanaona ni mchezo mzuri na kutake advantage,Ifikie hatua vijana wa ccm wakatae kuwa chambo kwani ni maisha yao na wakifa hakuna atakayewakumbuka.

Kesi iende mahakamani,hakuna atakayejitoa kwani mtuhumiwa wa mauaji hajitoi kugombea bali hupelekwa mahakamani,kama ingekuwa ni kujitoa kugombea basi Chenge asingekuwa anagombea.
 
Watu waliokuwa wananafuatilia mauaji yaliyOtokea kwenye jimbo la maswa wamepeleka maombi kwenye tume ya uchaguzi kuomba chadema wasimamishwe wasiendelee na kampeni kwenye hilo jimbo
source: TBC -TAARIFA YA HABARI SAA MBILI
my take:
:frusty:

Hao ni wakurupukaji. Wanataka kusema shibuda ameshapatikana na hatia mahakamani na kuhukumiwa? Wangeonekana na busara kama wangeomba kampeni zote zisimame. Mbona Mramba ana kesi mahakamani na anaendelea na kampeni sembuse Shibuda ambaye hata hajafikishwa mahakamani wamtoe kwenye kampeni!!!!!?????
Mijitu mingine bwana sijui inawaza kwa kutumia nini.

Kifo cha huyu mtu kimesababishwa na uzembe wake mwenyewe. Unachokoza wakati huwezi kujilinda? Yeye si ndo aliwaona CHADEMA akasimamisha gari???!!! Sitaki kushangilia kifo lakini ukweli ni kuwa ni kosa la marehemu kusimama kukojoa hadharani. Kwa nini asimamishe gari kukojoa mbele za watu?

Na ni tabia ya CCM kuchokoza mikutano ya Chadema kama ilivyoonekana wakati Slaa akihutubia Tanga .
 
Kwa nini unadhani makamba Kama karibu mkuu wa ccm hawezi kutoa amri ya kukamatwa mtu?
 
polisi na vyombo vingine vya usalama wameendelea kuichekea ccm, sasa na wao zamu yao imefika wanapigwa mtama na mgombea wa ccm, aibu!
 
lakini kweei kwa nn mramba na vijisenti bado wanadunda?
Hawa ccm watapata laana kali sana
wnatunyima haki zetu.
 

Makamba alikuwa kule siku ya tukio, bila shaka yeye ndiye aliyeingineer haya mambo yote. Lakini Mungu akiwa upande wetu ni nani atakuwa kinyume na sisi? Tuzidi kumwomba Labuka.
 
Hata wafanyaje kumdhulumu Shibuda haitasaidia kwa sababu wamejidhalilisha hakuna mwananchi wa Maswa ataheshimu Jeshi letu la Polisi baada ya kuona RPC amebariki OCD kukatwa ngwara na kuupuzia kilio cha OCD huyo ameongea na waandishi wa habari ameeleza kila kitu kwa uwazi akaweka heshima yake rehani mbele ya watoto wake,mke na jamii kwa ujumla kwa sababu aliona anadhurumiwa na kunyanyaswa akiwa mtumishi wa umma,akitumikia taifa Yusuphu Makamba ni pumba kabisa hili ajue kabisa Shibuda anachukua jimbo kwa sababu inaonyesha kwa uwazi kabisa anaonea anahusishwaje na wafuasi wakati yeye hakuwepo kwa nini mpaka sasa hatujapata ripoti yeyote kutoka kwa wafuasi wa chadema,namshukuru mungu polisi sio mahakama watamuweka rumande hata siku ya mwisho bado tuu hawatamfunga itabidi kesi iende mahakamani kama watamshitaki aibu sana kwamba nchi imefikia inaendeshwa kidikteta
 
TBC wanashuka hadhi kila kukicha viwership inashuka kwa kasi kuliko kawaida watasemaje chadema ifutwe kwenye uchaguzi wa Maswa wakati Masha aliyetishia kuumua Wenje anadunda,Mgombea wo wa Maswa kamkata mtama OCD na anaendelea kudunda,Rostam,Mramba,Chenge,Jakaya wote mafisadi waliokubuhu wanadunda thubutu,tatizo TBC propangadists hana dira amechangia sana kumshusha KIKWETE siku zote wananchi wanapoona kuna watu wanaonewa na chombo chao cha taifa cha utangazaji wanatabia ya kuwa upande wa yule anayeonewa wamempandisha chat wenyewe DR Slaa,kwa jinsi walianza kumsakama na anachukua nchi kwa kosa hilo tuu la TBC wameshindwa hata na Star TV baada ya ITV watu wanaangalia zaidi Star TV kwa jinsi ilivyojitahidi kutoa muda kwa wagombea mbalimbali kinyume cha TBC
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…