Sakata la mwanamke aliyefanyiwa ukatili na wafugaji

Sakata la mwanamke aliyefanyiwa ukatili na wafugaji

philltaya

Member
Joined
Sep 5, 2015
Posts
53
Reaction score
11
Mkuu wa wilaya ya Mvomero nashukuru kwa kulifuatilia swala hilo la ukatili alilofanyiwa mama Fatuma Hasani Diawi, lakini katika swala hilo polisi wanataka kujenga kitu mpaka sasa, baada ya kulifikisha hilo swala mahakamani, wanamtaarifu mlalamikaji kuwa taarifa zote atapata kutoka kwa mtendaji wa kijiji sasa je hii ni sheria mpya au ndiyo mwongozo wa kipolisi, au mtendaji ni hakimu?

Kwa namna hii mkiwakumbatia wafugaji wananchi wataendelea kuteseka polisi kazi yenu ni kukamata mtuhumiwa kumuhoji na kumfikisha panapo stahili baada ya kujiridhisha na kuviachia vyombo vingine vifanye kazi. Ombi mkuu wa wilaya tafadhali fuatilia mpaka mwisho swala la huyu mama ili aweze pata haki, maana inaonekana kama polisi wanataka kucheza na maisha ya watu. Wasitumie mwanya wa huyo mama kutokujua cha kufanya na kumdhulumu haki yake, watendaji wa vijiji timizeni majukumu yenu hacheni ubabaishaji juu ya maisha ya watu.

Pia nikuombe mkuu wa wilaya kwa kazi hiyo hiyo ambayo umeifanya Doma tafadhari fika Menge/Vianzi.
 
Kama kuna aliyeelewa.......
 
Kama kuna aliyeelewa.......

Hoja ni;


Serikali inakigugumizi gani juu ya migogoro ya wakulima na wafugaji, Morogoro



Najiuliza hivi serikali inajua kinachotokea Morogoro kupigwa kwa wakulima wawili na wafugaji kwa vijiji viwili tofauti mmoja Doma na mwingine Menge/Vianzi wilaya ya Mvomero? Wafugaji nguvu ya kufanya hivyo wanaitoa wapi?
Kuna mkuu wa wilaya na mkuu wa mkoa tafadhari tupieni sana jicho wilaya ya Mvomero hasa kijiji cha Menge/Vianzi wafugaji wanafanya makusudi kulisha mifugo kwenye mashamba ya wakulima na ukatili mkubwa na sheria zinaonekana kama hazina meno kwao.
Nimetuma post hii kwa uchungu kwakuwa kijiji hiki hakijafikiwa na serikali kikamilifu na ndiyo maana wafugaji wanapuuzia matamko ya serikali, na kufanya ukatili kwa wananchi, kiongozi wa kijiji ni wa hovyo kabisa na ndiyo huyo huyo amepita kwenye kura za maoni kiongozi atakaye ona hii post tafadhari tuondolee uzia hapo kijiji kwetu, ardhi ni nzuri kwa kilimo chochote lakini hatuwezi kufanya shughuli za kilimo ipasavyo kwakuwa ng'ombe zinashinda mashambani na mapoli yapo.
Ni mimi mkulima sina pa kupazia sauti yangu zaidi ya jukwaa hili
 
Back
Top Bottom