Sakata la Ngorongoro; Tusioelewa vizuri tueleweshwe

Sakata la Ngorongoro; Tusioelewa vizuri tueleweshwe

Ni kweli huelewi na wengi hawaelewi japo wanazungumzia ishu hii.
Kabla kuzungumzia migogoro iliyopo inabidi nikueleweshe kidogo kuhusu wilaya ya Ngorongoro.
Wilaya ina tarafa tatu yaani Tarafa ya Ngorongoro ambayo Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro ipo ndani yake,Tarafa ya Sale na Tarafa ya Loliondo.
Makao makuu ya Wilaya yapo Loliondo.
Kutoka Arusha hadi Loliondo ni takribani kilometa 324.
Na kutoka Arusha hadi Mamlaka ni takribani km 140.
Hadi hapo ushajua historia kidogo na umbali uliopo baina ya Tarafa ya Loliondo na ile ya Ngorongoro.
Tarafa hizi mbili zimetenganishwa na tarafa ya Sale.
Mgogoro.
Mgogoro upo wa aina mbili.
Mosi ni kati ya Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro na Wamasai wanaoishi ndani ya Mamlaka.
Na hawa ndio wanaohamishwa na serikali kwenda Handeni.
Kwa hiyo ishu ya kuhamisha Wamasai kwenda Handeni inawahusu wale wa Tarafa ya Ngorongoro tu!
Mgogoro wa pili ni ule wa wananchi wa
Loliondo hasa kata za Arash,Soitsambu, Ololosokwani,Oloipiri Oloirien na maeneo dhidi ya Mwarabu wa OBC.
Km za mraba zipatazo 1500 zinamegwa kwenye maeneo wanaoishi wananchi hao kwa ajili ya ushoroba wa wanyama(kati ya Serengeti na Masai Mara huko Kenya).
Wenyeji wenyewe wanadai sio kwa ajili ya ushoroba bali ni kwa ajili ya OBC.
Mgogoro huu ni wa muda mrefu sasa.
Hao wa Loliondo wenyewe hawapelekwi Handeni kama watu wasiojua wanavyozungumza ama wanavyopotosha.
Sasa naamini umeelewa kidogo.
Nyongeza ni kuwa vurugu zilizotokea zilikuwa loliondo na sio tarafa ya Ngorongoro.
Ahsanta
Nimekuelewa vizuri sana kiongozi.
Naomba uniongezee kidogo, watu tunaoambiwa wanaamishwa Ngorongoro kwenye hifadhi ni kweli wanafanya shughuli za kuharibu mazingira ndani ya hifadhi na kama yes zaidi ya overgrazing wanafanya nini kingine?
 
..mwanaharakati asumbuliwa kwa kutoa maoni yake kuhusu Ngorongoro na Loliondo.

 
..Ni vizuri pia kuelewa Wamaasai walifika vipi Ngorongoro.

..Na mchango wa kihistoria wa jamii hiyo ktk masuala ya uhifadhi.

 
Ni kweli huelewi na wengi hawaelewi japo wanazungumzia ishu hii.
Kabla kuzungumzia migogoro iliyopo inabidi nikueleweshe kidogo kuhusu wilaya ya Ngorongoro.
Wilaya ina tarafa tatu yaani Tarafa ya Ngorongoro ambayo Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro ipo ndani yake,Tarafa ya Sale na Tarafa ya Loliondo.
Makao makuu ya Wilaya yapo Loliondo.
Kutoka Arusha hadi Loliondo ni takribani kilometa 324.
Na kutoka Arusha hadi Mamlaka ni takribani km 140.
Hadi hapo ushajua historia kidogo na umbali uliopo baina ya Tarafa ya Loliondo na ile ya Ngorongoro.
Tarafa hizi mbili zimetenganishwa na tarafa ya Sale.
Mgogoro.
Mgogoro upo wa aina mbili.
Mosi ni kati ya Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro na Wamasai wanaoishi ndani ya Mamlaka.
Na hawa ndio wanaohamishwa na serikali kwenda Handeni.
Kwa hiyo ishu ya kuhamisha Wamasai kwenda Handeni inawahusu wale wa Tarafa ya Ngorongoro tu!
Mgogoro wa pili ni ule wa wananchi wa
Loliondo hasa kata za Arash,Soitsambu, Ololosokwani,Oloipiri Oloirien na maeneo dhidi ya Mwarabu wa OBC.
Km za mraba zipatazo 1500 zinamegwa kwenye maeneo wanaoishi wananchi hao kwa ajili ya ushoroba wa wanyama(kati ya Serengeti na Masai Mara huko Kenya).
Wenyeji wenyewe wanadai sio kwa ajili ya ushoroba bali ni kwa ajili ya OBC.
Mgogoro huu ni wa muda mrefu sasa.
Hao wa Loliondo wenyewe hawapelekwi Handeni kama watu wasiojua wanavyozungumza ama wanavyopotosha.
Sasa naamini umeelewa kidogo.
Nyongeza ni kuwa vurugu zilizotokea zilikuwa loliondo na sio tarafa ya Ngorongoro.
Ahsanta
faru John yupo?
 
Viongozi wa Afrika niwa jinga una ua raia wako kwa manufaa ya tumbo lako kwa uroho wa pesa na kuona waarabu ni muhimu Sana
we kwl ni mvivu hutaki ht kujielimisha. Ngorongoro hakuna uwindaji ni hifadhi, Hifadhini hawawawindi. wanakowinda ni Loliondo. Ngorongoro ni wilaya vivile kuna tarafa ya ngorongoro na kuna tarafa ya loliondo ila wilaya km eneo la utawala ni Ngongoro. Na kuna tarafa zingine km Sale. Mwarabu ataruhusiwa vp ndaani ya hifadhi? Ndani ya Hifadhi waliruhusiwa wamasai ndio hao wamekiuka utaratibu wa mwanzo kwa kujenga makazi ya kudumu, vilevile wamekuwa wengi na kuna wasiwasi kwa uwingi wa mifugo ile siyo ya wamasai wa Ngorongoro. Tuache serikali ifanye kazi yake. Pakiharibika nyie wa kwanza kuilaumu kuitukana. Tuiamini serikali
 
Achane Mwarabu ndio nini hana jina?take no jina la kama yuko Tanzania maana ya mtanzania, Acheni ubaguzi, tutawachoka. Namwambie asije anaondaka mnyamapori hata mmoja. Kama ataenda kwao kusalimia aende nyama na picha ukirudi aje ndugu wengine. Tanzania nchi ya kijamaa binadamu wote ni sawa
 
Back
Top Bottom