Sakata la Sugu na Blue: Nay wa Mitego amuomba Mr. Blue 'amuuzie kesi'

Interest

JF-Expert Member
Joined
Apr 11, 2015
Posts
3,434
Reaction score
7,072
Imbombo Ngafu!! Hii ngoma bado mbichi.. Afe kipa, afe beki!

Leo kupitia 255 ya Clouds FM, Nay wa Mitego amenukuliwa akitoa yake ya moyoni kuhusiana na ngoma ya 'Freedom' inayogombaniwa kati ya Mr. Blue na 'Sugu' ambae ameshaifanyia video na kunyofoa vocals za Mr Blue.

Nay anasema;

''Blue angekuwa ni mshikaji wangu ningemshauri na yeye amtoe Sugu halafu kama inawezekana aniweke mimi kwenye chorus halafu tuharibu hali ya hewa tutajuana huko mbele ya safari, halafu kama ni hela ya kuifanyia Video ngoma hii mimi nitalipa hata kwa GodFather au Hanscana‘:- Nay wa Mitego.

Tuwepo!
 
Filosofi ya Sugu tangu yupo kwenye game anasema piga hela ujiko utakuja wenyewe....

Nakumbuka waliwahi kumpambanisha Sugu na Dudu Baya kwenye "Nani Zaidi", kipindi hicho Radio One ndio ilikuwa redio ya town.

Dudu Baya akashinda kwa kura nyingi. Wapambe wakapiga Sana kelele. Sugu alipoulizwa akajibu simple tu.

Sifa bila hela haisaidii kitu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…