Sakata la TFF: FIFA yatua nchini

Sakata la TFF: FIFA yatua nchini

kirerenya

JF-Expert Member
Joined
Aug 27, 2013
Posts
1,696
Reaction score
2,253
FIFAAAA.jpg

Meneja Miradi ya Maendeleo wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) kwa Afrika, Mzimbabwe Solomon Mudege amewasili nchini kwa ajili ya kufuatilia mambo yanayoendelea katika shirikisho la soka Tanzania TFF.

Mudege tayari yupo nchini na pamoja na kukutana na Kamati ya Utendaji ya TFF, Dar es Salaam, pia atakuwa na kikao na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrisons Mwakyembe.

Bado haijafahamika Ofisa huyo amekuja kwa sababu zipi haswa na kama ameitwa na viongozi wa TFF au amekuja kwa maagizo ya FIFA tu.

Hata hivo hali si shwari katika uongozi wa soka Tanzania, kutokana na viongozi wakuu TFF yaani Rais Jamal Malinzi na Katibu wake Mwesigwa Selestine kuwekwa rumande tangu Juni 29 kwa tuhuma za ubadhirifu na matumizi mabaya ya madaraka na huenda Ofisa huyo akataka kujua kilichowasibu viongozi hao.

Chanzo: EATV
 
Aisee, ngoja tuone huo ujio wake utarekebisha TFF au vipi
 
Back
Top Bottom