Sakata la uchaguzi: Pesa kwenye damu

Sakata la uchaguzi: Pesa kwenye damu

SIMULIZI: ELECTION SAGA (MONEY IN BLOOD)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

UKURASA WA KUMI NA SABA
“Unajua mimi sikuwa nikiamini kama ni huyu kiongozi ndiye ambaye alikuwa amepigwa risasi mpaka nilipo hakikisha sura yake kabisa ndipo nikaamini kwamba ni yeye mwenyewe. Daah maskini mzee wa watu huyu ndiye aliyekuwa anategemewa kuja kuibadilisha nchi hii lakini wale ambao wanaonekana kwao madaraka ni kila kitu wameamua kumuua”
“Inakuwaje mtu mkubwa kama huyu anatembea bila walinzi?”

“Hata mimi nimeshangaa sana maana kwa tukio ambalo limetokea asubuhi la mtoto wake kuuawa ilitakiwa awe na ulinzi mara mbili zaidi ya hapa hata jeshi la polisi lilitakiwa kuwa naye sambamba. Mimi nilikuwa nimetoka kuchukua chakula pale KFC nikawa namuona mtu kama amelewa maana alikuwa anayumba yumba huku anakimbia lakini ghafala sana nikaiona Noah nyeusi ikiwa nyuma yake, akashuka mwanaume mmoja ambaye amejifunika uso wake akampiga risasi za kutosha kisha akaingia kwenye gari na kutoweka. Ndipo pale nilianza kupiga makelele na watu wakaanza kufika hapa”

“Kwamba hakuwa na mlinzi hata mmoja wakati hayo yote yanatokea?”
“Mimi nimemuona akiwa mwenyewe tu hakuwa na mlinzi yeyote yule mpaka nikawa nashangaa. Nimeogopa sana ndugu yangu, naona tatizo hata kurudi nyumbani mwenyewe maana usije ukakuta na mimi ndiyo siku yangu ya mwisho” yalikuwa ni maongezi ya vijana wawili ambao walikuwa wapo pembezoni mwa kundi kubwa la watu ambalo lilikuwa limeuzunguka mwili wa kiongozi huyo huku wengine wakiwa wanaupiga picha mwili huo kusubiri polisi wafike na kuiondoka nao maana walikuwa wanajua kwamba alikuwa ni mtu mfu tayari.

Wakati wanaendelea na hayo maongezi yao, pembeni alikuwa amesimama Tommy kwenye suti yake baada ya kushuka kwenye gari akiwa anawasikiliza kwa umakini sana, hicho ndicho kilimfanya atulie kwanza ili kuwasikiliza wanaume hao kile ambacho wanakizungumzia hapo. Baada ya kuwasikia kwa umakini alipenya katikati ya watu na kusogea mpaka ulipo mwili huku akishangazwa sana kutowaona polisi mpaka wakati huo kwani kwa muda ambao ulikuwa umepita polisi walikuwa wanatakiwa wawe tayari kuwepo hilo eneo.

Alimgusa baba yake mzazi kabisa shingoni huku watu wakiwa wanamshangaa lakini hata hakujali jambo hilo, baada ya kumgusa alishtuka na kumbeba haraka sana ambapo alikimbia naye mpaka kwenye gari na kuondoka hilo eneo kwa kasi sana watu wakiwa wanamchukua video na kumpiga picha akiwa na mwili wa kiongozi huyo ambao aliondoka nao huku hilo eneo watu wakibaki kwenye sitofahamu maana wao walikuwa wanaogopa hata kuugusa wakiogopa kuingia kwenye adha ya kukutana na polisi.

Mwanaume alinyoosha moja kwa moja mpaka hospitali kuu ya mhimbili ambapo alisistiza sana kwamba mtu huyo alikuwa hai bado hivyo walitakiwa kufanya uataratibu wa kumtoa risasi haraka sana huku akiwapigia simu walinzi wa nyumbani waweze kufika haraka sana ndani ya hilo eneo wengine wakitakiwa kubaki kuwalinda wadogo zake. Akiwa amesimama nje ya hilo wodi ambalo baba yake aliingizwa kwa ajili ya kufanyiwa upasuaji ili kuona namna ya kusaidia maisdha yake kwa kumtoa risasi polisi walifika hapo ambapo walimkwida na kumkamata Tommy tena kwa dharau sana, walinzi wake walitaka kuingilia aliwapa ishara ya kutulia huku akiwasisitiza wahakikishe baba yake yupo salama yeye angerudi.

Alipelekwa ndani ya kituo kikuu cha Osterbay kutokana na aina ya kesi ambayo alikuwa amejiingiza nayo.
“Wewe ni nani haswa mpaka uende kubeba mwili wa mtu tena kiongozi kama yule bila ya sisi polisi kufika?” ni polisi mmoja kati ya watatu ambao walikuwa wamemuingiza kwenye chumba cha mahojiano mwanaume huyo kwa sababu alifanya kosa kubwa sana la kuhusika na kuushika mwili kabla hata ya polisi kufika lile eneo kitu ambacho kisheria lilikuwa ni kosa. Hata hivyo Tommy hakujibu kitu akabaki anamtazama askari huyo kwa hasira kali sana kitu ambacho kilipelekea askari huyo kumpiga na kitako cha bunduki kwenye pua yake kwa kulidharau swali lake.

Damu ilianza kumtoka kwenye hilo eneo hata hivyo hakuwa na muda nayo, walikuwa wamemfunga vyema wakamvua na viatu kisha wakaanza kumshushia kipigo kwa kushindwa kuwa msikivu huku moja kati ya wale askari watatu akiwa ameganda tu maana ni kama hakuwa anaelewa kwamba ni kipi wenzake walikuwa wanakifanya. Waliacha kumpiga baada ya yule mwenzao kuguna kwa nguvu kitu ambacho kilikuwa ni kama ishara, ni kweli ndani ya dakika moja tu IGP alikuwa ameingia ndani ya hicho kituo na alihitaji kuelekezwa kwa mtu ambaye alikuwa amekamatwa na kuletwa hapo alipo kitu ambacho kilileta taharuki kubwa sana ndani ya kituo hicho kuweza kutembelea na kiongozi huyo mkuu wa jeshi la polisi.

Hapo ndipo alipo elekezwa kwenye hicho chumba ambacho Tommy alihifadhiwa, alikuwa kwenye spidi kubwa sana lakini wakati ule taarifa zilikuwa zinasambazwa kwa njia ya redio kwamba mheshimiwa IGP yupo hapo kituoni na kwa wakati huo alikuwa anaelekea kumuona mtu wake ambaye alikuwa amemfuata hapo. Wakati wale askari wawili wakiwa wanaendelea kumpiga Tommy ndio muda ambao taarifa hiyo ilitoka hivyo hawakusikia ila mwenzao ambaye alisikia aliguna kama kuwashtua kwamba muda wowote mheshimiwa alikuwa anaingia hapo ndani.

Walishtuka kwa huo mguno na jamaa akawapa ishara ya kuacha hicho walichokuwa wanakifanya, wakati bado wanashangaana walishangaa wanatangulia askari wawili ndani humo ambao walikuwa na vyeo zaidi yao, wakati wanatoa saluti za heshima ndipo walipopigwa na bumbuwazi baada ya huyo kiongozi mkuu wa jeshi la polisi alipoweza kuingia ndani ya chumba hicho. Ilikuwa ni ghafala sana hivyo walijikuta wanaanza kutetemeka hawakuutarajia huo ugeni kwa wakati huo kiasi kwamba wakawa wamesahau hata kutoa heshima ambapo walikuja kushtuka baadae baada ya kiongozi huyo kuweza kuwaangalia kwa hasira sana.
“Kwanini mnampiga huyu mtu na kwanini mmemkamata?” lilikuwa swali fupi sana ambalo lilihitaji majibu yenye maelezo ya kutosha ili waweze kwenda sawa kwenye huo uwanja wa kujibu.
“Mkuu huyu amekutwa kwenye eneo la tukio la mauaji na baada ya kufika pale akajichukulia sheria mkononi kwa kuondoka na mwili wa marehemu kabla hata polisi hawajafika. Hivyo tumemkamata ili tuweze kumhoji kwamba yeye ni nani na aliuchukua ule mwili kwa ajili ya kazi gani na alikuwa na maana gani kuweza kuupeleka hospitali asije kuwa ndiye muuaji mwenyewe” lilikuwa jibu jepesi ambalo hata IGP alibaki anajiuliza kijana huyo alifanikiwaje kupata kazi wakati alionekana kabisa kuwa wa hovyo sana.
“Muda wote huo hamkuwa mmefika eneo la tukio mlikuwa wapi?” aliwaongeza swali lingine
“Tulikuwa posta ila tuliambiwa kwamba mapolisi wa kule kule wangelishughulikia hivyo tukawa tumekaa mahali tunasubiri ripoti” alipokea kofi zito sana kutoka kwa huyo kiongozi wao ambaye ndiye aliwauliza wakati huo IGP aliwapaishara askari ambao alikuja nao waweze kumfungulia mtu huyo.
“Hiyo amri ya kuweza kukamatwa kwake na kumleta hapa ni nani amewapa?”
“Mkuu wa kituo”
“Una uhakika?”
“Ndiyo mheshimiw….” yule askari hakumalizia sentensi yake alipigwa risasi ya kichwa pale pale, wakati Tommy anasimama kutoka hiyo sehemu aliyokuwa amefungwa, alichomoa bastola moja kutoka kwenye kiuno cha askari mmoja kwa kasi sana kisha akairuhusu kwenye kuelekea kwenye kichwa cha mmoja wa maaskari ambao walikuwa wanamtesa hapo kisha akampiga na yule mwingine kwenye moyo ambaye naye alikuwa amejumuika na mwenzake kisha akamrudishia askari mwenye bastola yake mkononi huku akiinama na kuanza kuvaa viatu vyake.

Wote walibaki wanamshangaa hata IGP hakuwa akiamini kwamba hilo jambo lilikuwa limetendeka hapo.
“Umefanya nini bwana mdogo? Nmekuja hapa kukutoa kwa sababu baba yako alikuwa mtu mkubwa sana na aliwahi kunisaidia kipindi fulani mpaka mimi nikafanikiwa kuwa kwenye hii nafasi. Nilipopata taarifa kwamba umekamatwa halafu bila hatia maana nadhani hawa hawakujua kama wewe ni mwanae nikaamua kuja kukutoa lakini hasira zako zinakufanya mpaka umeua, huoni kama unaweza kufungwa hata kifungo cha maisha kwa kosa la kuua askari wawili? Kwanza unanipa maswali hata bastola kutumia umejulia wapi?” yalikuwa ni maswali mfululizo kutoa kwa IGP ambaye bado hakuwa na uhakika na kile ambacho alikuwa anakiona mbele yake maana mambo yalikuwa yanaenda kwa kasi sana.

“Mheshimiwa hivi kama ungekuwa wewe watu wa namna hii ungewafanya nini? Wapo sehemu wamejibanza wanamwangalia baba yangu anakufa halafu nayasaidia maisha yake wanakuja kunikamata na kunitesa? Walikuwa wapi kumlinda? Walikuwa wapi kuwahi eneo la tukio mpaka waje kuniwahi mimi? Nadhani umesema kwamba baba yangu aliwahi kukusaidia basi na mimi leo inabidi unisaidie kwenye hili maana ingekuwa ni mbaya sana kama ningeenda kwenye vyombo vya habari na kujitambulisha kama mimi ni mtoto wa Apson Limo kipenzi cha watanzania nilikuwa najaribu kuyasaidia maisha yake halafu nyie mkanikamata na kuanza kunitesa. Unahisi jeshi la polisi mtakuwa mmechafuka kwa kiasi gani? Mimi naenda mzee huenda siku nyingine tutapata wasaa wa kuzungumza vizuri zaidi ya leo” mwanaume alimuacha kwenye mshangao kiongozi huyo kisha akatoweka ndani ya hilo eneo ili kurudi hospitali kujua hali ya baba yake maana aliacha akiwa anafanyiwa oparesheni ya kutolewa risasi ambazo ziliingia kwenye mwili wake.

IGP alikuwa na hasira sana, baada ya kutoka humo ndani aliangalia saa yake na kukuta ni saa tano usiku, alisogea mpaka kwenye ofisi ya mkuu wa kituo ambaye alimkuta anapanga panga vitu vyake akiwa kama mtu anayehitaji kutoka hilo eneo. Alimfuata na kumzaba kibao kikali sana
“Una sababu ya msingi ya kunifanya nisikufukuze kazi usiku huu?” aliuliza kwa hasira akiwa anamwangalia kijana wake wa kazi huyo.
“Ndiyo mheshimiwa ninayo” alijibu haraka sana kwani kauli yake ndiyo ingemhakikishia aendelee kuupata mshahara, hakujibiwa zaidi ya kukaziwa macho hivyo akalazimika kuendelea kwa lazima.
“Nimepokea simu kutoka Ikulu, wameniambia kwamba nijiweke kando na hilo jambo na huyo bwana mdogo nimkamate mpaka kesho ndipo utaratibu uweze kuwa sawa, maana mpango ni kwamba ilitakiwa akamatwe kabla ya kufika hospitali na mgonjwa ila vijana wamechelewa ndiyo maana wamemkamatia hospitali” IGP alichoka mpaka akabaki anatabasamu tu maana hakutegemea jambo kama hilo.
“Umesema umepokea simu kutoka Ikulu?”
“Ndiyo mkuu”
“Kwahiyo lengo lao ni yule mzee asifike hospitali bali afe sio?”
“Hilo sijui mkuu”
“Na ulijua kwamba yule bwana mdogo ni mtoto wa damu wa Apson Limo?”
“Hapana mkuu” IGP hakuwa na neno la kuongeza, nafsi yake ilikuwa inamuuma isivyo kawaida yaani watu wanapambana kuilinda nchi halafu Ikulu ndo inaanza kurudisha mambo nyuma, alisonya na kuondoka hilo eneo kwa ghadhabu mno.


Taarifa zilikuwa zinasambaa kwa kasi sana mitandaoni, kila sehemu, kila chombo cha habari kilikuwa kipo busy sana kuzungumzia habari hizo. Ni kuhusu matatizo ambayo yalikuwa yametokea ndani ya familia ya Apson Limo kuanzia asububi ya siku hiyo ambapo mwanae wa kike alikuwa ameuliwa na watu wasio julikana na cha kushangaza sana kichwa cha mtoto huyo hakikuweza kupatikana hali ambayo ilizua taharuki kubwa sana lakini majira ya jioni ya siku hiyo zilianza kusambaa taarifa kwamba hata mtoto wake mkubwa wa kike alikuwa amepotea kwenye mazingira ambayo yalikuwa ya kutatanisha sana na kuzua taharuki nyingine.

Kabla hata habari hizo zote hazijatoka kwenye maskio ya watu ilikuja nyingine hiyo kubwa ambayo ndiyo iliwacha watu hoi huku wengine wakiwa wanatoa mpaka machozi. Mwanaume ambaye wao waliwekeza imani zao kwake, alidaiwa kuwa amekufa huku watu wengine wakidai kwamba alikuwa kwenye hali mbaya sana akiipambania afya yake kitandani na asingechukua muda mrefu ni lazima angeweza kufariki. Watu walianza kuvilaumu sana vyombo vya ulinzi na usalama kwa huo uzembe mkubwa wa kushindwa kumlinda kiongozi huyo ambaye walitamani kwamba ndiye anaweza akaisaidia nchi kutoka kwenye hali iliyokuwepo kuyafikia yale mafanikio mkubwa sana ambayo waliyatarajia kufanyika nchini mwao.

Naam naweka nukta sehemu ya kumi na saba.

Wasalaam,

Febiani Babuya.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
SIMULIZI: ELECTION SAGA (MONEY IN BLOOD)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

UKURASA WA KUMI NA NANE
Licha ya mambo yote hayo kuendelea bado vyombo vya ulinzi na usalama vilikuwa kimya sana, hakuna chombo chochote kile ambacho kilikuwa kimetoa taarifa yoyote kuhusu hilo jambo ambalo lilikuwa linafanyika. Wananchi hawakupewa kabisa muda wa kupumzika kwani usiku huo huo ilitoka taarifa rasmi kutoka kwenye ofisi ya DCI ambaye alikuwa ni kingozi aliyekuwa anahusika na mambo ya makosa ya jinai kwamba kiongozi huyo Apson Limo ambaye aliwahi kuwa kama waziri wa mambo ya nje alikuwa ana makosa ya jinai ambayo hayakuwekwa wazi moja kwa moja hivyo walikuwa wanatarajia kuyawasilisha mahakamani muda wowote ule kuanzia wakati huo ambao taarifa hiyo ilitoka.

Wananchi ni kama siku hiyo walichanganywa jumla na kuwafanya walale huku wakiwa hawaelewi ni kipi kilikuwa kinaendelea kwenye nchi yao kwani matarajio ya wengi walijua kwamba ingetoka taarifa ya mwenendo mzima wa kesi ya mtu huyo na usalama wake kwa ujumla lakini kibaya ni kwamba jina lake lilikuwa linazidi kuchafuliwa huku wengine wakianza kuwa na mashaka na mtu huyo na kuhisi kwamba huenda hawakuwa sahihi kuweza kumpa imani kwamba angewafikisha kwenye nchi ya ahadi kwani kama zimeanza hizo kesi za jinai basi huenda alikuwa ana mengi nyuma yake ambayo alikuwa anayaficha sana. Siasa ikawa inamtokea puani Apson Limo kama alivyokua anatabiri siku ambayo alikuwa anamwambia mkewe.

Wakati hayo yote yanaendelea kwenye moja ya majumba makubwa mwanaume mmoja mwenye kipara chake safi alikuwa anapata wine na warembo wawili huku akiwa amezungukwa na walinzi wa kutosha. Kwake habari hiyo ilikuwa njema isivyo kawaida kwani alikuwa akiisubiri kwa hamu sana, Hakuwa mwingine bali mr Mafupa ndiye ambaye likuwa amekaa mbele ya skrini yake kubwa akiwa anaifaidi taarifa hiyo ambayo ilimfrahisha bila shaka.

“Hahahahaha hahahahah hahahaha, kuna watu kwenye hii dunia ni wajinga sana, yaani nilimpa ofa kubwa sana ambayo ingemfanya aishi maisha mazuri yeye na wanae halafu yeye anaanza kujifanya mzalendo mbele yangu? Unakuwa mzalendo kwenye nchi ambayo hata raisi ni fisadi wa kutupwa na hana cha kuwafanya mafisadi wenzake? Uzalendo sio kwa nchi hii labda kama kitazaliwa kizazi kingine hiki kizazi kimesha laanika miaka mingi sana, tunatakiwa tumpate kiongozi ambaye ni katili sana halafu ni mzalendo yaani aue kila ambaye atakuwa anapingana na mafanikio ya taifa hapo tutafika ila sio kwa akina sisi. Apson alichemka sana kutaka kuanza kunitishia akiwa hajui anacheza na nani” mwanaume huyo akiwa anaifurahia taarifa hiyo ambayo kwake ilikuwa ni njema sana alicheka sana na kujisemea mwenyewe huku warembo ambao walikuwa karibu yake wakimvua nguo zake ndani ya hicho chumba kikubwa na kuanza kumlamba kila sehemu ambapo waliishia kuifanya mapenzi kwa fujo sana kana kwamba hawatakuja kuyafanya tena.

Baada ya kumaliza mr Mafupa alitoka mpaka nje, alinyoosha mpaka nyuma ya jumba hilo ambako kulikuwa na geti ukutani ambalo lilishonana na ukuta, aliweka mkono wake na kuingia huko ndani ambako nako kulikuwa na jumba kubwa sana, ni urefu wa ule ukuta ndio ambao ulifanya jumba hilo lisionekane kwa sababu lilikuwa chini chini sana huku likinakshiwa kwa vitu vya thamani isivyo kawaida. Baada ya kuingia hapo ndani alisikia vishindo na kelele za maumivu akawa anatabasamu tu, huko ndani mwanaume ambaye alijulikana kama Remsi alikuwa anapigana na wanaume sita ambao aliwapiga vibaya sana na wakati mzee huyo anaingia alikuta mwanaume huyo anamvunja mguu mtu wa mwisho.

Alifurahia sana kwani huyo alikuwa mwanae wa kumzaa japo watu hawakuwa wakimjua kabisa zaidi ya mr Oscar ambaye yeye mwenyewe ndiye ambaye alimpatia siri hiyo japo hakumtajia kwamba alikuwa anaitwa nani na mwanae huyo alikuwa ni yupi ila alimwambia tu kwamba nina mtoto.
“Una mpango gani baba?” mwanaume huyo aliuliza akiwa anajifuta jasho kwenye mwili wake
“Ikulu tunaenda kuichukua kirahisi sana halafu tuwafundishe namna wanaume wanavyo takiwa kufanya wanapopata nafasi kama hii”
“Na huyo bwana ambaye amegoma kutoka madarakani na anagombea tena unafanyaje kuhusu yeye?”
“Huyo hana shida kuna mtu anamalizana naye kisha tunaichukua ikulu kiwepesi sana. Unajua kwa sasa wakati tunaingia kwenye kampeni na uchaguzi kwa ujumla Ikulu kwa kiwango kikubwa itakuwa inaendeshwa na watu wa usalama wa taifa hivyo natakiwa kuzichanga karata zangu vizuri sana kwa CDF na mkurugenzi wa usalama hawa ndo kete za mhimu sana itakuwa ni kama kumsukuma mlevi kwenye mtaro nikiwaweka mkononi kwangu, changamoto alikuwa ni huyu Apson Limo”
“Naskia ana mtoto wa kiume, nimemuona kwenye ile video ambayo ameenda kumchukua baba yake kwenye lile eneo ambalo vijana wamemtupa ila haonekani kuwa mtu wa kawaida kama ulivyokuwa umesema mwanzo baba”
“Mhhhhh unamaanisha nini kusema hivyo R?”
“Udhaifu na uimara wa mtu unapimwa kwenye vitu vingi sana, wengi huwa wanaangalia miili tu kujaa kwa mazoezi lakini hiyo inaweza kuwa sababu ndogo kwani kuna gym siku hizi mtu yeyote anaweza kwenda lakini vitu vya mhimu sana kuna kasi ya macho, sidhani kama mtu wa kawaida anaweza kuwa na macho yenye kasi kubwa sana namna ile. Jambo lingine ni namna anavyo tembea, anaonekana kuwa mtu mwepesi isivyokuwa kawaida pia nimejaribu hata kuangalia namna alivyo mwangalia baba yake kama yupo hai pale na maamuzi ya haraka ambayo ameyachukua, nadhani kuna kitu atakuwa anakificha huyo mtu” R aliongea akiwa anamchambulia baba yake vyema baada ya kuhisi kwamba huyo mtu hakuwa yule ambaye alimdhania yeye.

“Nisikilize mwanangu ile ni hali ya kawaida sana hasa pale ambapo unampoteza mtu wa mhimu sana kwenye maisha yako. Hata mimi siku nimempoteza mama yangu nilikuwa kwenye hali ambayo haikuwahi kunipata hata siku moja kwani nilijikuta nafanya mambo ambayo yalikuwa nje ya uwezo wangu na kwa haraka sana. Yule ni kijana ambaye maisha yake yote ameishi akiwa anashika kalamu tu tena baada ya kugundulika kuwa moja ya wale watu ambao wana akili sana hivyo hana madhara yoyote kuhusu sisi, hata ingekuwa hivyo basi tungemmaliza haraka sana”
“Sawa mzee na huyu binti yake tutafanya naye nini?”

“Huyu endelea kumtunza kwanza atakuwa na kazi baadae endapo kutatokea lolote na haitakiwi alama yoyote ile ionekane kwamba wewe unahusika na hili maana itakuwa ni hatari sana na ukizingatia wewe kuna watu walikujua kama mpenzi wake hivyo ni vyema kama ukawa makini sana kwenye kila hatua ambayo unaipiga” alimaliza kuongea mr Mafupa ambapo kijana wake aliitikia kwa kutikisa kichwa wakaishia kukumbatiana kisha akatoka humo ndani.

Nickson,
Waweza kumuita Nick, lilikuwa ni jina la shushushu ambaye alikuwa amepewa kazi ya kuifuatilia familia ya Apson Limo huku pia akiwa amezifanya kazi nyingi sana za kijasusi nje ya nchi ndiyo maana kiongozi wake alikuwa amemuamini na kumpa kazi hiyo ambayo aliamini kwamba ni lazima kwamba angeifanya kwa usahihi sana kutokana na uzoefu wake mkubwa ambao alikuwa nao. Lingson Mfwomi, mkurugenzi mkuu wa idara ya usalama wataifa ndiye ambaye alikuwa amempa kazi hiyo Nick, mwanaume huyo alikuwa amekusanya taarifa za kutosha na usiku huo alikuwa amekutana na kiongozi wake ili aweze kuzitoa taarifa hizo kwa umakini sana.
“ulikuwa na taarifa za awali na kila ambacho kimetokea?”
“Hapana mkuu kulikuwa na viashiria tu ila hakukuwa na uhakika kama mambo yatatokea haraka sana namna hii na nilishindwa kujigawa kila sehemu kwa sababu ilikuwa inatakiwa kwa siku niondoke na mtu mmoja ninapokuwa natoka pale kwenye makazi ya mheshimiwa”
“Ok, umefikia wapi kwa sasa?”
“Nilikuwa na taarifa nyingi za kuihusu ile familia ila kwa bahati mbaya sana haya matatizo ambayo yameweza kutokea sidhani kama zitakuwa na umuhimu tena”
“Kwetu kila taarifa huwa ni ya mhimu sana kwani tunakuwa hatujui kama tutaihitaji lini na wapi hivyo nieleze kila ambacho sikifahamu”
“Mr Mafupa ndiye ambaye ameyafanya haya yote”
“Whaaaaat?”
“Ndiyo mkuu”
“Kivipi?”
“Wakati naendelea kuifuatilia ile familia kwa ukaribu sana, niligundua kwamba wengi hawakuwa na shaka zaidi ya ratiba zao za siku zote kwenda kama zilivyokuwa zinapangwa na familia ila mtu ambaye nilivutiwa kumfuatilia kwa ukaribu zaidi alikuwa ni mwanae wa kike”
“Enhe! Kafanyaje?”
“Yule binti ana mpenzi wake ambaye anaitwa Remsi, nadhani unamfahamu yule kijana ambaye anamiliki ile kampuni ya R LOGISTICS, CLEARING AND FOWARDING”
“Ndiyo namjua vyema”
“Sasa yule ndiye mpenzi wake na yule binti, baada ya kuona mahusiano yao nilivutiwa kuanza kuyafuatilia kwani niliona kwamba huenda kuna kitu kinaendelea kwa sababu sio kaaida sana kwa mfanya biashara kukimbilia kudate na mtu kutoka familia ambayo ipo kwenye siasa, huwa kuna faida zake lakini madhara yake ni mengi zaidi ndiyo maana nikaamua kuwafuatilia. Baadae nilikuja kugundua kwamba Remsi ni mtoto wa mr Mafupa kwani kuna siku niliona wanakutana kwa siri sana hivyo nikahitaji kujua ule mkutano kati ya mfanya biashara na mwanasiasa tena kwa siri unahusu nini. Nikawa na mashaka sana kwamba hao watu huenda wanajuana zaidi ya hapo kwani hata kuagana kwao waliagana kwa kukumbatiana huku mr Mafupa akimwangalia R kwa yale mapenzi ya baba, nikashtuka ikabidi nimrubuni binti mmoja pale kwenye kampuni yake nikawa nalala naye mpaka nilipopata nafasi ya kumuomba anaisaidie nywele za yule mtu” mwanaume alitulia kwanza kisha akaendelea;

“Sikujua binti alifanya nini ila aliniletea nywele zake nami nilihangaikia nywele za mr Mafupa na baada ya kwenda kupima DNA nikagundua kwamba ni baba na mtoto. Hapo nikashtuka, mr Mafupa ni mwanasiasa na binti yule baba yake ni mwanasiasa tena ambao wana upinzani mkubwa sasa hapo nikahitaji kujua kuna nini kinaendelea kwamba binti hajui kama yule ni mtoto wa kiume wa mr Mafupa?”

“Nilivyo chimbua kwa undani nikagundua kwamba binti hakuwahi kuujua uhalisia wa R, alikuwa amemdanganya kila kitu kuhusu maisha yake, sasa nikajua kwamba jamaa anamtumia bibie ili aweze kupata vitu anavyo vitaka kutoka kwake hivyo nikawa namfuatilia kwa umakini mkubwa sana. Baadae nikaja kugundua kwamba jamaa anafuatilia kuweza kuijua vyema ratiba ya familia ya mr Apson, uimara wao ni nini, udhaifu wao ni nini hasa ili wautumie kwa manufaa yao ya kisiasa. Na kwa sababu binti alikolea kwenye mapenzi alitoa siri zote ambazo alikuwa anaulizwa yeye akiamini kwamba yale ni mapenzi ya dhati asijue kwamba mwenzake alikuwa analichukulia hilo kama faida ya kukamilisha kile ambacho alikuwa anakitaka kwa mwanamke huyo”

“Sasa naada ya kupata kila ambacho walikuwa wanakihitaji ndipo wakaanza kutekeleza moja moja kwanza kuanza kumuua mtoto wa mzee yule wakijua ni lazima angepaniki, baada ya kufanya hilo ndipo ikajulikana kwamba hata binti yake wa kike hayupo amepotea kwenye mazingira ambayo hayaeleweki hivyo atakuwa ametekwa. Kama hesabu zao zilivyokuwa zimepangwa wakijua kwamba hiyo itamchanganya zaidi akili na kumfanya afanye maamuzi ya hovyo zaidi, walikuwa sahihi kwani naye ameingia kwenye mtego wao baada ya kufanya maamuzi ya kutumia hasira badala ya akili kwani aliondoka na kwenda kuwafuata watu ambao hana uhakika nao hivyo walijua hasira zake zitamfanya akurupuke na kweli aliondoka akiwa na mlinzi mmoja tu hivyo wakawa wamefanikiwa kumpiga zile risasi kiwepesi sana maana wenzake walijipanga muda mrefu yeye akawa amekurupuka”

Kumi na nane inafika tamati

Wasalaamu,

Febiani Babuya.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Ile riwaya ya"Document no. 72"ikiisha ndio nitaanza kusoma hii!
 
SIMULIZI: ELECTION SAGA (MONEY IN BLOOD)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

UKURASA WA KUMI NA TISA
“Ohhhhh shiiiit! Kuna muda ndiyo sababu kubwa huwa sitaki kuwaamini wanawake, wanaongozwa na mihemko ya hisia sana kuliko akili. Ushamba wake umeiponza familia yake mwenyewe. Kwahiyo unajua ni wapi alipo binti na nani kamteka?”

“Naweza kusema ndiyo japo sina uhakika sana”

“Una maanisha nini kusema hivyo”

“Kwa sababu wakati anatekwa mimi niliona na nikamfuatilia mtekaji mpaka nilipo iona sura yake maana alitumia gari yenye neno ZOO hivyo hata kama kamera zimenasa hazitaweza kujua gari ni ya nani. Nimemuona Remsi mwenyewe baada ya gari ile kwenda kupaki kwenye kampuni yake kisha kuna wanaume wakaja kumbeba yule mwanamke wakaingia naye ndani”

“Sasa unasemaje hauna uhakika wakati una taarifa kamili?”

“Nahisi ile ilikuwa ni kama kuzuga ili hata kama kuna mtu alikuwa anawafuatilia ajue kwamba mwanamke yule yupo pale ila mwisho wa siku ukienda pale huwezi kumpata kwani watakuwa wamemhamisha hapo wanakuwa wameua ndege wawili kwa jiwe moja. Maana yake kama kuna mtu amemuona lazima atamripoti hivyo atakuwa chini ya uangalizi mkali na ile kampuni yake itakaguliwa lakini pale itakapo kaguliwa na akagundulika kwamba hana hatia kabisa basi ataachwa na atasafishwa hivyo atakuwa amejitoa kwenye msala jumla. Ni michezo ya akili tu mkuu” mweanaume huyo aliyoosha maelezo kuonyesha kwamba alikuwa na uzoefu mkubwa sana wa hicho ambacho alikuwa anakifanya, hata mkuu wake alimkubali.

“Na mzee huyo wakati anapigwa risasi ulikuwa eneo la tukio?”

“Ndiyo mkuu”

“Haukuona haja ya kumsaidia?”

“Nadhani unatambua kwamba hilo halikuwa jukumu langu na sikujiandaa kwa hilo, kama ningefanya hivyo basi kulikuwa na hatari kubwa mbili, kujulikana au kuharibu kazi. Mimi baada ya yale yote kutokea niliamua kuwa karibu na yeye mwenyewe kumfuatilia kwa sababu nilijua kwamba angekuwa kwenye hali ya sitofahamu ambayo ingemfanya afanye vitu vya hovyo sana. Ndicho kimetokea amekurupuka na kutaka kuwafuata watu hao akaishia kupigwa risasi ambapo haijulikani kama amekufa au yupo hai”

“Amevamiwa na watu wangapi?”

“Hiyo ndiyo sababu kubwa ambayo imenifanya nishindwe kuingilia kila ambacho kilikuwa kinafanyika kwa sababu sikujua watu wapo wangapi ila nimeiona noah moja nyeusi ikiwa inamkimbiza huku naye anakimbia japo alionekana kwamba amechoka sana huenda kuna mtu alimuwekea kitu kama sio madawa. Ameshuka mwanaume mmoja kwenye ile Noah na kummiminia risasi zaidi ya sita kisha wakatoweka kwa kasi sana lile eneo”

“Wakati huo wote mlinzi wake alikuwa wapi?”

“Kwa mazingira yalivyokuwa maana gari ilitelekezwa hivyo atakuwa amemkimbia na nadhani ndiye mtu ambaye amempa madawa ya kumlegeza namna ile”

“Una maanisha kwamba huenda mlinzi wake alikuwa mtu wa mr Mafupa?”

“Bado sina uhakika na hilo mkuu”

“Kwanini hauna uhakika kwa sababu kwa mazingira yalivyo huenda ni muda tu alikuwa anatumika bila Apson mwenyewe kulitambua hilo”

“Wanasiasa ni watu wa ajabu sana, huenda wameangalia udhaifu wake wakautumia kumfanya aikamilishe kazi yao hivyo ni ngumu sana kuhitimisha moja kwa moja kwamba alikuwa anafanya kazi na watu hao”

“Hili jambo nahitaji libaki kwenye kifua chako kwa sasa, tusipo angalia kwa umakini nchi inaweza kuingia kwenye machafuko makubwa sana hivyo huu ni wakati ambao tunapaswa kuwa makini sana. Kila mtu analilia Ikulu na tukisema tuliache hili litokee tutaiingiza nchi kwenye hatari sana nadhani kwa sasa natakiwa kufanya maamuzi magumu sana” kiongozi huyo aliongea kwa masikitiko sana huku akiwa anakaa chini. Mwelekeo wa nchi ulikuwa upo kwenye sehemu mbaya sana maana kama umwagaji wa damu ulikuwa umeanza mapema sana namna hiyo mpaka wamalize sakata la uchaguzi maisha ya watu wengi sana hususani wasio na hatia yangekuwa yamepotea hivyo alijiona kwamba anapaswa kufanya maamuzi magumu ili kuweza kuzuia hali ya hatari yoyote ile isije ikatokea kwenye nchi yake maana aliona yeye ndiye angekuwa mtu wa kupata lawama kuliko yeyote yule japo wakubwa wake walikuwa wanamuweka kwenye mazingira magumu ambapo walitaka asikilize wanacho kitaka wao.

“Mkuu unataka tufanyaje juu ya hili jambo?”

“Nick, tungekuwa kwenye nchi kama Marekani hili jambo lilikuwa jepesi sana kwa sababu tungefanya mamauzi ambayo tunayataka sisi na tunaona yanafaa kwa maslahi ya taifa hata kama raisi akipinga lakini shida ya hii nchi, idara ya usalama ipo chini ya raisi na kiuhalisia ndiye bosi wangu na kimaamuzi yupo juu yangu hivyo kauli yake inazingatiwa sana na nikiidharau yanaweza kutokea mambo mabaya sana kwani vijana wangu wa karibu watatafutwa na kuuawa au kupewa kesi na familia zao kuingia kwenye hatari kubwa sana lakini mimi mwenyewe nakuwa sina kazi tena na naweza kuishia kupewa hata kesi ya ugaidi. Hivyo kwenye hii nafasi yangu sifanyi mamuzi kwa ajili yangu tu bali hata watu ambao wananizunguka kwani nao watakuwa kwenye hatari kubwa sana kama kuna jambo litatokea. Ila kwa sasa nahitaji uifanye kazi moja tu na ndiyo uiwekee umakini mkubwa sana” kiongozi huyo alikuwa anateta na kijana wake ambaye alikuwa akimwamini sana.

“Wananchi watakuwa na maswali mengi sana na hawatakubali hili lipite, yule mtu wanampenda sana na waliahidi kwamba watamfanya awe raisi hivyo kuna mengi yataibuka hapa kama hayo ya DCI ambaye inabidi nionane naye usiku huu huu anipe sababu za msingi za kuanza kumchafua kwa wananchi mzee huyo wakati hana hatia hata moja. Sasa wananchi wanaweza kuona kama hatufanyi kazi na tumeamua kuitelekeza familia hiyo, unatakiwa umfuatilie kila hatua huyo mtoto wake wa kiume lakini pia umlinde kwa nguvu zako zote maana huenda naye yupo kwenye hesabu za kuuawa mpaka pale hali itakapo badilika nitakupa maagizo mengine ya nini cha kukifanya zaidi” maelezo ambayo aliyatoa yalikuwa yakieleweka sana, hakuonekana kuvutiwa na mambo ambayo yalikuwa yanaendelea yeye kama kiongozi mkuu wa usalama nchini ila hakuwa na namna kwani wakubwa ndio ambao walikuwa nyuma ya mambo mengi yaliyokuwa yakiendelea.

“Sawa mkuu” Nickson alijibu huku akitoa heshima na kutoka humo ndani ili akayaanze majukumu yake mapya ya kuianza hiyo kazi ya kumfuatilia na kumlinda Tommy bila yeye kujua.


Saa sita kamili usiku, msafara wa gari tatu ambazo zilikuwa na namba za Ikulu, ulikuwa upo spidi sana kuelekea Masaki. Watu hao walitumia dakika thelathini tu kufika eneo ambalo walikuwa wamelikusudia nje ya jengo kubwa ambalo lilionekana kabisa kwamba mtu ambaye alikuwa anaishi ndani yake hakuwa na mawazo ya maisha wala wasiwasi wowote ule na kila ambacho kilikuwa kinaendelea kwenye maisha yake. Aliyeshuka ndani ya gari hiyo alikuwa ni mkurugenzi wa usalama wa taifa na hapo alikuwa amefika nyumbani kwa DCI kuja kuongea naye ili ampe sababu za msingi hasa za kuweza kutoa taarifa kwamba Apson Limo amekutwa na makosa ya jinai ambayo yalitakiwa kufikishwa mahakamani ili aweze kuchunguzwa haraka sana huenda alikuwa na mengi ambayo alikuwa anayaficha kuhusu nchi yake.

Mudrick Fiaso, ndilo lilikuwa jina la kiongozi huyo wa makosa ya jinai nchini DCI, wakati huo alikuwa yupo ndani na mkewe watoto wakiwa wamelala. Ni wakati ambao walikuwa wanaendelea kutazama movie tu huku nje walinzi wakiwa wametamalaki ili kudumisha ulinzi kwa kigogo mkubwa sana huyo. Aligongewa mlango na kushangaa sana kwa sababu muda kama huo haikuwa kawaida yeye kugongewa na walinzi wake labda kama yeye mwenyewe ndo angehitaji kutoka ndo angewapa taarifa vijana wake hao lakini wao kumgongea yeye ilimshtua sana hata mkewe aliingiwa na wasiwasi usio wa kawaida.

Alisogea mpaka kwenye kamera ambayo ilikuwa ineonyesha mlangoni, alimuona mlinzi akiwa na bunduki yake anagonga akiwa hana wasiwasi sana kiasi kwamba hakuona kama kuna hatari yoyote ile ya kutisha hivyo akaufungua mlango. Taarifa ambayo alipewa kidogo ilimshtua sana kwani aliambiwa kwamba kuna gari nje ya geti hilo ambazo zina namba za Ikulu na kuna mtu ambaye alihitaji kuweza kuzungumza naye. Alishtuka sana kwani haikuwa kawaida gari za Ikulu kufika kwake, hata kama mheshimiwa au watu wa ikulu walikuwa wana shida naye walikuwa wanaweza kumpigia simu yeye ndiye aende sasa hiyo ya kufuatwa hadi nyumbani kwake tena usiku kama huo haikuwa ishara nzuri sana ila hakuwa na namna zaidi ya kuwapa ishara walinzi hao waweze kumruhusu mtu huyo aweze kuingia. Wasiwasi wake ulizidi na moyo ulilipuka kwa aina ya mtu ambaye alikuwa anamuona hapo, mtu huyo alikuwa anazitumia gari za Ikulu ili kurahisisha majukumu yake kwani gari hizo zilikuwa na huduma maalumu popote pale na hiyo ilikuwa inasaidia watu wengi wasiweze kumjua kwamba uhalisia wake yeye alikuwa ni nani hasa.

DCI alikuwa anamjua vizuri sana mtu huyo kwani taasisi yake ndiyo taasisi ambayo ilikuwa inaogopwa na kila kiongozi, kila mwanasiasa na hata wafanya biashara hakuna ambaye alikuwa anapenda kuwa na vikwazo na taasisi hiyo kwani wakiamua kukubana na ukaingia kwenye kumi na nane zao basi hata hiyo nchi unaweza kutamani uihame maana utajuta haswa.

“Karibu sana kiongozi” alimchangamkia huku wakipeana mikono lakini mtu huyo hakumjibu chochote zaidi ya kuongoza nyuma ya nyumba hiyo ambako kulikuwa na sehemu ya kufanyia mazungumzo na aliamini huko wangefikia mwafaka wa kile ambacho kilikuwa kimemleta pale. Baaa ya kutojibiwa salamu DCI alijikohoza tena ili kumchangamkia mzee huyo

“Kiongozi ni hatari sana wewe kuwa pekeyako, mbona hauna walinzi?” hiyo ndiyo kauli ambayo ilimtoka mdomoni mwake na kumfanya mzee huyo amwangalie kwa umakini sana

“Hivi watu kama wewe huwa mnapataje nafasi kubwa kama hizo? Au ndo mnapewa kwa sababu mnajuana na watu? Unahisi mtu kama mimi naweza kutembea mwenyewe? Kwani mlinzi wako wakati anakuja kukupa taarifa alikwambia kuna gari imekuja au gari zimekuja? Kuwa makini na siku nyingine kukwepa aibu ndogo ndogo kama hizo halafu sijajua unaniulizaje swali jepesi kama hilo wakati unajua mimi naweza kuwa na watu sehemu yoyote ile hivyo usije ukashangaa hata siku unapo ambiwa mkeo ni kijana wangu”

“Nisamehe sana mheshimiwa na najua nimekosea sana kwenye hili, ila naomba kukuuliza kwamba hapa kimekuleta nini na usiku wote kama huu ambapo ungeweza kunipigia hata simu au hata kunikumbusha kesho tuweze kuonana?” DCI ni kama alikuwa anajishtukia yeye mwenyewe.

“Uko sahihi mimi sio kawaida yangu kuja sehemu namna hii hususani kwa mtu ambaye sina shida naye maana huwa sipendi kabisa kupoteza muda wangu ila mpaka nimekuja kwako basi ujue kuna jambo la umuhimu sana nyuma yake. Kama unavyojua bwana Fiaso, nina imani kwamba ulishawahi kusikia na unasikia kila siku namna sisi tunavyofanya kazi, nina taarifa za siri za viongozi wote wa taifa hili lakini pia watu wote wenye nyazifa kubwa ndani ya hili taifa ukiwepo wewe hapo na taarifa hizo zinaweza kutolewa au zisitolewe kulingana na umuhimu wake na mhusika mwenyewe ambaye zinakuwa zinamhusu moja kwa moja”

“Hilo ndilo linawafanya mtuogope sana na hata wewe ndiyo sababu ya kujifanya unaninyenyekea hapo wakati moyoni mwako huenda unanitukana na kutamani nife. Nataka nikukumbushe jambo moja tu ambalo huenda unahisi ulilifanyia gizani ila kuna watu wanalo, miaka miwili nyuma ulimteka binti mmoja ambaye alikuwa ni mrembo sana ukambaka na baada ya kutishia kukuumbua hadharani ukamuua na kuupoteza mwili wake ili ushahidi usipatikane, unakumbuka?” DCI uso wake ulianza kulowa jasho maana yalianza kufukuliwa makaburi ambayo hakuwa ameyafikiria kwa wakati huo na kumfanya aongeze mashaka huku nafsi yake ikianza kumuenda mbio isivyo kawaida.

Sina la nyongeza, ukurasa wa kumi na tisa unafika mwisho.

Wasalaam,

Febiani Babuya.
 
SIMULIZI: ELECTION SAGA (MONEY IN BLOOD)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

UKURASA WA ISHIRINI
“Unajua wananchi wakizisikia hizi habari itakuwaje? Unahisi mkeo ambaye anakuamini sana atakubali kuendelea kuishi na mwanaume kama wewe?” mheshimiwa alitulia kidogo akiwa anamwangalia DCI alivyokuwa anahangaika huku akiwa amejiinamia chini kwani mtu huyo hata hapo hapo kama angeamua kumuita mkewe ampe ukweli basi yangetokea matatizo mazito sana.

“Unahisi kwanini hizi habari hatuzitoi hadharani bwana Fiaso?”

“Hapana mheshimiwa sijui!”

“Sababu ya kwanza ni kulinda amani ya nchi kwa sababu wananchi wengi wanaamini kwamba kwa sababu nyie mmepewa nafasi kubwa basi mtakuwa wasafi hivyo matumaini yao yapo kwenu kama tukiseme tuanze kuuweka hadharani huu uozo wenu basi nchi inaweza kuingia kwenye machafuko kwani wanaweza wakatamani kumpinduaa hata raisi wao. Lakini sababu ya pili ni kwamba hizi taarifa huwa tunazihifadhi kwa ajili ya matumizi ya baadae hususani pale itakapobidi kuweza kuzitumia na itakapo lazimu hivyo kama ukitulazimisha kuziachia sisi hatuna tatizo tutaangalia namna ya kuwalinda wananchi wetu na jina la nchi yetu kisha wewe unaozea jela” mzee huyo hata hakuwa na haraka sana na kile ambacho alikuwa anakifanya, aliamini wanatakiwa kuongea kiume zaidi ili waende sawa.

“Unahitaji nini mheshimiwa?” alijibu kwa pupa kwani maamuzi ya nini kinachotakiwa kufanyika yalikuwa kwenye mkono wake mwenyewe na maamuzi ya mwisho yalikuwa kwake.
“Nahitaji unitajie jina la aliyekutuma wewe uweze kutoa ile kauli kutoka kwenye ofisi yako kumhusu Apson Limo” DCI alibaki ameduwaa tu kwani alicho ambiwa akifanye midomo yake ilikuwa mizito sana kuweza kukifanya kwa huo muda.

“Mimi sikulazimishi kunijibu, ila hicho ndicho nilikuwa nakitaka na nina imani hautanilaumu kwa kinacho enda kukukuta wewe na familia yako” kiongozi huyo nafasi yake haikuwa ikimpa hiyo huruma ya kuanza kumbembeleza mtu kwani mtu ambaye asingekuwa tayari kutoa ushirikiano wake basi yalikuwa yanatakiwa kufanyika maamuzi magumu ili aweze kuutoa kwa lazima hata kama asingehitaji kufanya hivyo. Alianza kuondoka baada ya kuona mtu huyo hayupo tayari kukifungua kinywa chake.

“Mheshimiwa raisi” ndilo jibu ambalo alilitoa huku akiwa anatetemeka maana kama mheshimiwa angejua kwamba mtu huyo ameanza kutoa siri zake ilikuwa ni hatari sana lakini pia hakuwa na namna ya kuweza kuukwepa huo mtego pia wa kiongozi mkuu wa idara ya usalama wa taifa.

“Kwahiyo tukio amefanya mwingine halafu tena baade mipango mingine anakuja kuitekeleza mwingine?”

“Ndiyo mheshimiwa”

“Hii nchi tumepata raisi mpumbavu sana japo ndiye bosi wangu” kiongozi huyo alikuwa anaongea huku akiwa amemgeukia DCI ambaye naye alikuwa amesimama kujua hatima yake maana kama kujibu alicho ulizwa alikuwa amejibu vyema hivyo alikuwa anasubiria maamuzi ya kiongozi huyo kujua kilichokuwa kinafuata ni kipi hasa.

“Nitakapo kuhitaji tena nitakupigia simu japo jambo hili litapaswa kusalia kwenye kifua chako juu ya haya ambayo tumeyaongea ila kama utaona friji lako haliwezi kugandisha unaweza ukatangaza unapo pataka mwenyewe kikubwa uwe tayari kwa matokeo yake” maneno hayo yalikuwa hitimisho la hayo mauzungumzo ambapo mkurugenzi huyo alitoweka hilo eneo akiwa amelipata jibu ambalo alikuwa analihitaji yeye.


Boniphace Walawala ambaye alikuwa ni raisi bado huku akiusubiria uchaguzi uweze kufanyika, alikuwa amekaa pembezoni mwa bwawa la kuogelea akiwa na wine yake mkononi na sigara yake kubwa ya bei ghali akiwa anapigwa na upepo ambao ulimfanya aifurahie sana hali ya hapo alipokuwa. Akiwa hilo eneo mzee ambaye ndiye alikuwa mshauri wake mkuu alifika hapo akiwa na mkoba wake, alitoa heshima kwa kiongozi wake kisha naye akaketi kando yake.

“Nikiwa kijana mdogo nakumbuka baba yangu aliwahi kunifunza kwamba kuna watu kama hauwezi kushindana nao basi hakikisha unaungana nao lakini ilikuwa tofauti kwa Apson Limo, yule bwana alikuwa anahisi yeye ndiye kila kitu, alikuwa anajiona kwamba hii nchi yeye ndiye anaijua sana huku akisahau kwamba kuna watu tuna historia ndefu sana na nchi hii mwisho wa siku akashindwa kuniheshimu hadi mimi raisi wake. Namsikitikia sana kwa kila ambacho kinaendelea kwani ni lazima afe kabisa sitaki aishi huyu mtu, kushindwa kunisikiliza mimi ni dharau kubwa ambayo siwezi kumsamehe kabisa” aliongea kwa majigambo huku akiwa anautolea moshi puani hata hivyo mshauri wake hakutaka kabisa kuingilia hiyo hoja.

“Mheshimiwa nasikia unanihitaji?” aliongea mzee huyo kwa heshima kwa sababu licha ya kuwa mtu mzima lakini huyo aliyekuwa mbele yake alikuwa ni raisi wa nchi hivyo heshima ilitakiwa kufuata mkondo wake.

“Ndiyo nimekuita, nimekuita kwa sababu umekuwa mtu wangu wa mhimu sana na ushauri wako unanisaidia mimi kwenye mambo mengi sana hususani haya ambayo yametokea. Nakumbuka siku ile uliniambia kwamba jambo la mhimu kama raisi sitakiwi kuruhusu mtu ambaye ananizidi akili kuwa mpinzani wangu hivyo nafurahia sana kwa mtu mwenye akili kama wewe kuwa upande wangu mimi na ushauri wako unafanya kazi sana ndiyo maana nimekuita tena ili nipate maarifa yako usiku huu wa leo kabla sijafanya maamuzi” mheshimiwa aliongea kwa kujitanua huku akiigida wine yake na kuendelea.

“Kweli nimeamini kwamba mr Mafupa ana akili ndogo sana hivyo tutaitumia akili yake kutimiza kila jambo langu. Ukurupukaji wake unatakiwa kuwa wa faida kwetu hivyo kila mpango ambao yeye anaupanga sisi tutakuwa tunautumia kwa faida ya kutimiza yaliyo yetu. Kwa mfano hili jambo la kumshambulia mr Apson, mimi nimehusika kwenye mambo machache sana baada ya kuujua mpango wake kwahiyo hata siku yakitokea mambo ya kutokea mimi sitakuwa nahusika kwa sababu yeye ndiye ambaye atajulikana kwamba anahusika moja kwa moja na haya mimi nitakuwa salama”

“Upo sahihi kabisa mheshimiwa”

‘Kwa sasa unanishauri nini kuhusu hii nafasi ambayo tunaigombania kati yangu mimi na yeye? Maana Apson Limo atakuwa ameshakufa tayari hivyo chama chake kitalazimika kumuweka mtu dhaifu ila ndani ya chama chetu itakuaje?” raisi huyo alihitaji kuyapata mawazo ya mzee huyo akiamini kwamba yangekuwa na maana kubwa sana kwenye hizo hatua zake ambazo alikuwa anatakiwa kuzipiga.

“Nadhani unatakiwa kuachia madaraka”

“Whaaaat?” mheshimiwa ni kama hakuweza kuamini kama kauli hiyo inatoka kwa mzee huyo, yaani kivipi mshauri wake anahitaji yeye aweze kuyaachia madaraka?

“Ndiyo mheshimiwa”

“Bado sijaielewa pointi yako ya msingi ni ipi?”

“Mheshimiwa labda nikuulize swali rahisi sana, kwani wewe shida yako kubwa ni kutimiza malengo yako au kukaa kwenye hicho kiti?”

“Mhhhhh malengo yangu yanatimia nikiwa kwenye hiki kiti tu na sio vinginevyo”

“Sio kweli mheshimiwa”

“Unataka kusema kwamba?”

“Kwani kati ya raisi na anaye muendesha raisi unahisi nani anakuwa kwenye nafasi nzuri zaidi ya kutimiza malengo yake?”
“Unataka kusema kwamba kuna mtu ananiendesha mimi?”
“Hapana mheshimiwa, jambo la msingi nadhani ungekubali tumalize haya mazungumzo vizuri hapo ungenielewa kwamba namaanisha nini napokuwa nakwambia hivyo”

“Ok nakusikiliza”

“Bado haujanijibu mheshimiwa”

“Raisi ndiye mtu ambaye anakuwa ana nafasi kubwa ya kufanya chochote anacho kitaka yeye sasa unahisi kuna mtu gani mwingine atakuwa na nafsi kubwa ya kutekeleza anayo yataka zaidi ya raisi?”

“Hapo ndipo unapo kosea kwenye kufanya maamuzi mheshimiwa, mtu anaye yatimiza malengo yake kirahisi kati ya hao wawili sio raisi wa nchi bali huyo mtu ambaye anakuwa anamuendesha raisi wa nchi hiyo”

“Mhhhhh kwanini?”

“Kwa sababu anakuwa anayafanya mambo yake bila presha, anakuwa anafanya kazi zake kama mzimu kiasi kwamba hata likitokea tatizo kubwa au madhara makubwa sana mtu ambaye atawajibika na kuchafuka ni raisi na sio yeye hivyo yeye anakuwa salama muda wote”

“Endelea ni kama kuna kitu naanza kukipata kwako”

“Moja kati ya makosa makubwa ambayo utakuwa unayafanya kwa sasa ni kuhisi kwamba wananchi hawaoni kinacho tokea na kinacho endelea nchini, watu wanaona kila kitu na wanaelewa kila kitu ila ukimya wa watu wengi inaweza kuja kuwa hatari sana hapo baadae kwa sababu huwa wanaibuka watu ambao hata hawajulikani wanakuja kufanya matukio ya kutisha inabaki historia na wewe kama raisi unaweza kuja kuchafuka na kuchukiwa isivyokuwa kawaida na mwisho wako utakuwa hapo. Haya mauaji ambayo yameanza kutokea yatalichafua sana jina lako kwa wananchi hata kama utashinda tena hivyo utakuwa unawaongoza watu ambao hawakutaki wala hawakupedi, kwahiyo wewe unatakiwa ukae kando ila umtumie mtu mwingine kuweza kuiendesha nchi na kutekeleza yale ambayo unayataka ili baadae haya mambo yanapokuja kulipuka wewe unakuwa umejiweka kando” mzee huyo alitulia akiwa anaitoa frash moja na kuiweka mezani kisha akaendelea.

“Mtu ambaye anatakiwa kuingia Ikulu ni Mr Mafupa, najua haya mambo ambayo yametokea kuna mmoja kati ya viongozi au mwanafamilia au wananchi wenye uchungu watakuja kuyazusha hapo baadae kama sio kisheria basi yanaweza kuwa mauaji maana usije ukahisi kwa sababu watu wanakusikiliza basi wanakupenda hautakiwi kuingia kwenye huo mtego. Hivyo wakati mambo yanakuja kuharibika wewe utakuwa haupo, mtu pekee ambaye atakutana na hilo balaa atakuwa mr Mafupa” mzee huyo alionyesha uwezo wake wa kufikiria sana ambao ulimfanya mpaka raisi huyo aheme kwa nguvu na kuizima sigara yake maana mambo ambayo yalikuwa yanaongelewa hapo yalianza kuonekana kuwa mazito sana kiasi kwamba alitakiwa kuwa makini ili kuweza kuyasikiliza kwa umakini usio wa kawaida.
“Mpango wako ni upi?” Ndilo swali ambalo aliliuliza

“Mheshimiwa wewe umeishi kama kivuli na umefanikiwa kuichukua nafasi hiyo ambayo kiuhalisia haikupaswa kuwa yako lakini ukawa raisi hivyo inatakiwa uishi pia kwenye sura ya mtu mwingine kama ulivyo ishi kwa miaka hii kadhaa ambapo jeshi lilijua wewe ulishakufa kabla ya kuwa kwenye hiyo sura ambayo inakufanya uliongoze taifa. Hiyo sura ndiyo ambayo itakufanya wewe uishi kwa namna unayo itaka wewe kwa sababu raisi atakuwa kibaraka wako”

Kwa mawazo yako unahisi huyu raisi ni nani haswa? Na ana vitu gani ambavyo vinaonekana kuwa vigeni na havijulikani kwa watu wengine? Ni kweli raisi anatakiwa kuondoka Ikulu na kwenda kuishi kwenye sura ya mtu mwingine? Hata mimi sina majibu, ukurasa wa ishirini unafika mwisho.

Wasalaam,

Febiani Babuya.
 
Back
Top Bottom