FEBIANI BABUYA
JF-Expert Member
- Mar 5, 2022
- 1,916
- 3,850
- Thread starter
- #121
SIMULIZI: ELECTION SAGA (MONEY IN BLOOD)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+
UKURASA WA THELATHINI NA NANE
Ndani ya dakika kumi baada ya yeye kuondoka, kuna msafara wa gari sita uliingia hapo, alikuwa mr Mafupa mwenyewe akiwa ameongozana na mwanae Remsi hivyo walichelewa kidogo sana kufika hilo eneo hali ambayo iliwafanya wapishane na mtu ambaye walikuwa wamemfuata.
Walikuwa kwenye mwendo mkali sana ili kuweza kuwahi ndani kujua kipi ambacho kilikuwa kimejiri humo lakini walicho fanikiwa kukiona yalikuwa ni mauaji tu tena mwanaume mmoja akiwa amekatwa kichwa chake kikahifadhiwa pembeni na kiwili wili chake. Waliwahi mpaka ndani ya chumba ambacho walikuwa wamemhifadhi Patrina, chumba kilikuwa kitupu bila mtu yeyote yule, walichoka sana.
Mr Mafupa aliitoa simu yake haraka mno na kuipiga mahali ambako ilionekana wazi kwamba ni kwa mr Oscar.
“Nakuja hapo sasa hivi” aliongea akiwa anahema kwa nguvu sana kichwa chake kikionekana kuvurugika moja kwa moja, hayo mambo kama yangeweza kufika kwa waandishi wa habari yangemharibia kila kitu ambacho alikuwa amekitengenza kwa muda mrefu sana na hakuwa tayari kabisa jambo hilo kuweza kutokea ndani ya nchi yake hata kama ingekuwa kwa kumwaga damu za watu kiasi gani. Aliondoka hilo eneo haraka sana akiwa kama mtu ambaye alivurugwa na ni kweli hayo mambo yalianza kumvuruga haswa.
Hakukuwa na muda wa kupoteza tena, usiku huo huo ambao Tommy alikuwa ametoka Kurasini alipitiliza moja kwa moja mpaka mhimbili kwenda kukabidhi kichwa hicho ambapo alisisitiza sana kwamba kichwa hicho kilitakiwa kuunganishwa pamoja na mwili wa mdogo wake ili uandaliwe kwa ajili mazishi maana hicho ndicho kitu pekee ambacho kilikuwa kinasubiriwa na familia, ingekuwa aibu kubwa sana kuweza kukizika kiwili wili pekee bila kichwa chake.
Baada ya kuhakikisha ametimiza hilo jukumu, alisogea mpaka kwenye wodi ambayo baba yake alikuwa amelazwa, alimwangalia sana baba yake pale kitandani ambapo alikuwepo, alikuwa anajihisi kuwa na hatia sana kwa kushindwa kuweza kuilinda familia yake.
“Nimewapa binti zako wote baba, wanao nimewarudisha” aliongea kwa hisia sana akiwa anaamini kwamba mzee huyo hakuwa akimsikia kabisa kisha akatoka humo ndani kwani alikuwa na kazi ya kumpeleka dada yake nyumbani. Lakini wakati ametoka humo ndani mwanaume huyo ambaye alikuwa amelala hapo kitandani, hakuwa na uwezo hata wa kuchezesha vidole vyake lakini machozi yalionekana yakishuka kwenye mashavu yake kitu kilichokuwa kinaashiria kwamba alikuwa anasikia kila kilichokuwa kinaendelea humo ndani.
Safari ya Tommy iliishia nyumbani kwao ambapo nje ya geti la nyumbani kwao alifanikiwa kumkuta daktari binafsi wa familia akiwa anamsubiria hapo ikiwa ni maagizo yake na hakutaka mtu huyo aiingie ndani kabla ya yeye kufika ndani ya hilo eneo. Waliongozana pamoja mwanaume akiwa amembeba dada yake kwenye mikono yake.
Baada ya geti hilo kufunguliwa, alimuona mama yake mzazi akiwa amekaa karibu na zilipo ngazi za kupandishia kwenye jengo hilo la kifahari. Muda ulikuwa umeenda sana hivyo ni wazi kwamba mama huyo sababu kubwa ya kukaa hapo alikuwa anamsubiri mwanae huyo arudi ili wawe na mazngumzo marefu sana lakini baada ya kumuona Tommy akiwa amembea dada yake alijikuta anatoa machozi na kumshika mtoto wake wa kike huyo ambapo ililazimika kupelekwa ndani kisha dakatari akaachwa aweze kuifanya kazi yake ambayo ilikuwa imemleta.
“Alikuwa amechomwa sindano za madawa ambayo yangemfanya alale kwa masaa kumi na nane ila nimemchoma sindano nyingine ambayo itamfanya asubuhi awe ameamka na atakuwa sawa hakuna kitu kibaya sana kwenye mwili wake ila anatakiwa kupatiwa muda mrefu zaidi wa kuweza kupumzika na asiwe karibu na vitu ambavyo vinaweza kumpatia msongo wa mawazo inaweza kumletea matatizo makubwa sana kwenye akili yake” daktari alitoa maelezo akiwa anamkabidhi Tommy dawa ambayo dada yake huyo alitakiwa kuitumia baada ya kuamka kisha yeye akatoka humo ndani kuelekea kwake.
Licha ya mama kuwa na furaha kubwa sana mwanae wa kike kuweza kupatikana na moyo wake kuonekana kutulia kwa kiasi kikubwa lakini alikuwa na wasiwasi mkubwa sana kwenye nafsi yake na ndiyo sababu kubwa haswa ambayo ilikuwa imemfanya aweze kumsubiria mwanae wakati wote huo ili aweze kufika hapo waweze kuongea kwa marefu zaidi juu ya yale ambayo yalikuwa yanaendelea.
“Nataka uniambie wewe ni nani na kila kitu ambacho kipo kwenye maisha yako. Kama unaniheshimu mimi kama mwanamke niliye kuzaa basi usije ukathubutu kunidanganya kama ulivyo nidanganya kwa miaka yote hii ambayo mimi sikuwa nakujua kabisa wewe, uliondoka tofauti na umerudi ukiwa mtu mwingine kabisa. Nahitaji uniambie kwamba wewe ni nani?” lilikuwa ni jambo la hatari sana mama yake mzazi ambaye alimzaa alikuwa amuuliza kwamba yeye ni nani. Mama alikuwa hamuamini tena mwanae huyo kwa sababu alihisi wanaishi na kiumbe ambacho hata wao hawakuwa wanakijua kwamba kipoje na kilikuwa kinafanya kazi zipi hasa kwenye maisha yake. Tommy alijisikia vibaya sana kupata maneno kama hayo kutoka kwa mama yake mzazi lakini njia pekee ambayo alikuwa nayo ya kuweza kufanya mama huyo amuelewe ilikuwa ni kumweleza ukweli wa maisha yake halisi ambayo alikuwa anayaficha sana.
“Mimi ni jasusi mama”
“Samahani, unamaanisha nini kusema hivyo?”
“Mimi ni mpelelezi wa siri kutoka ndani ya idara ya usalama wa taifa wa nchi ya Uingereza” mama huyo alibakia ameinamia chini akiwa hana hata la kusema maana alichoka sana kuyasikia hayo maelezo kutoka kwa mtoto ambaye alikuwa amemlea mwenyewe na kumtoa kwenye tumbo lake. Basi Tommy hakuwa na namna zaidi ya kuanza kumweleza mama yake ukweli wa mambo ulivyokuwa.
“Mimi kule wananijua kama T1 ikiwa na maana ya target namba moja kwa sababu kwenye huo mpango ambao ulinifanya mimi kuingia huko, mimi ndiye nilikuwa mtu wa mhimu zaidi kuliko mtu yeyote yule”
“Kwa mara ya kwanza tangu naenda kujiunga na masomo yangu ya elimu ya juu huko nchini Uingereza sikuwahi kabisa kuyajua haya mambo wala kufikiria kwamba siku moja na mimi nitakuwa mtu wa namna hii mpaka pale ambapo nilifanikiwa kukutana na mwanamke mmoja ambae anaitwa Harper”
“Baada ya kufika ndani ya kile chuo kila kitu kilikuwa kugeni sana kwangu, sikuwahi kumzoea mtu yeyote yule kwa sababu nilikuwa mtu mwenye aibu sana mama kama ulivyokuwa umeniambia mwanzo kitu ambacho kilifanya nihisi kwamba kila kitu kilikuwa kigeni na kigumu sana kwangu kwa sababu ya upweke wangu na nyie mlikuwa mbali sana na mimi. Ule upweke wangu ndio ambao ulimvuta mwanamke mmoja kuja karibu yangu mimi, mwanamke ambaye nilihisi kwamba alikuwa amekuja kwangu kwa sababu ya kuona kama mwanaume ninaye mfaa mama, mwanamke ambaye naweza kusema kwamba ndiye amekuja kuwa chanzo cha kila ambacho unakiona kinatokea kwenye maisha yangu”
“Ni mwanamke mrembo sana ambaye aliwahi kuniambia ana asili ya nchi ya Tanzania na Uingereza japo kwa baadae nilikuja kugundua kwamba alinidanganya pakubwa sana baada ya kujua kwamba alikuwa na asili ya Kiisyopia na kiingereza. Yule mwanamke alinifanya nisijihisi mpweke tena kwenye maisha yangu, akanifaya nikawa na furaha sana na kuyaona maisha ya kule yalikuwa mazuri sana na kwa mara ya kwanza nikajikuta naenza kuipenda nchi ambayo haikuwa nyumbani kwa sababu tu nilimpenda sana mwanamke yule”
“Nilimpenda kana kwamba ilifikia hatua nikawa namuamini sana, nikamuaonyesha mpaka kwangu nilipokuwa nakaa kwa sababu niliona kwamba ni mwanamke ambaye baada ya kumaliza masomo huenda ningekuja kuoana naye na kumtambulisha kwenu ila sikuwahi kuwa sahihi mama. Wanamwita H2 ikiwa na maana ya Honey Trap, mtego wa mapenzi ndio ambao huwa anautumia kushinda vita zake na anaitumia namba mbili kwa sababu baada ya mimi yeye ndiye ambaye ulikuwa mpango wa pili kwenye kulikamilisha hilo jambo ambalo walitarajia mimi ndiye niweze kulifanya”
“Yule mwanamke alikuja kwangu baada ya kugundua kwamba nina uwezo mkubwa sana kichwani hivyo walikuwa wanahitaji kukamilisha kuteketeleza mipango yao ya kuweza kuja kuishika dunia kwenye mikono yao kwa kutumia akili yangu hivyo ili kujua kila kitu kuhusu mimi wakalazimika kumtumia mwanamke huyo ambaye aliifanya hiyo kazi na baada ya kuona amepata kila ambacho alikuwa anakitaka kwangu ndipo siku moja alinijia na baadhi ya wakubwa wake wa kazi na kuniambia ukweli kwamba yeye alikuwa nani na lengo ambalo lilikuwa limewaleta pale”
“Waliniambia kwamba wanahitaji kukitengeneza kirusi pamoja na dawa yake na kirusi hicho walikuwa wanahitaji kukitumia kujilinda wao dhidi ya maadui zao na kwamba kingekuja kutumika kwenye kazi zingine za kisayansi hapo baadae kwenye nchi yao hususani kwa wasomi ambao walikuwa wanaendelea kuzalishwa kwenye mavyuo mbali mbali ndani ya nchi ya Uingereza. Mimi niligoma kabisa jambo hilo ndipo wakanisisitiza kwamba hawakuwa na lengo baya na kirusi hicho ambacho kingetengenezwa lakini bado niligoma kabisa kushiriki kwenye jambo la hatari sana namna hiyo”
“Baada ya kuona nimegoma, walinipa taarifa zote kuhusu familia yangu na wakanipa chaguo kwamba nitaamua mimi kama nahitaji familia yangu iachwe hai basi sina budi kuweza kukubali kazi yao lakini kama nikigoma basi nyie wote mngekuwa mmekufa muda mrefu sana. Hawakuishia hapo tu wakaniambia kwamba hata nchi yangu ingeingia kwenye machafuko makubwa sana ambayo yangefanya maisha ya watu wengi sana kuweza kupotea bila kusahau kuwekewa vikwazo vikali sana vya kiuchumi kwenye masoko ya kimataifa hali ambayo pia ingeifanya nchi yetu iingie kwenye umaskini mkubwa sana ambao ungekuwa ni mgumu hata kuweza kuulezea kwa lugha ya kawaida”
“Hivyo sikuwa na nguvu ya kuweza kukataa tena hilo ombi lao nikakubali kuifanya kazi yao kwa kuongeza sharti moja. Kwanza nilitaka wasije wakayafanya hayo ambayo waliyaorodhesha halafu ndipo nikahitaji na mimi wanitengeneze niwe binadamu hatari sana kwa sababu nilijua hayo mambo yanaweza kuja kuharibika baadae angalau wakati yanaharibika niwe na uwezo wa kuilinda familia yangu lakini pia niwe na uwezo wa kuilinda nchi yangu”
“Waliniambia ombi langu ni rahisi sana kulitekeleza ila kuna sheria zao na misingi yao, kama nikihitaji waweze kulifanya hilo zoezi maana yake nitatakiwa kuwa memba halisi wa shirika lao la kijasusi la MI6 kwani wasingeweza kunitengeneza mtu ambaye sikuwa mmoja wao kwani kama kazi ambayo nilikuwa naifanya ningelipwa hivyo ya gharama za kutengenezwa zilikuwa zinatoka kwa wale tu ambao wanakuwa ni miongoni mwao. Kulingana na unyeti wa tukio husika nikakubali na rasmi nikaapishwa kujiunga na shirika la kijasusi la nchi ya Uingereza kwa makubaliano kwamba nitakapo kamilisha kazi yao basi wataniruhusu niendelee na maisha yangu ya kawaida huku wakiniahidi kuilinda familia yangu kwa muda wote ambao ningekuwa mbali isipokuwa mwezi mmoja kabla ya mimi kurudi tulikubaliana waondoke kabisa na waache kuwa karibu na familia yangu maana nilitaka wakati narudi nisikute alama zao zozote kwani tungekuwa tumemalizana”
Ukurasa wa thelathini na nane nauhitimisha hapa, panapo majaaliwa tukutane wakati ujao.
Wasalaam,
Febiani Babuya.
Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+
UKURASA WA THELATHINI NA NANE
Ndani ya dakika kumi baada ya yeye kuondoka, kuna msafara wa gari sita uliingia hapo, alikuwa mr Mafupa mwenyewe akiwa ameongozana na mwanae Remsi hivyo walichelewa kidogo sana kufika hilo eneo hali ambayo iliwafanya wapishane na mtu ambaye walikuwa wamemfuata.
Walikuwa kwenye mwendo mkali sana ili kuweza kuwahi ndani kujua kipi ambacho kilikuwa kimejiri humo lakini walicho fanikiwa kukiona yalikuwa ni mauaji tu tena mwanaume mmoja akiwa amekatwa kichwa chake kikahifadhiwa pembeni na kiwili wili chake. Waliwahi mpaka ndani ya chumba ambacho walikuwa wamemhifadhi Patrina, chumba kilikuwa kitupu bila mtu yeyote yule, walichoka sana.
Mr Mafupa aliitoa simu yake haraka mno na kuipiga mahali ambako ilionekana wazi kwamba ni kwa mr Oscar.
“Nakuja hapo sasa hivi” aliongea akiwa anahema kwa nguvu sana kichwa chake kikionekana kuvurugika moja kwa moja, hayo mambo kama yangeweza kufika kwa waandishi wa habari yangemharibia kila kitu ambacho alikuwa amekitengenza kwa muda mrefu sana na hakuwa tayari kabisa jambo hilo kuweza kutokea ndani ya nchi yake hata kama ingekuwa kwa kumwaga damu za watu kiasi gani. Aliondoka hilo eneo haraka sana akiwa kama mtu ambaye alivurugwa na ni kweli hayo mambo yalianza kumvuruga haswa.
Hakukuwa na muda wa kupoteza tena, usiku huo huo ambao Tommy alikuwa ametoka Kurasini alipitiliza moja kwa moja mpaka mhimbili kwenda kukabidhi kichwa hicho ambapo alisisitiza sana kwamba kichwa hicho kilitakiwa kuunganishwa pamoja na mwili wa mdogo wake ili uandaliwe kwa ajili mazishi maana hicho ndicho kitu pekee ambacho kilikuwa kinasubiriwa na familia, ingekuwa aibu kubwa sana kuweza kukizika kiwili wili pekee bila kichwa chake.
Baada ya kuhakikisha ametimiza hilo jukumu, alisogea mpaka kwenye wodi ambayo baba yake alikuwa amelazwa, alimwangalia sana baba yake pale kitandani ambapo alikuwepo, alikuwa anajihisi kuwa na hatia sana kwa kushindwa kuweza kuilinda familia yake.
“Nimewapa binti zako wote baba, wanao nimewarudisha” aliongea kwa hisia sana akiwa anaamini kwamba mzee huyo hakuwa akimsikia kabisa kisha akatoka humo ndani kwani alikuwa na kazi ya kumpeleka dada yake nyumbani. Lakini wakati ametoka humo ndani mwanaume huyo ambaye alikuwa amelala hapo kitandani, hakuwa na uwezo hata wa kuchezesha vidole vyake lakini machozi yalionekana yakishuka kwenye mashavu yake kitu kilichokuwa kinaashiria kwamba alikuwa anasikia kila kilichokuwa kinaendelea humo ndani.
Safari ya Tommy iliishia nyumbani kwao ambapo nje ya geti la nyumbani kwao alifanikiwa kumkuta daktari binafsi wa familia akiwa anamsubiria hapo ikiwa ni maagizo yake na hakutaka mtu huyo aiingie ndani kabla ya yeye kufika ndani ya hilo eneo. Waliongozana pamoja mwanaume akiwa amembeba dada yake kwenye mikono yake.
Baada ya geti hilo kufunguliwa, alimuona mama yake mzazi akiwa amekaa karibu na zilipo ngazi za kupandishia kwenye jengo hilo la kifahari. Muda ulikuwa umeenda sana hivyo ni wazi kwamba mama huyo sababu kubwa ya kukaa hapo alikuwa anamsubiri mwanae huyo arudi ili wawe na mazngumzo marefu sana lakini baada ya kumuona Tommy akiwa amembea dada yake alijikuta anatoa machozi na kumshika mtoto wake wa kike huyo ambapo ililazimika kupelekwa ndani kisha dakatari akaachwa aweze kuifanya kazi yake ambayo ilikuwa imemleta.
“Alikuwa amechomwa sindano za madawa ambayo yangemfanya alale kwa masaa kumi na nane ila nimemchoma sindano nyingine ambayo itamfanya asubuhi awe ameamka na atakuwa sawa hakuna kitu kibaya sana kwenye mwili wake ila anatakiwa kupatiwa muda mrefu zaidi wa kuweza kupumzika na asiwe karibu na vitu ambavyo vinaweza kumpatia msongo wa mawazo inaweza kumletea matatizo makubwa sana kwenye akili yake” daktari alitoa maelezo akiwa anamkabidhi Tommy dawa ambayo dada yake huyo alitakiwa kuitumia baada ya kuamka kisha yeye akatoka humo ndani kuelekea kwake.
Licha ya mama kuwa na furaha kubwa sana mwanae wa kike kuweza kupatikana na moyo wake kuonekana kutulia kwa kiasi kikubwa lakini alikuwa na wasiwasi mkubwa sana kwenye nafsi yake na ndiyo sababu kubwa haswa ambayo ilikuwa imemfanya aweze kumsubiria mwanae wakati wote huo ili aweze kufika hapo waweze kuongea kwa marefu zaidi juu ya yale ambayo yalikuwa yanaendelea.
“Nataka uniambie wewe ni nani na kila kitu ambacho kipo kwenye maisha yako. Kama unaniheshimu mimi kama mwanamke niliye kuzaa basi usije ukathubutu kunidanganya kama ulivyo nidanganya kwa miaka yote hii ambayo mimi sikuwa nakujua kabisa wewe, uliondoka tofauti na umerudi ukiwa mtu mwingine kabisa. Nahitaji uniambie kwamba wewe ni nani?” lilikuwa ni jambo la hatari sana mama yake mzazi ambaye alimzaa alikuwa amuuliza kwamba yeye ni nani. Mama alikuwa hamuamini tena mwanae huyo kwa sababu alihisi wanaishi na kiumbe ambacho hata wao hawakuwa wanakijua kwamba kipoje na kilikuwa kinafanya kazi zipi hasa kwenye maisha yake. Tommy alijisikia vibaya sana kupata maneno kama hayo kutoka kwa mama yake mzazi lakini njia pekee ambayo alikuwa nayo ya kuweza kufanya mama huyo amuelewe ilikuwa ni kumweleza ukweli wa maisha yake halisi ambayo alikuwa anayaficha sana.
“Mimi ni jasusi mama”
“Samahani, unamaanisha nini kusema hivyo?”
“Mimi ni mpelelezi wa siri kutoka ndani ya idara ya usalama wa taifa wa nchi ya Uingereza” mama huyo alibakia ameinamia chini akiwa hana hata la kusema maana alichoka sana kuyasikia hayo maelezo kutoka kwa mtoto ambaye alikuwa amemlea mwenyewe na kumtoa kwenye tumbo lake. Basi Tommy hakuwa na namna zaidi ya kuanza kumweleza mama yake ukweli wa mambo ulivyokuwa.
“Mimi kule wananijua kama T1 ikiwa na maana ya target namba moja kwa sababu kwenye huo mpango ambao ulinifanya mimi kuingia huko, mimi ndiye nilikuwa mtu wa mhimu zaidi kuliko mtu yeyote yule”
“Kwa mara ya kwanza tangu naenda kujiunga na masomo yangu ya elimu ya juu huko nchini Uingereza sikuwahi kabisa kuyajua haya mambo wala kufikiria kwamba siku moja na mimi nitakuwa mtu wa namna hii mpaka pale ambapo nilifanikiwa kukutana na mwanamke mmoja ambae anaitwa Harper”
“Baada ya kufika ndani ya kile chuo kila kitu kilikuwa kugeni sana kwangu, sikuwahi kumzoea mtu yeyote yule kwa sababu nilikuwa mtu mwenye aibu sana mama kama ulivyokuwa umeniambia mwanzo kitu ambacho kilifanya nihisi kwamba kila kitu kilikuwa kigeni na kigumu sana kwangu kwa sababu ya upweke wangu na nyie mlikuwa mbali sana na mimi. Ule upweke wangu ndio ambao ulimvuta mwanamke mmoja kuja karibu yangu mimi, mwanamke ambaye nilihisi kwamba alikuwa amekuja kwangu kwa sababu ya kuona kama mwanaume ninaye mfaa mama, mwanamke ambaye naweza kusema kwamba ndiye amekuja kuwa chanzo cha kila ambacho unakiona kinatokea kwenye maisha yangu”
“Ni mwanamke mrembo sana ambaye aliwahi kuniambia ana asili ya nchi ya Tanzania na Uingereza japo kwa baadae nilikuja kugundua kwamba alinidanganya pakubwa sana baada ya kujua kwamba alikuwa na asili ya Kiisyopia na kiingereza. Yule mwanamke alinifanya nisijihisi mpweke tena kwenye maisha yangu, akanifaya nikawa na furaha sana na kuyaona maisha ya kule yalikuwa mazuri sana na kwa mara ya kwanza nikajikuta naenza kuipenda nchi ambayo haikuwa nyumbani kwa sababu tu nilimpenda sana mwanamke yule”
“Nilimpenda kana kwamba ilifikia hatua nikawa namuamini sana, nikamuaonyesha mpaka kwangu nilipokuwa nakaa kwa sababu niliona kwamba ni mwanamke ambaye baada ya kumaliza masomo huenda ningekuja kuoana naye na kumtambulisha kwenu ila sikuwahi kuwa sahihi mama. Wanamwita H2 ikiwa na maana ya Honey Trap, mtego wa mapenzi ndio ambao huwa anautumia kushinda vita zake na anaitumia namba mbili kwa sababu baada ya mimi yeye ndiye ambaye ulikuwa mpango wa pili kwenye kulikamilisha hilo jambo ambalo walitarajia mimi ndiye niweze kulifanya”
“Yule mwanamke alikuja kwangu baada ya kugundua kwamba nina uwezo mkubwa sana kichwani hivyo walikuwa wanahitaji kukamilisha kuteketeleza mipango yao ya kuweza kuja kuishika dunia kwenye mikono yao kwa kutumia akili yangu hivyo ili kujua kila kitu kuhusu mimi wakalazimika kumtumia mwanamke huyo ambaye aliifanya hiyo kazi na baada ya kuona amepata kila ambacho alikuwa anakitaka kwangu ndipo siku moja alinijia na baadhi ya wakubwa wake wa kazi na kuniambia ukweli kwamba yeye alikuwa nani na lengo ambalo lilikuwa limewaleta pale”
“Waliniambia kwamba wanahitaji kukitengeneza kirusi pamoja na dawa yake na kirusi hicho walikuwa wanahitaji kukitumia kujilinda wao dhidi ya maadui zao na kwamba kingekuja kutumika kwenye kazi zingine za kisayansi hapo baadae kwenye nchi yao hususani kwa wasomi ambao walikuwa wanaendelea kuzalishwa kwenye mavyuo mbali mbali ndani ya nchi ya Uingereza. Mimi niligoma kabisa jambo hilo ndipo wakanisisitiza kwamba hawakuwa na lengo baya na kirusi hicho ambacho kingetengenezwa lakini bado niligoma kabisa kushiriki kwenye jambo la hatari sana namna hiyo”
“Baada ya kuona nimegoma, walinipa taarifa zote kuhusu familia yangu na wakanipa chaguo kwamba nitaamua mimi kama nahitaji familia yangu iachwe hai basi sina budi kuweza kukubali kazi yao lakini kama nikigoma basi nyie wote mngekuwa mmekufa muda mrefu sana. Hawakuishia hapo tu wakaniambia kwamba hata nchi yangu ingeingia kwenye machafuko makubwa sana ambayo yangefanya maisha ya watu wengi sana kuweza kupotea bila kusahau kuwekewa vikwazo vikali sana vya kiuchumi kwenye masoko ya kimataifa hali ambayo pia ingeifanya nchi yetu iingie kwenye umaskini mkubwa sana ambao ungekuwa ni mgumu hata kuweza kuulezea kwa lugha ya kawaida”
“Hivyo sikuwa na nguvu ya kuweza kukataa tena hilo ombi lao nikakubali kuifanya kazi yao kwa kuongeza sharti moja. Kwanza nilitaka wasije wakayafanya hayo ambayo waliyaorodhesha halafu ndipo nikahitaji na mimi wanitengeneze niwe binadamu hatari sana kwa sababu nilijua hayo mambo yanaweza kuja kuharibika baadae angalau wakati yanaharibika niwe na uwezo wa kuilinda familia yangu lakini pia niwe na uwezo wa kuilinda nchi yangu”
“Waliniambia ombi langu ni rahisi sana kulitekeleza ila kuna sheria zao na misingi yao, kama nikihitaji waweze kulifanya hilo zoezi maana yake nitatakiwa kuwa memba halisi wa shirika lao la kijasusi la MI6 kwani wasingeweza kunitengeneza mtu ambaye sikuwa mmoja wao kwani kama kazi ambayo nilikuwa naifanya ningelipwa hivyo ya gharama za kutengenezwa zilikuwa zinatoka kwa wale tu ambao wanakuwa ni miongoni mwao. Kulingana na unyeti wa tukio husika nikakubali na rasmi nikaapishwa kujiunga na shirika la kijasusi la nchi ya Uingereza kwa makubaliano kwamba nitakapo kamilisha kazi yao basi wataniruhusu niendelee na maisha yangu ya kawaida huku wakiniahidi kuilinda familia yangu kwa muda wote ambao ningekuwa mbali isipokuwa mwezi mmoja kabla ya mimi kurudi tulikubaliana waondoke kabisa na waache kuwa karibu na familia yangu maana nilitaka wakati narudi nisikute alama zao zozote kwani tungekuwa tumemalizana”
Ukurasa wa thelathini na nane nauhitimisha hapa, panapo majaaliwa tukutane wakati ujao.
Wasalaam,
Febiani Babuya.
Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app