Sakata la ujenzi wa jengo la ghorofa 19 ikulu: Nani wa kumfunga paka kengere?

Sakata la ujenzi wa jengo la ghorofa 19 ikulu: Nani wa kumfunga paka kengere?

Miwatamu

JF-Expert Member
Joined
Oct 2, 2012
Posts
1,450
Reaction score
489
Tangu sakata la ujenzi wa jengo refu la ghorofa 19 lililopo karibu na Ikulu yetu kuanza kuwa gumzo hapa nchini, binafsi nimejitafakarisha mambo mengi kichwani mwangu. kitu cha kwanza ni kwamba kabla ya jengo hilo kujengwa yalikuwepo majengo ya serikali ambayo kwa idadi kubwa yalikuwa yakikaliwa na maofisa wa juu wa serikali. ufisadi na uvivu wa kufikiri wa viongozi waliopo Ikulu ndio uliochangia maeneo hayo yatolewe kwa watu binafsi japokuwa ukweli ni kuwa hata viongozi wenyewe wa Ikulu hiyo wamo kama wabia! Majengo hayo yamekuwa yakijengwa mchana kweupe! Rais wetu na mawaziri wake hiyo ndiyo njia yao wanayoitumia asubuhi na mchana na wote wamekuwa wakiona nini kinachoendelea hapo!
Sasa iweje leo baada ya jengo hilo kukamilika ndipo ionekane kuwa limejengwa kwa makosa? Je, usalama wa Taifa kazi yao ni ipi?! Au wanadhani ni kuvaa miwani myeusi na suti tu!

Je, inamaana kama FBI wasingekuja kwa ajili ya ujio wa Obama, wasalama wetu wasingegundua athari za jengo hilo? Mbona hata watu wa kawaida ambao wanapata huduma ya chakula kwa mama ntilie pale jirani wamekuwa wakiyasema hayo, inamaana usalama wetu ulikuwa haufiki pale na kupata maoni hayo?

Na, je, kuna sababu gani ya kusema jengo libomolewe wakati linaweza kutumika kwa matumizi ya serikali na mjenzi akafidiwa pesa yake?

Kwa hili maswali yapo mengi ambayo pengine hata majibu yake hayatakuwepo.

NDIYO MAANA CHADEMA INATAKIWA ILI IJE KUPITIA UPYA MIRADI KAMA HII.
 
Tangu sakata la ujenzi wa jengo refu la ghorofa 19 lililopo karibu na Ikulu yetu kuanza kuwa gumzo hapa nchini, binafsi nimejitafakarisha mambo mengi kichwani mwangu. kitu cha kwanza ni kwamba kabla ya jengo hilo kujengwa yalikuwepo majengo ya serikali ambayo kwa idadi kubwa yalikuwa yakikaliwa na maofisa wa juu wa serikali. ufisadi na uvivu wa kufikiri wa viongozi waliopo Ikulu ndio uliochangia maeneo hayo yatolewe kwa watu binafsi japokuwa ukweli ni kuwa hata viongozi wenyewe wa Ikulu hiyo wamo kama wabia! Majengo hayo yamekuwa yakijengwa mchana kweupe! Rais wetu na mawaziri wake hiyo ndiyo njia yao wanayoitumia asubuhi na mchana na wote wamekuwa wakiona nini kinachoendelea hapo!
Sasa iweje leo baada ya jengo hilo kukamilika ndipo ionekane kuwa limejengwa kwa makosa? Je, usalama wa Taifa kazi yao ni ipi?! Au wanadhani ni kuvaa miwani myeusi na suti tu!

Je, inamaana kama FBI wasingekuja kwa ajili ya ujio wa Obama, wasalama wetu wasingegundua athari za jengo hilo? Mbona hata watu wa kawaida ambao wanapata huduma ya chakula kwa mama ntilie pale jirani wamekuwa wakiyasema hayo, inamaana usalama wetu ulikuwa haufiki pale na kupata maoni hayo?

Na, je, kuna sababu gani ya kusema jengo libomolewe wakati linaweza kutumika kwa matumizi ya serikali na mjenzi akafidiwa pesa yake?

Kwa hili maswali yapo mengi ambayo pengine hata majibu yake hayatakuwepo.

NDIYO MAANA CHADEMA INATAKIWA ILI IJE KUPITIA UPYA MIRADI KAMA HII.

Hujaeleweka ndio maana thread hii imekosa wachangiaji. Hebu jaribu kujieleza vizuri zaidi tukuelewe
 
Usalama wetu mnawalalamikia bure tu kwani wao wamefunzwa kutesa kwa kung'oa kucha na meno masuala ya majengo watajua wapi? Walotoa kibali cha kujenga eneo hilo hawakufika ama walitoa ruhusa kupitia simu? Nani atakae wajibishwa hapa? Sitoshangaa ikaishia hivyo hivyo kama lile jengo lenye apartment nyingi pembeni ya ocean road
 
Hakuna point ya kuvunja jengo lile mimi naona jengolile liwe ofosi za serikali kuliko kuwa makazi ya watu.Kama ikiwa ni ofisi ya serikali itakuwa rahisi kulimonitor kuliko likiwa makazi ya watu
 
Hujaeleweka ndio maana thread hii imekosa wachangiaji. Hebu jaribu kujieleza vizuri zaidi tukuelewe

Ndugu yangu GeniusBrain siwezi kukulaumu kwani inadhihilisha ni kwajinsi gani akili yako ilivyolala na ndiyo maana huwezi hata kuipa muda wa kutafakari. Ila nashukuru kwamba umesoma na umeelewa nilichoongea ndiyo maana umecomment.
 
Last edited by a moderator:
Tangu sakata la ujenzi wa jengo refu la ghorofa 19 lililopo karibu na Ikulu yetu kuanza kuwa :bored::bored:gumzo hapa nchini, binafsi nimejitafakarisha mambo mengi kichwani mwangu. kitu cha kwanza ni kwamba kabla ya jengo hilo kujengwa yalikuwepo majengo ya serikali ambayo kwa idadi kubwa yalikuwa yakikaliwa na maofisa wa juu wa serikali. ufisadi na uvivu wa kufikiri wa viongozi waliopo Ikulu ndio uliochangia maeneo hayo yatolewe kwa watu binafsi japokuwa ukweli ni kuwa hata viongozi wenyewe wa Ikulu hiyo wamo kama wabia! Majengo hayo yamekuwa yakijengwa mchana kweupe! Rais wetu na mawaziri wake hiyo ndiyo njia yao wanayoitumia asubuhi na mchana na wote wamekuwa wakiona nini kinachoendelea hapo!
Sasa iweje leo baada ya jengo hilo kukamilika ndipo ionekane kuwa limejengwa kwa makosa? Je, usalama wa Taifa kazi yao ni ipi?! Au wanadhani ni kuvaa miwani myeusi na suti tu!

Je, inamaana kama FBI wasingekuja kwa ajili ya ujio wa Obama, wasalama wetu wasingegundua athari za jengo hilo? Mbona hata watu wa kawaida ambao wanapata huduma ya chakula kwa mama ntilie pale jirani wamekuwa wakiyasema hayo, inamaana usalama wetu ulikuwa haufiki pale na kupata maoni hayo?

Na, je, kuna sababu gani ya kusema jengo libomolewe wakati linaweza kutumika kwa matumizi ya serikali na mjenzi akafidiwa pesa yake?

Kwa hili maswali yapo mengi ambayo pengine hata majibu yake hayatakuwepo.

NDIYO MAANA CHADEMA INATAKIWA ILI IJE KUPITIA UPYA MIRADI KAMA HII.
:bored:Ndugu zangu msije mkawa mnamwandalia Kagame mahali muafaka pa kum HIT rais wetu. Kwa kweli kuweni makini. Hali hii inaweza ikamfanya rais kuwa na wasiwasi kila anapotoka au kuingia Ikulu.
 
Lazima tuelewe mfumo wetu wa ulinzi na usalama umekufa
Tangu za Mwalim kuna vijana wadogo hapa ikulu Miaka mitatu walk kuwa A'level sasa hivi wanaishi maisha anasa, statehouse sasa hivi ni ya familia pale.Othman,Zoka na wengi tu
Hata Mzee wa piga tu ndugu zake wapo kibao,Watanzania tusitegemee miujiza wengine tukihoji unaishia kwenye kisima cha maji au unapotea kabisa
 
Hakuna point ya kuvunja jengo lile mimi naona jengolile liwe ofosi za serikali kuliko kuwa makazi ya watu.Kama ikiwa ni ofisi ya serikali itakuwa rahisi kulimonitor kuliko likiwa makazi ya watu
Mbona ujiulizi jengo lile linamilikiwa na nani?au unadhani halina mwenyewe?
 
Mbona ujiulizi jengo lile linamilikiwa na nani?au unadhani halina mwenyewe?

Ndugu zangu mimi nadhani tuangalie mbali zaidi. Sehemu ilipo ikulu yetu kwa sasa sio salama tena kwa mambo mengi. Ni tishio hata kwa sunami, mazingira machafu yatokanayo na uchafu uelekezwao baharini, shuguli za kibinadamu kama za uvuvi na kata uchomaji taka hasa za hospitali iliyoko jirani. Sehemu ilipo ikulu kwa sasa ni lango kuu la bahari inayoingiza watu wenye nia njema na mbaya. Eneo la sasa ni wazi limekuwa sehemu ya mji na hatuwezi kukwepa pilikapilika zote tunazozifahamu za mijini. Sote tunajua siku za week ends shamrashamra zinazofanyika karimjee hall na viwanja vyake. Kelele zinazokuwepo huifanya ikulu isiwe mahali tulivu. Majengo mapya na marefu bila shaka yanahitajika jijini na yataendelea kujengwa. Kilichokuwa rahisi ili kutatua tuliyo nayo sasa na baadaye kwa mawazo yangu ni kuhamisha ikulu yetu na kuijenga sehemu salama zaidi hata ikibidi katikati ya kambi ya jeshi nje ya kidogo ya jiji. Ofisi za raisi zinaweza kuwa zaidi ya moja kuendana na mazingira yatakavyorurusu. Jengo linalozungumziwa sasa ni kivutio na linakidhi haja. Kwa umaskini tulio nao kufikiria kulivunja sio busara.
 
According to wadau flani, lile ni jengo la ridhone. Sasa kikwete hawezi bomoa jengo la mtoto wake wakati ye ndo mtoa hela
 
According to wadau flani, lile ni jengo la ridhone. Sasa kikwete hawezi bomoa jengo la mtoto wake wakati ye ndo mtoa hela

Kuna tetesi niliwahi kuzisikiaga tena humu humu jamvini wakati lile jengo linaanza kujengwa kuwa ni la Rostam Aziz. Sasa yupi mwenyewe?
 
Ndugu zangu mimi nadhani tuangalie mbali zaidi. Sehemu ilipo ikulu yetu kwa sasa sio salama tena kwa mambo mengi. Ni tishio hata kwa sunami, mazingira machafu yatokanayo na uchafu uelekezwao baharini, shuguli za kibinadamu kama za uvuvi na kata uchomaji taka hasa za hospitali iliyoko jirani. Sehemu ilipo ikulu kwa sasa ni lango kuu la bahari inayoingiza watu wenye nia njema na mbaya. Eneo la sasa ni wazi limekuwa sehemu ya mji na hatuwezi kukwepa pilikapilika zote tunazozifahamu za mijini. Sote tunajua siku za week ends shamrashamra zinazofanyika karimjee hall na viwanja vyake. Kelele zinazokuwepo huifanya ikulu isiwe mahali tulivu. Majengo mapya na marefu bila shaka yanahitajika jijini na yataendelea kujengwa. Kilichokuwa rahisi ili kutatua tuliyo nayo sasa na baadaye kwa mawazo yangu ni kuhamisha ikulu yetu na kuijenga sehemu salama zaidi hata ikibidi katikati ya kambi ya jeshi nje ya kidogo ya jiji. Ofisi za raisi zinaweza kuwa zaidi ya moja kuendana na mazingira yatakavyorurusu. Jengo linalozungumziwa sasa ni kivutio na linakidhi haja. Kwa umaskini tulio nao kufikiria kulivunja sio busara.

Umeongea kitu cha msingi sana. Angalia nchi nyingine. Ni kweli kwamba ikulu zao hazikabilianii na hali hiyo? Au ni mfumo mzuri tu wa kiusalama unao paswa kuwekwa? Nashuri watafute namna nyingine ya kufanya.
 
tangu sakata la ujenzi wa jengo refu la ghorofa 19 lililopo karibu na ikulu yetu kuanza kuwa gumzo hapa nchini, binafsi nimejitafakarisha mambo mengi kichwani mwangu. Kitu cha kwanza ni kwamba kabla ya jengo hilo kujengwa yalikuwepo majengo ya serikali ambayo kwa idadi kubwa yalikuwa yakikaliwa na maofisa wa juu wa serikali. Ufisadi na uvivu wa kufikiri wa viongozi waliopo ikulu ndio uliochangia maeneo hayo yatolewe kwa watu binafsi japokuwa ukweli ni kuwa hata viongozi wenyewe wa ikulu hiyo wamo kama wabia! Majengo hayo yamekuwa yakijengwa mchana kweupe! Rais wetu na mawaziri wake hiyo ndiyo njia yao wanayoitumia asubuhi na mchana na wote wamekuwa wakiona nini kinachoendelea hapo!
Sasa iweje leo baada ya jengo hilo kukamilika ndipo ionekane kuwa limejengwa kwa makosa? je, usalama wa taifa kazi yao ni ipi?! Au wanadhani ni kuvaa miwani myeusi na suti tu!

je, inamaana kama fbi wasingekuja kwa ajili ya ujio wa obama, wasalama wetu wasingegundua athari za jengo hilo? Mbona hata watu wa kawaida ambao wanapata huduma ya chakula kwa mama ntilie pale jirani wamekuwa wakiyasema hayo, inamaana usalama wetu ulikuwa haufiki pale na kupata maoni hayo?

na, je, kuna sababu gani ya kusema jengo libomolewe wakati linaweza kutumika kwa matumizi ya serikali na mjenzi akafidiwa pesa yake?

kwa hili maswali yapo mengi ambayo pengine hata majibu yake hayatakuwepo.

Ndiyo maana chadema inatakiwa ili ije kupitia upya miradi kama hii.

Mpaka hapo tupo PAMOJA mkuu!
 
Back
Top Bottom