Sakata la ujenzi wa jengo la ghorofa 19 ikulu: Nani wa kumfunga paka kengere?

Sakata la ujenzi wa jengo la ghorofa 19 ikulu: Nani wa kumfunga paka kengere?

Walitaifishe ziwe ofice za usalama afu watuajiri sisi vijana wenye sifa na uwezo wa kazi+maadili
 
Siku tutakapoamua kufuata sharia kuna watu wengi watakuwa majeruhi wa maamuzi yao yasiyotumia fikra...yangu macho! Thunderbolt strikes once...
 
Lazima tuelewe mfumo wetu wa ulinzi na usalama umekufa
Tangu za Mwalim kuna vijana wadogo hapa ikulu Miaka mitatu walk kuwa A'level sasa hivi wanaishi maisha anasa, statehouse sasa hivi ni ya familia pale.Othman,Zoka na wengi tu
Hata Mzee wa piga tu ndugu zake wapo kibao,Watanzania tusitegemee miujiza wengine tukihoji unaishia kwenye kisima cha maji au unapotea kabisa


WORD BROTHER :tape:
 
Ndugu yangu GeniusBrain siwezi kukulaumu kwani inadhihilisha ni kwajinsi gani akili yako ilivyolala na ndiyo maana huwezi hata kuipa muda wa kutafakari. Ila nashukuru kwamba umesoma na umeelewa nilichoongea ndiyo maana umecomment.

Kwani ikulu ikipigwa sisi watu wa vijijini kajamba nani tutapata hasara gani? shida zetu, karaha zetu, hatuna maji, hatuna masoko ya bidhaa zetu, watoto/wake zetu wanabakwa, usafiri tabu, huduma za afya ndo usiseme, tuna faida gani na ikulu?
 
Tangu sakata la ujenzi wa jengo refu la ghorofa 19 lililopo karibu na Ikulu yetu kuanza kuwa gumzo hapa nchini, binafsi nimejitafakarisha mambo mengi kichwani mwangu. kitu cha kwanza ni kwamba kabla ya jengo hilo kujengwa yalikuwepo majengo ya serikali ambayo kwa idadi kubwa yalikuwa yakikaliwa na maofisa wa juu wa serikali. ufisadi na uvivu wa kufikiri wa viongozi waliopo Ikulu ndio uliochangia maeneo hayo yatolewe kwa watu binafsi japokuwa ukweli ni kuwa hata viongozi wenyewe wa Ikulu hiyo wamo kama wabia! Majengo hayo yamekuwa yakijengwa mchana kweupe! Rais wetu na mawaziri wake hiyo ndiyo njia yao wanayoitumia asubuhi na mchana na wote wamekuwa wakiona nini kinachoendelea hapo!
Sasa iweje leo baada ya jengo hilo kukamilika ndipo ionekane kuwa limejengwa kwa makosa? Je, usalama wa Taifa kazi yao ni ipi?! Au wanadhani ni kuvaa miwani myeusi na suti tu!

Je, inamaana kama FBI wasingekuja kwa ajili ya ujio wa Obama, wasalama wetu wasingegundua athari za jengo hilo? Mbona hata watu wa kawaida ambao wanapata huduma ya chakula kwa mama ntilie pale jirani wamekuwa wakiyasema hayo, inamaana usalama wetu ulikuwa haufiki pale na kupata maoni hayo?

Na, je, kuna sababu gani ya kusema jengo libomolewe wakati linaweza kutumika kwa matumizi ya serikali na mjenzi akafidiwa pesa yake?

Kwa hili maswali yapo mengi ambayo pengine hata majibu yake hayatakuwepo.

NDIYO MAANA CHADEMA INATAKIWA ILI IJE KUPITIA UPYA MIRADI KAMA HII.

Ili waweze kupata habari za kutosha kuhusu Rais na maisha yake jengo kama hili inafaa liwepo. Chanzo kikubwa kuwepo hali hii yaani kuruhusu jengo refu kuchungilia ikulu ya Rais ni rushwa. Sasa hivi kumekuwa na maofisa usalama wa taifa wengi ambao ni raia wa kigeni, ukiuliza waliingiaje huko jibu la siri siri ni rushwa. Hujifanya wanafanya "VETTING" upuuzi mtupu. Kama kungekuwa na Intelligence makini jengo hili lilitakiwa kutaifishwa na serikali kwa ajili ya usalama wa nchi. Ipo siku tutakuja kusikia Mh. Rais amepigwa risasi na hawa snipers wala tusishangae kabisa kwani haya tunayalea sisi wenyewe. Mungu Ibariki Tanzania bila kuingiliwa na wageni hadi ngazi ya serikali.
 
hivi hili jengo si ndio makazi ya wajumbe wa tume ya katiba au?
 
Back
Top Bottom