Leak
JF-Expert Member
- Feb 22, 2012
- 52,916
- 43,505
Hating too much,
Nadhani hayo uliyoyaorodhesha ndiyo yanayowatofautisha wewe na yeye, yaani wewe una elimu na usimamizi mzuri na ndio maana upo hapo ulipo na yeye hana ndio maana yupo hapo alipo.
Busara ni kusubiri kumsikia na yeye anachosema badala ya kukimbilia kuhukumu kwa maelezo ya upande mmoja.
Nijuavyo mimi kila kizuri kina gharama, utamuelewa vipi mtu atakayekuja kwako na kukwambia anauza range rover evoque mpya kwa tsh milioni mbili ?.....kama ni mtu mzima na una akili timamu basi kitu cha kwanza utakachoweza kufanya ni kumuomba arudie alichosema, then nadhani kuepusha shari utajiondokea.....nadhani shughuli yake umeiona hapo kwenye video.
Na iwapo kuna alichokosea basi bado hata wewe unaweza kutoa ushauri afanye nini next time....nionavyo mimi bado ana nafasi ya kutafuta ushauri kwa waliomtangulia, na wazoefu wa mambo ya burudani iwapo kama alizengua.....sidhani kama kuna tatizo kuuuuuuuubwa hapa.
ukweli una sifa ya kuwasha - source miss strong
yani we FYATU mwenzio anaambiwa ukweli na anashauriwa lakini wewe unasema anachukiwa.huu ndio ukweli na kama umemsoma mwandishi huyo kwa utulivu utagundua kuwa amejaribu kuhakikisha diamond anaonekana mbaya na mjinga,kigeugeu,anajikweza kupitiliza.
hebu tueleze kama hayo aliyo yadai diamond yalikuwa ndani ya makubaliano au mkataba wa show, pengine waandaji walihamua kutimiza matakwa yake ili wasiwakwaze mashabiki.
Mwandishi amewafumba macho kwa kumpamba mwishoni lakini lengi lilikuwa ni kimshitaki diamond kwa mashabiki wake na wafanya biashara ya muziki.
Ni wazi kuna tatizo kwa diamond na hili swala linahitaji ufafanuzi maana habari hiyo si nzuri kwa biashara yake.
Last edited by a moderator: