na hiyo dhamana ay pesa???
nadhani nimekupata, atleast umetoa wazo la kupata ufumbuzi....kuliko hawa wanaokimbilia regime change!! atakuja rais mbowe na hili tatizo litakuwa pale pale, ila tofauti itakuwa hawa wazee watakuwa wanawakilishwa na vitukuu vyao.
tatizo kubwa hapa ni uzembe, chanzo ni Nyerere na hawa kina Kikwete wanafuata nyayo tu.....
YuonameisMINE ama mwaka 1977 ulikuwa hujazaliwa au unatawaliwa na chuki isiyo kifani na Mwalimu Nyerere.
Jumuiya ilikufa mwaka 1977 na zoezi la ugawaji mali za jumuiya lilichukua miaka saba na fedha za wastaafu zililipwa benki kuu ya Tanzania mwaka 1984. Zoezi la kuwalipa wahusika, baada ya uhakiki, lilitakiwa lianze mwaka 1985 wakati Mwalimu hayuko madarakani. Kati ya mwaka 1985 mpaka 1990 ilikuwa ni vigumu sana kulalamika na ukasikika kwa sababu ya monopoly ya vyombo vya habari. Hata hivyo mwaka 1991 ndio vilio vya hawa wazee vilianza kusikika kupitia magazeti binafsi kama Family Mirror. Kiongozi wa kwanza wa serikali chini ya Raisi Mwinyi kutamka kwa mbwembwe kuwa serikali haitawalipa hata wakipiga kelele nama gani alikuwa ni Mzee Cigwiyemwisi John Malecela, Waziri Mkuu na Makamu wa kwanza wa Rais. Huyo Malecela pia ndiye kabla ya hapo alikuwa balozi wetu Uingereza mwaka 1985 wakati "crown Agents" wanatoa hundi ya malipo haya kwa serikali ya Tanzania. Hizo fedha kwa pauni za kiingereza zililipwa moja kwa moja Benki kuu ya Tanzania.
EAC ilikuwa ni jumuiya ya kimataifa na ilikuwa na bunge lake, service commission yake, pensions fund yake na saving scheme yake. Makato ya pension yalitunzwa Uingereza kwa agents wa EAC waliojulikakna kama "crown agents". Mkataba wa EAC ulisema kuwa ikitokea jumuiya ikavunjika waajiriwa wake walipwe fedha zao kwanza ndio mengine yafuate, period. Pia waliainisha namna ya kulipa hizo kulingana na thamani halisi ya dola na riba ya asilimia 7%. Pia kumbuka kuwa baada ya kukalia hizi pesa kwa muda mrefu, serikali iliwahi kutamka kuwa madai yamekuwa makubwa kuzidi uwezo wa serikali - swali ni kwa nini hawakulipa mapema ? Hata kama kulikuwepo na matatizo ya kifedha nchini je serikali ilikuwa na haki gani kutumia fedha ambazo hazikuwa za serikali na kama walikopa ni kwa makubaliano yapi. Ukweli ni kuwa huu ulikuwa wizi wa kiwango cha kutisha kinachozidi hata hiki cha EPA.
Hawa hawakuwa wafanyakazi wa serikali na hizo fedha hazikuwa za serikali. Ni kama vile wewe unaaminiwa unapewa fedha umfikishie mag3, halafu wewe unaamua kuzitumia bila idhini yangu je, wewe siyo mwizi ? Kwa mfano mwingine karani wa fedha anapewa mshahara awalipe wafanyakazi, yeye anaamua kuzitumia je, si atakuwa ameiba ? Ni serikali iliyowaibia hawa wazee fedha zao na hivyo serikali inawajibika iwe ya Mwinyi, Mkapa au Kikwete si hoja. Mimi hili swali nalielewa vizuri sana kwa sababu nimekula miaka (lol). Kuna wakati hata wafadhili walikuwa tayari kuisaidia serikali kwa kuikopesha fedha iwalipe hao wastaafu kupunguza fedheha mradi tu serikali ieleze ilitumiaje hizo fedha. Kwa kuwa fedha zenyewe zilitumika kiajabu ajabu na katika mazingira yasiyoeleweka, serikali ilishindwa kufanya hivyo na hapo kuonyesha wazi kuwa fedha zilihujumiwa.
Katika kujaribu kujikosha kuna wakati serikali ilitoa malipo ya kati Tshs. 100.00 hadi 500,000.00 kwa kandika hundi katika kile kilichoonekana kama matusi kwa wastaafu. Serikali siyo tu imewaibia wananchi wake bali imekaidi hata amri ya mahakama kwa kutotekeleza makubaliano yaliyofikiwa. Madai ya wastaafu yamewatajirisha wezi serikalini na kinachonisikitisha ni ukimya wa bunge letu kwenye jambo hili. Wezi hawa wanatakiwa waache usanii na wazee wapewe haki yao ambayo haitapotea hata kama itadaiwa na vitukuu wao. Kwamba wabunge wanapigana vikumbo na hao wazee huko wizarani wakifuatilia posho zao bila chembe ya huruma kwao ni dalili ya uozo ndani ya nchi na ishara ya kupotea kwa maadili. Inasikitisha.
Kabla ya Raisi Mkapa kuondoka madarakani mwaka 2005 alitamka kwamba atahakikisha hamwachii mrithi wake hili deni ambalo lilikuwa limefikia karibu shilingi bilioni 450. Fedha zilitengwa na Waziri wa fedha Mramba alitangaza bungeni kuwa hawa wazee wangelipwa kwa awamu. Awamu ya kwanza wangelipwa bilioni 110 chini ya robo ya madai yao na wangeendelea kulipwa mpaka deni liishe. Hizo fedha zilizotengwa ziko wapi na nani aulizwe kama si serikali ya Kikwete ? Ajabu ni kuwa hizi fedha hazijalipwa hadi leo na wabunge wako kimya kama vile hawakuwa bungeni wakati huo na hivyo wazee kujikuta yatima kwenye nchi yao. Serikali haiwajali, bunge liko kimya na maamuzi ya mahakama yanadharauliwa - sasa nani asingelala barabarani ?
Taarifa zilizofika hivi punde ni kuwa wale wazee wetu wa iliyokua Jumuiya ya Afrika Mashariki wamekuja na style mpya ya kushinikiza madai yao baada ya kuamua kufunga barabara ya Ali Hasan Mwinyi karibia na Salender ili kuonyesha ni jinsi gani wamechoshwa na usanii na uonevu huu wa serikali yetu.
Hii ni hatua mpya binafsi nimependa style yao LAKINI JE SERIKALI YETU ITAWASIKILIZA au ndo yale yale ya kuziba masikio?
Taarifa zinasema kuwa kikosi cha askari kimetumwa kikiambatana na gari la maji ya kuwasha kwenda kuwaondoa bara barani.
Habari ndio hiyo,
KWELI TUMECHOKA NA MFUMO HUU WA LICHAMA HILI LA JEMBE NA NYUNDO huku kiukweli NI UFISADI NA UBINAFSI
...hapo ndio utakapo ona sisi tunaoambiwa tulikuwa hatujazaliwa mwaka 1977 ni werevu kushinda hivi vikongwe na mawazo yao mgando!! huu mshipa umeanzia kwa Nyerere, na kwa taarifa tu, mpaka watakapokubali kwamba mzizi wa fitina Tanzania ni Nyerere...basi hatutaenda popote na CCM itakuwa kidedea mwaka nenda mwaka rudi!!
.......Kabla ya Raisi Mkapa kuondoka madarakani mwaka 2005 alitamka kwamba atahakikisha hamwachii mrithi wake hili deni ambalo lilikuwa limefikia karibu shilingi bilioni 450. Fedha zilitengwa na Waziri wa fedha Mramba alitangaza bungeni kuwa hawa wazee wangelipwa kwa awamu. Awamu ya kwanza wangelipwa bilioni 110 chini ya robo ya madai yao na wangeendelea kulipwa mpaka deni liishe. Hizo fedha zilizotengwa ziko wapi na nani aulizwe kama si serikali ya Kikwete ? Ajabu ni kuwa hizi fedha hazijalipwa hadi leo na wabunge wako kimya kama vile hawakuwa bungeni wakati huo na hivyo wazee kujikuta yatima kwenye nchi yao. Serikali haiwajali, bunge liko kimya na maamuzi ya mahakama yanadharauliwa - sasa nani asingelala barabarani
..sasa hilo ni tatizo la nani!? na nini unajaribu kutuambia hapo? kwamba alikuwa dikteta au sio?? hilo ndio tatizo, braza...kwahiyo huyu "mswahili" wanamburuza kwa kuwa yeye si Nyerere au ni nini hasa?
Haya...mjadala mwema, mie najikata zangu!! siku njema...
of course lazima akimbie.. sasa mtu kaja anataka tumbebeshe lawama Nyerere, tumembebesha sasa tukishafanya hivyo tunatarajia kuwa matatizo ya hawa wazee yatakuwa yameanza kutatuliwa. Nimeomba basi atueleze baada ya kukubali lawama zote za matatizo yetu tumemtwisha Nyerere now what next... ? anasema "anajikata"... well.. asirudi na hoja ya kumlaumu Nyerere aje na mapendekezo ya kuona jinsi gani wazee hawa wanatatuliwa matatizo yao.
lakini hilo hawezi kwani linahitaji kufikiri zaidi. Atakachorudi nacho ni "hatuwezi kuanza kufikiria utatuzi wa matatizo ya wazee hawa kwani Nyerere ameshikilia mawazo na fikra zetu, hatu tujitanzue kutoka kucha zisizoachialia za Nyerere ndio tutaweza kuannza kufikiri vizuri".
Tangu Babu amuambie "Nyerere" ndiye mbaya wao basi ndio imekuwa kasheshe.. sasa..
Brazakaka,
Sidhani kama umri wangu au nimezaliwa lini ni nyeti ktk huu mjadala! lakini kama itasaidia basi mie umri wangu ni kati ya miaka 28-32....
Chuki sina na bwana Nyerere na hata ikitokea siku nimekutana nae mbele za haki, basi mie nitamueleza yalo alotuachia na li chama lake bovu aliloliasisi..
Umetoa maelezo mengi mazuri na marefu, lakini kimsingi umejichanganya sana na mwisho wa siku bila kujijua umekuja upande wangu ktk hii debate....kwamba monster hapa ni serikali ya awamu ya kwanza chini ya Nyerere na baada ya hapo wamekuwa wanapokezana vijiti!! Kusema sehemu umeandika, "mkataba wa EAC ulisema kuwa ikitokea jumuia ikavunjika, basi waajiriwa wake walipwe fedha zao kwanza ndio mengine yafuate, period." Mwisho wa kunukuu....sasa kama hivyo ndivyo kwanini wao waliamua kutofuta hicho kipengele na badala yake wakatumia miaka saba kugawana mali na malipo ya hawa vikongwe yakawa mwisho?? kosa la nani kama sio mkuu wa nchi wa wakati huo ambae ni Mchonga (mungu amrehemu)!!.
Kisha kuna sehemu umeuliza swali, "kwanini hawakulipa mapema."?? Kwa mawazo yako tokana na kipengele nilicho quote hapo juu unadhani lawama za kutolipa mapema ni za nani?? wote tunajua kuwa deni likikaa muda mrefu riba ina pile na hivyo kuongezeka, njia rahisi na lengo hasa la kusema waajiriwa walipwe kwanza ilikuwa ni ku-avoid hiyo mess...lakini ni awamu ya kwanza iliyoruhusu hiyo delay na kufika hapa tulipo leo.
Maana ya kutomwachia mrithi wako deni ni kwamba unakuwa umelipa kabla ya kuondoka!! vinginevyo kiswahili labda pia sijui siku hizi, hizi story za kusema, "oooh simwachi mrithi wangu deni" halafu baadae unasema nilimwachia fedha alipe ni usanii mwingine! Pia, hakuna ushahidi kwamba Mkapa aliacha fwedha za kulipwa hawa wazee.......ktk hili sakata lawama nyingi zaidi ni kwa awamu ya kwanza, pili, tatu na kidogo sana kwa awamu ya nne! Nionacho mimi, hii finger pointing ikome, kilichobaki tuje na jinsi ya kuwalipa hawa wazee fwedha zao...lakini story za kupaka matope wa wa awamu ya nne kusema kwamba wao ndio waliovunja EAC siwezi kukubaliana nalo.
Mkini-label kuwa namtetea Kikwete pouwa tu......lakini mie sizimii CCM wala Chadema, napenda kusema kweli!!.
njioni njema....
Asante YournameisMINE
Lakini nafikiri kuna kitu hukukielewa katika maelezo yangu. Kwanza nia yangu haikuwa kumtetea Nyerere bali kuelezea mtiririko wa sakata lenyewe. Pili kwa huo umri uliyoutaja ni wazi kuwa iliyokuwa EAC hukuijua na historia yake hukuijua.
1. Mgawanyo wa mali ya defunct EAC ulisimamiwa na World Bank na uliendeshwa na mtaalamu wa benki hiyo aliyejulikana kama Dr. V. Umbritch.
2. Uhakiki wa mali kwa nchi zote tatu, Kenya Uganda na Tazania, haukuwa kazi ndogo kama unavyofikiria na ulijumuisha mashirika na idara zote za jumuiya kwa kuzingatia assets na liabilities zote za jumuiya nje na ndani ya Afrika Mashariki na hasa Ulaya.
3. Viongozi wakuu wa nchi hizi tatu walikabidhiwa report mwaka 1984 na baada ya kuikubali walitakiwa waweke saini zao. Report ilikuwa kubwa na ndefu na ilihitaji muda kusoma na kupitia kila kipengele. Kama sikosei nafikiri ilikua na kurasa zisizopungua mia nne.
4. Baada ya hapo hesabu za malipo zilifanywa na hundi moja kutolewa kwa kila nchi kulipa raia wake waliohusika. Uhakiki wa wadai ulifanyika na mwaka 1987 ulikuwa uwe mwanzo wa malipo.
5. Kwa sababu zisizoeleweka serikali ya Mwinyi haikuweza kutekeleza hilo na wadai pamoja na kulalamika kimya kimya hawakuwa na namna nyingine ya kusikika kwa kuwa hakuna gazeti wala redio iliyoweza kutoa habari hizo. Juhudi zao za kukutana na kuandamana zilidhibitiwa vilivyo na FFU ambao wakati huo walikuwa wamepata zana za kisasa za kusambaratisha mkusanyiko wowote.
6. Baada ya kusikia wenzao wa nchi zingine wanalipwa ndio wakazidi kupaza sauti na mwaka 1991 madai yao yaliweza kuchapishwa kwenye vyombo vya habari vya binafsi kama Family Mirror. Ni wakati huo serikali iliweza kutoa tamko kupitia kwa waziri mkuu.
7. Ingawa sikumbuki vizuri kuna wakati walijaribu kumwona Mwalimu ambaye wakati huo ailshastaafu hata uenyekiti wa CCM na inasemekana alistushwa sana kusikia hawajalipwa.
9. Wakati jumuiya ikingali hai, Jakaya Kikwete aliwahi kuwa kwenye baraza la Mawaziri wa EAC na anaelewa vizuri sana hili jambo hivyo ukimya wake unashangaza kweli.
10. Ukimya wa wabunge, waandishi, watetea haki za binadamu na makundi mbali mbali kwenye hili swala ndio unaowasukuma hawa wazee kujiuliza maswali ambayo majibu yake ni kitendawili na kuamua kulala barabarani.
Ahsante sana Mag3 kwa maelezo yako mazuri.
Mimi swali langu kwako ni kivipi Mwalimu Nyerere nae asilaumiwe kwenye hili suala la kuwanyima haki zao hawa wafanyakazi wa iliyokuwa jumuiya ya EAC Kama marais wengine waliomfuata?
Je kutokana na hiyo tetesi ya hao wazee kumuona Mwalimu Nyerere na yeye kushtushwa kwa kutolipwa kwa hawa wazee, ni uamuzi gani aliouchukua kuhakikisha hawa wazee wanalipwa huku ikijulikana kabisa yeye katika mwaka huo wa 1987 alikuwa na influence kubwa sana serikalini na kama sikosei alikuwa bado mwenyekiti wa CCM.
Man...I'm tired of hearing Nyerere this...Nyerere that.....can you people get over him? Geeeez!!! The man is dead and he ain't coming back. Get over him....
tatizo langu lipo palepale kwamba, "waajiliwa wa EAC walipaswa kulipwa kwanza incase jumuia inavunjika." Hayo ni maneno yako msee, sasa kama ndivyo hivyo kwanini hilo lisiwe la kwanza na badala yake limekuwa la mwisho?
Kama Nyerere alikuwa muadilifu, mpenda maslahi ya watu wake na kumweka nje ya hii mess (kilawama) ilitakiwa asimamie utekelezaji wa waajiliwa kulipwa kwanza kabla ya hayo mengine.
tatizo la TZ, viongozi wanapokezana vijiti, wananchi wengi ni myopic na wavivu wa kufikiria...watu wanataka short term fixes bila kuangalia mzizi wa tatizo kiasi kwamba liking'olewa ndio iwe mwanzo na mwisho! na hiyo ndio tofauti kati yangu/yetu na nyie mliobaki.