Salama na Fatma Karume (Shangazi)

Salama na Fatma Karume (Shangazi)

Nafaka

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2015
Posts
12,154
Reaction score
31,246
Jana nimebahatika kutazama kipindi cha Salama Jabir akipiga story na Fatuma Karume.

Wamezungumzia mambo mengi ila mimi kwangu hasa nilichokiona kwa Shangazi ni kwamba ni mtu ambaye hana furaha (ni mtazamo wangu) kutokana na muonekano wake. Na hii ninahisi inasababishwa na mtazamo wake kuhusu mambo yanayoendelea hasa akilalamika sana kuhusu mfumo wa kutoa haki hasa mahakama kuwa hazifanyi kazi kwa haki na kuwa kama mhimili unaojitegemea.

Pia, katika maelezo yake nahisi jambo lingine linalomsumbua, ni kwamba anaona kuna watu wanaonewa wanakandamizwa na hawajui kama wanaonewa wala kukandamizwa bado wanaona kila kitu ni sawa na hata ukiwaeleza hawaelewi unachowaeleza. Hili jambo uwa linawasumbua wengi nadhani Zitto akiwa mmoja kati ya watu ambao uwa wanachambua mambo ambayo wengi uwa hawayaelewi na wala kumsikiliza.

Pia, alijaribu kughusia kuhusu ofisi yao kuchomwa moto japo Salama alimuwahi akamwambia hataki kwenda huko na pia aligusia kuwa kafungiwa kufanya shughuli za uwakili, na akaendelea kuwa anaishi kwa kufanya shughuli za arbitration huko Uingereza na ni shughuli aliyokuwa akiifanya hata kabla hajaanza kufanya masuala ya uwakili Tanzania.

Ilikuwa interview nzuri nilipata kumfahamu zaidi huyu shangazi. Mungu ampatie maisha marefu huyu mwanamama.

fatmaa.jpg
 
Kuna saa huwezi kumuelewa mtu aliyekulia maisha ya juu hata kama anakueleza ukweli unabaki kuona anakusimanga,anakusumbua,hajui shida zako bali anaigiza kuzifahamu. Hali anayopitia shangazi ni hali wanayopitia wengi.

Angalia wataalam wa masuala ya watoto,wamama wakishafahamu huyo mtaalam hana au hajawahi kuwa na mtoto basi wanaona hafai hata kama ana utaalam wa kiasi gani.
 
Kuna saa huwezi kumuelewa mtu aliyekulia maisha ya juu hata kama anakueleza ukweli unabaki kuona anakusimanga,anakusumbua,hajui shida zako bali anaigiza kuzifahamu. Hali anayopitia shangazi ni hali wanayopitia wengi.

Angalia wataalam wa masuala ya watoto,wamama wakishafahamu huyo mtaalam hana au hajawahi kuwa na mtoto basi wanaona hafai hata kama ana utaalam wa kiasi gani.
Very true mfano mimi uwa nina tabia ya kuwaambia akina dada kwanini uwa wanachukua ushauri kwa hawa wakina mama wanaonekana kwenye tv au redio ambao hawana waume kuwashauri kuhusu ndoa.
 
Wanahabari wa Tanzania wengine ovyo sana.

Unamuita mtu kwenye mahojiano, anataka kufunguka, halafu unamkataza mengine asiongee?

Upumbavu gani huu?

Wamekua waoga sana wanakwepa Rungu la TCRA kwamba katika mahojiano utawajibika kwa kile atakachosema mgeni wako

Miaka hii 5 imetupatia "normal" nyingi mpya

Unfortunately na Uongo/kujikomba/kuficha/uoga ni OUR NEW NORMAL
 
Shangazi yulo REAL, wala sio kwamba hana furaha. Sema tu upande alioamua kuutumikia una madudu mno, na wengi wamekaa kimya sasa ulitaka nani mwengine ayazungumzie hayo madudu yaliyomo kwenye system?. Shangazi ameletwa duniani kwa kazi maalum, hakika kazi yake tunaiona ni yeye peke yake ndo anayoifanya.

Ukija na uzi wa Maria Sarungi uniTag.
 
Jana nimebahatika kutazama kipindi cha Salama Jabir akipiga story na Fatuma Karume.

Wamezungumzia mambo mengi ila mimi kwangu hasa nilichokiona kwa Shangazi ni kwamba ni mtu ambaye hana furaha (ni mtazamo wangu) kutokana na muonekano wake. Na hii ninahisi inasababishwa na mtazamo wake kuhusu mambo yanayoendelea hasa akilalamika sana kuhusu mfumo wa kutoa haki hasa mahakama kuwa hazifanyi kazi kwa haki na kuwa kama mhimili unaojitegemea.

Pia, katika maelezo yake nahisi jambo lingine linalomsumbua, ni kwamba anaona kuna watu wanaonewa wanakandamizwa na hawajui kama wanaonewa wala kukandamizwa bado wanaona kila kitu ni sawa na hata ukiwaeleza hawaelewi unachowaeleza. Hili jambo uwa linawasumbua wengi nadhani Zitto akiwa mmoja kati ya watu ambao uwa wanachambua mambo ambayo wengi uwa hawayaelewi na wala kumsikiliza.

Pia, alijaribu kughusia kuhusu ofisi yao kuchomwa moto japo Salama alimuwahi akamwambia hataki kwenda huko na pia aligusia kuwa kafungiwa kufanya shughuli za uwakili, na akaendelea kuwa anaishi kwa kufanya shughuli za arbitration huko Uingereza na ni shughuli aliyokuwa akiifanya hata kabla hajaanza kufanya masuala ya uwakili Tanzania.

Ilikuwa interview nzuri nilipata kumfahamu zaidi huyu shangazi. Mungu ampatie maisha marefu huyu mwanamama.

Huyu wakamchunze uraia wake. Atakuwa anauraia wa uingereza hivyo anatakiwa aishi kwa kibali hapa nchini.

Huyu mama baba yake alikuwa madarakani miaka 10, aliwafanyia nini wazanzibari? Mbona hatukumsikiaga kutetea haki zao? Alafu hao wanaokandamizwa wako Bara tu?

Mbona haendi kwao kuwaeleza wananchi wao jinsi chama cha baba yake na baba yake akiwemo vilivyowakandamiza?

Baba yake hakumuibiaga Maalim kura mara mbili huyu? Mbona hakujitokeza kumpigania Maalim?

Wakati wapemba wanalishwa shaba 2001, nani alikuwa raisi wa Zanzibar? Mbona hatujawahi kumsikia akiwapazia sauti?

Shenzi type tu. Watanzania tuache unafki. Akili hata za kugelezea zinatushinda?
 
Huyo mama ni kilaza tu

Akili za darasani akaenazo mwenyewe sisi tunataka matokeo mtaani

Mbona hajawahi kuwa mwanaharakati babaake akiwa madarakani?

alikiri baba yake alikuwa na madhaifu na pia alifanya makosa katika urais wake kama binadamu wengine. Pia aliongelea vitu vingi tu kwa maswali yanayofikirisha ambayo "vilaza" wenzie baadhi tumemuelewa

sidhani hata kama umeangalia interview yenyewe na kama umeangalia bhasi uliitazama kwa angle uliyotaka wewe.
 
Back
Top Bottom