Sale Mti wa kimila kwa Wachange - Kwa Lugha ya Kingereza mti huu unaitwaje

Kurunzi

JF-Expert Member
Joined
Jul 31, 2009
Posts
9,753
Reaction score
10,747


Kwa ndugu zangu wachagga natumaini mtakuwa mnaujua mtii huu, Sale (Isale) ambao ni mti wa asili kwa imani za asili za kabila la wachagga.

Nimejaribu sana kuugoogle na hata kuulizia mti huu kwa jina la kingereza au kikitaalamu lakini sikupata jibu au majibu.

Hivyo naomba kwa yule mwenye ufahamu wa mti huu anijuze.

Zaidi natanguliza shukrani zangu kwenu.

Wasalaam, Kurunzi.
 

Unaulizia majina ya miti ya JADI, unataka kutambikia?. au umepata demu wa kichaga?; ok; mti unaitwa Dicapitulum stuhlumanii var mozambicans.
 
Huu mmea ni kweli una nafasi kubwa sana katika mila za Wachagga, kwanza kuwekea mipaka ya vihamba, hutumika pia katika kuombea msamaha kwa mtu uliyemkosea, pia hupandwa makaburini kuonyesha makao ya mwisho ya mwili wa marehemu, Kwa kiswahili si ufahamu wala kiingereza ila Isale ni mmea wakipekee kwa jadi ya wachagga.
 
unabaki kuwa isale hata kwa kiingereza kwani si upo uchagani
wachaga washaupa jina toka zamani
you have to honor your language
 
Nadhani huu mmea unatumiwa pia na makabila mengine. Kwa mfano wahaya wanauita EKILAMULA na unatumika katika kuweka mipaka ya mashamba na pia kuwa alama ya makaburi
 

Karunzi hebu weka picha ya huo mti(Isale) kwa post ili tuende pamoja tukusaidie coz wengine chenga tupu humu ndani
 
Nadhani huu ni aina fulani ya mbono kaburi, ngoja niende lab niacheki
 


Mmea wa kuombea radhi mnapokosana.
Mmea wa kuombea mkopo bila kukataliwa.
Nadhani hata ukimuendea Binti aliyeshindikana kutongozeka ukampatia "sale" hawezi kataa.
 
Kurunzi na Bubu Msemaovyo,

Mti huo kwa kichaga unaitwa 'Isale" na kwa kipare unaitwa 'isae" kwa kitaalamu unaitwa 'Dracaena mannii'

Karibu,

Haya sasa Kurunzi leta habari zaidi ya huu mti, si umeona Bubu Msemaovyo amelianzisha taratibu….
 

unaitwa sales
 
Huu mti ni muhimu sana kwenye makabila yanayo hodhi ardhi, yaani wachaga na wahaya. Sehemu yenye ardhi bwerere haina haja ya mipaka labda miaka 100 ijayo nao wataanza kuweka kutumia miti mingine.
 
Mi nadhani unaitwa dracaena fragans
 
Kurunzi na Bubu Msemaovyo,

Mti huo kwa kichaga unaitwa 'Isale" na kwa kipare unaitwa 'isae" kwa kitaalamu unaitwa 'Dracaena mannii'

Karibu,

Haya sasa Kurunzi leta habari zaidi ya huu mti, si umeona Bubu Msemaovyo amelianzisha taratibu….

Nimejaribu ku google hilo jina hapo juu lakini napata result ambayo inaonekana ni mti tofauti kwani ISALE huwa haitoji matunda tofauti na huu uliuonyesha hapa.
 
Nimejaribu ku google hilo jina hapo juu lakini napata result ambayo inaonekana ni mti tofauti kwani ISALE huwa haitoji matunda tofauti na huu uliuonyesha hapa.

Kurunzi, weka picha ya "Isale" unaoujua/unaousema wewe ili tusaidiane kulipata botanical name yake.
 
Nadhani huu mmea unatumiwa pia na makabila mengine. Kwa mfano wahaya wanauita EKILAMULA na unatumika katika kuweka mipaka ya mashamba na pia kuwa alama ya makaburi

Maana yake "mwamuzi", si ndiyo? Kwa maana kuwa una mamlaka makubwa sana sababu mwamuzi ana mamlaka makubwa sana ndani ya jamii
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…