Tetesi: Salim Abdallah ‘Try Again’ katika jaribio la kumng’oa Mo Dewj Simba!

Tetesi: Salim Abdallah ‘Try Again’ katika jaribio la kumng’oa Mo Dewj Simba!

View attachment 2966280

Moto unawaka SSC! Ni vita kubwa!
Klabu ya Simba ipo katika kipindi kigumu cha vita inayozidi kukomaa kila uchwao baina ya Mwenyekiti wa bodi ya Wakurugenzi ya Simba Salim Abdallah Muhene Try Again dhidi ya Rais wa heshima wa Simba Mohamed Mo Dewj.

Wawili hao walianza kukosa maelewano baada ya Mo Dewj kuhamisha makazi yake nchini ambapo taarifa za uhakika ni kwamba anaishi Dubai hadi hivi sasa.

Baada ya Mo Dewj kuhamisha makazi uwekezaji wake Simba ulisuasua, ikitaarifiwa kumuachia mzigo mkubwa wa uendeshaji timu Try Again ambao ulimuelemea!

Try Again alijitahidi kadiri ya uwezo wake baada ya tajiri kujitenga kiaiana, akihaha huku na huko kutafuta namna ya kuinusuru Klabu ya Simba ambayo kwa msimu wa tatu sasa mfululizo imekuwa na matokeo ya kusuasua. Jitihada zake hizo zikionekana kuzaa matunda kwa kiasi kisichoendana na kipindi ambacho muwekezaji alikuwa ameshikilia usukani.

Try Again adhamiria mapinduzi, amlenga Said Salim Bakhressa!
Baada ya Try again kususiwa timu na muwekezaji Mo Dewj, Try Again aliona uwezekano wa kupindua meza, na kama ilivyo ada ya wafanyabiashara wakubwa kuwa na jicho angavu la udhia, S.S Bakhressa hakusita kupenyeza rupia!

Vita kubwa iliyopo hivi sasa ni Try Again aliyeko kwenye mikakati thabiti ya kumpindua Mo Dewj kama muwekezaji kisha nafasi hiyo apewe muwekezaji asiye na mbambamba S.S. Bakhressa, huku Mo Dewj nae akiwa katika mipango ya kujidhatiti kushikilia nafasi yake hiyo adhimu ambayo huitumia mara nyingi kama kielelezo cha mali zake (SSC)

Serikali yakoleza vita!
Hivi karibuni, Serikali imetoa agizo la kuanzishwa upya kwa mchakato wa undeshwaji wa kisasa kwa klabu ya Simba. Kama mtakumbuka vyema mchakato huo ulioanza miaka kadhaa nyuma, haukuwahi kukamilika.

Serikali imetoa agizo hilo baada ya kujiridhisha kuwa mchakato wa awali ulikuwa na makosa mengi, hivyo ulikuwa batili ukikosa uhalali.

Agizo hilo limekuwa chachu kwa Try Again na timu yake, kwani endapo ukifanikiwa kuanza kuna uwezekano mkubwa wa S.S. Bakhressa na wawekezaji wengine kujitokeza na kushika hatamu katika mgawanyo wa hisa, huku ikielezwa kwamba Mo Dewj atarudishiwa fedha zake alizolipia katika mchakato wa awali uliohuishwa ambako alijitwalia hisa 49% za umiliki wa klabu ya Simba.

Mo Dewj atupa shilingi mechi ya Yanga!
Hii ni tahadhari kwa Klabu ya Yanga, Hersi na wenzio kama hamjaipata nawapa hii…

Mo Dewj amejipanga kuitumia mechi ya tarehe 20/04/2024 dhidi ya Yanga kama turufu yake ndani ya Simba.

Mo Dewj ambaye inaarifiwa ametenga fungu nono kuhakikisha Simba inashinda mechi hiyo, amejipanga sawia na mkakati wake huo ambao tayari ameshaanza utekelezaji.

Mkakati huu wa Mo ni kwamba endapo Simba ikishinda mechi hiyo, atafanikiwa kurudisha imani na mapenzi kwa mashabiki, hivyo kutumia hilo kama zengwe la kuwang’oa Try Again na Mangungu pale Simba.

Kila mmoja ana mpango kazi!
Try Again ambaye hapo awali alitumia janja janja kuwang’oa aliyekuwa CEO wa Klabu bibie Barbara na Rweyemamu ambaye alikuwa meneja wa timu kwa kuwachonganisha na muwekezaji Mo Dewj, anahaha kulinda maslahi yake kwani endapo Mo Dewj akishinda vita hii (Kwa Simba kushinda dhidi ya Yanga) amepanga kuwarejesha Barbara, Rweyemamu ambaye hivi sasa yupo Kikosi B na aliyekuwa Mwenyekiti wa bodi ya Wakurugenzi ambaye alijiengua Mkwabi.

Try Again ambaye wameungana na Mangungu kumuhujumu Mo Dewj, nao hawako nyuma. Wanatumia turufu yao ya ujanja wa mjini kuhakikisha Mo Dewj anang’oka Simba kwa namna yoyote!

Inaarifiwa hata agizo la kuanza upya kwa mchakato wa uendeshaji wa kisasa wa timu umechagizwa na connection za Try Again pamoja na S.S.B na mpaka hivi sasa mpango wao umetiki.

Je, nani ataibuka mshindi katika vita hii? Ni watoto wa mjini Salim Abdallah, Try again au tajiri Mo Dewj?

Ni mimi na chanzo changu nyeti,

Nifah.

Pia soma
- Tetesi: - Simba imepasuka. Kuna Simba ya Try Again na Simba ya Mo, Kila upande unauroga upande mwingine
Uzi bado unadunda ama sasa ndiyo umefikia kikomo?

Hebu tuambie madam, isijekuwa vita sasa inahamia nje.
 
Uzi bado unadunda ama sasa ndiyo umefikia kikomo?

Hebu tuambie madam, isijekuwa vita sasa inahamia nje.
Tunamsubiria tajiri mwenye masimango atoe tangazo kwa umma!

Ndani ya dk 35 kutoka sasa taarifa atakuwa ameitoa
20240611_215855.jpg
 
Mo arejea kama Mwenyekiti wa bodi na kamteua Try Again kua mjumbe wa Bodi, kiko wapi sasa?

Tuliwambia mapema hizi taarifa ni feki zipuuzeni mkakaza shingo, mkamwaga misifa kwa mzushi uchwara, akawa anatupiga vijembe

Mzushi uchwara katelekeza uzi kwa aibu ya kuaminisha watu uongo, na walioukubali uongo wa mzushi uchwara wanaupita uzi kama vile wanaaga maiti iliyopata ajali ya moto
 
Unaelewa kinachoendelea ndani ya Simba ewe shabiki maandazi? Kwa Sasa ikutoshe kuelewa tu kwamba Kuna danadana inapigwa hapo,Mudi ni mjanja sana na Hilo li timu lizee ni kama shamba lake hivyo anachoma vichaka atakavyo Hadi makolo mtapopata ufahamu,Kwa Sasa mmelala usingizi mzito nyie mizigo..Kwa kifupi ni kwamba imebadilika chupi tu ila mkundu ni ule ule
Unaongelea hasira, wazee wa kusambaza taarifa za uongo mmepanic baada ya mambo kwenda tofauti na uzushi wenu,

Mo karudi kama mwenyekiti wa bodi na try again kateuliwa kua mjumbe, hii ni ngumi ya mdomo kwenu nyinyi wazushi wote sasa mmepagawa, jishikilieni ufalme wa mnyama unarejea, ile miaka 4 ya umwenyekiti wake mlipitia mateso makali sana lazima muogope mtetemeke

Simba ipo Imara mashabiki na wanachama tunamkubali Mo na tunamuamini, nyinyi mnaumia nini?


"Mo,Ninarejea nikiwa na nguvu na ari mpya mpaka Simba itakaporejea kwenye hali yake ya kawaida", amesema Dewji na kuongeza:-

"...naongozwa zaidi na ushabiki wa Simba, siyo uwekezaji, wala ufadhili wala udhamini......sitaiacha Simba leo wala kesho".
 
  • Thanks
Reactions: Tsh
Watu wa kuzusha na kusambaza taarifa za uongo
Mimi nashangaa mnapoteza muda kusikiliza uzushi.Si huyo huyo aliyedai eti Hersi anatoka na Mobeto.Eti mdhamini ni shemeji yake yaani GSM.Wakati Hersi ameoa Arusha wala hajaoa dada wa mdhamini wa Yanga.Ni mzushi njaa apuuzwe.
 
Unaongelea hasira, wazee wa kusambaza taarifa za uongo mmepanic baada ya mambo kwenda tofauti na uzushi wenu,

Mo karudi kama mwenyekiti wa bodi na try again kateuliwa kua mjumbe, hii ni ngumi ya mdomo kwenu nyinyi wazushi wote sasa mmepagawa, jishikilieni ufalme wa mnyama unarejea, ile miaka 4 ya umwenyekiti wake mlipitia mateso makali sana lazima muogope mtetemeke

Simba ipo Imara mashabiki na wanachama tunamkubali Mo na tunamuamini, nyinyi mnaumia nini?


"Mo,Ninarejea nikiwa na nguvu na ari mpya mpaka Simba itakaporejea kwenye hali yake ya kawaida", amesema Dewji na kuongeza:-

"...naongozwa zaidi na ushabiki wa Simba, siyo uwekezaji, wala ufadhili wala udhamini......sitaiacha Simba leo wala kesho".
Sasa tusubiri usajili.
 
Mimi nashangaa mnapoteza muda kusikiliza uzushi.Si huyo huyo aliyedai eti Hersi anatoka na Mobeto.Eti mdhamini ni shemeji yake yaani GSM.Wakati Hersi ameoa Arusha wala hajaoa dada wa mdhamini wa Yanga.Ni mzushi njaa apuuzwe.
Huyu dada ni muongo sana
 
Huyu dada ni muongo sana
Hivi wewe una akili timamu kweli? Habari niliyoileta ilikuwa vita ya madaraka kati ya Mo na Salim, na niliuliza kabisa ni nani ataibuka mshindi?

Sikuweka hitimisho la kwamba Mo atashindwa, na ni kweli kwamba vita ilikuwepo baina yao na wengi waliripoti.

Uongo uko wapi?
 
Hivi wewe una akili timamu kweli? Habari niliyoileta ilikuwa vita ya madaraka kati ya Mo na Salim, na niliuliza kabisa ni nani ataibuka mshindi?

Sikuweka hitimisho la kwamba Mo atashindwa, na ni kweli kwamba vita ilikuwemo baina yao na wengi waliripoti.

Uongo uko wapi?
Unavuthibitisho wa hiyo vita uuweka hapa? Yani watu wawe kwenye vita ya madaraka wateuane tena inakuingia akilini.?

Kwenye conent ulikua unatamba na kuzodoa watu kwa kujifanya taarifa yako ni ya kweli.

Chutama dada umepuyanga, tulikuambia toka mwanzo kua huu ni uzushi ukashupaza shingo

Ukaja na Uzi mwingine wa kuhusu Eng Hersi na mke wake eti ni shemeji yake GSM, kitu ambacho si kweli

Punguza uongo na uzushi
 
  • Nzuri
Reactions: Tui
Mo arejea kama Mwenyekiti wa bodi na kamteua Try Again kua mjumbe wa Bodi, kiko wapi sasa?

Tuliwambia mapema hizi taarifa ni feki zipuuzeni mkakaza shingo, mkamwaga misifa kwa mzushi uchwara, akawa anatupiga vijembe

Mzushi uchwara katelekeza uzi kwa aibu ya kuaminisha watu uongo, na walioukubali uongo wa mzushi uchwara wanaupita uzi kama vile wanaaga maiti iliyopata ajali ya moto
Halafu wanamuita eti jasusi.,[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Jasusi my kimba! [emoji706]
 
Unavuthibitisho wa hiyo vita uuweka hapa? Yani watu wawe kwenye vita ya madaraka wateuane tena inakuingia akilini.?

Kwenye conent ulikua unatamba na kuzodoa watu kwa kujifanya taarifa yako ni ya kweli.

Chutama dada umepuyanga, tulikuambia toka mwanzo kua huu ni uzushi ukashupaza shingo

Ukaja na Uzi mwingine wa kuhusu Eng Hersi na mke wake eti ni shemeji yake GSM, kitu ambacho si kweli

Punguza uongo na uzushi
Sikia, sijakulazimisha kusoma ninavyoandika. Kama unaona ni uzushi si uache kufuatilia? Uzushi na bado unasoma kila ninachokileta?

Acha kufuatilia taarifa/habari ninazozileta, simple.
 
Halafu wanamuita eti jasusi.,[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Jasusi my kimba! [emoji706]
Halafu kila uzi ninaouleta mmejaa tele 😂😂
 
Sikia, sijakulazimisha kusoma ninavyoandika. Kama unaona ni uzushi si uache kufuatilia? Uzushi na bado unasoma kila ninachokileta?

Acha kufuatilia taarifa/habari ninazozileta, simple.
Siwezi Kuacha Kusoma Nyuzi humu Jf, na Siwezi kuukalia kimya uongo na Uzushi,

Jasusi wa Mchongo
 
  • Kicheko
Reactions: Tui
Back
Top Bottom