Salome Makamba: Mabando ya simu yasiwe na ukomo wa muda wa kuisha

Salome Makamba: Mabando ya simu yasiwe na ukomo wa muda wa kuisha

Nyendo

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2017
Posts
1,336
Reaction score
4,731
Mbunge Salome Makamba, amesema kuwa habari ya mabando kuisha muda wake baada ya kujiunga ni sawa na kuwaibia watanzania, adai kuwa ukijuinga bando la simu liwe la dakika za maongezi au la data unaweza usilitumie kutokana na changamoto nyingi sana zikiwemo za kukosekana kwa mtandao wa simu au mambo mengine, kulikata kisa muda kuisha si sahihi kwani kampuni za simu zinakuwa zimechukua pesa nyingi kwa watanzania ambayo walilipia ila hawajatumia huduma.

Amesema kuwa kampuni za simu zikichukua sh. 200 kutokana na mabando ambayo yameisha muda bila kutumika yanaweza kusanya pesa nyingi kwa mwezi sawa na bajeti ya wizara ya habari, mawasiliano na teknolojia ya habari.

Ameitaka serikali kuwasaidia watanzania ili makampuni yaache tabia hiyo kwani amesema mambo ya mabando kuisha muda kwa sasa hayapo katika nchi nyingine duniani.

Akitetea hoja yake amesema kuwa kuna mapendekezo ya kuwa ili kuzuia hilo labda mtu aongeze salio kabla ya muda wa kuisha bando la awali ili kulinda bando lisiishe muda, amesema hiyo si sawa kwani itakuwa ni kumlazimisha mtu kufanya matumizi ya pesa yake ambayo alikuwa hajayapanga ili tu kulinda bando lisiishe muda, amesimamia hoja ya mabando yatumike hadi yaishe na si ku- expire.
 
Ameongea vema ila utekelezaji ndio mtihani mkubwa..
 
Mbunge Salome Makamba, amesema kuwa habari ya mabando kuisha muda wake baada ya kujiunga ni sawa na kuwaibia watanzania, adai kuwa ukijuinga bando la simu liwe la dakika za maongezi au la data unaweza usilitumie kutokana na changamoto nyingi sana zikiwemo za kukosekana kwa
Kumbe kuna baadhi ya wabunge wana akili...
 
Wanatumia mchana kwenye. Hii ni kero kubwa sana. Hongera zake.
 
Ameongea point muhimu. hivi halichachi iliishia wapi?
 
Kuna jamaa alikuwa anatuletea update humu kuhusu nia yake ya kuyashitaki makampuni ya simu kwenye hili aliishia wapi?
 
KWANINI HAWA WATU WAMEKUWA WAKIPEWA NAFASI ZA KUCHANGIA BUNGENI BAADA YA KUFUKUZWA CHADEMA?
 
Kipindi anafanya kazi pale vodacom makao makuu kwa nini hakusema haya anayoyasema leo au ni kutafuta cheap popularity
 
Mbunge Salome Makamba, amesema kuwa habari ya mabando kuisha muda wake baada ya kujiunga ni sawa na kuwaibia watanzania, adai kuwa ukijuinga bando la simu liwe la dakika za maongezi au la data unaweza usilitumie kutokana na changamoto nyingi sana zikiwemo za kukosekana kwa
Wabunge kama wewe wana thamani kubwa sana kwa watanzania!! Huo ndio uwakilishi wa wananchi uliotukuka!! Naomba uchaguliwe tena 2025 na Mungu akupe maisha marefu. Kwa hoja yako hiyo umeigusa mioyo ya watanzania! Tatizo makampuni ya simu yanatoa rushwa sana kwa mamlaka zinazohusika. Utashangaa hoja kama hii haitafuatiliwa wala kuungwa mkono!! Naomba mbunge wetu uchukue hatua ya ziada ya KUJA NA HOJA BINAFSI BUNGENI KUHUSU JAMBO HILI!!
 
Mbunge Salome Makamba, amesema kuwa habari ya mabando kuisha muda wake baada ya kujiunga ni sawa na kuwaibia watanzania, adai kuwa ukijuinga bando la simu liwe la dakika za maongezi au la data unaweza usilitumie kutokana na changamoto nyingi sana zikiwemo za kukosekana kwa mtandao wa simu au mambo mengine, kulikata kisa muda kuisha si sahihi kwani kampuni za simu zinakuwa zimechukua pesa nyingi kwa watanzania ambayo walilipia ila hawajatumia huduma.

Amesema kuwa kampuni za simu zikichukua sh. 200 kutokana na mabando ambayo yameisha muda bila kutumika yanaweza kusanya pesa nyingi kwa mwezi sawa na bajeti ya wizara ya habari, mawasiliano na teknolojia ya habari.

Ameitaka serikali kuwasaidia watanzania ili makampuni yaache tabia hiyo kwani amesema mambo ya mabando kuisha muda kwa sasa hayapo katika nchi nyingine duniani.

Akitetea hoja yake amesema kuwa kuna mapendekezo ya kuwa ili kuzuia hilo labda mtu aongeze salio kabla ya muda wa kuisha bando la awali ili kulinda bando lisiishe muda, amesema hiyo si sawa kwani itakuwa ni kumlazimisha mtu kufanya matumizi ya pesa yake ambayo alikuwa hajayapanga ili tu kulinda bando lisiishe muda, amesimamia hoja ya mabando yatumike hadi yaishe na si ku- expire.
yupo sahihi ila amesahau waliyopanga hayo ni ccm
 
Nampenda huyu mama hayo ndio maneno ya kuwawakilisha wananchi wanyonge bungeni., haya makampuni yanaiba sana hela za watu, dhumla tupu haya makampuni ya simu, kuna siku unakuwa unajiunga bando la internet bila ya matumizi yoyote apo apo unaambiwa una MB 0 uongeze nyengine
 
Back
Top Bottom