Salome Makamba: Uchumi wa Tanzania umesimama tu tangu 2001. Rais haambiwi ukweli na wateule wake

Makamba alisema tatizo hilo linatokana na uchumi wa Tanzania kusimama tangu mwaka 2001 na kudai wateule wanashindwa kumwambia ukweli Rais ili abadili mfumo wa maisha.
Wenyewe wanasema eti Magufuli ameutembeza mpaka kufika kwenye "uchumi wa kati". Sijui hii dhana ya uchumi kufika level za kati huwa inapimwaje na hawa wataalamu wetu ?
 
Tunaomba wabunge wasimamie na kuhakikisha wizara zinazoshughulikia kilimo, mifugo na uvuvi zipewe kipaumbele ili watu tusije kufa njaa, maana yake tunapoelekea Mungu ndiye ajuaye. Basi bora tuwe na chakula cha kutosha hata kama tukikosa maendelo lakini chakula kiwepo siku zisonge mbele.
 
kwamba kwa siku hatumii vocha ya 500, hanunui mafuta ya kula ya 500, hanunui dagaa wa 500, hasagi unga kwa 500, hanunui sukari ya 500 au 1000, hanunui majani ya sh 50, anafikaje kesho huyo bila kula?
Hata huko kwenu usukumani kuna watu hawanywi chai kwa mwezi mzima, dagaa wanazisikia redioni sembuse kununua vocha? Acha kijifaragua wewe?
 
kwamba kwa siku hatumii vocha ya 500, hanunui mafuta ya kula ya 500, hanunui dagaa wa 500, hasagi unga kwa 500, hanunui sukari ya 500 au 1000, hanunui majani ya sh 50, anafikaje kesho huyo bila kula?
Amini nakwambia kuna sehemu nchi hiii...ukimuita mtoto umpe andazi hajui cha kulifanyia,maana hajawahi kuliona.
 
Huyu kakosea mlango wa kuingia... hili bunge ni la sifa na mapambio kwa msukuma.
 
Inakuwaje daktari anashindwa hata kuwekewa oxygen anaposhindwa kupumua mpaka anakufa wakati wabunge ambao hata hawajachaguliwa na wananchi wanachezea kodi za wananchi????
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…