TANZIA Salum Shamte wa Katani Ltd afariki dunia

TANZIA Salum Shamte wa Katani Ltd afariki dunia

Ni jambo la kusikitisha kuwa Bwana Shamte amekufa akiwa "mfungwa" ambaye hakuwa amepata nafasi ya kujitetea ....ili kuongea upande wake mahakamani, tumesikia habari za upande mmoja ambazo ndio kama zilikuwa zimemuhukumu .....amekufa akiwa bado yuko ndani kwa makosa ambayo hayana dhamana na ilibidi kupelekwa pale na Magereza kwakua bado alikuwa kizuizin


KOSA LA SHAMTE NI KUWA MWENYEKITI WA TPSF ....ALIKUWA AMESHAONYESHA WAZI KUWA HAMTAKI NA ALITUMIA NJIA HIYO KUMUONDOA ...KWA MUDA WOTE AMBAO SHAMTE AMEKUA MWENYEKITI WA TPSF ...AMEKUWA AKIRUKWA KWENYE MAMBO MENGI YA KIKAZI TOKA JUU NA BADALA YAKE AMEKUWA AKITUMIWA MAKAMU WAKE ...AMBAYE "WANAONGEA LUGHA MOJA" ....NA NDIYE AMEKUWA AKIPELEKA MANENO YOTE YA UCHONGANISHI YALIYOFANIKISHA SHAMTE KUPINDULIWA PALE KWA HIYO KESI ILI ASIWE KIONGOZI WA WAFANYABIASHARA
Kinachosikitisha zaidi, zama hizi hata utetezi hauna maana. Kosa ni la kubambikiwa, ushahidi kamwe hautakamilika, kwa makusudi, imewekwa hilo kosa la kubambikiwa halina dhamana. Unatumikia kifungo bila ya kuhukumiwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Anko is at peace at last.. His soul has resten at last. Let them reap what they have sown!
Amen. Sitaandika tena kuhusu Shamte, roho yangu imetulia sasa! Tulipitia kipindi kigumu sana sana! Wote tuwasafiri na Wapitaji humu duniani hatuna mji udumuo. Karma is a bitch. It is over now Mshana Jr

Jr[emoji769]
 
Katani ilijenga kiwanda cha kwanza duniani cha kuzalisha umeme kutoka kwenye mabaki au takataka za mkonge ambazo awali zilikuwa zinatupwa tu – (FIRST IN THE WORLD SISAL ENERGY PLANT AT HALE ESTATE). [emoji117][emoji117][emoji117][emoji117]huo ugunduzi ulikuwa wa mtu aliyeitwa Gideon Seng'enge ambaye hakimiliki zake alidhulumiwa na Shamte... PENGINE kuna siku tafiti zake zitatambuliwa RASMI na kuifanya familia yake ifaidike... Tafiti nyingine ni za maji ya mkonge kutengeneza POMBE KALI na mabaki ya mkonge kutengeneza chakula cha kuku Elli
UKWELI KUHUSU KAMPUNI YA KATANI LTD
UUNDWAJI WA KAMPUNI:
Kampuni ya Katani Limited iliundwa wakati wa zoezi la ubinafsishwaji wa shirika lililo julikana kama TANZANIA SISAL AUTHORITY (TSA) – kwa Kiswahili – MAMLAKA YA MKONGE TANZANIA (MMT).
Katani Limited ilishinda zabuni na kununua hisa 999,999 kati ya hisa 1,000,000 za Kampuni ya MGC (sehemu ya TSA/MMT) zilizouzwa na The Presidential Parastatal Sector Reform Commission (PSRC). Katani Limited ni kampuni ya uwekezaji na uongozi (Investment & Management Company) ambayo ilikuwa inamilikiwa na wanahisa wafuatao:
Wawekezaji wa nje ambao kwa pamoja walimiliki asilimia 90 ya hisa za Katani Limited. Makampuni hayo ni;
Grecian Investment (UK) Ltd, ambayo mmiliki wake ni raia wa Kigiriki ambaye aliwahi kuwa mkulima wa mkonge Tanzania.
Wigglesworth & Co Ltd, ambayo ni kampuni ya Uingereza ijulikanayo duniani kama ni wanunuzi, wauzaji na wasambazaji wakubwa wa mkonge na bidhaa zake. Kampuni hii imekuwa inafanya shughuli hizi kwa zaidi ya miaka 105.
Dekowe GmbH ambayo ni kampuni ya Kijerumani inayotengeneza, kusambaza na kuuza mazulia ya mkonge, Amerika ya Kaskazini, Ulaya, Japani na Bara la Asia. Pia ina viwanda Portugal, Romania na India. Kampuni hii imekuwa ikifanya shughuli hizi kwa zaidi ya miaka 120.
Umoja wa wafanyakazi 87 akiwemo Salum Shamte na wenziwe 86 ambao walikuwa wataalamu waajiriwa wa ofisini na mashambani. Hao kupitia mafao yao kwa pamoja waliweza kulipia asilimia 10 ya hisa za Katani Ltd., kupitia kampuni waliyoisajiri na iliyojulikana kwa jina la Mkonge Investments and Management Co. Ltd (MIM).
Katani Limited iliingia mkataba na Serikali wa kununua baadhi ya mali hizo za TSA (ambazo zilihamishiwa kwenye kampuni ya MGC), tarehe 13 Februari 1998.
MALIPO YA AWALI, UWEKEZAJI NA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA MAUZO:
Wawekezaji hao wanne kwa ujumla wao walilipa malipo ya awali na kuanza uwekezaji kama ilivyo kwenye mkataba.
Hali ya mashamba na mitambo kabla ya kuanza uwekezaji ilikuwa mbaya sana;
Chini ya TSA (ambalo lilikuwa ni Shirika la Umma lililopewa dhamana ya kusimamia na kuendesha shughuli za mkonge baada ya utaifishaji); uzalishaji wa mkonge ulishuka kutoka tani 234,000 mwaka 1964 hadi tani 19,000 mwaka 1997;
Miundombinu ilikuwa imechakaa na kuharibika;
Mashine zilikuwa zimechakaa na mitambo ilikuwa mibovu;
TSA ilikuwa imetengeneza hasara kwa zaidi ya miaka 15 kabla ya kubinafsishwa.
Mchakato wa ubinafsishaji ulichukua takribani miaka 6 kabla ya kukamilika Februari 1998.
Kipengele muhimu kwenye mkataba wa mauzo ni upatikanaji wa hati za mali zilizohamishiwa MGC kutoka TSA, ambazo Serikali iliahidi kuzitoa ndani ya miezi sita.
Uwekezaji ulianza mara moja kwa wawekezaji kutumia fedha zao.
Kiwanda cha TANCORD, kilichokuwa kimefungwa, kilifanyiwa ukarabati na ndani ya miezi saba tu kilianza kazi.
UKIUKWAJI WA MAKUBALIANO YA MKATABA WA MAUZO
Wawekezaji walifuatilia hati hizo kwa muda wa miezi 22 bila mafanikio;
Hati zilikuwa ni nyenzo muhimu kwa wawekezaji kutafuta mitaji na mikopo ndani na nje ya nchi;
Desemba 1998 Wawekezaji wa Nje walisimamisha utoaji wa fedha zao na Desemba 1999 waliamua kuondoka na kuuza hisa zao kwa kampuni ya KiTanzania HIGHLAND ESTATES LTD.;
Highland Estates Ltd nayo ilifuatilia hati bila mafanikio. Iliwekeza kiasi cha dola laki nane za Kimarekani (US$ 800,000);
Highland Estates Ltd iliposhindwa kupata hati, mwaka 2000 nayo iliuza hisa zake kwa kampuni nyingine ya Ki-Tanzania AFRIKA MPYA LTD.;
Wakati wote huo MIM (Kampuni ya Wafanyakazi) ilikuwa bado ipo palepale na hisa zao asilimia 10.
MZOZO WA UKIUKWAJI WA MASHARTI YA MAUZO YA HISA BAINA YA PSRC NA KATANI LTD NA USULUHISHI WAKE
(AFRIKA MPYA na MIM) wakiwa kama KATANI Ltd iliendelea kufuatilia upatikanaji wa hati na ilipofika Februari 2002 Katani na PSRC walifikishana mbele ya Wasuluhishi wa mgogoro huo kama ilivyo elekezwa kwenye mkataba.
Wasuluhishi katika mgogoro huo walikuwa Wanasheria nguli wafuatao:
Marehemu Mzee Peter Bakilana (Wakili wa Kujitegemea) - Mwenyekiti
Mheshimiwa Mzee Joseph S. Warioba (Waziri Mkuu Mstaafu) – Mjumbe
Mzee Mohamed Ismail (Wakili wa Kujitegemea) - Mjumbe
Katika shauri hilo, yafuatayo yalibainika:
Katani ililipa mikupuo miwili ya bei ya mauzo ya mali za MGC kama ilivyotakiwa kwenye mkataba:
Katani ilitekeleza baadhi ya vipengele vilivyo kwenye Mpango wa Biashara (Business Plan), ambao ulikuwa ni sehemu ya mkataba;
Katani haikuharibu na ililinda mali na miundombinu iliyo karabatiwa, kinyume na madai ya PSRC;:atani haikukiuka haki za Serikali kama PSRC ilivyodai.
HUKUMU - Ilielekeza Katani waingie makubaliaano upya na Serikali. Hii ilipelekea Katani na Serikali kutengeneza na kutiliana saini Hati ya Makubaliano (Memorandum of Understanding), Aprili 2005 na kusaini Mkataba Mpya Machi 2007, ULIOTHIBITISHA KATANI LTD HAIDAIWI NA SERIKALI.
KUINGIZWA KWA MFUMO WA WAKULIMA WADOGO NA WA KATI
Katani Ltd iliasisi mfumo wa Wakulima Wadogo wa mkonge kuanzia mwaka 2000, ili kupanua milki ya mashamba ya mkonge. Mfumo huo ulifanikiwa kwa kiasi kikubwa sana.
Kwa kuwa Katani ilipewa baadhi tu ya hati mwaka 2005; iliona badala ya kung’ang’ania hati iwashirikishe wananchi wengine 2100 ambao wengi walikuwa wafanyakazi katika mashamba hayo, na kuwaendeleza ili wawe Wajasiriamali Vijijini;
Kila Kaya ya hao wananchi 2100 pamoja na wote wa MIM walipewa kila kaya eka 15 bure.
Serikali ilitoa hamasa kubwa sana iliyopelekea watu wengi kujitokeza kuchukua mashamba hayo.
Masharti ya mashamba hayo ni kwa kila Mkulima kulima mkonge ingawa katikati ya miraba walilima mazao ya chakula.
USHIRIKI WA NSSF KATANI LTD
Katani Ltd ilitambua kuwa wengi wa wakulima wadogo hawana uwezo wa kuendeleza mashamba hayo. Lakini hata wakulima wa kati hawakuwa na uwezo hasa ukitilia maanani zao la mkonge linalochukua miaka mitatu kabla kuanza kuvunwa.
Kwa mantiki hiyo Katani Ltd iliomba ushiriki wa NSSF ili watoe mkopo kwa kuendeleza kilimo cha mkonge.
Ili kukidhi mahitaji ya Mpango mzima wa miaka kumi (10) wa Biashara, Katani Ltd iliomba mkopo wa dola za Kimarekani milioni sabini (US$70 milioni). NSSF ilikuwa iungane na mashirika mengine ya fedha ili kufanikisha mkopo huo.
NSSF, kama ilivyo mifuko ya jamii/penseni ulimwenguni ndiyo chanzo kimoja kikuu kwa kukuza uchumi na inatumika duniani hasa kwa mikopo ya muda mrefu.
Kwa bahati mbaya sana NSSF haikufanikiwa kupata fedha zilizohitajika za Mpango wa miaka kumi wa Biashara, wa Dola za Kimarekani milioni sabini (70). Waliweza kutoa sehemu ndogo sana, ya kiasi cha Dola za Kimarekani milioni sita na laki saba (US$6.7 milioni).
NSSF walikubali kwa masharti kuwa Katani watoe mkopo huo kwa wakulima kwa njia ya HUDUMA ambazo ni;
KUWALIMIA
KUWAPANDIA MBEGU BORA
KUWAPA UTAALAMU
KUWASAIDIA UPATIKANAJI WA MASOKO
Mkopo wa NSSF wa US$ milioni 6.7 uligawanywa katika sehemu mbili;
Ununuzi wa vifaa kama matrekta, mabuldoza, makatapila, mashine za uendeshaji wa mashamba na viwanda;
Uendeshaji kwa Katani Ltd.
Kadhalika, ilielekezwa malipo kutoka kwa wakulima yatakatwa watakapo anza kuvuna na kulipwa;
MATOKEO YA UFANISI WA MKOPO
Uzalishaji ulipanda kutoka Tani 849 mwaka 2005 mpaka Tani 5,420 mwaka 2017.
Katani Ltd iliweza kukarabati viwanda vitatu na kujenga viwanda vipya vinne vya kusindika mkonge katika wilaya ya Korogwe ambavyo awali vilikuwa vimekufa kwa zaidi ya miaka 15.
Katani ilijenga kiwanda cha kwanza duniani cha kuzalisha umeme kutoka kwenye mabaki au takataka za mkonge ambazo awali zilikuwa zinatupwa tu – (FIRST IN THE WORLD SISAL ENERGY PLANT AT HALE ESTATE).
Katani iliweza kukarabati na kupanua Kiwanda cha Tancord cha kuzalisha bidhaa za mkonge.
Katani iliweza pia kutoa gawio kwa Wanahisa mwaka 2013, 2014 na 2015.
USHIRIKI WA NSSF KAMA WANAHISA
NSSF waliona upungufu mkubwa wa mahitaji ya fedha zaidi kwa Katani Ltd kama waliyoomba awali.
Hii ilitokana na wananchi zaidi kutaka kuingia kwenye mradi, ikiwa ni pamoja na Wahariri wa baadhi ya Vyombo vya Habari ambao walifanya kazi nzuri sana ya kuhamasisha wananchi.
Wananchi waliona mabadiliko mazuri ya wenzao walioko kwenye mradi wanavyoweza kuyakabili maisha.
NSSF baada ya kuombwa na kujadiliana na Katani Ltd ilikubali;
Kuubadilisha mkopo wa kwanza wa US$6.7 milioni kuwa hisa na walikubaliana hisa asilimia 49 (49%);
Kutoa mkopo wa ziada kukidhi ongezeko la mahitaji.
NSSF walikubali kwa masharti yafuatayo;
Mwenyekiti wa Bodi ya Katani Ltd ateuliwe na NSSF na mjumbe mmoja mwingine wa Bodi.
NSSF ishiriki kumteua Mkurugenzi mpya wa Fedha na walishiriki kumteua Ndugu Fadhili Mhina kama Mkurugenzi wa Fedha wa Katani Ltd.
NSSF ifanye ukaguzi wa Katani Ltd kila miezi 6.
Isitoshe, ilikubaliwa kwamba Meneja Mwandamizi kutoka idara ya Mipango na Uwekezaji ya NSSF atakuwa anahudhuria mikutano yote ya Bodi ya Katani ambapo atapata taarifa ya maendeleo ya miradi inayotekelezwa kwa fedha za mkopo kutoka NSSF.
Hayo yalikuwa yakinafanyika bila kukosa. Hali ya Katani Ltd ilikuwa inaimarika kila walivyokuwa wanaendelea.
KILICHO TEREMSHA UTENDAJI WA KATANI LTD BAADA YA MAAGIZO YA MKUU WA MKOA – MHESHIMIWA MARTIN SHIGELA NA ATHARI ZAKE KWA KAMPUNI, TAIFA NA WANANCHI HUSUSAN WA MKOA WA TANGA
Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Ndugu Martin Shigela alileta vikwazo vingi kwa kampuni.
Kibaya zaidi aliifungia kwa nguvu Katani Ltd isizalishe kwenye viwanda vyake vyote kwa muda wa miezi sita (6) mwaka 2018.
Huu ni muda mrefu sana kwa kampuni kubwa kama Katani kufungiwa.
Alielekeza mkonge wote uuziwe kampuni ya Kichina pekee.
Kiwanda cha TANCORD kilinyimwa mkonge. Hata uliokuwa unatoka kwenye mashamba ya Wanahisa, alielekeza pia auziwe Mchina ambaye mkonge wote alikuwa anaupeleka China.
Kiwanda chetu ambacho ni cha kwanza kwa ukubwa Afrika kiliporomoka na kuzalisha asilimia 20 tu kwa kukosa mali ghafi.
Kiwanda kilibidi kipunguze wafanyakazi kufuatana na uzalishaji.
Serikali ilikosa kodi mbalimbali kwani Katani Ltd ni mmoja kati ya walipaji wakubwa wa kodi mkoani; na mauzo ya nje ya takriban shilingi bilioni kumi (bilioni 10).
Katani Ltd tarehe 3 Septemba 2018 ilimuandikia barua Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa yenye kichwa cha habari “ATHARI ZA MAAGIZO YA KIKAO CHAKE CHA AGOSTI 2018 NA KUORODHESHA ATHARI ZOTE NA USHAURI”.
Katani Ltd bado wanasisitiza kuangaliwa upya maagizo hayo ambayo kimsingi yanaua zao la mkonge Tanzania na tutakuja juta.
Menejimenti na Wafanyakazi wa Katani Ltd wamekuwa kwenye soko la mkonge kwa zaidi ya miaka hamsini (50), na inazijua mbinu zote ambazo zinaweza kutumika ikiwemo bei, upatikanaji, n.k. ambazo zitalenga kwenye kuididimiza Sekta ya Mkonge Tanzania.
MKOPO WA SHILINGI MILIONI 400 KWA TANZANIA PHARMACEUTICALS LIMITED
Tunapenda Umma uelewe kwamba, kampuni hizi mbili, Katani Ltd na Tanzania Pharmaceutical Industries Ltd (TPI) ni Kampuni binafsi (Private Companies), ambazo zina mamlaka kamili ya kukopa na kukopesha, kushtaki na kushtakiwa. Ndio maana Katani Ltd iliweza kukopa popote ilipokubalika.
Kampuni nyingi za binafsi (Private Companies) zina utaratibu wa kukopeshana, iwe fedha na/au malighafi. Kwa mantiki hiyo, Katani Ltd ilipokuwa na UKATA na kukosa fedha za kuendeshea mkutano wa Kimataifa wa Nyuzi Ngumu Asilia (International Conference on Hard Natural Fibres), ambapo Ndugu Salum Shamte alikuwa ni Mwenyekiti wa “FAO Conference on Hard Fibres”; na mkutano huo ulikuwa unafanyika Tanga, Tanzania, Katani iliomba mkopo kutoka TPI. TPI iliikopesha Katani Ltd fedha hizo. Mkutano ukafanyika, na Katani ilipokuwa na UKWASI, walizirejesha fedha hizo.
Kadhalika TPI ilipopata dharura na kuhitaji kile kinachoitwa “bridging finance”, iliomba mkopo kutoka Katani Ltd. Katani Ltd ilitoa mkopo huo kwa TPI kwa riba ya asilimia kumi na sita (16%). TPI iliurejesha mkopo huo wote, ikiwa ni pamoja na riba. Uhusiano huu ulikuwa ni wa kibiashara na pande zote mbili zilinufaika. Na hiyo ndio biashara.
NYUMBA YA LONDON ILIYOKUWA NI MALI YA TASMA LTD.
Zimetolewa tuhuma pia, zikielekezwa kwa Ndugu Salum Shamte kwamba aliuza nyumba (na pesa kutia mfukoni mwake), mali ya Mamlaka ya Mkonge Tanzania, iliyoko London na ambayo alikuwa akiishi alipokuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Tanganyika Sisal Marketing Association (TASMA); Kampuni tanzu ya Tanzania Sisal Authority (TSA). Nyumba hiyo ya London ipo Edgware na Salum Shamte alipoondoka aliiacha mikononi mwa Ubalozi wa Tanzania. Ushahidi upo. Na mpaka leo kuna Afisa wa Ubalozi wa Tanzania nchini Uingereza anayekaa humo. Haingii akilini kwanini “TUME” ilishindwa kuwasiliana na Ubalozi wa Tanzania nchini Uingereza na kupata ukweli. BADALA YAKE, WANAOMBA RUHUSA YA KWENDA LONDON “KUFANYA UCHUNGUZI…!”
NYUMBA YA TANGA ALIYOUZIWA SALUM SHAMTE
Nyumba ya Salum Shamte anayokaa Tanga aliuziwa wakati wa Ubinafsishaji, miaka ya 1990/2000. Mauzo haya yalifanyika kihalali kama yalivyofanyika kwenye nyumba nyingine za Mashirika ya Umma yaliyo binafsishwa kama vile Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), Tanzania Breweries Limited, Tanzania Cigarette Company Limited, SIMU 2000 – kwa kuyataja baadhi tu ya mashirika. Isitoshe, kuna nyumba nyingi ziliuzwa kwa wafanyakazi wa Serikali na Mashirika ya Umma waliokuwa wanaishi kwenye nyumba hizo. Hatuamini kuwa Serikali ina nia ya kuwanyang’anya maelfu ya Watanzania hao nyumba zao walizouziwa kihalali kutokana na maamuzi sahihi ya Serikali ya wakati huo.
MWISHO
Kwa kuwa taarifa ile ilisomwa kwa Umma, basi Umma ni lazima upate taarifa ya upande wa pili, ili uwe kwenye nafasi nzuri ya kupambanua kati ya HAKI na BATILI. Siku zote tunaambiwa kwamba ili haki sio tu inatakiwa itendeke, bali inatakiwa ionekane kuwa inatendeka. Ni muhimu Ndugu Shamte na wenzake wapewe fursa ya kujibu tuhuma zilizoelekezwa kwao na “Tume” ya uchunguzi.

Sent using Jamii Forums mobile app

Jr[emoji769]
 
Kwa hiyo Shamte kaiba na kadhulumu??????, mie namuona kama shujaa aliyekatishwa uhai na utawala wa kidhalimu wa mtukufu Jiwe. Shamte ni victim mwingine wa udikteta na utawala wa kimabavu usiozingatia utawala wa kisheria.

Mnawaweka lumande washua kwao ni zaidi ya Kifo manake hawajazoea taabu, sononi lazima iwaue na ukichanganya na umri ndio kabisa. Hapa sasa Jiwe na wafuasi wake roho kwatu.
Usilolijua ni kama usiku wa giza. Tumwombee tu hayo mengine msikufuru, kuhukumu na kubambika watu mara jiwe, mara sijui nini!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Daaah pole sana bwana Elli mjomba wako alikuwa Malaika mzuri sana.


Nenda mwanakwenda Shamte. Ulimdhulumu sana Uncle wangu, akawa demoted, wewe na akina Marehemu Ibrahim Kaduna, mkamfanya aishi maisha magumu na ya stress sana. Mkadhulumu haki miliki za tafiti zake, aligundua jinsi ya kutengeneza pombe kwa kutumia maji ya mkonge, chakula cha kuku kwa kutumia mabaki ya mkonge na umeme kwa kutumia maji maji ya mkonge.

aliandika vitabu kuhusu mkonge lakini hakufaidika navyo. Alinieleza haya 2007 na mwaka huo huo akapata stroke, nilimuuguza Tanga, mkashindwa kumlipia hata Ambulance kutoka Tanga to Muhimbili.

nilipowatafuta kwa ajili ya matibabu yake mkaishia kunipa Tzs 50,000. Mzee Shamte unakumbuka siku ile uliniita pale fire? Ukampa dereva bahasha yenye hio pesa?
Baadae ali-recover bado mkagoma kumlipia bill, na MKUMBUKE alistahili sio kwamba ilikua fadhila.

Siku moja jioni ya 12 tukiwa tumerudi kutoka kwenye mazoezi ya viungo pale Morocco Physiotherapy clinic, STARTV wakawa wanaonyesha kipindi cha mkonge na walionyesha hizo products ambazo huyu mzee wangu ndio alikua amwzifanya yeye ila zilitangazwa kama vile ni kazi iliyofanywa na mtoto wa Shamte. Kwakuwa nilikua nine Shaun vanish a dots, nikachukua remote nikataka kubadili Chanel, ananiambia nisiondoe.

Next day akiwa kwenye mazoezi napata second stroke na ndio ikawa mwisho wake. Akina Shamte bado walishindwa hata kumsafirisha.

sina nia mbaya, kifo ni kifo but kwa kusema haya naamini nimemtendea haki Marehemu Mentor wangu. He was a true friend of Mine.
 
Salum Shamte kauliwa na watu wenye roho za kishetani, hata Lucifer hajui atawaweka wapi watakapo kuwa wamepata hukumu ya mwisho. Huyu Jiwe aka Meko ni hatari
 
Hizi nyuzi za zamani hazina tija hapa jamvini inaonekana great thinkers tuna lack content kama ulitaka ku connect dotes siungechukua link tu ingetosha
 
Back
Top Bottom