Samatta hatomaliza misimu miwili ndani ya Ligi Kuu ya Uingereza (EPL)

Shida ni kwamba watu wanafanya analysis ya kitu walichokiona , hafu wao wanaleta zarau

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hongera kwako pia mkuu kwa kuwa na jicho la tatu, very few people can see beyond.
 
Huyu Samatta soon atapelekwa Uturuki kumalizia mpira wake baada ya timu yake kuwa imeshuka daraja.

Hana mpira wa kucheza EPL yule, ni kweli alibahatisha tu kwani hata spidi ya EPL hawezi.
Ili Ni Kaburi la tar 24 June,

Marehemu Alkua na mdomo Sana[emoji1]
 
yametimia na iyo sentensi ya mwisho ndio imetimia zaidi...
 
Mleta maada pongezi kwa kuona kile ambacho wengi hatukuona au pale tulipoona, kama ulivyoandika tuliona haya kusema kama kawaida yetu.

Mods: Napendekeza hii thread iwe sticky ili tuitumie kama rejea na kutanua wigo wa mjadala. Kwamba ikiwa mpambanaji kama Samatta kashindwa kufanya kazi epl, tunajifunza nini.

Binafsi nimejifunza mengi. Kwa leo nijadili hili moja. Kwamba "mfumo wetu wa soka hauna uwezo wa kuandaa mchezaji wa kiwango cha epl".

Baada tu ya mchezo wake wa kwanza Samatta alinukuliwa akisema kuwa dk 90 za epl ni sawa na kucheza mechi 2 mpaka 3 kwa Ubelgiji. Hivyo alichoka mapema na kufanya ishara ya kumtaarifu kocha kuwa afanyiwe mabadiliko (alikwenda chini).

Pia akadai kuwa kucheza pale kunahitaji nguvu sana ambayo hakuwa nayo hivyo akanuiya kuongeza mazoezi ya kujenga mwili (gym), kitu ambacho anakifanya mpaka sasa.

Kwa maneno yake yeye mwenyewe (kupitia Shaffi Dauda) ni kwamba angetumia zaidi advantage ya kasi na wepesi alionao ili kupata anachotaka.

Pendekezo:

Suala la shule za soka (vituo vya kukuzia watoto wanasoka) tusilichukulie kiutani utani tena. Serikali na TFF waje na mkakati thabiti wa kuhakikisha tunakuwa na vituo bora vya aina hii (soccer academies).

Huku tunajua watoto wataanza kupikwa mapema katika kila nyanja kuanzia ubongo, mtazamo, miguu, mpaka lishe bora. Lishe duni kwa wanamichezo ni sababu mojawapo ya kutokidhi ubora wa kimataifa wanapokua (hili liko dhahili).

Binafsi naamini kwamba huenda hata Samatta alianza kupata lishe bora (kwa mwanasoka) alipofika TP Mazembe! Unategemea nini hapo!

Nawasilisha.
 

[emoji848]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…