TANZIA Same: Wanakwaya watano KKKT Usharika wa Wazo Hill wafariki dunia wakielekea kwenye mazishi

TANZIA Same: Wanakwaya watano KKKT Usharika wa Wazo Hill wafariki dunia wakielekea kwenye mazishi

Chachu Ombara

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2012
Posts
6,067
Reaction score
10,938
Mkuu wa Wilaya ya Same, Kasilda Mgeni, leo Oktoba 22,2024, amesema basi hilo limepata ajali majira ya alfajiri, wakati likitokea Jijini Dar es Salaam kuelekea Machame, Wilaya ya Hai kwenye shughuli za maziko ya mwanakwaya mwenzao.

Kwa mujibu wa DC Mgeni, basi hilo liliacha njia na kugonga kalavati dogo la Kirinjiko.

"Ni kweli watu watano wamepoteza maisha, wakiwamo wanawake watatu na wanaume wawili. Wote hawa ni wana kwaya KKKT waliokuwa wakitokea Dar es Salaam kuelekea Machame,"amesema.

Basi hilo lilikuwa likiongozana na mabasi mengine manne, na dereva wake alisinzia na ghafla alishtuka ameligonga kalavati hilo.
 
Kwenye basi zima wamekufa watu watano tu!? ambao wote waliokufa ni wanakwaya!?.. hakuna abiria mwingine aliyefariki wala kujeruhiwa??,hali ya dereva ikoje!?,weka taarifa kamili ikibidi na picha kupunguza sintofahamu vichwani mwa watu.
 
Basi hilo lilikuwa likiongozana na mabasi mengine manne, na dereva wake alisinzia na ghafla alishtuka ameligonga kalavati hilo.
Poleni wafiwa

Uzoefu wa kuendesha safari ndefu atakuwa hana

Au kuna tatizo la Mombo yaani Mombo problem

Maiti zinazoenda Moshi huwa zinasimama pale Mombo wafiwa na madereva wale nyama choma na kunywa pombe kutafuta steam ya kutungua kilio kabla kuendelea na safari na madereva huwa wanatandika pombe pale

Niwaombe Traffic wakae kule mbele ya Mombo misafara yote ya maiti waisimamishe na wawapime ulevi madereva wote walioko kwenye msafara watawadaka wengi
 
Mkuu wa Wilaya ya Same, Kasilda Mgeni, leo Oktoba 22,2024, amesema basi hilo limepata ajali majira ya alfajiri, wakati likitokea Jijini Dar es Salaam kuelekea Machame, Wilaya ya Hai kwenye shughuli za maziko ya mwanakwaya mwenzao.

Kwa mujibu wa DC Mgeni, basi hilo liliacha njia na kugonga kalavati dogo la Kirinjiko.

"Ni kweli watu watano wamepoteza maisha, wakiwamo wanawake watatu na wanaume wawili. Wote hawa ni wana kwaya KKKT waliokuwa wakitokea Dar es Salaam kuelekea Machame,"amesema.

Basi hilo lilikuwa likiongozana na mabasi mengine manne, na dereva wake alisinzia na ghafla alishtuka ameligonga kalavati hilo.
Wapumzike kwa amani
 
Poleni Wanakwaya na familia nzima ya KKKT
God gives
God takes

Jina la bwana lihidimiwe 🙏🏽
 
Poleni wafiwa

Uzoefu wa kuendesha safari ndefu atakuwa hana

Au kuna tatizo la Mombo yaani Mombo problem

Maiti zinazoenda Moshi huwa zinasimama pale Mombo wafiwa na madereva wale nyama choma na kunywa pombe kutafuta steam ya kutungua kilio kabla kuendelea na safari na madereva huwa wanatandika pombe pale

Niwaombe Traffic wakae kule mbele ya Mombo misafara yote ya maiti waisimamishe na wawapime ulevi madereva wote walioko kwenye msafara watawadaka wengi
Watawadaka haswa
 
Usingizi ni muuaji mkubwa sana barabarani.
Nimeshakoswa sana na ajali kwa sababu ya usingizi,either nimesinzia au gari linalokuja mbele yangu dereva kasinzia,hii mara nyingi hutokea usiku mkubwa mida ya saa 8 mpaka saa 11 alfajri,ni Mungu tu anatulinda ila huwa ni hatari sana...
 
Mkuu wa Wilaya ya Same, Kasilda Mgeni, leo Oktoba 22,2024, amesema basi hilo limepata ajali majira ya alfajiri, wakati likitokea Jijini Dar es Salaam kuelekea Machame, Wilaya ya Hai kwenye shughuli za maziko ya mwanakwaya mwenzao.

Kwa mujibu wa DC Mgeni, basi hilo liliacha njia na kugonga kalavati dogo la Kirinjiko.

"Ni kweli watu watano wamepoteza maisha, wakiwamo wanawake watatu na wanaume wawili. Wote hawa ni wana kwaya KKKT waliokuwa wakitokea Dar es Salaam kuelekea Machame,"amesema.

Basi hilo lilikuwa likiongozana na mabasi mengine manne, na dereva wake alisinzia na ghafla alishtuka ameligonga kalavati hilo.
Uandishi haujakamilika
  1. Kwaya gani?
  2. Usharika gani?
  3. Jimbo gani?
  4. Majina ya marehemu yamekosekana kabisa?
  5. Je kuna majeruhi?
  6. Hali zao zikoje?
  7. Nini kinaendelea hadi sasa kwa waliosalimika pamoja na mwili wa marehemu aliyekuwa anasafirishwa?
  8. Ajali imehusisha gari lenye usajili gani na mali ya nani?
 
Back
Top Bottom